Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hebu tupia hayo mavesi hapa tusikoe mistari na biti!, Enrico bado anarekodi muziki?...walikuwa wanawanyanyasa sana madogo na vistudio vyao mshenzi.Mwaka 2001 nilitoka zangu Temeke studio za Soundcrafters kwa Enrico kuchukua single yangu niipeleke Clouds.
nikapitia IFM kwa mpenzi wangu wa kipindi hicho tukapata dinner,ilikuwa mishale ya saa mbili usiku,marehenu Steve B alinipa maagizo kuwa hiyo CD niiache kwa dada flani nadhani ilikuwa floor ya 7,la haulaaaa,kufika floor ys tatu lift ikazima,niko mwenyewe tu,niliyepanda nae alishuka floor ya pili.
Nilijaribu kuiachanisha kwa mikono wapi, nikajaribu kupiga mlango wapi,simu yangu siemens 25 imeshaisha chaji sina ujanja,nikaanza kupiga kekeke wapi,nikabonyeza kengele ya dharura wapi sipati msaada,nikaamua kukaa chini kusubiri muujiza,hapo Oxygen inazidi kuisha,kijasho kinanitoka,nikavua shati nikajaribu tena kupanua mlango nikafanikiwa kwa kiasi cha kupitisha kiganja tu,nikavua kiatu changu na kukiweka jatikati ya milangi ilihewa iingie huku nikisikilizia kama kuna mtu atapita au kushuka hiyo floor,
Mungu si athumani nikasikia mlango wa lift jirani unafunguka ndio nikapiga kelele ya kuomba msaada,yule mshangazi sijui alifanyaje nikaona wanakuja technician na kufungua mlango.
Ile CD nilisahau mulemule Kwenye lift nikarudi zangu nyumbani hapo ni saa nne usiku.Niko tumbo wazi mpaka maeneo ya Steers ndio nikakumbuka kulivaa
Baadae nikafuatilia kopi ya ile single yangu studio,nikaipeleka tena Clouds safari hii kwa tahadhari zote, ule wimbo ulipigwa mara moja tu nikajua nyota njema huonekana asubuhi.
Ingekuwa nchi za watu OTIS watengenezaji wa lift wangenilipa mamilioni
Pesa ngawira michuzi notiHebu tupia hayo mavesi hapa tusikoe mistari na biti!, Enrico bado anarekodi muziki?...walikuwa wanawanyanyasa sana madogo na vistudio vyao mshenzi.
😂😂DahKuna zile lift hazina sensor, ole wako ikukute ukatize kwenye mlango kilegevu...milango itakubamiza hadi usijue kama ulikuwa unaingia au unatoka!
Mwanajf, kwani Kiswahili hakina lahaja? Ningependa kujifunza zaidi"Tuwekee hio nyimbo na sie tusikilize"❌
"Tuwekee huo wimbo na sisi tusikilize"☑️
Jifunze tu Kiswahili,,kwani kuna katazo lolote au pingamizi limekukumba na likaleta shida katika kujifunza Kwako?Mwanajf, kwani Kiswahili hakina lahaja? Ningependa kujifunza zaidi
Mahari yako kiasi gani? Unaonekana unapenda kutunzwaMiaka 23 tu sio mingi
Sasa 2001 unasema kitambo?nahisi ni la miaaka ya l 70s hukoKumbe lile jengo la kitambo, juzi nilipita pale nilienda floor ya 13 ile lift yao ikifika unakoenda kuna mtikisiko fulani hivi.
Ndio naomba unifundishe je Kiswahili hakina lahaja? Je lahaja za Kiswahili hazitambuliki? Ningependa kujifunza zaidiJifunze tu Kiswahili,,kwani kuna katazo lolote au pingamizi limekukumba na likaleta shida katika kujifunza Kwako?
Kudadake wazee mko makini ni umoja na wingi"Tuwekee hio nyimbo na sie tusikilize"❌
"Tuwekee huo wimbo na sisi tusikilize"☑️
Pole sana Mkurugenzi.... Lift hizi Huwa zinaogopesha sana.... Nikiingiaga Huwa nawaza mara mbilimbili....
Kingine Huwa nawaza, vipi ikiporomoka downward! Yaani ifyatuke kushuka chini.... Lahaulaaa....