Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kasema alikesha kwenye usafiri ngoja tuwe na subra AntonniaKumbe Stiv ni yanga bana eti Ndiomana jana hajatupia Hahah!!
Ngoja tusubirie leo tuone!
Iwe mapema basi, sio usiku wa manane mana kesho job...Samahani kwa kutopost jana. Mazingira hayakuwa rafiki kabisa maana nilishinda kwenye usafiri njiani. Leo tunaendelea.
.....[emoji419]Sehemu ya Sita:
Lakini ilikuaje?
Siku hiyo mama mkwe alokuja, sikupata kuzungumza jambo na wala sikutaka, hata pale bwana Mgaya aliponisogelea kwaajili ya swala hilo nilimkwepa kwa kumwambia sipo katika hali ya maongezi, aniache kwa muda.
Siku hiyo nilikaa kwa kujitenga, mara nyingi huwa nafanya hivyo nikiwa na msongo wa mawazo, najitenga ili nipate kuyatafakari yanayonisibu pasipo usumbufu hivyo badala ya kukaa ndani mimi nilienda kuketi huko nje baada ya mtoto kulala, lakini huko badala ya kutafakari, ajabu, nikawa najikuta nabubujikwa na machozi, nilijutia sana maamuzi yangu ya kipumbavu, maamuzi ya kuolewa na yule bwana.
Yalikuwa ni maamuzi ya kukurupuka ambayo sasa yananigharimu.
Ingali nikiwa hapo, nawaza na kumwagilia ardhi kwa machozi yangu, nyakati ni kama saa nne hivi ya usiku, mara nikasikia sauti ya kishindo cha mtu, mtu anayetembea, kuangaza nikamwona Amiri akiwa anatokea kule bandani.
Kijana huyo alikuwa amevalia suruali aloikunja mpaka magotini, miguu yake imejawa na matope, chini yu pekupeku.
Alinifuata moja kwa moja pale nilipokuwapo akanisalimu, nikamjibu pasipo kumtazama, sikutaka ajue nasumbuliwa na uchungu ndani yangu, lakini ajabu kijana yule alinipa pole kwa yanayonisibu, hapo nikalazimika kumwangalia usoni.
"Pole ya kitu gani?"
Akaniambia aliniona nikiwa nalia tangu akiwa umbali ule wa bandani, ameniona nikifanya hivyo kwa dakika kadhaa na ndo' maana amesogea hapo kunipa pole. Baada ya kunieleza hayo, aliniuliza kama anaweza akafanya chochote kunisaidia, mimi nikamwambia hapana, ni mambo binafsi tu, nitayamaliza kwa mikono yangu mwenyewe.
Akaniuliza, "kwa mikono yako mwenyewe?"
Sikuelewa anamaanisha nini na swali hilo ila mimi nikamjibu ndivyo, nitayamaliza kwa mikono yangu mwenyewe, basi akaniaga na kwenda zake, alirudi kule mabandani alipotokea. Sikujua alikuwa anafanya nini huko lakini sikujali, alimradi nilibaki peke yangu basi ilinitosha.
Niliangaza kule mabandani, kwa umbali ule nilokaa sikuweza kuona jambo lolote zaidi ya giza, Amiri alinionaje kama nalia? Nilijiuliza, au upande ule alokuwapo aliweza kuona upande wangu sababu ya mwanga? Yawezekana.
Nilihitimisha hivyo na sikukaa tena hapo nikaondoka kwenda zangu ndani, sebuleni nikamkuta mama yule ameketi anatazama runinga, sikusumbuka naye mimi nikanyoosha zangu niende chumbani, hatua nne akaniita.
Aliniuliza kama chakula chake nimeshamwandalia, nikamjibu ndivyo, kila kitu kipo tayari. Hii ilikuwa ni mara ya pili ananiuliza, mara ya kwanza alifanya hivyo nikiwa natoka kwenda kule nje, nikamwambia kila kitu kipo tayari na pia nikamuuliza kama angependa nimhudumie? Akakataa.
