Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ushameza ARV zako?WA HOVYO SANA HUYU UMUGHAKA . AJE ASEME STORY IMEISHIA HAPA TUWAZE MAMBO MENGINE[emoji35][emoji35]
Humu kweli kuna watu hawana akili timamu, kabisa yaani kama huyu jamaa ni mwehu kabisa.KWANI HUJAENDA NA SIMU, AU UNAANDIKA KUPITIA DESKTOP. KAMA MATERIAL YAKO KICHWANI NA SIMU UNAYO HAPO MSIBANI KWENYE MAJAMVI SI UNAWEZA KUANDIKA TU VIZURI TUKAPATA UHONDO!![emoji16][emoji16]jokes.
Anyway, pole kwa msiba. UMUGHAKA
Wakichanga mkuu...wewe inakuhusu nini ni pesa yako? Kama unaona inakuuma meza mate...acha wivu utakonda na kufa na preshaDon't hate me lazima tuwe na mitazamo tofauti
Watanzania wengi ni wajinga acha tuwasaidie
Hapa wataibiwa tu
Mkuu kamalizia hapo mwisho kwa kusema anafanya utaniHumu kweli kuna watu hawana akili timamu, kabisa yaani kama huyu jamaa ni mwehu kabisa.
Ndugu kasema wazi kuna mahali wamepeleka msiba, It means wamefiwa! huko alipo yupo msibani..
Imagine mtu uko msibani unamajonzi halafu wakati huo huo unashauriwa uandike story ya kuwaburudisha watu! only Crazy can think that way...
SIKU UKIFIWA NA BASHA WAKO NDO UTAJUA Maana ya “Msiba usikie kwa mwenzio”WA HOVYO SANA HUYU UMUGHAKA . AJE ASEME STORY IMEISHIA HAPA TUWAZE MAMBO MENGINE[emoji35][emoji35]
Hakuna cha utani wala nini tizama amepost tena Upupu Hata 1 hour haijapita.Mkuu kamalizia hapo mwisho kwa kusema anafanya utani
Mbona umeishia hapa? Kupitia comments zote mtihani hapa natafuta bandiko lako tuNilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 20.
Gari ilitembea tukaikamata njia ya Sirari,sasa tukawa kama tunaelekea Musoma.Yule jamaa akamwambia yule demu aliyekua akiendesha gari ya kwamba inapaswa tuweke kituo kwanza Lamadi tukapate msosi kisha ndiyo tuondoke.
Baada ya kufika lamadi na kupata Msosi tuliondoka kuelekea Bariadi,sikuwahi kufika bariadi ni hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika huko,sasa baada ya kuiacha bariadi tulianza kuingia vijijini huko ndani ndani ambako sikuvifahamu kwa haraka maana sikuwa mwenyeji huko.
Kituo chetu cha mwisho kilikuwa kwenye kijiji cha Mwanaungu ambako baada ya kushushwa hapo,yule jamaa alimwambia yule demu kwamba amsubiri kwanza atupeleke halafu waondoke!.
Mtatiro "Mwanangu kwahiyo mnatuacha?"
Jamaa "Tutarudi kuwachukua ondoa shaka!"
Tulitembea kwa umbali mrefu kidogo hatimaye tukafika kwenye mji mmoja ambao ulikuwa umezungushiwa minyaa ya kutosha,baada ya kufika hapo tulikuta kuna vijumba vingi vya nyasi huku kukiwa na watu ambao wengine walikuwa wamelala kwenye majamvi huku wengine wakiendelea na shughuli zao!.Kuna mwanamke akaja kutupokea kwa salamu ya kisukuma huku akipiga magoti,sasa mimi kwakuwa nilikaa usukumani kwa kipindi fulani wakati baba yangu mdogo akiwa headmaster,ile salamu haikunipa taabu kabisa!,na siyo salamu tu,naweza kukizungumza kisukuma ingawaje cha kuombea maji!.
Baada ya ile salamu yule mwanamke alituletea viti ambavyo havikuwa na watu kwa wakati huo.Basi baada ya muda mfupi yule mwanamke akaja na daftari akatutaka kila mmoja wetu kutaja jina lake na kuandikwa,sasa tulipoandikwa akatuchania vikaratasi vikiwa na namba,mimi nilipewa namba 16 na Mtatiro akapewa namba 17,yule jamaa yeye akamwambia yule mwanamke kwamba anahitaji kuonana na Mwami(Ng'wana Mwami).Yule mwanamke akamtaka asubiri kwanza.
