Niliyoyabaini katika Operesheni ya Polisi dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road - Dar es salaam

Wewe bwana mdogo hapa utaandika mengi ukijikita kwenye sheria na utaratibu na wala sio facts. Inawezekana kweli kabisa polis hawachunguzu vya kutosha, lakini kwa hali ilipofikia ilihitajika mbinu ya kupunguza speed ya uhalifu wa panya road.

Fuatilia matukio ya panya road, wanakua mpaka vijana 30 kwenda kupora, sasa vikundi vya watu 30 vipo vingapi? Kila kijana akifunguliwa faili la upelelezi itachukua muda gani polis kumaliza kazi? Hao polis hawana shughuli nyingine?

Najua wanasiasa mnapenda sana public attention, ila suala la usalama wa watu ni priority namba moja kwa kila nchi. Leo panya road wanaua watu ambao sio ndugu zako, pengine ipo siku tukio litakugusa moja kwa moja na utajifunza kitu.

Ni lazima tuzungumze uhalisia, nchi hii ni masikini mifumo ya sheria na haki ina matatizo makubwa, upelelezi ni gharama hivyo mahakama huachia watuhumiwa wengi wa uhalifu kwa kukosekana ushahidi wa moja kwa moja, lakini sio kweli kua watuhumiwa ni wasafi. Na hii ni loophole ambayo hadi wahuni wanaijua... polis wakilegeza kamba panya road watashinda hii vita, kama yalivyo makundi ya ulanguzi wa dawa za kulevya pale Mexico.
 
Huwa kuna utendaji wa kawaida wa kipolisi siku kwa siku,halafu huwa kuna operesheni maalumu,operesheni huwa ni za muda Fulani maalumu,baada ya hali kuwa mbaya na kutishia Amani ya taifa letu,polisi kwa intelegensia yao huwa na record za wahalifu sugu wenye matukio ya Mara kwa Mara vituoni.
 
Hata kama tuseme ni wahalifu, mamlaka ya Polisi kuwapiga Risasi Watuhumiwa wa uhalifu mamlaka hayo wameyatoa wapi?. Mnatetea ExtraJudicial Killings
"Tufamu hili neno " OPERESHENI MAALUMU KWANZA"tutenganishe na taratibu za kawaida za kiutendaji,nadhani mnakumbuka operesheni majangili miaka hiyo!
 
"Tufamu hili neno " OPERESHENI MAALUMU KWANZA"tutenganishe na taratibu za kawaida za kiutendaji,nadhani mnakumbuka operesheni majangili miaka hiyo!
Yaani anataka kwenye operesheni tutumie taratibu za kawaida? Sasa hivi watu wa Dar angalau wanapumua! Walikuwa hawatoki ndani muda wa jioni!
 
Yaani anataka kwenye operesheni tutumie taratibu za kawaida? Sasa hivi watu wa Dar angalau wanapumua! Walikuwa hawatoki ndani muda wa jioni!
Jamaa anataka kujifunza lugha na misamiati mbalimbali ya kiswahili huyu,
OPERESHENI MAALUMU NI KITU GANI?
Ni utendaji maalumu kwa wakati maalumu ambapo vyombo vya ulinzi ufanya kazi ya udharura katika kukabiliana na tukio au matukio ambayo kwa wakati huo huwa yana atarisha usalama wa jamii nyingine,uwe binadamu au ndege au wanyama wa porini,au lolote lile la kiusalama.
 
Narudia Tena acha siasa kwenye Mambo muhimu,wanakamatwa mara ngapi wanarudi uraiani?wanaua watu bila kosa,wanabaka wanajeruhi na hakuna kinachoendelea ngoja washughulikiwe kwanza,hizo sheria zenu za kwenye vitabu bakini nazo
 
Abdul wewe ni politician, Anza na structure, power na funding katika ngazi ya mjumbe, mwnykiti serikali za mitaa na Uwepo wa police katika vituo vidogo masaa yote. It's absurd eti Jiji la DSM watu wanavamiwa huu ni uzuzu na states organs zipo na zina matawi. a committee of public inquiry ni muhimu, why na police wapo na hayo maeneo nafasi ya police ikoje, kituo kipo na miongozo yao Kwa wananchi ikoje, namba za simu police OCS zinafahamika, je wapo masaa 24, ufa ulikuwa wapi siku na maeneo husika, hawa police cid Kwa sasa ufanisi wao ukoje wanakidhi?