Sasa nilirudia tena kumuuliza, nikuhudumie mama? Napo akakataa, hakusema kitu bali alitikisa tu kichwa chake, basi mimi nikaenda zangu chumbani, huko nikamkuta bwana yule ameegamia kingo ya kitanda, yuko 'busy' na simu yake. Sikutaka kuhangaika naye, nikafanya taratibu ya kwenda bafuni kuoga ili nilale zangu mapema maana kesho kuna kwenda kazini.
Nilipoingia bafuni, sijakolea na kuoga, nikasikia sauti ya mama mkwe ikimuita Mgaya kule sebuleni. Mgaya alifungua zake mlango akaenda huko, baada ya hapo sikusikia kitu tena mpaka nilipokuja kutoka bafuni.
Kule sebuleni kulikuwa na maongezi yanaendelea baina ya mama na mwana, nami sikuyajali sana nikaendelea na mambo yangu, wakati huo najifutafuta maji mwilini, kidogo mlango wa chumbani ukafunguliwa bwana Mgaya akaingia ndani, bwana huyo alikuwa amefura sura yake, alipoingia aliufunga mlango akasimama hapo akiwa ananitazama.
"Bwana vipi?" Nilimuuliza, hapo nikawa nimefungulia rasmi koki ya maneno, bwana huyo akaanza kunimwagia maneno yaso na kifani. Alinisema simjali mama yake, simpatii chakula na wala simuagui. Hakunipa hata muda wa kuongea, aliyasema maneno yote mwenyewe nisibakiziwe hata moja la kutamka.
Nilimsihi basi apunguze sauti ili tusimwamshe mtoto lakini hakujali, hasira ilikuwa imemkaba koo, hakuweza kujimudu, ninachoshukuru mtoto hakuamka hata na yote yale.
Lakini,
Ubaya wangu mimi ulikuwa ni nini? Mbona niliamka mapema kufanya maandalizi yote na hata kumpikia mama yule chakula kinachoendana na hali yake ya ugonjwa? Mbona nilimfuatia na kumtimizia kila alichoniagiza? Sikuelewa.
Wakati mume wangu anaongea hayo, nikasikia sauti ya yule mama, sauti ambayo ilinifanya niwaze hivi kweli mama yule alikuwa anaumwa au lah? Mwanamke yule alipaza sauti akisema ni heri arudi nyumbani akauguzwe na Momo, Momo ni yule mwanamke aliyeolewa na Mgaya kule kwao, kweli kauli hiyo ikanipenya kama mkuki wa moto kifuani mwangu, mdomo wangu haukusema jambo lakini macho yangu yalieleza, ilifikia kipindi nikawa sioni kwa mboni zangu kumezwa na machozi.
Nilijilaza kitandani nisiseme na mtu, baada ya muda mchache nilimezwa na usingizi nisijue hata ni saa ngapi ulinikwapua. Nilizama humo kwenye kiza cha usingizi angalau nipate ahueni ya maisha yangu halisi, ahueni ya yale niliyokuwa nayapitia, lakini napo ilishindikana! Sikupata unafuu wowote ule.
Katikati ya usiku huo,
Niliamka nikamtazama mume wangu, alikuwa anakoroma kama gari moshi, nikamtazama mwanangu pia, naye anamwaga mate kwa utamu wa usingizi, basi taratibu nikaamka kuufuata mlango kwa kunyata, niliufungua mlango huo pasipo kutoa sauti yoyote ile, taratibu sana kama mwizi, niliposhika korido nikajongea kuufuata mlango wa chumba alichokuwamo mama mkwe wangu, hapo pia nikaufungua mlango huo kwa umakini sana, taratibu mno pasipo kutoa sauti kisha nikazamia humo.
Nilitupia macho kitandani, nikamwona mama yule amelala kifudifudi, kwenye dari feni linapepea kwa kasi sana, sauti ya feni hiyo ndo' imemeza chumba kile kizima.
