Niliyoyabaini katika Operesheni ya Polisi dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road - Dar es salaam

Niliyoyabaini katika Operesheni ya Polisi dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road - Dar es salaam

Nchi yetu Ina katiba ,sheria za mienendo ya Makosa ya jinai ,PGO,Kanuni za Jumla za Adhabu sheria zote hizi zimeweka utaratibu wa kushughulikia makosa ya uhalifu .

Hakuna sehemu Polisi amepewa mamlaka ya kuuwa mtu kama njia ya kupambana na uhalifu , Polisi wamepewa wajibu wa kuchunguza na kupeleleza sio kuhukumu kwa kupiga mtu Risasi ni Mahakama tuu ndiyo yenye jukumu la kutoa adhabu iwe ni adhabu ya kifo ,kifungo Cha maisha au miaka yeyote hayo hufanywa na Mahakama. Mimi unanishambulia Nina taka Sheria tulizojiwekea tuzifuate na kuziheshimu ,kama hatuzitaki zimepitwa na wakati ktk kupambana na uhalifu tuzibadili, kwanini tuzivunje ???


Ndio maana tuna sheria,katiba , kanuni na taratibu zimeweka utaratibu wa namna ya kupambana na uhalifu .

Ndio maana kuna Mahakama siku zote , ingekuwa Polisi wanaaminika kwa kila Uchunguzi au upelelezi wao kungekuwa hakuna haja ya Mahakama kupima ushahidi na kila siku Polisi wangekuwa wanashinda kesi , ndio maana kuna Mahakama ,ni muhimu sana Ndugu zangu uhalifu ukapambanwa kwa mujibu wa sheria,kama sheria zetu hazifai kupambana na uhalifu tuzibadili ila sio kuzikeuka kwa kumuuwa na kumpiga Risasi Mtuhumiwa.

Hata hao Panya Road wanaofanya uhalifu sheria zipo wakikutwa na hatia wanaadhibiwa sawa na sheria inavyosema kuna kifungo adhabu ya kifo , kifungu cha maisha ,miaka 30 na adhabu zingine . Kwanini wasishtakiwe kwa mujibu wa sheria wajibu wa Polisi ni kufanya upelelezi na uchunguzi kuisaidia Mahakama kufanya maamuzi sio kuuwa watuhumiwa.

Kama tunaona hakuna haja ya kuchunguza na kushtaki Polisi washinikize sheria zibadilishwe ili iwe rahisi wao kufanya wanachokifanya , hakuna mtu anatetea wahalifu ,ninachotaka utaratibu ufuatwe ktk kupambana na uhalifu na kama sheria zetu ni Butu basi tuzibadili na sio Polisi kuchukua hatua ya kuuwa Watuhumiwa bila kuwapeleka mahakamani.
Nakubaliana na wewe 100% lakini tatizo linakuja pale ambapo Jamii hii hii hatushikamani linapokuja suala la Uvunjifu wa sheria na kuwafanya raia wema kukosa amani.e.g. Hao panya rodi walipovuma sana kwa uhalifu huo watu hatukusimama wote dhidi yao ila lawama na kejeli nyingi sana zilielekezwa kwa Serikali na hususan polisi.
Huwezi amini kuwa vijana(Panya rodi) wanafanya msako hata kuweka vizuizi katika mtaa wenye watu wengi(na pengine watu katika mtaa huo wanazo silaha e.g. zile wanazoenda nazo baa kutishia walevi wenzao Lakini hakuna anayetoka au uongozi wa mtaa kufanya mobilisation ya kuwadhibiti hao panya rodi. Kwa hiyo polisi wachache waliopo eti wao ndo watoke wakapambane na hao panya rodi. Kumbuka hoja ya mahakamani ni nzuri sana lakini inachukua muda na pengine itawaweka baadhi ya watu hatarini kwani mtu apatikane na hatia ni lazima kuwepo na kithibiti, mtuhumia huwa na haki ya dhamana na yote hayo huchukua muda mrefu. Mara nyingi, na uzoefu unaonesha watuhumiwa wa wizi, kama hakuna kithibiti hushinda kesi na kuachiwa huru. Je, itakuwaje usalama wa wale walioshiriki kutoa ushahidi mahakamani? Tukumbuke Polisi nao ni watu kama mm na ww. Wanachoka na hawapendi kwenda kudhalilika mahakamani pale kesi inapotupiliwa mbali kwa kukosa ushahidi. LAKINI ukweli unajulikana kabisa kwamba fulani ni Jambazi,ni panya rodi etc.Mbona tunaishi nao humuhumu mitaani? Sasa polisi wanasaidia kutupunguzia hao wahalifu tunaowalinda/tunaowahifadhi/ tunaowaonea haya/tunaowaogopa na kukaa kimya. Vijana tuwazae halafu wageuke kuwa Nunda kwetu? Ndio maana nikasema Kimya kiendelee wakati ambapo ni zamu ya serikali kuwashughulikia panya rodi the same kama tulivyokaa kimya wakati panya rodi wanafunga mitaa na kuwajeruhi watu, kupora mali, kubaka n.k. Si tunawasetiri ni ndugu zetu?? Basi kwa Polisi hao sio ndugu hata kidogo. Zingatia hili: Kwa Mwanajeshi yeyote huwa unatekeleza amri kwanza maswali ni baadaye. Panya rodi nao walikuja na kanuni/maswali yanayofanania kama hivyo eti unaulizwa (tena ujibu haraka) unataka bokoboko au pilau? Ukichelewa kujibu wanakutolea jibu chap wao wenyewe. We acha tu, panyarodi sitaki hata kuwasikia aisee.
 
Serikali imetangaza vita dhidi ya panya road kama kwa mfano serikali za Kenya na Somalia zilivyotangaza vita dhidi ya Al Shabaab au serikali ya Nigeria ilivyotangaza vita dhidi ya Boko Haram. Panya road wamewekwa kwenye kundi la maadui wa kivita (enemy combatant). Sheria zinazowalinda raia wa kawaida haziwalindi maadui wa kivita. Hapa ni Geneva convention ndiyo inasimamia.

Ni muhimu sana kufanya upelelezi na kujua walioko nyuma ya panya road. Na wakijulikana lazima wachukuliwe hatua maana wanahatarisha amani ya nchi kwa sababu za kisiasa. Nani anawafadhili, nani anawapa madawa ya kulevya ili kuwatayarisha kisaikolojia kufanya maovu. Ni muhimu kujua.
mbona wanajulikana sana tu. kuna watu wanajuliakana kwa majina ni madalali wa vitu vya wizi kama simu, tv nk endapo tukio limefanyika mali ikaibiwa baada ya muda ikaonekana mahali. atakamatwa mtumiaji au mnunuzi akiulizwa atamwonyesha dalali aliyemuuzia nae atakamatwa. kwahiyo haya majina yapo huko vituoni. nashangaa sana mtu anapokuja kudai eti polisi wanaaua raia wa kawaida sio wahalifu.
 
Ndio maana inatakiwa mshukiwa apelekwe mahakamani ukweli wa kosa udhibitike, na adhabu stahiki itolewe. Sio sahihi kuruhusu polisi wasio na weledi kuua watu wanaowatuhumu.
Panya Road ni ngumu sana kupata ushahidi ingawa huko mitaani wanafahamika! Kama unaishi mtaani na kujihusisha na mambo ya kijamii utafahamu viongozi wa serikali za mitaa wanajua kila nyumba na uhalifu wake ingawa ushahidi ni mgumu sababu lazima umkamate mtu na kidhibiti.

Siungi mkono mtu kuuawa bila ushahidi wa kutosha lakini wakati mwingine "nawaelewa" polisi. Siku ukipigwa tukio na hao vijana nakuapia utawaelewa polisi! Siku wakuvamie na familia yako ndio utajua walivyo wanyama kama utabakia hai.

Kuna eneo nimeishi, mnaishi jirani na mtu ni bingwa wa kuchora ramani na kutuma vijana kutoka mbali kuja kuvamia! Tulipata shida kubwa kupata ushahidi ingawa wakazi wote tulishajua kinachoendelea! Mara kadhaa kila ulipotokea wizi tulihakikisha amekamatwa kwa mahojiano lakini ushahidi haukupatikana na polisi walisema hawawezi kutumia nguvu sababu ya wamezuiwa "kubinya" watuhumiwa.

