Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

kuna malalamiko kuwa wanachama wanasema unawacheleweshea story.. kama vipi kaa chini tunga maliza ndo uje upost kuliko kuwacheleweshea. tutaanza kugombana mimi na wewe. mimi nasimamia sana ustawi wa wasomaji. sipendi wawe na hasira au manung'uniko. kama umeshindwa kazi acha siyo kutaka waanze kukubembeleza. hadithi nyepesi kama hii unashindwaje itunga kwa haraka tu ukamaliza? angalia sana dogo usije sema mimi mbaya hakikisha kila siku unaleta episodes za kutosha.
 
kuna malalamiko kuwa wanachama wanasema unawacheleweshea story.. kama vipi kaa chini tunga maliza ndo uje upost kuliko kuwacheleweshea. tutaanza kugombana mimi na wewe. mimi nasimamia sana ustawi wa wasomaji. sipendi wawe na hasira au manung'uniko. kama umeshindwa kazi acha siyo kutaka waanze kukubembeleza. hadithi nyepesi kama hii unashindwaje itunga kwa haraka tu ukamaliza? angalia sana dogo usije sema mimi mbaya hakikisha kila siku unaleta episodes za kutosha.
Naunga mkono hoja nashangaa sana eti dogo analeta story saa tisa za usku alfu inayofata anaenda kupost saa saba za usku nin sasa hyo si bora akaushe tu apate muda wa kutosha ashushe episod za kutosha na siyo hbr za kuleta story saa tisa za usku ujinga huu sana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
kuna malalamiko kuwa wanachama wanasema unawacheleweshea story.. kama vipi kaa chini tunga maliza ndo uje upost kuliko kuwacheleweshea. tutaanza kugombana mimi na wewe. mimi nasimamia sana ustawi wa wasomaji. sipendi wawe na hasira au manung'uniko. kama umeshindwa kazi acha siyo kutaka waanze kukubembeleza. hadithi nyepesi kama hii unashindwaje itunga kwa haraka tu ukamaliza? angalia sana dogo usije sema mimi mbaya hakikisha kila siku unaleta episodes za kutosha.

[emoji23][emoji23][emoji23] tunga yako ww
 
Sehemu ya Nane:

Macho ya Zai yalikuwa yanasema jambo.

Jambo lililonitisha.

Si bure alikuwa anafahamu kitu na kitu hicho kilinifanya nitetemeke kwa hofu. Nilitaka kuendelea kuwapo hapo ili anieleze ni nini anajua lakini sababu ya muda nililazimika kuondoka, labda nirejee tena muda mwingine.

Kama si yule mwalimu mkuu kunikawiza kule shuleni, huenda siku ile ningeyasikia yote toka kwenye kinywa cha Zai.

Niliondoka zangu lakini kichwa nilikiacha palepale hospitali kwa mawazo, kweli sikwenda nacho, kuanzia kwenye daladala mpaka nyumbani kwangu nilikuwa nikiyatafakari yale nilosikia, hata chakula sikuhisi ladha yake.

Nilifungua simu yangu nikampigia Anwari, kwasababu nilikuwa nimemblock, ilibidi nimu-unblock kwanza kisha ndo' nifanye zoezi langu, kidogo simu kuita bwana yule akapokea, hakujua kama ni mimi maana namba ilikuwa ngeni lakini aliponisikiliza nilipotamka maneno mawili aliita; "Magreth!"

Sikumwitikia, nilimuuliza moja kwa moja ni nini amemwambia Zai, hapo akakwama kusema, hakutaka kujibu, badala yake aliniomba tuonane mahali ili tupate kuyajenga. Muda na siku nipange mimi mwenyewe.

Aliniambia,

"Nimekutafuta mno lakini sikufanikiwa, hakukuwa na haja ya kufikia huku, mpenzi."

Hilo neno 'mpenzi' kweli likanikera, sijui kwanini lakini lilininiga koo, ujumbe huo nikaufuta papo hapo nisipate kuuona tena. Baada ya hapo niliendelea na maandalizi yangu binafsi, kuandaa chakula cha nyumbani na kufanya kazi zingine ndogondogo, lakini niwe mkweli, hamna nilichofanya nikafanya vema, kuna muda nilihisi mikono yangu inatetemeka kwa kuwaza dhambi nilofanya.

Dhambi nilofanya na Anwari.