Baada ya muda yule mwanamke akaja akamuita yule jamaa akampeleka mpaka kwenye kinyumba cha nyasi kilichokuwa kikubwa kati ya vile vinyumba tulivyovikuta pale.Baada ya muda yule jamaa akatoka akaja akatuambia angerudi baada ya siku mbili,hatukujua alipoingia mle ndani alienda kuzungumza kitu gani na huyo aliyekuwa humo ndani!.Jamaa aliondoka akatuacha pale,hiyo ilikuwa mida ya mchana saa 7.
Ilipofika mida ya saa 10,kuna mwanamke alitoka kwenye kile kijumba huku akijinyoosha kana kwamba alikuwa amechoka sana!.Alianza kuwazungukiwa watu kadhaa waliokuwa pale nje huku akiongea nao kisukuma na kiswahili!.Alipofika kwetu alitusalimia kisukuma na kama kawaida nami nilimuitikia kisukuma,sasa Mtatiro halikuwa haelewi kabisa hata salamu ndipo nilimwambia yule mama ya kwamba mwenzangu haelewi kisukuma,aliamua kumsalimu kiswahili kisha akaendelea na watu wengine!.Yule mama ndiye aliyekuwa mwenyeji wetu na alikuwa mganga!.
Mtatiro "Mwanangu kisukuma kumbe unakipiga fresh"
Mimi "Nimekaa nao,dingi yangu mdogo alikuwa headmaster shule moja huko Tabora hivyo nilikinyaka kiasi fulani"
Ilipofika mida ya saa 12 jioni kuna watu takribani 7 ambao walikuwa wanaume 3 na wanawake 4 waliingia pale nyumbani huku wakiwa wamebeba majembe,mimi nilidhani ni ndugu tu wanaoishi hapo kumbe walikuwa wateja wa huyo mama.Sasa utaratibu ulikuwa ni kwamba,unapofika kwa huyo mama unapewa namba kama sisi tulivyopewa,wakati ukiendelea kusubiri ili namba yako iitwe ilipaswa kila kunapokucha ukamate jembe umfuate mwenyeji akakuelekeze shamba la kulima na ulikuwa unapewa kipande chako ili upambane nacho,na kipande chenyewe hakikuwa cha kitoto,yaani kama ukimaliza kile kipande ndipo unaambiwa sasa umekolifai kupatiwa matibabu na yule mama.Sasa wakati unasubiri matibabu ndipo mnaitwa kwa namba ambazo hata sisi tulipewa.(Yule mganga alikuwa mjanja sana,badala ya kulima mashamba yake,sisi wapumbavu ambao tulifahamika kama wateja wake ndio tuliomlimia wakati yeye akiwa ametulia nyumbani,Daaah![emoji23][emoji23],na kila mtu aliyefika hapo kwake ni lazima ilikuwa akamatishwe jembe aingie shambani![emoji23][emoji23]).
Mimi na Matatiro tulikomaa na vipande vyetu ambavyo tulivianza siku iliyofuata kwasababu siku tuliyofika tulikuwa tumechelewa,bahati nzuri ilikuwa ni palizi na hakukuwa na nyasi sana!.Siku hiyo tulipomaliza kupalilia lile shamba ilikuwa mida ya saa 9 alasiri,tuliporudi hapo nyumbani kiukweli tulikuwa tumechafuka miguu na kunuka majasho hatari,sasa nilimfuata yule mama aliyetupokea siku ile nikawa nimemwambia atupatie maji ili tuoge,alituambia inapaswa tuwasubiri wenzetu ambao nao walikuwa hawajamaliza sehemu zao ili tupate chakula kwa pamoja kisha ndio tuoge!.
Wale walipotoka huko shambani,tulitengewa ugali wa udaga kwa na furu wa kuchemsha.Sasa tulipaswa kukaa watu watatu watatu kwa ajili ya chakula,mimi nilikaa na Mtatiro kama kawaida pamoja na jamaa mmoja ambaye alikuwa mteja kama sisi!.Siku hiyo ikapita kapa bila kuitwa namba lakini kuna watu wao waliitwa wakaendelea kupewa huduma kama kawaida!.