Huyo mtu ilitulazimu wakazi tumfungie "kazi" wenyewe na baada ya hapo aliondoka na mkewe eneo letu tukarudisha amani mtaani. Kudeal na wahalifu kwenye hizi nchi zetu za kimaskini ni mtihani mkubwa sababu ya mapungufu ya kisheria, uwezo wa kiuchunguzi, tamaduni n.k
 
Unaota ndoto ya alinacha mkuu.
Dola inapofanya kazi yake Kwa ajili ya kulinda amani na usalama wa nchi kamwe hakuna mtu anayeweza kushitakiwa.

Huwezi kumshtaki Obama Kwa sababu ya vita au Bush. Walifanya Yale Kwa ajili ya uslama wa nchi yao na Mali zao.

Hata wewe ukiwajulikana kuwa unawaunga mkono Panya rod watakula kichwa.

Labda ujifiche TU huku kwenye uhuru wa KUTUKANA na kusema chochote.

Hali ya Jiji imerejea wewe unaleta siasa hapa.?

Rwanda ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika lakini amani Ile haikujengwa Kwa maneno Bali vitendo. Eti tukemee uhalifu. Sijui upuuzi Gani bila kuchukua hatua Kali. Rwanda imefikia pale Kwa sababu ya kudili na Wahalifu Kwa nguvu zote.
Mpaka Leo Kigoma Kuna Majambazi Toka Burundi. Kwa Nini hawaingii Rwanda wakaiba na kupora na bunduki zao wanakimbilia Tanzania. Ni Kwa sababu watanzania mtu akishavaa suti mchana tunamuona ni Mtakatifu.
Matokeo yake uhalifu hauishi.

Nondo ni miongoni mwa vinasaba vya kihalifu wa kijambazi Toka Burundi. Tukimsikiliza tutaitumbukiza nchi kubaya kama kwao Burundi.
Miaka ya nyuma majambazi kule Kigoma waliotokea Burundi walikua wanapora na Kubaka.

Kuna watu ni jeuri sana mitaani. Wanabaka watoto wa shule ,wanafira watoto,wanavuta bangi hadharani lakini hatumuoni Mshenzi hata mmoja kama Nondo akisema iundwe tume ikachunguze kiwango Cha uhalifu na mmomonyoko wa maadili na kuomba Polisi waongezewe vifaa vya utendaji au hata kusema kila mitaa zifungwe CCTV Camera kuwabaini Wahalifu. Au kuharakisha vitu kama Vitambulisho vya utaifa. Kuhakikisha kila mtu anajulikana Kwa DNA na Alama za vidole n.k.
Niliowataja hawana kinga yoyote, benchmark ya kesi itasimama kwa kurejea kesi ya Lengai Ole Sabaya ambaye anasulubiwa leo kwa kutumwa na viongozi wakubwa wenye kinga ya kushitakiwa. Kwa hiyo usijipe moyo eti kwa ajili ya kulinda usalama, mnatengeza magaidi bila kujitambua.
 
Vile ni vyombo vya Dola mkuu.
Kama unabisha subiri siku Panya Road wawe wengi na wafanye matukio mfululizo halafu Jeshi lichukue nafasi ya kulinda amani ndio Utajua Nini maana ya Dola.
Jeshini jambo la muhimu ni kutumia silaha Kwa kulenga kichwa.

Panya rod ni hatari sana mkuu. Wasikie TU Kwa mbali. Achana na watoto walioamua kuua watu. Hata kwenye vita vya waasi wanatumia Vijana wadogo kupambana na Majeshi ya serikali na kufanya uvamizi na uasi Kwa sababu wanajua watoto wadogo wakishika silaha wanajua kuua TU hawajui kuwa mtu amejisalimisha au la . Na hua hawaogopi kuuawa ndio maana wanavamia muda wowote bila kujali kuwa watakamatwa au laa.
Kwa hiyo kusema eti mpaka uchunguzi ufanyike ndio wakamatwe kama mwizi mmoja mmoja ni jambo gumu sana . Nchi itaingia kwenye machafuko makubwa .

Wale wangesalia miezi miwili ndio ingekua basi mana wangefikia wakati wapo kila mahali na wangekua Sasa wanapora maduka , masheli ya mafuta,super market n.k, Tena wakiwa Kwa Makundi. Wale ni Wahalifu wa kimakundi Kwa hiyo ni rahisi sana kuwabaini anapopatikana mmoja.
Na watanzania wanadhani nchi yetu Haina wataalam kwenye vyombo vya Dola. Wapo wengi na wanafanya kazi Kwa kushirikiana na wataalam wengine kubaini Wahalifu.

Haiwezekani mtu awe na rekodi ya uhalifu halafu wakifuatilia kisayansi kwenye mitandao aonekane alikua na ukaribu na Wahalifu kwenye tukio Fulani basi asikamatwe. Na akionekana mkorofi wakati wa ukamataji nadhani hakuna namna nyingine tusiwalaumu polisi ,tuwalaumu Panya rod.

Tunaomba wapelekwe mahakamani wale njuka wanaojifunza uhalifu lakini wazoefu Kwa kweli ni kuwapa lawama Polisi Bure . Hapana Hawa ndio waliosababisha Kodi zetu zikatumika Kununua Bunduki za kuua binadam na sio dawa ya mbu.
Jeshi la wananchi wanafundishwa kulenga kichwani tu ndio, lakini polisi wanafundishwa kulenga miguuni ili wamkamate mtuhumiwa na kumpeleka kwenye chombo cha kutoa haki sio kuua.

Tambua Jeshi la wananchi na Polisi ni vitu viwili tofauti. Kama kuna tatizo Jeshi la wananchi hawana majadiliano lakini wana nafasi hiyo kufanikisha upatikanaji wa kiini cha tatizo baada ya kupeleleza.

Polisi walioua, aliyewatuma na kuagiza operesheni hiyo atashitakiwa tu, Kesi rejea ni Lengao Ole Sabaya hii itakuja kuwasumbua sana mpaka kuna baadhi watakimbia nchi
 
Uko sahihi sana, kama kweli wanachokifanya polisi cha kuua wezi ni sahihi, kuna mtu alikamatwa kwa kujiunganishia bomba la mafuta hapo nyumbani kwake. Mbona mtu huyu hatujasikia kapigwa risasi maana yeye kaiba kikubwa kuliko panya road?

Shida ya panya road ni body attack wanazofanya kumpiga mtu mapanga kumchoma na bisibisi pia marungu ndo maana tunaona ni sahihi ata wao kuuliwa ivo, kama wangekua wanatapeli tuu kijanja janja bila kukaba basi wangeuliwa ata mimi ningekataa ila nimeshidua mtu alie dhurika na hao na ghalama familia yake ilizotumia kumtibisha asee hata kwa risasi naona kama wanawadekesha ilitakiwa wakatwekatwe vipande wazima alafu wawe wanaeushia ngurue na fisi.
 