Basi nikajongea na kukwea kitandani kisha nikamkalia mama yule na kumfunika uso wake kwa nyama za mto.
Kufa! Kufa! Kufa!
Alipapatuka kutafuta hewa lakini sikumpatia hiyo nafasi kabisa. Nilitumia nguvu zangu zote nilizonazo kuhakikisha ninammudu na kweli hakunishinda. Mto ulifyonza pumzi yake yote aliyoitoa mapafuni lakini asipate pumzi nyingine ya kuingiza, muda si mwingi mama huyo akakubali kuongozana na kifo, kuongozana nacho kwenda huko kusikojulikana, miguu na mikono yake ilitulia tuli, nikajiaminisha tayari nishamaliza kazi.
Basi nikamtazama uso wake, uso ulomezwa na umauti, moyo wangu ukafurahi, sasa mnongwa huyo alikuwa amekwenda, aende sasa huko aendako akaharibu ndoa za malaika kama zipo, dunia imemshinda ustaarabu.
Nikiwa hapo, natabasamu na huku feni yanipuliza, mara nikakurupuka baada ya kusikia mtu anaufungua mlango, kutazama namwona mume wangu akiwa anaingia bafuni, kiunoni amefunga taulo, kumbe muda wote huo nilikuwa kitandani nikiyaota yalotokea.
Nilikuwa naota? ...
Hapana, hapana!
Nilisema mwenyewe nikijipapasa mwili kama mwehu. Kama kweli ilikuwa ni ndoto mbona mikono yangu, humu mabegani, pananiuma? Sikuelewa. Nilinyanyuka nikaenda kutazama mlango ule wa chumbani, nikauona una upenyo mdogo wa uwazi, mlango haukuwa umefungwa, nikafungua kutazama koridoni, hapana mtu, nikatazama mlango wa chumba alicholala mama mkwe, nao mlango wake nikauona u wazi, tena si kama huu wa kwangu, la hasha, wenyewe ulikuwa umeachama kama behewa.
Upesi nikafunga mlango wangu kisha nikarudi kitandani, sikupata tena usingizi mpaka majira ya saa kumi na moja, majira ambayo ndo' huwa naamka kumwandaa mtoto na mimi pia kwaajili ya kwenda kazini.
Nilimwamsha mtoto nikamwandaa vema kisha nami nikaanza kujishughulikia, muda wote huo bwana Mgaya akiwa amelala hana hili wala lile. Nilipokuwa bafuni naoga akili yangu ikawa inarejelea mambo ya ndoto ile, ndoto niliyoota usiku wa manane.
Niliitafakari hatua kwa hatua nikiyakanda mabega yangu yalokuwa na maumivu kwa mbali, maumivu kana kwamba nilibeba kiroba cha mawe, nikisema na nafsi yangu; maumivu haya nimeyatolea wapi?
Niliitazama mikono yangu, vidoleni kupanda mpaka kwenye viwiko, hakukuwa na kitu, nikaibinua mikono kutazama nyuma ya vidole na mgongo wa viganja vyangu, kwenye mkono wa kushoto, nikaukuta mkwaruzo mdogo.
Niliugusa mkwaruzo huo nikahisi maumivu kwa mbali, ulikuwa ni mkwaruzo mbichi, sikukumbuka niliupatia wapi na nilikuwa nikifanya nini, nikamalizia zangu kuoga kisha nikatoka kwenda kuvaa.
Niliweka kila kitu sawa hapo nyumbani, ikiwemo kuacha chakula cha mgonjwa na pia cha Amiri na bwana Mgaya, bwana huyo alishanambia ana mapumziko ya siku kadhaa hapo nyumbani hivyo kwangu haikuniwia ugumu kuondoka kuendelea na majukumu yangu.
Muda si mrefu, basi la shule lilifika kutuchukua mimi na mwanangu, tukakwea humo na safari ya kwenda shuleni ikaanza. Nikiwa nimeketi kwenye kiti nilitoa simu yangu nikawa naitazama kupotezea muda na kufupisha safari.
