Nyie ndio wabishi kwa kuona bodaboda ni kazi ya chini wakati kuna watu wanalea familia, wamejenga sababu ya bodaboda. Kweli siku haziwezi kufanana lakini bodaboda ina hela sana kama mtu yupo serious na kazi yake. Kinachowaponza bodaboda na bajaji ni ulevi, bangi, umalaya na kamali ndio zinaishia hela zao na madeni juu. Sibishi mimi kazi yangu ilikuwa pembeni kijiwe cha bodaboda nilijifunza mengi sana kuwahusu.
Bodaboda yupo radhi atoe 20000 ya guest kula mzigo na akampeleka mtu huyo bure ruti ndefu labda mbezi hadi gmboto hapo kashapoteza kiasi gani. Bado hajalewa na kucheza kamali. Na wala hawajali kuhusu kesho as wanajua kesho ikifika nitapata tena.
Sikushauri kununua bodaboda kuwapa madereva wao wanachojali ni kula, kulewa na kamali yupo radhi asipeleke hela ya bosi ila akacheze dubwi amalize hata 40000 huko. Pamoja na urafiki nao kindakindaki siwezi kurisk kununua bodaboda kumpa dereva anajua hata asipokupa hela yako utachukua chuma yako leo kesho anapata nyingine maisha yanasonga.
Kwa mtu anayejielewa na kujua nini anafanya kutoboa kwa bodaboda ni rahisi sana sometimes biashara inakuwa ngumu kwao ila nina ushahidi usio wa stori kuwahusu.
Sent using
Jamii Forums mobile app