Mkorinto , Ndio maana kuna Mahakama siku zote , ingekuwa Polisi wanaaminika kwa kila Uchunguzi au upelelezi wao kungekuwa hakuna haja ya Mahakama kupima ushahidi na kila siku Polisi wangekuwa wanashinda kesi
sheria na mahakama ni kielelezo cha ustaarabu lakini sio omega ya kutoa haki. mfano kwa sasa adhabu ya kunyongwa haitekelezwi!!unadhani mhukumiwa anakuwa katendewa haki na mahakama kwa kosa atakaloshitakiwa nalo???kumbe haki ya hapa mahakamani ni mtambuka.
, ndio maana kuna Mahakama ,ni muhimu sana Ndugu zangu uhalifu ukapambanwa kwa mujibu wa sheria,
makosa mengi yametafsiriwa kisheria na adhabu zake,lakini upande wa uhalifu na ugaidi sheria zinaonekana kupitwa na wakati hasa ukizngatia uhalifu ni mpya kila leo.
changamoto inabaki kwa mtendaji wa mwisho(polisi)anayetarajiwa atoe huduma ya usalama lakini pia atende haki kwa wote mhanga na mtuhumiwa.mahakama wanasoma kipi kimeandikwa wapi tukioanisha na kilichopo mbele yetu.
kama sheria zetu hazifai kupambana na uhalifu tuzibadili ila sio kuzikeuka kwa kumuuwa na kumpiga Risasi Mtuhumiwa.
nguvu ingeongezwa hapo,lakini ni upuuzi kusema polisi waache kudeal vyema na watu amabo wanasababishia wengine madhara vifo na hasara.
Hata hao Panya Road wanaofanya uhalifu sheria zipo wakikutwa na hatia wanaadhibiwa sawa na sheria inavyosema kuna kifungo adhabu ya kifo , kifungu cha maisha ,miaka 30 na adhabu zingine . Kwanini wasishtakiwe kwa mujibu wa sheria wajibu wa Polisi ni kufanya upelelezi na uchunguzi kuisaidia Mahakama kufanya maamuzi sio kuuwa watuhumiwa.
sheria inasema mtu mpaka akutwe na hatia inayeoweza kumweka matatani ni pale itakapothibitika bila shaka kwamba yeye kwa kushiriki au kusaidia kutenda kosa fulani kwa vielelezo,embu nieleze kwa aina ya uhali panyaroad wanavyofanya ni lini utakuja kumkuta na hatia???
Kama tunaona hakuna haja ya kuchunguza na kushtaki Polisi washinikize sheria zibadilishwe ili iwe rahisi wao kufanya wanachokifanya , hakuna mtu anatetea wanalifu
sheria ndizo zitabadilika,lakini wahalifu na uhalifu na polisi watabaki vile vile,point yako na maandishi tu kitabuni yafuatwe!!!unahisi wanaonewa sababu sheria tu haisemi hivyo!!!
,ninachotaka utaratibu ufuatwe ktk kupambana na uhalifu na kama sheria zetu ni Butu basi tuzibadili na sio Polisi kuchukua hatua ya kuuwa Watuhumiwa bila kuwapeleka mahakamani.
mahakamani hapelekwi mtu kama anakwenda kuchukua mgao wa shati kaka,ni zoezi refu.sheria wacha zibaki hivyo maana hata uwezo wa kuhudumia wafungwa hatuna.
 
Kama sheria imeshindwa kumaliza panya road acha njia zilizo nje ya sheria zijaribiwe.Siwapendi polisi lakini ninawachukia zaidi hao watoto wasela mavi.Wao wanaumiza,wanaiba na wanaua kirahisi tuu..kisela mavi tuu.Hapana,wauawe tuu.Tena operation iendelee hata miezi sita,vibaka wote polisi wamalizane nao kihunihuni hivyohivyo....Muhimu ni kuwa wahakikishe ni watu sahihi,na nina uhakika polisi wanawajua na hadi kupewa kibali cha kuwamaliza ni lazima wanajiridhisha kwa kiasi kikubwa..Hatuwezi kuishi kwa kuhofia masela mavi tuu eti...wapigwe risasi wote.Pumbavu sana
 
Unaota ndoto ya alinacha mkuu.
Dola inapofanya kazi yake Kwa ajili ya kulinda amani na usalama wa nchi kamwe hakuna mtu anayeweza kushitakiwa.

Huwezi kumshtaki Obama Kwa sababu ya vita au Bush. Walifanya Yale Kwa ajili ya uslama wa nchi yao na Mali zao.

Hata wewe ukiwajulikana kuwa unawaunga mkono Panya rod watakula kichwa.

Labda ujifiche TU huku kwenye uhuru wa KUTUKANA na kusema chochote.

Hali ya Jiji imerejea wewe unaleta siasa hapa.?

Rwanda ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika lakini amani Ile haikujengwa Kwa maneno Bali vitendo. Eti tukemee uhalifu. Sijui upuuzi Gani bila kuchukua hatua Kali. Rwanda imefikia pale Kwa sababu ya kudili na Wahalifu Kwa nguvu zote.
Mpaka Leo Kigoma Kuna Majambazi Toka Burundi. Kwa Nini hawaingii Rwanda wakaiba na kupora na bunduki zao wanakimbilia Tanzania. Ni Kwa sababu watanzania mtu akishavaa suti mchana tunamuona ni Mtakatifu.
Matokeo yake uhalifu hauishi.

Nondo ni miongoni mwa vinasaba vya kihalifu wa kijambazi Toka Burundi. Tukimsikiliza tutaitumbukiza nchi kubaya kama kwao Burundi.
Miaka ya nyuma majambazi kule Kigoma waliotokea Burundi walikua wanapora na Kubaka.

Kuna watu ni jeuri sana mitaani. Wanabaka watoto wa shule ,wanafira watoto,wanavuta bangi hadharani lakini hatumuoni Mshenzi hata mmoja kama Nondo akisema iundwe tume ikachunguze kiwango Cha uhalifu na mmomonyoko wa maadili na kuomba Polisi waongezewe vifaa vya utendaji au hata kusema kila mitaa zifungwe CCTV Camera kuwabaini Wahalifu. Au kuharakisha vitu kama Vitambulisho vya utaifa. Kuhakikisha kila mtu anajulikana Kwa DNA na Alama za vidole n.k.

Duuu, mkuu Kwahiyo vita ya Burundi ilisababishwa na panya road wa huko? Mkuu hao watu wanaobaka, kuvuta bangi nk ni wa taasisi gani ya kimamlaka ili tuseme hawafanyi sawa?
 
Mbuta , ninachokifanya Nina tetea sheria zetu ,katiba na kanuni .

Niliyoyasema yote ni matakwa ya Sheria zetu ,kama sheria zetu hazifai basi tuzibadili.
Amini bro. Hizo sheria unazotetea zilishafeli kitambo. Na wakiachwa matukio yakaendelea utakuja tens kuwalaumu polisi wameshindwa kazi.. Kuna mdau kakushauri upite kuhoji wananchi wanaowafahamu vizuri hao marehemu tabia na shughuli zao zilikuwa vp. Huenda hata baada ya kujua maisha yao usingekuja post huu Uzi. Kutumia ushahidi wa risiti na duka alilonunua TV haitoshi. Uliza pesa ya kununua TV aliipataje. Utachoka. Acha wauwawe tu kwasababu nao waliua
 
Ndio maana inatakiwa mshukiwa apelekwe mahakamani ukweli wa kosa udhibitike, na adhabu stahiki itolewe. Sio sahihi kuruhusu polisi wasio na weledi kuua watu wanaowatuhumu.
Mpaka kufikia kuuwawa inamaana ukweli wa makosa yao tayari umeshathibitika. Mbona hawajakuuwa wewe, mimi au huyo Nondo?
Wewe unafikiri polisi hawana informs za kutosha juu ya hao wauaji? Unafikiri polisi walipita nyumba ngapi mpaka kufikia nyumba za hao waliowauwa?
Kama ingekuwa ni kuuwa tu basi si wangeanza na nyumba zingine kabla ya kufikia hizo za hao vijana waliofatwa kwao na kwenda kuuwawa?

Tatizo lenu wengi wenu mmekuwa mkiingiza siasa uchwara katika mambo ya msingi. Nina imani kama yule binti alieuwawa bila hatia kule kawe angekuwa ni dada yako wala usingekuja kuandika haya uliyoandika.
Kama Nondo na nyie mnaomuunga mkono mnategemea kupata kura kupitia sakata hili la mauaji ya panya road, basi mjue mmeshindwa mapema kabla hata ya kuanza.

Hakuna mwanasiasa uchwara atakaepigiwa kura kwa sababu ya kuwatetea panya road dhidi ya polisi.

Hawa panya road kabla ya kuanza kuuwawa walikuwa washakamtwa si zaidi ya mara 1 na kuhukumiwa, lkn kila wanapotoka baada ya hukumu huendelea na matendo yao ya kinyama dhidi ya raia wema wasiokuwa na hatia yeyote na matokeo yake wanasababisha mauaji, ulemavu, hasara nk.
 
Mpaka kufikia kuuwawa inamaana ukweli wa makosa yao tayari umeshathibitika. Mbona hawajakuuwa wewe, mimi au huyo Nondo?
Wewe unafikiri polisi hawana informs za kutosha juu ya hao wauaji? Unafikiri polisi walipita nyumba ngapi mpaka kufikia nyumba za hao waliowauwa?
Kama ingekuwa ni kuuwa tu basi si wangeanza na nyumba zingine kabla ya kufikia hizo za hao vijana waliofatwa kwao na kwenda kuuwawa?