Nilitumia muda huo kutazama 'messages' za bwana Mgaya, messages ambazo zilikuwa zimejaa pomoni lakini sikuhangaika kuzisoma wala kuzijibu, nilizipitia moja baada ya nyingine.
Ujumbe wa kuniomba msamaha kwa yale yalotokea kule Iringa, niliouona, ujumbe wa kuniambia ameachana na yule mwanamke tuijenge familia, niliuona, ujumbe wa kwamba anakuja na mama yake kumuuguzia Dar, niliuona, ujumbe wa kunitaka tuongee na kuyamaliza, niliuona, yani kila kitu nilikiona.
Lakini ilikuwa 'too late', Mgaya.
Tulishachelewa.
Sasa tuko nje ya muda.
... Wakati tunaingia kwenye uzio wa shule, simu yangu iliita na nilipotazama nikaona jina la Mgaya. Nilipokea simu hiyo, kabla sijasema kitu Mgaya akaniambia kwa pupa mama amezidiwa sana sana, yuko njiani pamoja na Amiri wakielekea hospitali.
Alinitajia jina la hospitali hiyo.
Nami pasipo kupoteza muda, punde tu baada ya kumwacha mtoto darasani, nilikimbilia kwenda huko hospitali huko kutazama. Kufika, Mgaya ananiambia mama amekwishafariki. Sababu ya kifo chake ni sukari na presha iliyopanda kwa mkupuo!
***
....[emoji419]Sehemu ya Nane:
Macho ya Zai yalikuwa yanasema jambo.
Jambo lililonitisha.
Si bure alikuwa anafahamu kitu na kitu hicho kilinifanya nitetemeke kwa hofu. Nilitaka kuendelea kuwapo hapo ili anieleze ni nini anajua lakini sababu ya muda nililazimika kuondoka, labda nirejee tena muda mwingine.
Kama si yule mwalimu mkuu kunikawiza kule shuleni, huenda siku ile ningeyasikia yote toka kwenye kinywa cha Zai.
Niliondoka zangu lakini kichwa nilikiacha palepale hospitali kwa mawazo, kweli sikwenda nacho, kuanzia kwenye daladala mpaka nyumbani kwangu nilikuwa nikiyatafakari yale nilosikia, hata chakula sikuhisi ladha yake.
Nilifungua simu yangu nikampigia Anwari, kwasababu nilikuwa nimemblock, ilibidi nimu-unblock kwanza kisha ndo' nifanye zoezi langu, kidogo simu kuita bwana yule akapokea, hakujua kama ni mimi maana namba ilikuwa ngeni lakini aliponisikiliza nilipotamka maneno mawili aliita; "Magreth!"
Sikumwitikia, nilimuuliza moja kwa moja ni nini amemwambia Zai, hapo akakwama kusema, hakutaka kujibu, badala yake aliniomba tuonane mahali ili tupate kuyajenga. Muda na siku nipange mimi mwenyewe.
Aliniambia,
"Nimekutafuta mno lakini sikufanikiwa, hakukuwa na haja ya kufikia huku, mpenzi."
Hilo neno 'mpenzi' kweli likanikera, sijui kwanini lakini lilininiga koo, ujumbe huo nikaufuta papo hapo nisipate kuuona tena. Baada ya hapo niliendelea na maandalizi yangu binafsi, kuandaa chakula cha nyumbani na kufanya kazi zingine ndogondogo, lakini niwe mkweli, hamna nilichofanya nikafanya vema, kuna muda nilihisi mikono yangu inatetemeka kwa kuwaza dhambi nilofanya.
Dhambi nilofanya na Anwari.
Vipi yale ya gizani yakaja mbele ya mwanga tele? Nitachimbia wapi uso wangu kujificha nisishikwe na haya hii? Wapi nitakatiza nisigeuke kuwa mada?
Hilo lilininyima raha.