Siku iliyofuata tukaitwa majina watu kama wanne,sasa kwakuwa mimi na Mtatiro tulikuwa na shida moja ilibidi tuambiwe tusubiri kwanza amalizane na wale wa wawili.Zamu yetu ilifika na tukaitwa ndani kwa yule mama,hatukujieleza hata kidogo bali tulipoingia ndani alitutaka tuvue shati ili kitendo cha kupigwa chale kuchukue nafasi!.
Yule mama alitupiga chale kwa kutumia kisu kilichokuwa kikali kama wembe,alituchanja kila sehemu aliyoona yeye inafaa,baada ya hapo alituchanja pia kwenye ulimi kila mtu!.Alipomaliza kutuchanja na kutupaka dawa,alichukua kitu kilichokuwa kimefungwa na kukazwa sana na kutakiwa kila mmoja akivae kiunoni,ile alituambia ni irizi na asije akatokea mtu akaivua,alisema endapo ikitokea ukaivua basi usije ukamlaumu!.
Mpaka wakati huo hatukufahamu kwa huyo mganga tulipelekwa kufanya nini,ingawa tuliambiwa tunakwenda kutengenezwa ili hatukujua utengenezwaji ulikuwa na faida gani katika ile kazi yetu mpya ambayo tungeianza siku chache zilizokuwa mbele yetu!.
Yule mama alituambia ya kwamba,ile irizi haikupaswa kabisa kutolewa kiunoni hata iweje. Basi baada ya kumaliza ile shughuli tulitoka nje tukaendelea kumsubiri jamaa aliyetuambia angekuja kutuchukua!.Ile siku jamaa hakutokea kabisa,hivyo ikatubidi tulale tena kwa yule mama.
Yale mazingira yalikuwa ya hovyo sana lakini ilibidi tukubaliane na hali kwasababu tuliitamani pesa!.Ilipofika mida ya saa 5 asubuhi ya siku iliyofuata yule jamaa alirudi kutuchukua na kisha tukaondoka,sasa tulipoingia kwenye ile Noah tulikuta kuna mabegi kadhaa na kulikuwa na jamaa mmoja akiwa amekaa siti za abiria,dereva alikuwa ni yuleyule demu ambaye alikuwaga azungumzi na mtu!.
Jamaa "Wanangu safari ni moja kwa moja Arusha"
Mtatiro "Kaka mngeturudisha kwanza tukachukue nguo"
Jamaa "Nguo sio sehemu ya kuwazia,utazikuta huko"
Hatukuwa na swali,tuliamua kukausha na safari kuanza.Tulitembea sana na hatimaye tukaikamata lami kuelekea Musoma,baada ya kuivuka lamadi kwa mbele,tukaikamata geti la Ndabaka linaloingia Serengeti.
Ha ha haUmenikumbusha mjomba aliwahi kusema nilikua nimepanda bunda naenda punda"
Labda akauzie watu watamthilia lakini hawa wa humu hivyo vitabu vyenyewe unavyosema kuna wana jf walitoa mie hata sijawahi kuviona hivyo vitabuNdugu mwandishi tafadhali usiwasikilize hao wanaokujaza upepo eti ukatoe kitabu utapata pesa. Mkuu hao ni watanzanua na watanzania na kusoma vitabu ni vitu tofauti kabiiiisa, mtu anaweza kua anapenda kusoma kitabu ila kutoa 15K anunue kutabu hawezi.
Kuna mtu humu alileta stori ya uchawi mwaka jana ikapendwa wakamjaza atoe kitabu jamaa kweli akatoa kitabu. Waulize ni wangapi wenye kitabu chake, sio huyo tu kuna The Bold alitoa kitabu sidhani kuna mwana jf alinunua na walikua wanamjaza kweli huko jf intelligence.
Hear, hear.
Kama umeamua kutuburudisha kwa kushea uliyopitia endelea kufahya hivyo. Ila kama unaplan za kutoa kitabu hakikisha iwe imetoka ndani mwako na sio kwa kushawishiwa na hawa wanaosoma hapa ukitegemea eti watakuunga mkono kwa kununua.
Keep ya Head Up Hawa ni watanzania tena wa JF [emoji124]
View attachment 2403735
Unaroho nguvu wewe kama wabeba mawe!Hatujamlazimisha, wala kumuomba
Mkuu unamsalimu nani?
dickhead[emoji23][emoji23]Hajakutwa na kitu.
He had other options.
Read and go about his business.
Read and applaud the writer for his time.