Tatizo lenu wengi wenu mmekuwa mkiingiza siasa uchwara katika mambo ya msingi. Nina imani kama yule binti alieuwawa bila hatia kule kawe angekuwa ni dada yako wala usingekuja kuandika haya uliyoandika.
Kama Nondo na nyie mnaomuunga mkono mnategemea kupata kura kupitia sakata hili la mauaji ya panya road, basi mjue mmeshindwa mapema kabla hata ya kuanza.

Hakuna mwanasiasa uchwara atakaepigiwa kura kwa sababu ya kuwatetea panya road dhidi ya polisi.

Hawa panya road kabla ya kuanza kuuwawa walikuwa washakamtwa si zaidi ya mara 1 na kuhukumiwa, lkn kila wanapotoka baada ya hukumu huendelea na matendo yao ya kinyama dhidi ya raia wema wasiokuwa na hatia yeyote na matokeo yake wanasababisha mauaji, ulemavu, hasara nk.

Unachofanya hapa ni kuhalalisha utetezi wako dhidi ya mauaji ya polisi dhidi ya watuhumiwa. Hilo neno siasa ww na wengine mnalitumia ili kuondoa uhalali wa tunaotaka sheria ifuatwe. Polisi wetu wangekuwa na weledi nisingepata shaka juu ya mauaji ya hao washukiwa wa uhalifu. Kwa maneno marahisi siku hizi mtu akitaka sheria ifuatwe ili kutekeleza jambo fulani, basi hiyo ni siasa?
 
Operesheni ya Polisi-Dar es salaam dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road ichunguzwe.

Kukithiri kwa vitendo vya Panya Road Mkoa wa Dar es salaam ,kumezua hofu miongoni mwa jamii kwa makundi hayo kuvamia,kupora na hata kuuwa ,mfano.Kifo cha mwanafunzi wa SJMC(UDSM) Maria Basso kilichotokea tar.14 Sept.2022 saa 2:30 usiku kwao Kawe- Mzimuni.Mungu amlaze mahali Pema.

Matendo haya ya kihalifu ni kinyume na katiba ya JMT- 1977 ibara ya 14,ni kinyume na kanuni ya adhabu sura 16,kifungu cha 287 na 288 (kudhuru kwa lengo la kuiba ) na kifungu cha
196 ,197 kinachohusu kuuwa kwa kukusudia na adhabu yake ni kifo kwa mujibu wa sheria na adhabu hutolewa na mahakama kwa mujibu wa katiba ya JMT- 1977 ibara ya 107 A(1) kwamba mahakama ndicho chombo chenye maamuzi ya mwisho katika utoaji haki.

Jamii na kila mtu tulifarijika tulipoanza kusikia viongozi wa serikali na Polisi wakiahidi kupambana ili kukomesha kadhia na uhalifu huu wa Panya Road kwa mujibu wa sheria.

Kwa kuamini ya kuwa nchi yetu ni nchi inayoamini katika misingi ya utawala wa sheria (Rule of Law),ni wazi kila mwananchi aliamini ya kwamba njia zitakazotumiwa na Polisi kukabiliana na uhalafu huu hazitakuwa kinyume na katiba ,sheria na taratibu bali kwa kutumia maarifa ,elimu na taaluma yao katika upelelezi,uchunguzi na Intejensia na kushughulikia kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20, kifungu cha 4(1,2) na sheria zingine zinazohusu wajibu wa Polisi kuchunguza makosa yote ya jinai na kuyashugulikia kwa mujibu wa sheria".

Jambo la kushangaza sana, ni kauli aliyoitoa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ,Mh.Amos Makalla tar.15 /Sept./2022 alipokutana na wananchi kata ya Zingiziwa ,Chanika Wilaya ya Ilala akisema " Wazazi wenye watoto Panya Road kuanzia leo tar 15/ Sept.2022 ,asipomuona nyumbani mtoto wake ,asihangaike akamtafute Polisi kituoni au Hospital (Monchwari)

Kauli ya Mkuu wa Mkoa Mh.Amosi Makala ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama Mkoa, ilichochea Polisi kujipa mamlaka ya kutuhumu ,kukamata na kuhukumu kwa kutoa adhabu ya kifo. Na hiki ndicho kilichotokea kuanzia tar.16 ,17,18 na 19 Sept. 2022 vijana kadhaa waliotuhumiwa kuwa Panya Road katika maeneo tofauti tofauti waliuliwa na Polisi kwa Risasi na miili yao kupelekwa Muhimbili (Monchwari ) na njia waliyokuwa wakitumia ni kuwatafuta vijana watukutu mtaani waliowahi kuwa na rikodi ya kukamatwa na Polisi huko nyuma aidha kwa tuhuma za Bangi au wizi na kuwakamata kuwapeleka kutuo cha Polisi, na kuwapiga ili wataje na wengine hivyo vijana wengine walikuwa wanakamatwa sababu wametajwa na hatimaye kupigwa Risasi na miili yao kupeleka muhimbili.

Achana na tukio alilotangaza Kamanda Jumanne Muliro la watu 6 waliotuhumiwa Panya Road kuuwawa Makongo Juu tar 18/Sept/2022 .Hilo walitoa sababu zao Polisi kwamba walikuwa wanajihami siwezi zungumzia sababu sijui ukweli wake.

Mimi nitazungumzia matukio ambayo hayajazungumziwa na Polisi ya vijana watatu waliotuhumiwa kuwa ni Panya Road kutoka katika Familia tatu ,huko Tandika waliokamatwa na polisi kutokea nyumbani kwao na kupelekwa kituo cha Polisi Maturubali (Mbagala) wakauliwa kwa kupigwa Risasi na maiti zikapelekwa muhimbili (Monchwari) ,kinyume kabisa na katiba ya JMT- 1977 ibara ya 14 na ibara ya 107 A(1) kinyume,pia ni kinyume kabisa na sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kifungu cha 196 na 197, kinyume kabisa na kanuni za Jumla za Jeshi la Police (Police General Order-PGO) kifungu cha 4, kifungu cha 15,kifungu cha 16 (kifungu hiki kinaelezea kuhusu Police kutumia nguvu inapohitajika kifungu hiki pia hakikuzingatiwa ,sababu watu walipigwa Risasi za shingo /Unlawful killings), kifungu cha 19,kifungu cha 20, kifungu cha 27, kifungu cha 28, kifungu cha 33 na kifungu cha 34 lakini pia ni kinyume kabisa na Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 kifungu cha 4(1,2),ni pia na sheria ya inquest act sura ya 24 , kifungu cha 14(1)(c).

Kama mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT Wazalendo Taifa na Waziri Kivuli wa vijana ACT Wazalendo ,Jana tar.28 /Sept/2022 niliamua kufuatilia familia baadhi ambazo zimepoteza vijana wao waliotuhumiwa kuwa Panya Road ili nipate kujua zaidi kuhusu yaliyojificha katika Operesheni hii ya Polisi .

Nilipata fursa kufika katika Familia 3 ,zote zipo Tandika,mtaa wa Nyambwela.

Familia ya kwanza.

Hii ni Familia ya Bi.Amina Allawi Alli ,ambaye mtoto wake aliyeuwawa alikuwa anaitwa Amiry Athuman Hassan , umri miaka 25 alikuwa akiishi na wazazi wake Tandika mtaa wa Nyambwela.

Kwamba tarehe 17/09/2022 ,saa 10 usiku-Alfajiri Polisi walivamia nyumbani kwao wakigonga mlango kwa nguvu,kusukuma na kufanikiwa kuingia ndani ,wakavunja milango ya vyumba vitatu wakimtafuta huyo kijana Amiry waliomtuhumu kuwa ni Panya Road na mwizi,wakamkuta ndani amelala wakamuamsha kwa vibao na kumwambia yeye ni mwizi hata TV waliyoikuta ndani kwamba ni ya wizi wakamchukua yeye na TV wakaichukua.

Mtuhumiwa alijiaribu kujitetea kwamba hana hatia na hata TV hiyo alinunua Dukani Tandika ,Duka la Gaza Electronics tar 29/05/2022 na Risiti anayo ,Polisi hawakusikia wakaondoka nae.