Baadae mume wangu alirejea nyumbani, mapema ya saa tatu, na siku hiyo alirejea pamoja na vitu tele, vitu vya nyumbani na zawadi zangu binafsi.
Nakumbuka aliniletea chupa kadhaa za marashi ya ghali, viatu bila kusahau magauni, hakumsahau mtoto, naye alimletea nguo kadha wa kadha akijigamba na kujivunia ya kwamba mtoto yule ni 'jembe' lake.
Siku hiyo bwana alikuwa na furaha sana, alitabasamu kila mara, akacheka na kunikumbatia, ni baadae ndo' akanieleza ya kwamba kule kazini amepandishwa nafasi, sasa hatokuwa anaendesha tena watu huku na kule bali atakaa ofisini kuwasimamia madereva wenzake.
Madereva hao sasa watamwita 'boss' naye atawaita vijakazi. Maisha yamebadilika.
Basi siku ile tukala na kunywa vema, tulifanya hivyo kuyasheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, kila mmoja wetu alijumuika mezani ikiwamo kijana wetu, Amiri, mimi kazi yangu ikawa kuigiza furaha nisokuwa nayo, kukenua meno na kujichekesha huku ndani yangu nawaza mambo mengine.
Nawaza furaha ya yule bwana. Nawaza furaha ya familia yetu. Furaha ambayo ndo' kwanza ilikuwa inachipukia baada ya mapito kadhaa.
Bwana Mgaya alifungua chupa kadhaa za ulabu, chupa alizokuja nazo na zingine zilizokuwamo katika jokofu, akanywa kwa kujipongeza.
Alipiga mafundo kadha wa kadha akisindikizia michapo ya hapa na pale, baada ya muda pombe ikaanza kumpangia cha kusema na kumwongoza namna ya kutenda, akaanza kusema namna gani anavyonipenda, namna gani atakavyonipambania.
Aliyasema mambo lukuki lakini pombe haikumpa akayamaliza, punde akapitiwa na usingizi mzito. Alijilaza kwenye kochi akiwa hana hili wala lile.
Hapo Amiri alinisogelea akaniuliza kwa sauti ya chini, "uko sawa kweli?"
Nikamtazama, kisha nikamtazama mume wangu alokuwa amelala kama mbwa alochoka pale kwenye kochi, hamna habari alonayo, nikamrejea kijana Amiri na kumuuliza kunani akaniuliza hivyo?
Amiri akasema sina furaha, ni kweli sikuwa nayo lakini alitambuaje? Siku ile sikulia na nilijitahidi kadiri ninavyoweza kuigiza furaha usoni mwangu mbele ya mume wangu, yeye katambuaje?
Wakati nikijiuliza hayo kichwani, aliniongezea swali jinginewe, "kitu gani kinakusumbua au umemkumbuka mama mkwe wako?"
Nikamshukuru kwa kujali lakini nikamsisitiza hamna jambo lolote lile, tule na tunywe kusheherekea mafanikio ya bwana Mgaya, tusiharibu tafrija yetu kwa kuleta mawazo hasi yasokuwa na faida.
Basi baada ya muda kidogo, Amiri akaniaga na kwenda zake nje, alinambia anaenda kukagua na kutazama mifugo kabla hajaenda kulala, alipotoka nikabaki mwenyewe sebuleni kama mtu mwenye ufahamu, nilimalizia kinywaji changu nikamsindikiza bwana Mgaya kwenda chumbani kupumzika.
Nilipomlaza nikaanza kujishughulikia mwenyewe mahususi kwaajili ya kulala maana asubuhi nahitajika kudamka mapema na jua.
Jambo la kwanza nilofanya nilitoa pedi yangu nilovaa tangu mchana, nilikuwa kwenye siku zangu siku hiyo nikianzia tokea majuzi yake, nikaiweka pedi hiyo pembeni kisha nikaoga na nilipomaliza nikaichukua kwenda kuihifadhi kwenye 'bin' maalum tunapowekea taka.
