Nilikuwa napita jioni kuelekea job. Si mnajua night shift zetu walinzi ndugu zangu. Nilikuwa nimempa lift mdanyakazi mwenzangu tukitokea Chanika.
Sasa nafika NMB Gongolamboto nikiwa barabarani jamaa akaniambia ona ile foleni, nikacheki kushoto nakuta foleni ya haja. Nikakumbuka kuwa ni tarehe ya mshahara. Mimi tayari nishatoa kwa simu, nina karibu mwaka siijui ATM machine.
Kwanini niseme niliyoyaona ni aibu kwa watumishi wa umma?
1. Hivi enzi hizi bado mtu na akili zake timamu anapoteza muda kwenye foleni huku makato ukitoa kupitia internet au sim banking yanalingana. Huu muda unaopotea kuokoa mia 4, buku au mia 5 mtu haoni ni hasara.
2. La pili linalotia aibu ni kwamba watumishi wengi wameambatana na wadeni wao ambao ndio walimiliki ATM card zao mpaka siku ya mshahara.
Jamaa yangu aliniambia wale waliokaa kwenye mawe ni wadau wanaowakopesha watumishi na kumiliki kadi zao na kuwapa siku ya mshahara wanapokutana kwenye ATM.
Nikafanya utafiti kuhusu hilo na kujihakikishia kuwa ni kweli. Aibu hii itaisha lini?
Serikali ipeleke wataalamu wa fedha na uchumi kwenye taasisi zake ili kuwafunda watumishi. Pamoja na maslahi ndogo ila mambo mengine yanatokana na ujinga (kukosa elimu ya kiuchumi na fedha) kwa watumishi.
Mtu anashindwa hata kui sacrifice laki 3 kujitosa kwenye ufugaji wa kuku. Aibu.
Je, Hao wataalam Wataalamu itakaowapeleka wao wanalipwa mishahara sawa na walimu ?
Watumishi wote wanaoishangilia CCM wanalipwa mishahara midogo Kwa sababu mabosi wao ni makada wa CCM kuanzia wizarani mpaka chini?
Walimu Wanaosimamiwa na Wakurugenzi ambao ni makada wa CCM.
Fedha zinazoibiwa kwenye Halmashauri Kwa mwaka zingetosha kabisa kuwalipa walimu Mishahara mizuri. Halmashauri ndio majambazi namba Moja kwenye nchi hii wakifuatiwa na wakuu wa Wizara zote kuanzia wenye dhamana za Wizara.
Makada wengine wanaolipwa mishahara midogo ni mapolisi, wakubwa wao ni makada watetezi waliowekwa kulinda maslahi ya CCM na watawala.
Wengine ni Jeshi la Wananchi ,Hawa pona ya maisha ni Kwa sababu ya mission za kimataifa kwenye nchi zenye vurugu. Yaani wanapata angalau fedha za kuweza kuendesha maisha yao na kujenga nyumba na kuwa na usafiri sio Kwa sababu wanalinda amani ya Tanzania Bali Kwa sababu wanalinda amani ya Kongo ,Sudan n.k. Yaani Tanzania inayolindwa na kuwa kisiwa Cha amani lakini Watawala hawaoni umuhimu wa wanaoilinda hiyo amani mpaka wapata mission zinazosimamiwa na UN.
Yaani Wazungu wanapowachukua Wanajeshi wetu kwenda kulinda Wizi wao kule Kongo wanawalipa vizuri kuliko watawala wanaolindwa ili kufanya wizi wao na kujilimbikizia Mali na kupora uchaguzi ili watawala na kuendelea kukwapua Mali za umma.
Kwa hiyo kuwananga walimu au watumishi wa umma ni kuwavunjia heshima. Tuibane serikali iwajali watumishi wake. Nchi za Kiafrika zimatawaliwa na watu waovu kuliko Wakoloni waliotawala Karne ya 19 yaani waingereza. Hata wale Waarabu waliotawala Karne ya 12 mpaka 16 kule Kilwa walikua na utu kuliko Hawa watawala wa Leo wa nchi za Kiafrika.
Hivi unategemea Nini kama Kila Mtanzania unayemuona anatakiwa kujenga nyumba yake au kujengewa na mzazi wake Vinginevyo itabidi apange kwenye soko la pango la nyumba lisilo na usimamizi Wala udhibiti wa serikali.? Kila mtu anawaza kujenga nyumba ampangishie Mfanyakazi au mfanyabiashara Kwa Bei kubwa. Kinachofanyika ni mfanyakazi kukopa ili aepukane na kadhia ya kupanda.Matokeo yake Shule au Hospitali Iko Posta Daktari au Mwalimu anaishi Vikindu .Anaamka saa Tisa usiku na kurudi saa Tano usiku kila siku. Mtu kama huyo hawezi kuwa na akili nzuri ya kuwahudumia watu au hata kujisomea na kupata maarifa zaidi au hapa kupumzisha akili yake .
Ndio maana Tuna watumishi wengi wa ajabu ajabu hata ukiwakuta ofisini hawana Mawazo yenye tija zaidi ya Kupiga dili.
Kila idara ni hovyo Kwa sababu ya mifumo ya kuweka Welfare nzuri Kwa watumishi.
Enzi za mkoloni na mwanzoni mwa miaka ya 62 kabla ya kuja Chama Cha majambazi watumishi wengi walikua ni Darasa la Saba lakini walikua na uwezo mkubwa sana na walifanya kazi Kwa juhudi na ubunifu kuliko wasomi wa Leo waliotelekezwa na serikali ili kila mmoja ale Kwa urefu wa kamba yake akajenge anakojua Kwa pesa atakazojua Mwenyewe pa kuzipata kulingana na kamba yake.
Tusiwalaumu Walimu ,urefu wa kamba yao ni Kukopa ili nao wajenge mana hata kiinwa mgongo nacho serikali imekichukua Kwa Siri.