Vipi yale ya gizani yakaja mbele ya mwanga tele? Nitachimbia wapi uso wangu kujificha nisishikwe na haya hii? Wapi nitakatiza nisigeuke kuwa mada?

Hilo lilininyima raha.

Baadae mume wangu alirejea nyumbani, mapema ya saa tatu, na siku hiyo alirejea pamoja na vitu tele, vitu vya nyumbani na zawadi zangu binafsi.

Nakumbuka aliniletea chupa kadhaa za marashi ya ghali, viatu bila kusahau magauni, hakumsahau mtoto, naye alimletea nguo kadha wa kadha akijigamba na kujivunia ya kwamba mtoto yule ni 'jembe' lake.

Siku hiyo bwana alikuwa na furaha sana, alitabasamu kila mara, akacheka na kunikumbatia, ni baadae ndo' akanieleza ya kwamba kule kazini amepandishwa nafasi, sasa hatokuwa anaendesha tena watu huku na kule bali atakaa ofisini kuwasimamia madereva wenzake.

Madereva hao sasa watamwita 'boss' naye atawaita vijakazi. Maisha yamebadilika.

Basi siku ile tukala na kunywa vema, tulifanya hivyo kuyasheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, kila mmoja wetu alijumuika mezani ikiwamo kijana wetu, Amiri, mimi kazi yangu ikawa kuigiza furaha nisokuwa nayo, kukenua meno na kujichekesha huku ndani yangu nawaza mambo mengine.

Nawaza furaha ya yule bwana. Nawaza furaha ya familia yetu. Furaha ambayo ndo' kwanza ilikuwa inachipukia baada ya mapito kadhaa.

Bwana Mgaya alifungua chupa kadhaa za ulabu, chupa alizokuja nazo na zingine zilizokuwamo katika jokofu, akanywa kwa kujipongeza.

Alipiga mafundo kadha wa kadha akisindikizia michapo ya hapa na pale, baada ya muda pombe ikaanza kumpangia cha kusema na kumwongoza namna ya kutenda, akaanza kusema namna gani anavyonipenda, namna gani atakavyonipambania.

Aliyasema mambo lukuki lakini pombe haikumpa akayamaliza, punde akapitiwa na usingizi mzito. Alijilaza kwenye kochi akiwa hana hili wala lile.

Hapo Amiri alinisogelea akaniuliza kwa sauti ya chini, "uko sawa kweli?"

Nikamtazama, kisha nikamtazama mume wangu alokuwa amelala kama mbwa alochoka pale kwenye kochi, hamna habari alonayo, nikamrejea kijana Amiri na kumuuliza kunani akaniuliza hivyo?

Amiri akasema sina furaha, ni kweli sikuwa nayo lakini alitambuaje? Siku ile sikulia na nilijitahidi kadiri ninavyoweza kuigiza furaha usoni mwangu mbele ya mume wangu, yeye katambuaje?

Wakati nikijiuliza hayo kichwani, aliniongezea swali jinginewe, "kitu gani kinakusumbua au umemkumbuka mama mkwe wako?"

Nikamshukuru kwa kujali lakini nikamsisitiza hamna jambo lolote lile, tule na tunywe kusheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, tusiharibu tafrija yetu kwa kuleta mawazo hasi yasokuwa na faida.

Basi baada ya muda kidogo, Amiri akaniaga na kwenda zake nje, alinambia anaenda kukagua na kutazama mifugo kabla hajaenda kulala, alipotoka nikabaki mwenyewe sebuleni kama mtu mwenye ufahamu, nilimalizia kinywaji changu nikamsindikiza bwana Mgaya kwenda chumbani kupumzika.

Nilipomlaza nikaanza kujishughulikia mwenyewe mahususi kwaajili ya kulala maana asubuhi nahitajika kudamka mapema na jua.

Jambo la kwanza nilofanya nilitoa pedi yangu nilovaa tangu mchana, nilikuwa kwenye siku zangu siku hiyo nikianzia tokea majuzi yake, nikaiweka pedi hiyo pembeni kisha nikaoga na nilipomaliza nikaichukua kwenda kuihifadhi kwenye 'bin' maalum tunapowekea taka.

'Bin' hiyo ilikuwa nje ya nyumba kwenye kibaraza cha mlango wa nyuma.