Parenting ya police katika ngazi zote iko vizuri, katika local government police wanaheshimika, wanabajetiwa, ofisi ya mkurugenzi inaweka police kama sehemu ya bajeti item zake,. Haya ni baadhi ya maswali muhimu.

Narudia hao panya road kama hamjui ni mbegu ya uasi na uasi kijeshi response yake ni shoot and kill.

Hii habari kuhusu panya road msilete upuuzi wowote wa kijinga jinga, hangaika na muundo, uwajibikaji na malezi ya vitengo vya kiutawala.


We can't go the mahakama way Kwa hawa waasi katika jamii.


Abdul these Panya roads ndio utawatumia siku ukitaka kuandamana ndio watakuwa front kuiba, kuvunja na kuharibu usalama wa raia na Mali zao. Na hautaweza kupata fursa kuandaa peaceful political and legal public demonstrations for justice sake. These are normally based on states peace and citizens behaviors.

Hili halina mjadala na kamwe hatuwezi kufanya ujinga hata wa kuunda tume kuchunguza vifo vya hawa mbwa.

We need a committee to investigate on what's shot with the police. Kwa nini panya roads wawepo wakati Police wapo na Kwa nini iwe desturi kujirudia rudia? Je, police wanaona aibu na haya? Mamlaka za juu na kamati ya usalama ya kitaifa ipo!!? No, it can't be this way?

Kwa ufupi Police na Mkuu wao wamekaripiwa ndio ishara na lazima wawajibike vinginevyo waache kazi ya upolice.

Hawa panya roads wamelelewa na kukuzwa na police wenyewe Sasa tuache wateketeza mazao yao.

We need prosperity and constant security for our people to create wealthy. Finally we talk of a country with good economy and that would attract FDI (uwekezaji wa kigeni) and local investors.
 
Nyuma ya Jaji panakua na askari mwenye silaha ya moto. Unategemea kazi ya Ile silaha ni Nini ?

Acha siasa za kijinga KWENYE mambo yanayohusu amani na usalama wa nchi.

Hizo pesa za kihalifu wa kimtandao mnazoanza kufadhiliwa nazo zitaliangamiza Taifa hili kama hamtashughulikiwa na nyie . Huku kuwa Polisi wanashirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama linapokuja suala la Oparation au unafikiri wewe ni mjuaji kuliko watanzania wote.

Kuna watu wanaowatuma hao Panya rod na wao wanakaa kutengeneza mazingira ya kuwanunulia mapanga , madawa ya kulevya na pombe na kuwapa Hela wanapouza vitu . TV zinazouzwa unategemea zinanunuliwa na akina nani?
Watu wanavamia nyumba ya mtu wanaiba na kuharibu kila kitu halafu unataka Hakimu ndio akawakamate na Kalam mkononi.?

Kama Polisi kazi yao ni kuua TU bila sababu basi wangetumaliza. Kwa Nini waache Malaki na maelfu ya Watu waende Kwa mtu mmoja.

Wewe unafikiri hii nchi Kwa kiwango Gani uhalifu Upo na wewe umekaa kimya unafurahiya TU kuona watanzania wanaumizwa Kwa jasho lao halali.

Unataka Polisi waende kukamata wakiwa wameshika Biblia na Korani mkononi kama wahubiri?

Na wewe dawa yako inatakiwa iwe hiyo hiyo Vinginevyo urudi Burundi mana ni zao la kihalifu na wewe usituharibie nchi sisi hatuna pa kwenda.