Palipo kucha wazazi walifuatilia katika vituo vyote vya Polisi Makangarawe, Chang'ombe,Maturubali,Stakishari ,Tazara hadi Central bila mafanikio siku ikaisha bila mafanikio, tar 18 ,Sep.2022 wakamkia tena Kituo cha Maturubali-Mbagala sababu jana yake walimuona Polisi mmoja ambaye alikuwa miongoni mwa waliomkamata kijana wao hapo Maturuba,wakiwa Kituo cha Polisi Maturubali walijibiwa waendelee kutafuta vituo vingine au waende Muhimbili Monchwari, walienda muhimbili na kweli walikuta maiti ikiwa na alama mbili za Risasi shingoni.

Walinyimwa kupewa Maiti hadi waende na Polisi ,ikabidi wakarejea Kituo Cha Polisi Maturubali -Mbagala kuomba waende na Polisi ili wapate Maiti ya mtoto wao ,Polisi alihitaji fedha ya nauli elf 20 ndio wakaenda nae kutoa Maiti ya kijana wao,na Muhimbili waliombwa pia kulipa fedha ili kutoa Maiti.

Nilichukua hatua ya kufuatilia hilo Duka ambalo marehemu alinunua hiyo TV ambayo Polisi waliichukua kwa kusema ni ya wizi ,nilipata Duka hilo lipo Tandika ,linaitwa Gaza Electronics karibu na Stendi ya Gari za Mbezi ,niliuliza wakakiri kwamba ni kweli ni Risiti ya Duka lao na huyo kijana ni kweli walimuuzia TV hiyo aina ya Solar Max inch.32 .

Na niliamua kumtafuta Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Nyambwela anaitwa Ndug.Bushiri Ali Napwiri kumuuliza kuhusu tukio hili akasema yeye alienda Polisi Kituo cha Maturubali-Mbagala akiwaambia huyo kijana Amiry hana tabia hizo kwa sasa,wamuache ni Kijana mwema.

Polisi walimjibu Mwenyekiti Bushiri akubali wamuache huyo kijana Amiry ili wamkamate yeye (Mwenyekiti) kumuweka lock up, Mwenyekiti ikabidi aondoke na hata Kijana Amiry alipouwawa Mwenyekiti alipewa taarifa na Polisi kwamba kijana tayari ameuwawa, Mwenyekiti anasema aliogopa kuipa familia taarifa sababu hakujua aanzaje.

Familia nyingine.

Familia nyingine ni ya Bi.Asha Ally na kaka yake Ndug.Swedy Ally Shoo ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi (CCM) huko Kiwalani anapoishi sasa.Bi Asha Ally alikuwa na watoto wawili tuu mmoja wa kike na mwingine wa kiume aliyeuwawa, alikuwa anaitwa Khatibu Said Kabwele au Tosha.

Kwamba tar 17/Sept/2022 saa 12 Asubuhi,Polisi walifika wakigonga mlango ,wakiomba kuongea na huyo kijana Khatibu au Tosha waliulizwa wao ni nani, wakasema ni Polisi wanaongea nae tuu wanamuacha akaamshwa na Mama yake ,na Polisi wakaondoka nae wakisema yupo mikono salama atarudi ikapita tar 17,18, tar 19,Sept.2022 baada ya kuzunguka vituoni katika Kituo hicho hicho cha Maturubali-Mbagala walijibiwa waende Muhimbili Monchwari, Polisi alikataa kwenda nao Muhimbili akiomba fedha elf 40 ya nauli wakampa na walipofika Muhimbili Familia ilitoa tena fedha ya kulipia maiti kuhifadhiwa Monchwari na kukuta Maiti ya kijana wao ikiwa na alama za Risasi Begani na katika koromeo.

Tukio lingine.

Kijana aliyefahamika kwa jina la Khalfan Jongo,mkazi wa Sandali-Tandika alifuatwa nyumbani kwa kutajwa na wenzake,akachukuliwa tar 16 ,Familia inasema walikuja kujua baada ya siku kadhaa kupita,wakaenda Muhimbili wakakuta Maiti ya kijana wao ikiwa na alama za Risasi shingoni.

Tukio lingine.

Ni kijana aitwaye Mbwana Kambi,Mkazi wa kata ya Tandika mtaa wa Nyambwela,alikamatwa na sungusungu tar 23 ,Sept.2022 akapelekwa kituo cha Polisi Makangarawe,akaambiwa atoe laki mbili asipotoa anapewa kesi ya Panya Road,hakutoa fedha hiyo hivyo tar 24 /Sept/2022 wakampeleka kituo cha Police Chang'ombe na kesi ya Panya Road,amekaa chang'ombe akipigwa na nyaya hadi tar 27 ,Sept/2022 Ndugu zake walivyofuatilia ndio akaachiwa hajui kama ndugu walitoa fedha au aliachiwa tuu.

Kwa matukio haya,ndio maana nimehitimisha kwa kusema kwamba Operesheni ya Polisi Dar es salaam dhidi ya Panya Road ichunguzwe,kuna viashiria vingi kwamba Polisi hawafanyi uchunguzi, bali wana tuhumu, wanakamata na kuadhibu jambo ambalo ni kinyume na katiba na Sheria nilizozitaja hapo juu, haya mambo yakiachwa yanaweza kupelekea wasio na hatia kukumbwa, lakini pia Polisi kujichukulia Sheria mkononi na kudharau utawala wa Sheria inaweza tengeneza Precedents kwamba hakuna haja ya kuchunguza wala kupeleka Mahakamani ,matokeo yake Haki (Justice) itatoweka, utawala wa sheria utatoweka nchini ,ni kinyume na Kanuni za Jumla za Jeshi la Polisi (PGO) kifungu cha 20, kinachohitaji Polisi kuzingatia dhana ya Presumption of innocence kwamba katika hatua ya kukamata na kupeleleza lazima Polisi ione aliyekamatwa hana hatia hadi itakapothibitishwa na mahakama.

Kama Polisi wanaona uchunguzi na kushtaki mahakamani sio njia sahihi ya kupambana na uhalifu basi wabadili sheria ,Polisi hao hao ndio wajipe mamlaka ya kutuhumu,kukamata , kuhukumu au kuadhibu kwa kifo kama wanavyofanya sasa katika Operesheni hii katika baadhi ya maeneo niliyoyataja.

Hao Polisi waliofanya matendo hayo wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria iwe waliagizwa au walifanya kwa utashi wao ili wawajibike ,lakini pia Tume huru iundwe ili kuchunguza haya matukio ya namna hii katika Operesheni hizi za Polisi,tulinde utawala wa sheria ndio nguzo ya Haki na usawa kwa wananchi na katika Taifa.

Tunaunga Mkono jitihada za Polisi za kupambana Panya Road na uhalifu mwingine wowote ikiwa tuu jitihada hizo za kupambana na uhalifu zitafanyika kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu, kanuni na miongozo tuliyo nayo tofauti na hapo hayo ni mauaji (Extrajudicial Killings).

Mfano,Police wanaweza kujitetea kwamba walitumia nguvu ilipohitajika kwa mujibu wa sheria ya Jeshi la Polisi sura ya 322 na Kanuni za Jumla za Jeshi la Polisi( PGO) kifungu cha 16 , ndio maana hao wakapigwa Risasi ,lakini tujiulize swali je ni kweli kutumia nguvu inapohitajika (Reasonable force) inahalalishwa kwa kumpiga mtu Risasi ya shingo? au kifua?

Hiyo kweli ni Reasonable force? .Kwanini mtu asipigwe ya mguu kama kweli kulikuwa na haja ya kutumia nguvu ili kukabiliana, Je, mtu aliyemchukuliwa kutoka nyumbani kwao na akakubali kutoka kweli kulikuwa na haja ya kutumia hiyo nguvu?

Mashiriki ya Haki za Binadamu ,Chama Cha mawakili -TLS, vyama vya siasa, wanaharakati na kila Mtanzania kwa pamoja tulaani mienendo hii ya Polisi na matendo yao katika kupambana na uhalifu nchini.

Na hatua zichukuliwe ili matendo haya yakome na yasizidi kuota mizizi katika nchi yetu ambayo utawala wa sheria ndio nguzo yetu.

Na Jambo la msingi sana,sasa tuone umuhimu na haja kubwa ya kubadili sheria na mifumo ya Jeshi letu la Police tuwe na Jeshi la Polisi la kisasa (Modern Police Service)/Democratic Police.