Nikiwa na taulo langu kifuani, nilielekea huko na nikafanya kile kilichonipeleka, lakini kabla sijafunga mfuniko wa ndoo ile maalum ya taka, niligundua jambo fulani lililonichukulia muda wangu.

Kwa mara ya kwanza kutazama, sikuamini, lakini nilivyopepesa macho kukagua nilihakikisha nilichokiona kilikuwa sahihi.

Pedi zangu za nyuma, takribani tatu kwa idadi, hazikuwamo mule ndani! Sikujua zimeenda wapi na nani kazichukua.

Nikiwa hapo, bado nabung'aa, mara nikasikia sauti za kuku kule bandani, kuku walipiga kelele kana kamba wamekurupushwa na kitu fulani, nikapaza sauti kuita;

"Amirii!"

Kimya.

"Amiri ... ni wewe?"

Sikujibiwa.

Kuku wakapiga tena kelele, kwaaakwakwakwaaa! Moyo wangu ukalipuka na wasiwasi, niliwaza pengine kuna mnyama ama mdudu hatarishi ameingia kwenye banda la kuku, nikasogea taratibu nikiendelea kuita Amiri Amiri, ni wewe uko bandani?

Nilisogea mpaka kwenye uzio wa mabanda, nikasimama na kutazama, nilitamani kuingia humo ndani lakini niliogopa sababu ya kiza, kule mabandani hapakuwa na taa, mtu angeingia kwanza ndani kisha ndo' aichukue kurunzi iliyokuwa inang'ining'inia kwenye kuta ya ng'ombe kwaajili ya kujipatia mwanga.

Mimi hata kuingia humo sikutaka kabisa.

Nilisimama nikisikia kelele za kuku pasipo kuwa na msaada, sauti hizo hazikudumu muda mrefu kukawa shwari, hapo ndipo mimi nikarejea ndani kwaajili ya kupumzika.

Mpaka naingia ndani ya chumba changu sikupata kumwona kijana Amiri. Nilijiaminisha labda alisharejea chumbani kwake na sasa ameupumzisha mwili wake kitandani. Kitu kilichonifanya nikaamini hivyo ni ule mlango wa grill.

Niliufunga mlango huo na hakuna aliyeugusa mpaka asubuhi nilipoamka.

Kesho yake baada ya kumaliza majukumu yangu kazini, niliwasiliana na Anwari nikimtaka tuonane pahali fulani.

Kwasababu ya kujiweka salama, nilimuelekeza aje mgahawa mmoja hivi ambao haukuwa mbali sana na shule ninapofanyia kazi, faida yake haitanichukua muda mrefu kumpitia mwanangu niliyemuacha shule, nikimaliza tu maongezi basi dakika chache tunajiondokea kwenda zetu nyumbani.

Kweli, ndani ya muda mfupi, Anwari aliwasili kama vile tulivyowekeana miadi.

Bwana huyo alikuja hapo na gari yake akanipendekeza tuongelee mambo yetu ndani ya gari badala ya pale mgahawani, hoja yake mule ndani ya gari ni salama zaidi kuliko mbele ya macho ya watu, mimi pia nikaona wazo hilo ni jema basi nikaliheshimu.

Niliingia kwenye gari maongezi yetu yakaanza kwa mimi kuuliza maswali mengi yenye pupa na hasira, maswali juu ya makubaliano yetu tuloweka, makubaliano ya siri, nikauliza makubaliano hayo yamefikaje kwenye masikio ya Zai?

Naye akaniuliza, "ulitaka mimi nifanye nini kama sikupati kwa kila njia? Namba yako haiiti, unapofanyia kazi sipafahamu, ningefanyaje?"

Kweli lengo langu lilikuwa ni kumpoteza bwana huyu katika ramani ya maisha yangu, na niliyapanga hayo pasipo kumshirikisha mtu yeyote yule kwani Anwari kwangu nilimrejea kwaajili ya jambo moja tu, kunisaidia pale nilipokuwa nimekwama, kwahiyo baada ya kupata msaada huo kwangu hakubaki na tija tena, nilitamani nifute kurasa yake lakini nafuta nini?

Naufutaje?

Na hapo nilipokuwa namsikiliza ndo' nikaamini kabisa kuwa kipande cha Anwari hakikuwa ukurasa mmoja bali ni kitabu kizima!