Kama unafurahiya kila siku kusikia panyarodi wakiongezeka pasi nenda mahakamani kawatetee mana wapo wengi tu waliopelekwa Huko.

Unafikiri kumkamata mhalifu anayejijua kabisa kuwa anatafutiwa na ni Mtu mwenye stress za maisha ni jambo rahisi.

Achana na siasa za kijambazi nyie ndio mnashangilia mpaka ugaidi .
 
Kuna vitu vingi vya msingi vya kupigania ili kushinikiza katiba ifatwe katika nchi hii lakini sio haya mambo ya panya road waache waende kuzimu maana ndo walikokuchagua
 
Vessel , Upelelezi na kupeleka Mahakamani ndio njia sahihi ya kila mtu aadhibiwe kwa haki bila kuonea au kuacha mhalifu bila Adhabu ,sio sawa Polisi kuuwa.Hawana hayo mamlaka kaka ,tusitetei haya.
Chakujiuliza ni je hiyo mifumo ya kuachiwa ifanye kazi ipo katika hali gani,huenda mara nyingi hata wewe imeshakuwa mhanga wa hiyo mifumo
 
Well said,HONGERA SANA.
 
I don't know any one miongoni mwa walio uliwa , ninacho Pinga Mimi ni Police namna wanavyoendesha hii Operesheni ,wanakamata pasi uchunguzi wa kutosha mbaya zaidi hawapeleki Mtuhumiwa mahakamani wanauwa ,hii kwangu sio sahihi .
Huo uchunguzi Kwa Nini usiufanye wewe na hao mnaojiona mnajua kuchunguza Kisha mkatoa ushirikiano na Polisi. Au katiba inakukataza kulinda nchi yako na ulinzi wa Mali yako. Kwani unajua panyarodi Watakuja kwako lini?

Majeshi yetu yanapofanya Oparation wanatumia Vikosi vyote vyenye uwezo wa kila namna ndio maana hata ugaidi Tanzania unashindwa tofauti na nchi nyingine japo wafandhili wa Magaidi wanamwaga Hela ili nchi isitawalike. Ndizo zinazowapa midomo ya kubwabwaja.

Polisi Mkamateni Abdul Nondo Kuna Wahalifu wengi nyuma yake kuanzia kwao Burundi.

Kama hutaki Oparation hiyo hamia Kwenu Burundi Ile nayo ni nchi. Tanzania ni ya wote wanaopenda amani na kufuata SHERIA .
 
Waliojenga kibanda cha mlinzi kwa milioni 11,wafikishwa mahakamani.Aliyehisiwa kua Panyaroads,auawa.
Ndomaana baadhi ya viongozi walikaa wakafikiria,bora kutoa kodi ya moja kwa moja,na kuileta INDIRECTLY, reactions za watu,haziwi kama ingekua directly.
Meigulu et al,abane hapohapo,na wale wanaoweza kuiba kwa kalamu waibe sana,jamii yetu BADO SANA.
 
Jamani jamani. Nakubaliana na Abdul Nondo asilimia Mia. Sheria za nchi zifuatwe. Na hayo ndio Abdul anasisitiza. Polisi wamevunja sheria. Iko wazi. Wawajibishwe. Hata kama ni kweli kuwa hao ni panya road. Polisi wametoa wapi kibali cha kuwaua? Naililia Tanzania. Tinakoenda siko.
 
Noooo this is not politics, issue iliyopo hapa ni jinsi hawa guy's in uniforms walivyogeuka kuwa majambazi, huwezi kujichukulia sheria mkononi, police lazima wafanye kazi kwa mujibu wa sheria, hii mob justice ni ukatili at its best, lawama za mkasa wako zielekeze police maana wameshindwa kukulinda,uzuzu wako unaelekeza hasira kwa soft targets maana uoga wako kwa police unakufanya upoteze uwezo wako wa kufikiri, we have courts of law nchi hii na hizi ndizo pekee zenye uwezo wa kuamua sio kangaroo courts
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…