Lakini pia ni muda sasa tuwe na chombo kitakacho simamia matendo ,mienendo ya Jeshi la Polisi na kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi kutokana na makosa au matendo ya Polisi dhidi ya wananchi ,chombo hicho kiitwe Independent Policing Oversight Authority -IPOA.

Ahsante,

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT Wazalendo Taifa.

Waziri Kivuli wa vijana, kazi na Ajira -ACT Wazalendo.

29/Sept./2022.View attachment 2371373View attachment 2371374View attachment 2371376View attachment 2371375View attachment 2371377View attachment 2371379View attachment 2371380View attachment 2371378View attachment 2371381
Sisapoti kwa hicho kilichotokea lakini vijana tujaribu kuishi maisha mbali ya kufanya au kujishughulisha na mambo ya kihalifu, mie mwaka jana mwezi wa 8 nilifatwa na polis nyumbani kwangu kwa kutumia simu ya wizi na walikuja na difenda na silaha juu,

Lakini sikufungwa pingu na wala sikupanda difenda yao bali niliwasha gari yangu na tukaongozana mpaka kituoni ambako ndani ya nusu saa tu alikuja,mjumbe,mwenyekiti,na diwani wa ilala kuthibitisha kuwa siyo mhalifu na the way nilivyokamatwa tu sikuguswa hata shati na askari wenyewe wakawa wanakataa kuwa siwez kuwa mhalifu.

Niliandika maelezo na aliyeibiwa mwwnyewe alishangaa na kukataa kata kata kuwa siyo mimi niliyemuibia simu hyo iliyokuwa na thamani ya 1m+,

hapo ukifatilia kwa makini huenda wakawa ni kweli ni panya road au siyo au wanajihusisha na uhalifu na mda mwengine unaweza kuwa syo mfanya uhalifu lakini unavyojiweka katika jamii watu wanakuchukulia kama mhuni,hasa kimavazi,maneno yako,na hata matendo yako unaweza kuwa si mhalifu lakini ni mvutaji bange au muuza bange mkubwa mtaani.

Na usilofahamu ni kwamba hao oye waliouliwa wana record za uhalifu polisi na mpka kuja hapo kukamatwa jua kuwa kuna wajumbe,mwenyekiti au askari jamii wamewapoint hao watu
 
Huko Kunyongwa Hadi kufa kutokane na mchakato na maamuzi ya Mahakama kama sheria zetu zinavyosema ,ninachopinga ni watu humu kuja kutetea Polisi kuuwa watuhumiwa,sio sahihi na tunatengeneza tatizo kubwa sana hapo baadaye . Maana ya uchunguzi na upelelezi wa Polisi na kushtaki maana yake Mahakama ndio chombo Cha kutoa Haki ,sio Polisi kuuwa watuhumiwa.
Nondo you're more than this bro.

Please respect yourself!

Suala la Demokrasia mnalitumia vibaya ndugu zangu!

Hata hizo nchi mnazoziita za kidemokrasia kuna muda ukifika unakuwa muuaji WA raia unauawa Tu!

Ghaddafi aliuawa na Marekani mnaesema ni Baba WA Demokrasia.

Sadam Hussein alikuwa raisi Halali WA Iraq akauawa na USA.

Ninaelewa mapungufu ya Jeshi la police Ila Kwa hili kwakweli Acha panya road wauawe!


Ni Sawa na kule kigoma Kuna majambazi wanaua halafu eti wakamatwe wapelekwe mahakamani. Hapana. Ni Shaba Kwa shaba

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Operesheni ya Polisi-Dar es salaam dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road ichunguzwe.

Kukithiri kwa vitendo vya Panya Road Mkoa wa Dar es salaam ,kumezua hofu miongoni mwa jamii kwa makundi hayo kuvamia,kupora na hata kuuwa ,mfano.Kifo cha mwanafunzi wa SJMC(UDSM) Maria Basso kilichotokea tar.14 Sept.2022 saa 2:30 usiku kwao Kawe- Mzimuni.Mungu amlaze mahali Pema.

Matendo haya ya kihalifu ni kinyume na katiba ya JMT- 1977 ibara ya 14,ni kinyume na kanuni ya adhabu sura 16,kifungu cha 287 na 288 (kudhuru kwa lengo la kuiba ) na kifungu cha
196 ,197 kinachohusu kuuwa kwa kukusudia na adhabu yake ni kifo kwa mujibu wa sheria na adhabu hutolewa na mahakama kwa mujibu wa katiba ya JMT- 1977 ibara ya 107 A(1) kwamba mahakama ndicho chombo chenye maamuzi ya mwisho katika utoaji haki.

Jamii na kila mtu tulifarijika tulipoanza kusikia viongozi wa serikali na Polisi wakiahidi kupambana ili kukomesha kadhia na uhalifu huu wa Panya Road kwa mujibu wa sheria.

Kwa kuamini ya kuwa nchi yetu ni nchi inayoamini katika misingi ya utawala wa sheria (Rule of Law),ni wazi kila mwananchi aliamini ya kwamba njia zitakazotumiwa na Polisi kukabiliana na uhalafu huu hazitakuwa kinyume na katiba ,sheria na taratibu bali kwa kutumia maarifa ,elimu na taaluma yao katika upelelezi,uchunguzi na Intejensia na kushughulikia kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20, kifungu cha 4(1,2) na sheria zingine zinazohusu wajibu wa Polisi kuchunguza makosa yote ya jinai na kuyashugulikia kwa mujibu wa sheria".

Jambo la kushangaza sana, ni kauli aliyoitoa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ,Mh.Amos Makalla tar.15 /Sept./2022 alipokutana na wananchi kata ya Zingiziwa ,Chanika Wilaya ya Ilala akisema " Wazazi wenye watoto Panya Road kuanzia leo tar 15/ Sept.2022 ,asipomuona nyumbani mtoto wake ,asihangaike akamtafute Polisi kituoni au Hospital (Monchwari)

Kauli ya Mkuu wa Mkoa Mh.Amosi Makala ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama Mkoa, ilichochea Polisi kujipa mamlaka ya kutuhumu ,kukamata na kuhukumu kwa kutoa adhabu ya kifo. Na hiki ndicho kilichotokea kuanzia tar.16 ,17,18 na 19 Sept. 2022 vijana kadhaa waliotuhumiwa kuwa Panya Road katika maeneo tofauti tofauti waliuliwa na Polisi kwa Risasi na miili yao kupelekwa Muhimbili (Monchwari ) na njia waliyokuwa wakitumia ni kuwatafuta vijana watukutu mtaani waliowahi kuwa na rikodi ya kukamatwa na Polisi huko nyuma aidha kwa tuhuma za Bangi au wizi na kuwakamata kuwapeleka kutuo cha Polisi, na kuwapiga ili wataje na wengine hivyo vijana wengine walikuwa wanakamatwa sababu wametajwa na hatimaye kupigwa Risasi na miili yao kupeleka muhimbili.

Achana na tukio alilotangaza Kamanda Jumanne Muliro la watu 6 waliotuhumiwa Panya Road kuuwawa Makongo Juu tar 18/Sept/2022 .Hilo walitoa sababu zao Polisi kwamba walikuwa wanajihami siwezi zungumzia sababu sijui ukweli wake.

Mimi nitazungumzia matukio ambayo hayajazungumziwa na Polisi ya vijana watatu waliotuhumiwa kuwa ni Panya Road kutoka katika Familia tatu ,huko Tandika waliokamatwa na polisi kutokea nyumbani kwao na kupelekwa kituo cha Polisi Maturubali (Mbagala) wakauliwa kwa kupigwa Risasi na maiti zikapelekwa muhimbili (Monchwari) ,kinyume kabisa na katiba ya JMT- 1977 ibara ya 14 na ibara ya 107 A(1) kinyume,pia ni kinyume kabisa na sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kifungu cha 196 na 197, kinyume kabisa na kanuni za Jumla za Jeshi la Police (Police General Order-PGO) kifungu cha 4, kifungu cha 15,kifungu cha 16 (kifungu hiki kinaelezea kuhusu Police kutumia nguvu inapohitajika kifungu hiki pia hakikuzingatiwa ,sababu watu walipigwa Risasi za shingo /Unlawful killings), kifungu cha 19,kifungu cha 20, kifungu cha 27, kifungu cha 28, kifungu cha 33 na kifungu cha 34 lakini pia ni kinyume kabisa na Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 kifungu cha 4(1,2),ni pia na sheria ya inquest act sura ya 24 , kifungu cha 14(1)(c).