Be a dickhead. Unfortunately he opted for this. [emoji2960][emoji2960]
Pole sana kwa msibaWakuu habari za leo?
Bila shaka nyie ni wazima kabisa ndugu zangu,poleni sana,Aisee nimetoka kidogo nje ya mji nipo mkoani tulileta Msiba,hivyo nisubirieni nikirudi nakuja kuendelea na kumalizia sehemu kidogo iliyobaki!.
Pia niwatoe hofu hakuna mtu yeyote aliyenitisha wala kuzuia eti nisisimulie,hilo wala lisiwape tabu!.
Vilevile nimejaribu kupitia comments za watu nimeona positive na negative opinions,hii ndiyo akili ya mwandamu siku zote,ukipenda tu usifiwe katika maisha basi wewe utakuwa na matatizo ya utindio wa ubongo!,mimi niendelee kuwaomba watu wanaotoa negative comments wala wasitukanwe na kukejeliwa!,acheni nao waji mwaye mwaye kwa kutumia uhuru vizuri wa kutoa maoni!.
Nilisema nia na lengo ni kufundisha watu,wengine haya ndiyo yalikuwa maisha yetu enzi hizo.
Narudia tena kuwaambia ya kwamba mimi kazi yangu ni bodaboda na napatikana bunju,yeyote anayetaka kuonana na mimi kuja kijiweni napo paki bodaboda yangu basi aje pm nimtumie namba anitafute nimuelekeze aje anione tupige stori,sasa mkiendelea kubisha ya kwamba mimi si bodaboda hiyo haisaidii kwasababu utakuwa ni mjinga tu unayetaka kubisha bila sababu ya msingi wakati mimi muhusika nipo bunju tu hapo ambapo unaweza kufika ili ubishi wako uishe!.Kama nilikuwa mpiga debe ni kitu gani kinizuie kuendesha bodaboda?,mimi sichagui kazi wakuu ili mradi iwe halali,sasa hivi sitaki kuiba cha mtu!.
Mimi kuandika vizuri ndiyo ikufanye uamini mimi si bodaboda?.Kupanga ni kuchagua.
Vumililieni narudi mjini kesho kutwa,nikifika naendelea ndugu zangu!.
😂😂 mafanikio ya kuangalia kwa macho ni rahisi sana. Nyuma ya pazia ndiyo unagundua tajiri na pesa zake.Jamaa inaonesha ndo wale watu ambao maisha yao yapo straight yani mtu kasomeshwa shule ya msingi nzuri ,secondary nzuri kafaulu vizuri alilishwa vizuri na wazee ametafutiwa kazi nzuri ila kuna watu wanaraha sana haya maisha kila kitu wamefanyiwa kmmk [emoji16].
Sasa ndo unawakuta wanabisha tu kila kitu wakiambiwa hawaijui dunia wao ni school - chuo - kazini asubuh hadi jioni
Mimi nishapewa Mil1.5 kuna dili ilitakiwa tukamilishe yani ile ilikua kama kishawish tu yani chambo unavutwa moyo uingie mzima mzima kwenye game na hayakuwa malipo yani iyo fanya maandalizi yako ujitengeneze kimazingira ya kazi baada ya wiki nikapewa tena kama laki 4
Nilichokifanya nilikimbia na ile pesa moyo wangu haukuwa tayari kufanya ule mchongo kwaiyo kupewa pesa kabla ya kazi kwa ishu haramu ni kawaida
Ila ndugu zangu aya maisha bora usakwe na polisi unaweza pona ukaishia nyuma ya nondo sio wahuni
Now nipo free nilisha clear tofauti zangu na wahuni[emoji16]
Hujawahi kufiwa wewe, yaani kuwafurahisha wana jf ushindwe kufanya majukumu ya maana embu kuwa muungwana basi hata kidogo usilete utani kwenye msiba wa mwenzioKWANI HUJAENDA NA SIMU, AU UNAANDIKA KUPITIA DESKTOP. KAMA MATERIAL YAKO KICHWANI NA SIMU UNAYO HAPO MSIBANI KWENYE MAJAMVI SI UNAWEZA KUANDIKA TU VIZURI TUKAPATA UHONDO!![emoji16][emoji16]jokes.
Anyway, pole kwa msiba. UMUGHAKA
Eti "lamda" hebu tulia bwanaHiyo ni stori ya kutunga lamda km sio msomaji wa vitabu