"Lakini Anwari," nilisema naye kwa mkazo, "ni nani aliyekwambia mimi nina mtoto? Na ni nani aliyekwambia kuwa mtoto yule ni wako? Au umekaa tu ukaanza kuyatengeneza maghorofa yako kichwani?"

Niliuliza huku nafsi yangu ikinisuta maana nilijua kabisa najidanganya mwenyewe. Ukweli ndani yangu unanizodoa. Ukweli ambao hapa najitahidi kuuficha kwa nyavu nikiamini hautaonekana mbele za watu.

Miaka miwili na miezi kadhaa nyuma, mimi mwenyewe, wala si kwa kusingiziwa wala kusemewa wongo, nilirejea kwenye mlango wa Anwari baada ya kushindwa kuhimili presha kuwa kubwa kutoka kwa mama mkwe wangu.

Mama huyo alianza kuninyooshea kidole, miezi michache tu kupita baada ya kufunga ndoa na bwana Mgaya, akisema mimi ni mgumba nisiyeshika mimba.

Mama huyo hakutambua wala hakujali ni namna gani tulijaribu kutafuta mtoto mimi pamoja na mwanaye, nikicheza na kalenda yangu kwa ustadi mkubwa, lakini hatukupata matunda.

Swala hilo likanifanya nihofie kumpoteza mume wangu kwa wanawake wengine, wanawake wenye mayai yao, punde watakapomfanikishia kumpa mtoto basi kwangu itakuwa ndo' kwaheri ya kuonana.

Lakini baadae nilikuja kupata shaka, vipi kama mwanaume yule ndo' mwenye matatizo na si mimi kama ninavyojiwazia?

Vipi kama bwana Mgaya hana uwezo wa kunipa ujauzito?

Kwa kipindi hiko nilikuwa na shakashaka, lakini baadae bwana Mgaya alivyokuja kusema kuhusu mwanamke yule wa kijijini, Momo, ya kwamba amemuacha hana mimba wala mtoto wake, nikazidi kuthibitisha kichwani mwangu kuwa bwana yule alikuwa na shida bayana kwenye via vyake vya uzazi.

Basi kwasababu ya ile kiu ya mtoto na hivi muda huo sikuwa na uhakika na utimamu wangu wala wa utimamu wa bwana Mgaya, ndipo nikakutana na Anwari katika siku zangu za hatari.

Nilishiriki tendo na bwana huyo mara moja tu ikatosha kabisa kubadilisha wiki yangu ilofuata kwani nilianza kuhisi mwili wangu haupo kawaida na vile nilivyouzoea.

Baada ya juma la pili nilipima na kuhakikisha nina ujauzito, hapo ndo' nikaona ni muda muafaka sasa wa kumpoteza Anwari katika maisha yangu kwa kum-block kila kona, kila mtu aendelee na njia yake .

Lakini sasa ni wazi nishafeli. Anwari niko naye hapa kwenye gari akinieleza mambo ya mtoto, hata akipata kauli kama mimi na yeye hatupo kwenye mahusiano basi haina shida kabisa, yeye anamtaka tu mtoto wake.

Ati mtoto wake?

Hahahaha Anwari ....

Mtoto gani?


****
 
Sehemu ya Nane:

Macho ya Zai yalikuwa yanasema jambo.

Jambo lililonitisha.

Si bure alikuwa anafahamu kitu na kitu hicho kilinifanya nitetemeke kwa hofu. Nilitaka kuendelea kuwapo hapo ili anieleze ni nini anajua lakini sababu ya muda nililazimika kuondoka, labda nirejee tena muda mwingine.

Kama si yule mwalimu mkuu kunikawiza kule shuleni, huenda siku ile ningeyasikia yote toka kwenye kinywa cha Zai.

Niliondoka zangu lakini kichwa nilikiacha palepale hospitali kwa mawazo, kweli sikwenda nacho, kuanzia kwenye daladala mpaka nyumbani kwangu nilikuwa nikiyatafakari yale nilosikia, hata chakula sikuhisi ladha yake.

Nilifungua simu yangu nikampigia Anwari, kwasababu nilikuwa nimemblock, ilibidi nimu-unblock kwanza kisha ndo' nifanye zoezi langu, kidogo simu kuita bwana yule akapokea, hakujua kama ni mimi maana namba ilikuwa ngeni lakini aliponisikiliza nilipotamka maneno mawili aliita; "Magreth!"

