Niliyojifunza kutoka ujenzi wa nyumba yangu ya kwanza

Niliyojifunza kutoka ujenzi wa nyumba yangu ya kwanza

Dunia tunapita mwenye akili kamwe hajengi njiani

So jengeni susi kazi yetu kula kunywa na Beebe sana
 
Binafsi naamini sana kuwa na sehemu yako ya kuishi bila bugudha ya kodi wala maudhi ya wapangaji wengine,
Mambo machacho kuhusu mimi
1. Niko under 30
2. Kipato changu ni kati ya 500k - 550 k kwa mwezi

Baada ya kununua kiwanja، nilianza kununua maatofali kidogo kidogo.
Mambo niliojifunza

1. Anza kujenga na ulicho nacho, kwenye fungu ndio kwenye nyongeza, ukishaweka tofali kama kweli unania ya kugenga kichwa kitapata moto, Mungu atakufungulia

2. Msingi wa nyumba ndio kila kitu, nilipoanza kujenga nilikua na bajeti ndogo, ujenzi ulikuaa wa kimasikini kweli, matokeo yake, sasa nyumba imeisha ila msingi uko chini na kuna vitu ningetamani vingekuepo ila ndo nyumba ishamalizika, hili silijutii kwani ni funzo, hata hapa nilipofika sikutegemea kufika.

3. Hata kama fundi unamuamin, ni muhimu sana kuwepo wakati wa ujenzi, kuna makosa mengi ambayo yanaweza kutokea, kusimamia ujenzi sio kwa kuzuia uizi tu bali hapa usahihi wa nyumba unavyotaka iwe. Nyakati muhimu za kuwepo ni wakati wa kuset msingi wa nyumba, wakati wa kufunga mkanda wa nyumba, ukataji wa madirisha na milango, na kufunga lenta makosa mengi yanatokea hapa

4. Ujenzi hauna gharama kamili, kama ulipiga bajeti ya milioni 30, hakikiaha una milioni tano ya extra. Mengi yanatokea, ikiwemo vitu kupanda bei

5. Kuna muda utakua unajua kua fundi amekula hela ila hakuna jinsi, ikiwa hujui vifaa vya plumbing au umeme, chukua bei ya fundi, nenda madukani kaulizie, ukipata tofauti isio kubwa na ukiwa na uhakika wa kuletewa kitu original ambacho wewe unahofu ya kuuziwa fake , basi mpe tu fundi hela ( kwa wasio na uzoefu)

6. Siku unayomaliza kupaua ndio ujenzi unaanza, kati ya vitu ambayo ni kuhimu katika nyumba na vina gharama kubwa ni kama mfumo wa maji, umeme, milango ya mbao na grill, hivi vitu usivichukulie kirahisi kwenye budget, gharama zake hua ni M M tu.

7. Unapotaka jugenga aim for high, nilikua nimeingia mtego wa kutaka kujenga chumba kimoja na sebure, ila nilipoamua kujenga nyumba ya vyumba vitatu niliona kabisa kama ni kitu ambaacho hakiwezekani ila hatimae imewezekana, lesson-- panga kwa kuangalia wewe unakua au unataka kua nani nani na si sasa hivi una hali gani .
Plan besed on who you want to be not who you are, by this utaepuka regret za kujenga kitu ambacho baadaae hukifurahii sana
Msingi wa nyumba ndio kila kitu au ukipaua ndio ujenzi unaanza ?

Chagua moja.
 
Gharama kubwa inaanzia kupaua. Yangu ilinikula 15m kupaua tu. Aluminium 6 m, milango ya mbao complete 840k kila mmoja, milango ya kisasa ya chuma 2,200,000 wa mbele na nyuma. Tiles 20m za India, hizi ni pamoja na za skirting nje. Umeme, maji etc ni shida. Bado grills za madirisha, fundi tiles, fensi etc. Nyumba ya kisasa ni gharama sana. Ila Mungu ni mwema niko kwangu

Tiles expensive kuliko kupaua/kuezeka?
 
Natamani ningefanya hivyo ila nilishajibu hapo nyuma, kuna watu wakiiona nyumba watagundua ID yangu, kifupi ni nyumba ya vyumba vitatu, kimoja masta, sitting room imeunganika na dinning room, public toilet na jiko, nyumba ina urefu wa mita 9 na upana wa mita 11

Ulitumia matofali mangapi?mpaka kwenye linta
 
Grill Mlango wa mbele na nyuma,kwa wakati husika Mlango utakua maPazia

kuna boya mmoja napga nalo story kila siku lishamaliza kupaua,lishatia grill madrisha yote

ila linalalamika kila siku halina hela linatafuta hela ndio lihamie kwake, mi imefika wakati namwambia

mwanangu usiniletee mastory yako ya huna hela,shida unazitaka mwenyewe,lipo tunaendelea nalo umia

kwenye ma kodi yale unampa mwenye nyumba hela huku roho inakuuma,una nena kwa lugha zote kimoyo moyo,ila halikomi wala halijifunzi.
Huyu mbona kama mimi🤣🤣
 
Ulitumia matofali mangapi?mpaka kwenye linta
Ni kati ya 3000-3500 nyumba nzima ukijumlisha na shimo la choo, sema kwenye shimo la choo tofali walikata sio kuweka nzima so hii inakula tofali nyingi
 
Msingi wa nyumba ndio kila kitu au ukipaua ndio ujenzi unaanza ?