Kama mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT Wazalendo Taifa na Waziri Kivuli wa vijana ACT Wazalendo ,Jana tar.28 /Sept/2022 niliamua kufuatilia familia baadhi ambazo zimepoteza vijana wao waliotuhumiwa kuwa Panya Road ili nipate kujua zaidi kuhusu yaliyojificha katika Operesheni hii ya Polisi .

Nilipata fursa kufika katika Familia 3 ,zote zipo Tandika,mtaa wa Nyambwela.

Familia ya kwanza.

Hii ni Familia ya Bi.Amina Allawi Alli ,ambaye mtoto wake aliyeuwawa alikuwa anaitwa Amiry Athuman Hassan , umri miaka 25 alikuwa akiishi na wazazi wake Tandika mtaa wa Nyambwela.

Kwamba tarehe 17/09/2022 ,saa 10 usiku-Alfajiri Polisi walivamia nyumbani kwao wakigonga mlango kwa nguvu,kusukuma na kufanikiwa kuingia ndani ,wakavunja milango ya vyumba vitatu wakimtafuta huyo kijana Amiry waliomtuhumu kuwa ni Panya Road na mwizi,wakamkuta ndani amelala wakamuamsha kwa vibao na kumwambia yeye ni mwizi hata TV waliyoikuta ndani kwamba ni ya wizi wakamchukua yeye na TV wakaichukua.

Mtuhumiwa alijiaribu kujitetea kwamba hana hatia na hata TV hiyo alinunua Dukani Tandika ,Duka la Gaza Electronics tar 29/05/2022 na Risiti anayo ,Polisi hawakusikia wakaondoka nae.

Palipo kucha wazazi walifuatilia katika vituo vyote vya Polisi Makangarawe, Chang'ombe,Maturubali,Stakishari ,Tazara hadi Central bila mafanikio siku ikaisha bila mafanikio, tar 18 ,Sep.2022 wakamkia tena Kituo cha Maturubali-Mbagala sababu jana yake walimuona Polisi mmoja ambaye alikuwa miongoni mwa waliomkamata kijana wao hapo Maturuba,wakiwa Kituo cha Polisi Maturubali walijibiwa waendelee kutafuta vituo vingine au waende Muhimbili Monchwari, walienda muhimbili na kweli walikuta maiti ikiwa na alama mbili za Risasi shingoni.

Walinyimwa kupewa Maiti hadi waende na Polisi ,ikabidi wakarejea Kituo Cha Polisi Maturubali -Mbagala kuomba waende na Polisi ili wapate Maiti ya mtoto wao ,Polisi alihitaji fedha ya nauli elf 20 ndio wakaenda nae kutoa Maiti ya kijana wao,na Muhimbili waliombwa pia kulipa fedha ili kutoa Maiti.

Nilichukua hatua ya kufuatilia hilo Duka ambalo marehemu alinunua hiyo TV ambayo Polisi waliichukua kwa kusema ni ya wizi ,nilipata Duka hilo lipo Tandika ,linaitwa Gaza Electronics karibu na Stendi ya Gari za Mbezi ,niliuliza wakakiri kwamba ni kweli ni Risiti ya Duka lao na huyo kijana ni kweli walimuuzia TV hiyo aina ya Solar Max inch.32 .

Na niliamua kumtafuta Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Nyambwela anaitwa Ndug.Bushiri Ali Napwiri kumuuliza kuhusu tukio hili akasema yeye alienda Polisi Kituo cha Maturubali-Mbagala akiwaambia huyo kijana Amiry hana tabia hizo kwa sasa,wamuache ni Kijana mwema.

Polisi walimjibu Mwenyekiti Bushiri akubali wamuache huyo kijana Amiry ili wamkamate yeye (Mwenyekiti) kumuweka lock up, Mwenyekiti ikabidi aondoke na hata Kijana Amiry alipouwawa Mwenyekiti alipewa taarifa na Polisi kwamba kijana tayari ameuwawa, Mwenyekiti anasema aliogopa kuipa familia taarifa sababu hakujua aanzaje.

Familia nyingine.

Familia nyingine ni ya Bi.Asha Ally na kaka yake Ndug.Swedy Ally Shoo ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi (CCM) huko Kiwalani anapoishi sasa.Bi Asha Ally alikuwa na watoto wawili tuu mmoja wa kike na mwingine wa kiume aliyeuwawa, alikuwa anaitwa Khatibu Said Kabwele au Tosha.

Kwamba tar 17/Sept/2022 saa 12 Asubuhi,Polisi walifika wakigonga mlango ,wakiomba kuongea na huyo kijana Khatibu au Tosha waliulizwa wao ni nani, wakasema ni Polisi wanaongea nae tuu wanamuacha akaamshwa na Mama yake ,na Polisi wakaondoka nae wakisema yupo mikono salama atarudi ikapita tar 17,18, tar 19,Sept.2022 baada ya kuzunguka vituoni katika Kituo hicho hicho cha Maturubali-Mbagala walijibiwa waende Muhimbili Monchwari, Polisi alikataa kwenda nao Muhimbili akiomba fedha elf 40 ya nauli wakampa na walipofika Muhimbili Familia ilitoa tena fedha ya kulipia maiti kuhifadhiwa Monchwari na kukuta Maiti ya kijana wao ikiwa na alama za Risasi Begani na katika koromeo.

Tukio lingine.

Kijana aliyefahamika kwa jina la Khalfan Jongo,mkazi wa Sandali-Tandika alifuatwa nyumbani kwa kutajwa na wenzake,akachukuliwa tar 16 ,Familia inasema walikuja kujua baada ya siku kadhaa kupita,wakaenda Muhimbili wakakuta Maiti ya kijana wao ikiwa na alama za Risasi shingoni.

Tukio lingine.

Ni kijana aitwaye Mbwana Kambi,Mkazi wa kata ya Tandika mtaa wa Nyambwela,alikamatwa na sungusungu tar 23 ,Sept.2022 akapelekwa kituo cha Polisi Makangarawe,akaambiwa atoe laki mbili asipotoa anapewa kesi ya Panya Road,hakutoa fedha hiyo hivyo tar 24 /Sept/2022 wakampeleka kituo cha Police Chang'ombe na kesi ya Panya Road,amekaa chang'ombe akipigwa na nyaya hadi tar 27 ,Sept/2022 Ndugu zake walivyofuatilia ndio akaachiwa hajui kama ndugu walitoa fedha au aliachiwa tuu.

Kwa matukio haya,ndio maana nimehitimisha kwa kusema kwamba Operesheni ya Polisi Dar es salaam dhidi ya Panya Road ichunguzwe,kuna viashiria vingi kwamba Polisi hawafanyi uchunguzi, bali wana tuhumu, wanakamata na kuadhibu jambo ambalo ni kinyume na katiba na Sheria nilizozitaja hapo juu, haya mambo yakiachwa yanaweza kupelekea wasio na hatia kukumbwa, lakini pia Polisi kujichukulia Sheria mkononi na kudharau utawala wa Sheria inaweza tengeneza Precedents kwamba hakuna haja ya kuchunguza wala kupeleka Mahakamani ,matokeo yake Haki (Justice) itatoweka, utawala wa sheria utatoweka nchini ,ni kinyume na Kanuni za Jumla za Jeshi la Polisi (PGO) kifungu cha 20, kinachohitaji Polisi kuzingatia dhana ya Presumption of innocence kwamba katika hatua ya kukamata na kupeleleza lazima Polisi ione aliyekamatwa hana hatia hadi itakapothibitishwa na mahakama.

Kama Polisi wanaona uchunguzi na kushtaki mahakamani sio njia sahihi ya kupambana na uhalifu basi wabadili sheria ,Polisi hao hao ndio wajipe mamlaka ya kutuhumu,kukamata , kuhukumu au kuadhibu kwa kifo kama wanavyofanya sasa katika Operesheni hii katika baadhi ya maeneo niliyoyataja.