Sikumwitikia, nilimuuliza moja kwa moja ni nini amemwambia Zai, hapo akakwama kusema, hakutaka kujibu, badala yake aliniomba tuonane mahali ili tupate kuyajenga. Muda na siku nipange mimi mwenyewe.

Aliniambia,

"Nimekutafuta mno lakini sikufanikiwa, hakukuwa na haja ya kufikia huku, mpenzi."

Hilo neno 'mpenzi' kweli likanikera, sijui kwanini lakini lilininiga koo, ujumbe huo nikaufuta papo hapo nisipate kuuona tena. Baada ya hapo niliendelea na maandalizi yangu binafsi, kuandaa chakula cha nyumbani na kufanya kazi zingine ndogondogo, lakini niwe mkweli, hamna nilichofanya nikafanya vema, kuna muda nilihisi mikono yangu inatetemeka kwa kuwaza dhambi nilofanya.

Dhambi nilofanya na Anwari.

Vipi yale ya gizani yakaja mbele ya mwanga tele? Nitachimbia wapi uso wangu kujificha nisishikwe na haya hii? Wapi nitakatiza nisigeuke kuwa mada?

Hilo lilininyima raha.

Baadae mume wangu alirejea nyumbani, mapema ya saa tatu, na siku hiyo alirejea pamoja na vitu tele, vitu vya nyumbani na zawadi zangu binafsi.

Nakumbuka aliniletea chupa kadhaa za marashi ya ghali, viatu bila kusahau magauni, hakumsahau mtoto, naye alimletea nguo kadha wa kadha akijigamba na kujivunia ya kwamba mtoto yule ni 'jembe' lake.

Siku hiyo bwana alikuwa na furaha sana, alitabasamu kila mara, akacheka na kunikumbatia, ni baadae ndo' akanieleza ya kwamba kule kazini amepandishwa nafasi, sasa hatokuwa anaendesha tena watu huku na kule bali atakaa ofisini kuwasimamia madereva wenzake.

Madereva hao sasa watamwita 'boss' naye atawaita vijakazi. Maisha yamebadilika.

Basi siku ile tukala na kunywa vema, tulifanya hivyo kuyasheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, kila mmoja wetu alijumuika mezani ikiwamo kijana wetu, Amiri, mimi kazi yangu ikawa kuigiza furaha nisokuwa nayo, kukenua meno na kujichekesha huku ndani yangu nawaza mambo mengine.

Nawaza furaha ya yule bwana. Nawaza furaha ya familia yetu. Furaha ambayo ndo' kwanza ilikuwa inachipukia baada ya mapito kadhaa.

Bwana Mgaya alifungua chupa kadhaa za ulabu, chupa alizokuja nazo na zingine zilizokuwamo katika jokofu, akanywa kwa kujipongeza.

Alipiga mafundo kadha wa kadha akisindikizia michapo ya hapa na pale, baada ya muda pombe ikaanza kumpangia cha kusema na kumwongoza namna ya kutenda, akaanza kusema namna gani anavyonipenda, namna gani atakavyonipambania.

Aliyasema mambo lukuki lakini pombe haikumpa akayamaliza, punde akapitiwa na usingizi mzito. Alijilaza kwenye kochi akiwa hana hili wala lile.

Hapo Amiri alinisogelea akaniuliza kwa sauti ya chini, "uko sawa kweli?"

Nikamtazama, kisha nikamtazama mume wangu alokuwa amelala kama mbwa alochoka pale kwenye kochi, hamna habari alonayo, nikamrejea kijana Amiri na kumuuliza kunani akaniuliza hivyo?

Amiri akasema sina furaha, ni kweli sikuwa nayo lakini alitambuaje? Siku ile sikulia na nilijitahidi kadiri ninavyoweza kuigiza furaha usoni mwangu mbele ya mume wangu, yeye katambuaje?

Wakati nikijiuliza hayo kichwani, aliniongezea swali jinginewe, "kitu gani kinakusumbua au umemkumbuka mama mkwe wako?"

Nikamshukuru kwa kujali lakini nikamsisitiza hamna jambo lolote lile, tule na tunywe kusheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, tusiharibu tafrija yetu kwa kuleta mawazo hasi yasokuwa na faida.