'Bin' hiyo ilikuwa nje ya nyumba kwenye kibaraza cha mlango wa nyuma.
Nikiwa na taulo langu kifuani, nilielekea huko na nikafanya kile kilichonipeleka, lakini kabla sijafunga mfuniko wa ndoo ile maalum ya taka, niligundua jambo fulani lililonichukulia muda wangu.
Kwa mara ya kwanza kutazama, sikuamini, lakini nilivyopepesa macho kukagua nilihakikisha nilichokiona kilikuwa sahihi.
Pedi zangu za nyuma, takribani tatu kwa idadi, hazikuwamo mule ndani! Sikujua zimeenda wapi na nani kazichukua.
Nikiwa hapo, bado nabung'aa, mara nikasikia sauti za kuku kule bandani, kuku walipiga kelele kana kamba wamekurupushwa na kitu fulani, nikapaza sauti kuita;
"Amirii!"
Kimya.
"Amiri ... ni wewe?"
Sikujibiwa.
Kuku wakapiga tena kelele, kwaaakwakwakwaaa! Moyo wangu ukalipuka na wasiwasi, niliwaza pengine kuna mnyama ama mdudu hatarishi ameingia kwenye banda la kuku, nikasogea taratibu nikiendelea kuita Amiri Amiri, ni wewe uko bandani?
Nilisogea mpaka kwenye uzio wa mabanda, nikasimama na kutazama, nilitamani kuingia humo ndani lakini niliogopa sababu ya kiza, kule mabandani hapakuwa na taa, mtu angeingia kwanza ndani kisha ndo' aichukue kurunzi iliyokuwa inang'ining'inia kwenye kuta ya ng'ombe kwaajili ya kujipatia mwanga.
Mimi hata kuingia humo sikutaka kabisa.
Nilisimama nikisikia kelele za kuku pasipo kuwa na msaada, sauti hizo hazikudumu muda mrefu kukawa shwari, hapo ndipo mimi nikarejea ndani kwaajili ya kupumzika.
Mpaka naingia ndani ya chumba changu sikupata kumwona kijana Amiri. Nilijiaminisha labda alisharejea chumbani kwake na sasa ameupumzisha mwili wake kitandani. Kitu kilichonifanya nikaamini hivyo ni ule mlango wa grill.
Niliufunga mlango huo na hakuna aliyeugusa mpaka asubuhi nilipoamka.
Kesho yake baada ya kumaliza majukumu yangu kazini, niliwasiliana na Anwari nikimtaka tuonane pahali fulani.
Kwasababu ya kujiweka salama, nilimuelekeza aje mgahawa mmoja hivi ambao haukuwa mbali sana na shule ninapofanyia kazi, faida yake haitanichukua muda mrefu kumpitia mwanangu niliyemuacha shule, nikimaliza tu maongezi basi dakika chache tunajiondokea kwenda zetu nyumbani.
Kweli, ndani ya muda mfupi, Anwari aliwasili kama vile tulivyowekeana miadi.
Bwana huyo alikuja hapo na gari yake akanipendekeza tuongelee mambo yetu ndani ya gari badala ya pale mgahawani, hoja yake mule ndani ya gari ni salama zaidi kuliko mbele ya macho ya watu, mimi pia nikaona wazo hilo ni jema basi nikaliheshimu.
Niliingia kwenye gari maongezi yetu yakaanza kwa mimi kuuliza maswali mengi yenye pupa na hasira, maswali juu ya makubaliano yetu tuloweka, makubaliano ya siri, nikauliza makubaliano hayo yamefikaje kwenye masikio ya Zai?
Naye akaniuliza, "ulitaka mimi nifanye nini kama sikupati kwa kila njia? Namba yako haiiti, unapofanyia kazi sipafahamu, ningefanyaje?"