Hao Polisi waliofanya matendo hayo wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria iwe waliagizwa au walifanya kwa utashi wao ili wawajibike ,lakini pia Tume huru iundwe ili kuchunguza haya matukio ya namna hii katika Operesheni hizi za Polisi,tulinde utawala wa sheria ndio nguzo ya Haki na usawa kwa wananchi na katika Taifa.

Tunaunga Mkono jitihada za Polisi za kupambana Panya Road na uhalifu mwingine wowote ikiwa tuu jitihada hizo za kupambana na uhalifu zitafanyika kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu, kanuni na miongozo tuliyo nayo tofauti na hapo hayo ni mauaji (Extrajudicial Killings).

Mfano,Police wanaweza kujitetea kwamba walitumia nguvu ilipohitajika kwa mujibu wa sheria ya Jeshi la Polisi sura ya 322 na Kanuni za Jumla za Jeshi la Polisi( PGO) kifungu cha 16 , ndio maana hao wakapigwa Risasi ,lakini tujiulize swali je ni kweli kutumia nguvu inapohitajika (Reasonable force) inahalalishwa kwa kumpiga mtu Risasi ya shingo? au kifua?

Hiyo kweli ni Reasonable force? .Kwanini mtu asipigwe ya mguu kama kweli kulikuwa na haja ya kutumia nguvu ili kukabiliana, Je, mtu aliyemchukuliwa kutoka nyumbani kwao na akakubali kutoka kweli kulikuwa na haja ya kutumia hiyo nguvu?

Mashiriki ya Haki za Binadamu ,Chama Cha mawakili -TLS, vyama vya siasa, wanaharakati na kila Mtanzania kwa pamoja tulaani mienendo hii ya Polisi na matendo yao katika kupambana na uhalifu nchini.

Na hatua zichukuliwe ili matendo haya yakome na yasizidi kuota mizizi katika nchi yetu ambayo utawala wa sheria ndio nguzo yetu.

Na Jambo la msingi sana,sasa tuone umuhimu na haja kubwa ya kubadili sheria na mifumo ya Jeshi letu la Police tuwe na Jeshi la Polisi la kisasa (Modern Police Service)/Democratic Police.

Lakini pia ni muda sasa tuwe na chombo kitakacho simamia matendo ,mienendo ya Jeshi la Polisi na kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi kutokana na makosa au matendo ya Polisi dhidi ya wananchi ,chombo hicho kiitwe Independent Policing Oversight Authority -IPOA.

Ahsante,

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ACT Wazalendo Taifa.

Waziri Kivuli wa vijana, kazi na Ajira -ACT Wazalendo.

29/Sept./2022.View attachment 2371373View attachment 2371374View attachment 2371376View attachment 2371375View attachment 2371377View attachment 2371379View attachment 2371380View attachment 2371378View attachment 2371381
Kinacho nisikitisha ni kuona nyie mnaojiita watetezi wa Haki za Binadamu ni kuwa tayari kuna upande wenu mmeuchagua wa kutetea na mara nyingi mmekuwa mpo upande wa wahalifu.
Imefikia hatua tumeona kuwa watetezi wa Haki za Binadamu ni watetezi wa haki za wahalifu.
Wakati hao vijana wanaojiita Panya road wakifanya uhalifu wao taarifa mlizisikia lakini hamkuonekana kutoka hadharani kukemea dhuluma dhidi ya Haki za Binadamu zinazofanywa na kundi hilo kwa Raia wasio na hatia kwa kuwapora mali zao, kuwajeruhi na hata kuwaua raia wema bila kosa lolote lile.
Ila kwasasa Serikali imeanza kuchukua hatua kikamilifu dhidi ya hao wahalifu ndiyo mnajitokeza sasa kulaani hatua zinazochukuliwa na Serikali dhidi ya kukomesha vitendo hivyo vya uvunjifu wa amani katika jamii..
1. Je, watu mnaojiita watetezi wa Haki za Binadamu mlitaka Taifa lisichukue hatua dhidi ya wahusika wa vitendo hivyo?
2. Mnafurahia vitendo vya uvunjifu wa amani na kuzua taharuki kwenye jamii?
3. Dhumuni lenu mnataka nchi isitawalike kutokana na kukithiri vitendo vya uvunjifu wa Amani?
4. Mna ajenda gani ya siri na makundi haya ya wahalifu?
5. Kuna watu wanafadhili na kuwachagulia ni kundi lipi ndiyo mtetee haki zao?


Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Allah Akbar!! Kwa kweli inasikitisha kusoma habari kama hii katika nchi ambayo ina uhuru kwa mika sitini!Sialaumu sana kwani najua huu ndio uwezo wako.Saudi Arabia inakat watu vichwa kila Ijumaa,je uhalifu umekwisha Saudi Arabia?Uhalifu na kukengeuka katika jamii (social deviance) ni jambo la kawaida na hata ungechukua hatua kali kiasi gani bado wapo watu ambao wataangukia hapo na ndipo ambapo magereza yanahitajika ili angalau watu wajifunze na warekebishwe tabia.La pili ni jamii ya sasa ya Watanzania,ni wa kuonea huruma,leo bodaboda kawa swahiba wa polisi mpka anaandamana kumpongeza Polisi kuua!!!
Someni barua ya kujiuzulu Mwinyi angalau mueleimike.
Abdul Nondo,umetimiza wajibu wako na najua umehatarisha usalam wako.
Acha kumshirikisha Mungu katika matendo yenu machafu. Wakati mnapowatuma panya road wakavunje nyumba zao watu usiku waibe, wajeruhi na wengine wauwe mbona haujagi humu kuwakemea kwa wanayoyafanya? Leo hii na wao kufanyiwa yale wanayofanyia wenzao ndo umekuja haraka haraka kujifanya unaguswa na vifo vyao!

Aisee nyie mnaowatumia panya road na panya road wenu mnachekesha sana. Kifupi mkae mkijua kwamba sasa muda wenu wa kufanya machafu katika nchi yetu umekwisha.
 
Ni mtu mpumbavu sana tu ndiye anayeweza kuandika upumbavu kama huu. Hujui watu tunataka sheria zifuatwe ili kuondoa kosa la watu kuuawa bila makosa? Hujakutana na watu wenye makosa ya kubambikiwa wewe? Hujasikia mpaka rais anayekiri kuwa kuna watuhumiwa wengi wenye makosa ya kubambikiwa? Kwa nini mtu anapokamatwa wasitumie muda kujiridhisha kuwa ni mhalifu na badala yake waue hapo kwa hapo? Kuna kuna mijitu mingine kama wewe ni hatari kuliko hata hao panya road. Mijitu kama wewe mpaka ndugu yako auawe kimakosa ndiyo utasikia inahaha. Idiot!
Tafuta kazi ya halali ufanye kijana, ukikaa nyumban kwa kutegemea kuvamia nyumba za watu usiku uibe, ujeruhi na kuuwa basi na wewe utauwawa tu haijalishi mauaji yako yamefata sheria ua la.
 
Acha kumshirikisha Mungu katika matendo yenu machafu. Wakati mnapowatuma panya road wakavunje nyumba zao watu usiku waibe, wajeruhi na wengine wauwe mbona haujagi humu kuwakemea kwa wanayoyafanya? Leo hii na wao kufanyiwa yale wanayofanyia wenzao ndo umekuja haraka haraka kujifanya unaguswa na vifo vyao!

Aisee nyie mnaowatumia panya road na panya road wenu mnachekesha sana. Kifupi mkae mkijua kwamba sasa muda wenu wa kufanya machafu katika nchi yetu umekwisha.
Watetezi wa panya rodi wanataka kutufikisha huku👇👇👇
 

Attachments

wazungu wanasema"you nailed it all"kwa lugha yetu ya kibantu inamaanisha umemaliza kila kitu!sina cha kuongeza!vijana wanatakiwa wafanye kazi kwa bidii hii njia ya shot cut haisaidii!hata vitabu vyote vinasema mshahara wa dhambi ni mauti
Kweli mkuu, wakati mwingine ni lazima tuelezane ukweli ili kudhibiti tatizo mapema.
Waswahili washasema mficha maradhi kifo humuumbua. Hawa kina Nondo na genge lake tukiwaacha waendelee kuandika upuuzi wao hapa jukwaani, basi tutakuwa tunaendelea kulifuga tatizo la panya road sisi wenyewe.
 
Back
Top Bottom