Basi baada ya muda kidogo, Amiri akaniaga na kwenda zake nje, alinambia anaenda kukagua na kutazama mifugo kabla hajaenda kulala, alipotoka nikabaki mwenyewe sebuleni kama mtu mwenye ufahamu, nilimalizia kinywaji changu nikamsindikiza bwana Mgaya kwenda chumbani kupumzika.

Nilipomlaza nikaanza kujishughulikia mwenyewe mahususi kwaajili ya kulala maana asubuhi nahitajika kudamka mapema na jua.

Jambo la kwanza nilofanya nilitoa pedi yangu nilovaa tangu mchana, nilikuwa kwenye siku zangu siku hiyo nikianzia tokea majuzi yake, nikaiweka pedi hiyo pembeni kisha nikaoga na nilipomaliza nikaichukua kwenda kuihifadhi kwenye 'bin' maalum tunapowekea taka.

'Bin' hiyo ilikuwa nje ya nyumba kwenye kibaraza cha mlango wa nyuma.

Nikiwa na taulo langu kifuani, nilielekea huko na nikafanya kile kilichonipeleka, lakini kabla sijafunga mfuniko wa ndoo ile maalum ya taka, niligundua jambo fulani lililonichukulia muda wangu.

Kwa mara ya kwanza kutazama, sikuamini, lakini nilivyopepesa macho kukagua nilihakikisha nilichokiona kilikuwa sahihi.

Pedi zangu za nyuma, takribani tatu kwa idadi, hazikuwamo mule ndani! Sikujua zimeenda wapi na nani kazichukua.

Nikiwa hapo, bado nabung'aa, mara nikasikia sauti za kuku kule bandani, kuku walipiga kelele kana kamba wamekurupushwa na kitu fulani, nikapaza sauti kuita;

"Amirii!"

Kimya.

"Amiri ... ni wewe?"

Sikujibiwa.

Kuku wakapiga tena kelele, kwaaakwakwakwaaa! Moyo wangu ukalipuka na wasiwasi, niliwaza pengine kuna mnyama ama mdudu hatarishi ameingia kwenye banda la kuku, nikasogea taratibu nikiendelea kuita Amiri Amiri, ni wewe uko bandani?

Nilisogea mpaka kwenye uzio wa mabanda, nikasimama na kutazama, nilitamani kuingia humo ndani lakini niliogopa sababu ya kiza, kule mabandani hapakuwa na taa, mtu angeingia kwanza ndani kisha ndo' aichukue kurunzi iliyokuwa inang'ining'inia kwenye kuta ya ng'ombe kwaajili ya kujipatia mwanga.

Mimi hata kuingia humo sikutaka kabisa.

Nilisimama nikisikia kelele za kuku pasipo kuwa na msaada, sauti hizo hazikudumu muda mrefu kukawa shwari, hapo ndipo mimi nikarejea ndani kwaajili ya kupumzika.

Mpaka naingia ndani ya chumba changu sikupata kumwona kijana Amiri. Nilijiaminisha labda alisharejea chumbani kwake na sasa ameupumzisha mwili wake kitandani. Kitu kilichonifanya nikaamini hivyo ni ule mlango wa grill.

Niliufunga mlango huo na hakuna aliyeugusa mpaka asubuhi nilipoamka.

Kesho yake baada ya kumaliza majukumu yangu kazini, niliwasiliana na Anwari nikimtaka tuonane pahali fulani.

Kwasababu ya kujiweka salama, nilimuelekeza aje mgahawa mmoja hivi ambao haukuwa mbali sana na shule ninapofanyia kazi, faida yake haitanichukua muda mrefu kumpitia mwanangu niliyemuacha shule, nikimaliza tu maongezi basi dakika chache tunajiondokea kwenda zetu nyumbani.

Kweli, ndani ya muda mfupi, Anwari aliwasili kama vile tulivyowekeana miadi.

Bwana huyo alikuja hapo na gari yake akanipendekeza tuongelee mambo yetu ndani ya gari badala ya pale mgahawani, hoja yake mule ndani ya gari ni salama zaidi kuliko mbele ya macho ya watu, mimi pia nikaona wazo hilo ni jema basi nikaliheshimu.