Kweli lengo langu lilikuwa ni kumpoteza bwana huyu katika ramani ya maisha yangu, na niliyapanga hayo pasipo kumshirikisha mtu yeyote yule kwani Anwari kwangu nilimrejea kwaajili ya jambo moja tu, kunisaidia pale nilipokuwa nimekwama, kwahiyo baada ya kupata msaada huo kwangu hakubaki na tija tena, nilitamani nifute kurasa yake lakini nafuta nini?
Naufutaje?
Na hapo nilipokuwa namsikiliza ndo' nikaamini kabisa kuwa kipande cha Anwari hakikuwa ukurasa mmoja bali ni kitabu kizima!
"Lakini Anwari," nilisema naye kwa mkazo, "ni nani aliyekwambia mimi nina mtoto? Na ni nani aliyekwambia kuwa mtoto yule ni wako? Au umekaa tu ukaanza kuyatengeneza maghorofa yako kichwani?"
Niliuliza huku nafsi yangu ikinisuta maana nilijua kabisa najidanganya mwenyewe. Ukweli ndani yangu unanizodoa. Ukweli ambao hapa najitahidi kuuficha kwa nyavu nikiamini hautaonekana mbele za watu.
Miaka miwili na miezi kadhaa nyuma, mimi mwenyewe, wala si kwa kusingiziwa wala kusemewa wongo, nilirejea kwenye mlango wa Anwari baada ya kushindwa kuhimili presha kuwa kubwa kutoka kwa mama mkwe wangu.
Mama huyo alianza kuninyooshea kidole, miezi michache tu kupita baada ya kufunga ndoa na bwana Mgaya, akisema mimi ni mgumba nisiyeshika mimba.
Mama huyo hakutambua wala hakujali ni namna gani tulijaribu kutafuta mtoto mimi pamoja na mwanaye, nikicheza na kalenda yangu kwa ustadi mkubwa, lakini hatukupata matunda.
Swala hilo likanifanya nihofie kumpoteza mume wangu kwa wanawake wengine, wanawake wenye mayai yao, punde watakapomfanikishia kumpa mtoto basi kwangu itakuwa ndo' kwaheri ya kuonana.
Lakini baadae nilikuja kupata shaka, vipi kama mwanaume yule ndo' mwenye matatizo na si mimi kama ninavyojiwazia?
Vipi kama bwana Mgaya hana uwezo wa kunipa ujauzito?
Kwa kipindi hiko nilikuwa na shakashaka, lakini baadae bwana Mgaya alivyokuja kusema kuhusu mwanamke yule wa kijijini, Momo, ya kwamba amemuacha hana mimba wala mtoto wake, nikazidi kuthibitisha kichwani mwangu kuwa bwana yule alikuwa na shida bayana kwenye via vyake vya uzazi.
Basi kwasababu ya ile kiu ya mtoto na hivi muda huo sikuwa na uhakika na utimamu wangu wala wa utimamu wa bwana Mgaya, ndipo nikakutana na Anwari katika siku zangu za hatari.
Nilishiriki tendo na bwana huyo mara moja tu ikatosha kabisa kubadilisha wiki yangu ilofuata kwani nilianza kuhisi mwili wangu haupo kawaida na vile nilivyouzoea.
Baada ya juma la pili nilipima na kuhakikisha nina ujauzito, hapo ndo' nikaona ni muda muafaka sasa wa kumpoteza Anwari katika maisha yangu kwa kum-block kila kona, kila mtu aendelee na njia yake .
Lakini sasa ni wazi nishafeli. Anwari niko naye hapa kwenye gari akinieleza mambo ya mtoto, hata akipata kauli kama mimi na yeye hatupo kwenye mahusiano basi haina shida kabisa, yeye anamtaka tu mtoto wake.
Ati mtoto wake?
Hahahaha Anwari ....
Mtoto gani?
****
Thanks. Ndo napita leo
TunakusubirSamahani kwa kutopost jana. Mazingira hayakuwa rafiki kabisa maana nilishinda kwenye usafiri njiani. Leo tunaendelea.
I told you yesterday not to wait and so I am telling you the same thing today 😄 wait at your own riskSteveMollel tulale au tusubiri