Chagua moja.
1. Msingi ndio kila kitu katika kutengeneza shape ya nyumba, kuanzia muonekano wa nje na structure ya ndani, urefu wa msingi na style ya kutenganisha msingi na boma.


2. Ukimaliza kupaua ndo ujenzi umeanza nikimasnisha vitu vingi vingi in term ya gharama like grill, blundering, plasta, frame na top za milango, rough floor na tiles, wiring, plumbing, alminium window kama unahitaji na gypsum. Hapo ukipiga hesabu ya hivyo vitu utaelewa
nilichosema

so kauli hizo mbili zinajitegemea na huhitaji kuchagua kati ya moja
 
1. Msingi ndio kila kitu katika kutengeneza shape ya nyumba, kuanzia muonekano wa nje na structure ya ndani, urefu wa msingi na style ya kutenganisha msingi na boma.


2. Ukimaliza kupaua ndo ujenzi umeanza nikimasnisha vitu vingi vingi in term ya gharama like grill, blundering, plasta, frame na top za milango, rough floor na tiles, wiring, plumbing, alminium window kama unahitaji na gypsum. Hapo ukipiga hesabu ya hivyo vitu utaelewa
nilichosema

so kauli hizo mbili zinajitegemea na huhitaji kuchagua kati ya moja
Kwa hiyo msingi, kuta na paa ujenzi unakuwa haujaanza.

Kwa sababu msingi, kuta na paa havina gharama kama finishing, si ndio?
 
Binafsi naamini sana kuwa na sehemu yako ya kuishi bila bugudha ya kodi wala maudhi ya wapangaji wengine.

Mambo machacho kuhusu mimi

1. Niko under 30
2. Kipato changu ni kati ya 500k - 550 k kwa mwezi

Baada ya kununua kiwanja، nilianza kununua maatofali kidogo kidogo.
Mambo niliojifunza

1. Anza kujenga na ulicho nacho, kwenye fungu ndio kwenye nyongeza, ukishaweka tofali kama kweli unania ya kugenga kichwa kitapata moto, Mungu atakufungulia

2. Msingi wa nyumba ndio kila kitu, nilipoanza kujenga nilikua na bajeti ndogo, ujenzi ulikuaa wa kimasikini kweli, matokeo yake, sasa nyumba imeisha ila msingi uko chini na kuna vitu ningetamani vingekuepo ila ndo nyumba ishamalizika, hili silijutii kwani ni funzo, hata hapa nilipofika sikutegemea kufika.

3. Hata kama fundi unamuamin, ni muhimu sana kuwepo wakati wa ujenzi, kuna makosa mengi ambayo yanaweza kutokea, kusimamia ujenzi sio kwa kuzuia uizi tu bali hapa usahihi wa nyumba unavyotaka iwe. Nyakati muhimu za kuwepo ni wakati wa kuset msingi wa nyumba, wakati wa kufunga mkanda wa nyumba, ukataji wa madirisha na milango, na kufunga lenta makosa mengi yanatokea hapa

4. Ujenzi hauna gharama kamili, kama ulipiga bajeti ya milioni 30, hakikiaha una milioni tano ya extra. Mengi yanatokea, ikiwemo vitu kupanda bei

5. Kuna muda utakua unajua kua fundi amekula hela ila hakuna jinsi, ikiwa hujui vifaa vya plumbing au umeme, chukua bei ya fundi, nenda madukani kaulizie, ukipata tofauti isio kubwa na ukiwa na uhakika wa kuletewa kitu original ambacho wewe unahofu ya kuuziwa fake , basi mpe tu fundi hela ( kwa wasio na uzoefu)

6. Siku unayomaliza kupaua ndio ujenzi unaanza, kati ya vitu ambayo ni kuhimu katika nyumba na vina gharama kubwa ni kama mfumo wa maji, umeme, milango ya mbao na grill, hivi vitu usivichukulie kirahisi kwenye budget, gharama zake hua ni M M tu.

7. Unapotaka jugenga aim for high, nilikua nimeingia mtego wa kutaka kujenga chumba kimoja na sebure, ila nilipoamua kujenga nyumba ya vyumba vitatu niliona kabisa kama ni kitu ambaacho hakiwezekani ila hatimae imewezekana, lesson- panga kwa kuangalia wewe unakua au unataka kua nani nani na si sasa hivi una hali gani.

Plan besed on who you want to be not who you are, by this utaepuka regret za kujenga kitu ambacho baadaae hukifurahii sana.
Mm mwenyewe nimeanza kujenga mwenz uliopita mdogo mdogo ntafika nakipato changu nikidogo tu. Ila dar chamoto nakiona
 
Duh milango ya chuma mbele na nyuma tu M ngapi? Duh tunaomba utupe picha ya hio milango wakati mi hio milango wa mbele na nyuma ya chuma nilitumia laki 3 yote kweli ujenzi tunatofautiana kutoa ela si mchezo.
Ulinunua wapi hiyo milango ya laki Tatu tunaomba namba please
 
Back
Top Bottom