Niliingia kwenye gari maongezi yetu yakaanza kwa mimi kuuliza maswali mengi yenye pupa na hasira, maswali juu ya makubaliano yetu tuloweka, makubaliano ya siri, nikauliza makubaliano hayo yamefikaje kwenye masikio ya Zai?

Naye akaniuliza, "ulitaka mimi nifanye nini kama sikupati kwa kila njia? Namba yako haiiti, unapofanyia kazi sipafahamu, ningefanyaje?"

Kweli lengo langu lilikuwa ni kumpoteza bwana huyu katika ramani ya maisha yangu, na niliyapanga hayo pasipo kumshirikisha mtu yeyote yule kwani Anwari kwangu nilimrejea kwaajili ya jambo moja tu, kunisaidia pale nilipokuwa nimekwama, kwahiyo baada ya kupata msaada huo kwangu hakubaki na tija tena, nilitamani nifute kurasa yake lakini nafuta nini?

Naufutaje?

Na hapo nilipokuwa namsikiliza ndo' nikaamini kabisa kuwa kipande cha Anwari hakikuwa ukurasa mmoja bali ni kitabu kizima!

"Lakini Anwari," nilisema naye kwa mkazo, "ni nani aliyekwambia mimi nina mtoto? Na ni nani aliyekwambia kuwa mtoto yule ni wako? Au umekaa tu ukaanza kuyatengeneza maghorofa yako kichwani?"

Niliuliza huku nafsi yangu ikinisuta maana nilijua kabisa najidanganya mwenyewe. Ukweli ndani yangu unanizodoa. Ukweli ambao hapa najitahidi kuuficha kwa nyavu nikiamini hautaonekana mbele za watu.

Miaka miwili na miezi kadhaa nyuma, mimi mwenyewe, wala si kwa kusingiziwa wala kusemewa wongo, nilirejea kwenye mlango wa Anwari baada ya kushindwa kuhimili presha kuwa kubwa kutoka kwa mama mkwe wangu.

Mama huyo alianza kuninyooshea kidole, miezi michache tu kupita baada ya kufunga ndoa na bwana Mgaya, akisema mimi ni mgumba nisiyeshika mimba.

Mama huyo hakutambua wala hakujali ni namna gani tulijaribu kutafuta mtoto mimi pamoja na mwanaye, nikicheza na kalenda yangu kwa ustadi mkubwa, lakini hatukupata matunda.

Swala hilo likanifanya nihofie kumpoteza mume wangu kwa wanawake wengine, wanawake wenye mayai yao, punde watakapomfanikishia kumpa mtoto basi kwangu itakuwa ndo' kwaheri ya kuonana.

Lakini baadae nilikuja kupata shaka, vipi kama mwanaume yule ndo' mwenye matatizo na si mimi kama ninavyojiwazia?

Vipi kama bwana Mgaya hana uwezo wa kunipa ujauzito?

Kwa kipindi hiko nilikuwa na shakashaka, lakini baadae bwana Mgaya alivyokuja kusema kuhusu mwanamke yule wa kijijini, Momo, ya kwamba amemuacha hana mimba wala mtoto wake, nikazidi kuthibitisha kichwani mwangu kuwa bwana yule alikuwa na shida bayana kwenye via vyake vya uzazi.

Basi kwasababu ya ile kiu ya mtoto na hivi muda huo sikuwa na uhakika na utimamu wangu wala wa utimamu wa bwana Mgaya, ndipo nikakutana na Anwari katika siku zangu za hatari.

Nilishiriki tendo na bwana huyo mara moja tu ikatosha kabisa kubadilisha wiki yangu ilofuata kwani nilianza kuhisi mwili wangu haupo kawaida na vile nilivyouzoea.

Baada ya juma la pili nilipima na kuhakikisha nina ujauzito, hapo ndo' nikaona ni muda muafaka sasa wa kumpoteza Anwari katika maisha yangu kwa kum-block kila kona, kila mtu aendelee na njia yake .

Lakini sasa ni wazi nishafeli. Anwari niko naye hapa kwenye gari akinieleza mambo ya mtoto, hata akipata kauli ati kama mimi na yeye hatupo kwenye mahusiano basi haina shida kabisa, yeye anamtaka tu mtoto wake.

Ati mtoto wake?

Hahahaha Anwari ....

Mtoto gani?


****
Antonnia Kalpana Numbisa Angel Nylon Depal Watu8 Shunie
 
Back
Top Bottom