Niliyoyaona jana kwenye ATM ya NMB Gongolamboto yanatia aibu kwa watumishi

Sio kwamba tunajipendea boss tuna matatizo mengi.... Hela kabla hujaipokea imeisha
Pole sana mkuu nilipoanza kazi miaka hiyoo nilipata shida sana mwaka wa kwanza kuishi kwa kutegemea salary. Baadae wazoefu wakanipa mbinu za kujiongeza... Nikaanza na genge duka, nikaenda kijijini kumchukua dogo aje town tupambane. From genge duka ikawa duka kweli, from duka ikawa duka grocery... Eneo sasa likawa dogo nikatafuta eneo kubwa kwa ajili ya duka na pembeni grocery. Ilifika mahala pesa yote ya mshahara naiweka Benki ili niweze kununua kiwanja na kuanza ujenzi. Hata hivyo, kama ilivyo biashara yoyote kuna changamoto nyingi na kama hauko imara unaweza yumba au kufunga. Mfano dogo baadae ilibidi nimuendeleze kielimu hivyo alivyoondoka niliyempata alinisumbua sana kwa wizi na kutoweka hesabu vizuri, so ilinichukua muda mpaka kumpata mwingine kutoka nyumbani. Hitimisho ni kwamba kama mtumishi salary kamwe haiwezi kukutoa kimaisha... Lazima utafute other sources of income
 
Yataisha.
I hope
Atafika Rais atakayekomesha umaskini na fufukara wa watumishi
Jidanganye, Hakuna Rais anayeweza kuondoka umasikini wa Raia wa Nchi yake.

Zaidi yeye Rais hutengeneza uwezekano wa upatikanaji rahisi wa huduma za kijamii Kama maji, barabara, umeme,elimu Bora na Afya.

Kupata utajiri ni utashi wa mtu binafsi pamoja na bahati yake Ila sio Rais.
 
Hivi najiuliza kitu, ni kweli wengi huwa wanakopa na kuwekeza kadi za benki, sasa ikatokea nineunganisha simbanking na nikakopa nikaweka kadi mwisho wa siku mkopeshaji anabaki na kadi isiyo na msaada.

Wanafanyaje kuepuka kupigwa hawa wakopeshaji?
Wengine wanawapiga, ila waliowengi wanaona hivyo vibanda umiza ni kama mwajiri wao, kadi inakaa huko miaka 3 yaani mtumishi au mstaafu anakuwa mtumwa wa hicho kibanda
 
Kufuga kuku ni mfano tuu wa shughuli yoyote ya kukuingizia kipato kulingana na maeneo ulipo. Mfano kuna rafiki yangu mwalimu kuna mwaka aliniambia anataka kuchukua mkopo wa milioni 10 je aufanyie nini? Nikampa ushauri aje TURIANI Morogoro (mimi huwa nalima huko na kununua mazao) aone shughuli mbalimbali halafu atafanya maamuzi kipi kinafaa? Akaja nikampokea na kuzunguka naye wiki nzima. Mwisho akaamua anunue mpunga na kuweka stoo ili bei ikipanda auze,nami nikamwambia hiyo ni nzuri. Alianza kununua mpunga wakati wa mavuno gunia elfu 35 na baadae ikafika elfu 40. Alinunua gunia 200 na gharama zote yaligharimu milioni 9. Baadae alikuja kuuza wakati bei ya gunia moja imefikia elfu 70 hivyo alipata milioni 14.
 
Ndio akili za kiafrika hizo ulizonazo,hii aibu instokana na serikali fisadi ambazo hazijali wananchi wao
 
Mkuu rudishiako ka avatar picha yako ile Kagame kavaa kofia kama mfugaji
 
Hiyo no.2 inaonyesha jinsi gani ulivyomuongo muongo!
 
Alikua Gill ta mi
 
Pia huwa kuna changamoto, katika utoaji hela, toka benki kwenda kwenye simu; benki inatoka, kwenye simu haifiki, mpaka kuja kuipata hiyo, mtasumbuana sana na benki na inaweza kuchukua mwezi mzima kwa kuandikiana mabarua.
 
Waweke ATM za kutosha
 
Kwani amesema ni Walimu??
 
Je, Hao wataalam Wataalamu itakaowapeleka wao wanalipwa mishahara sawa na walimu ?

Watumishi wote wanaoishangilia CCM wanalipwa mishahara midogo Kwa sababu mabosi wao ni makada wa CCM kuanzia wizarani mpaka chini?

Walimu Wanaosimamiwa na Wakurugenzi ambao ni makada wa CCM.
Fedha zinazoibiwa kwenye Halmashauri Kwa mwaka zingetosha kabisa kuwalipa walimu Mishahara mizuri. Halmashauri ndio majambazi namba Moja kwenye nchi hii wakifuatiwa na wakuu wa Wizara zote kuanzia wenye dhamana za Wizara.

Makada wengine wanaolipwa mishahara midogo ni mapolisi, wakubwa wao ni makada watetezi waliowekwa kulinda maslahi ya CCM na watawala.
Wengine ni Jeshi la Wananchi ,Hawa pona ya maisha ni Kwa sababu ya mission za kimataifa kwenye nchi zenye vurugu. Yaani wanapata angalau fedha za kuweza kuendesha maisha yao na kujenga nyumba na kuwa na usafiri sio Kwa sababu wanalinda amani ya Tanzania Bali Kwa sababu wanalinda amani ya Kongo ,Sudan n.k. Yaani Tanzania inayolindwa na kuwa kisiwa Cha amani lakini Watawala hawaoni umuhimu wa wanaoilinda hiyo amani mpaka wapata mission zinazosimamiwa na UN.
Yaani Wazungu wanapowachukua Wanajeshi wetu kwenda kulinda Wizi wao kule Kongo wanawalipa vizuri kuliko watawala wanaolindwa ili kufanya wizi wao na kujilimbikizia Mali na kupora uchaguzi ili watawala na kuendelea kukwapua Mali za umma.

Kwa hiyo kuwananga walimu au watumishi wa umma ni kuwavunjia heshima. Tuibane serikali iwajali watumishi wake. Nchi za Kiafrika zimatawaliwa na watu waovu kuliko Wakoloni waliotawala Karne ya 19 yaani waingereza. Hata wale Waarabu waliotawala Karne ya 12 mpaka 16 kule Kilwa walikua na utu kuliko Hawa watawala wa Leo wa nchi za Kiafrika.

Hivi unategemea Nini kama Kila Mtanzania unayemuona anatakiwa kujenga nyumba yake au kujengewa na mzazi wake Vinginevyo itabidi apange kwenye soko la pango la nyumba lisilo na usimamizi Wala udhibiti wa serikali.? Kila mtu anawaza kujenga nyumba ampangishie Mfanyakazi au mfanyabiashara Kwa Bei kubwa. Kinachofanyika ni mfanyakazi kukopa ili aepukane na kadhia ya kupanda.Matokeo yake Shule au Hospitali Iko Posta Daktari au Mwalimu anaishi Vikindu .Anaamka saa Tisa usiku na kurudi saa Tano usiku kila siku. Mtu kama huyo hawezi kuwa na akili nzuri ya kuwahudumia watu au hata kujisomea na kupata maarifa zaidi au hapa kupumzisha akili yake .

Ndio maana Tuna watumishi wengi wa ajabu ajabu hata ukiwakuta ofisini hawana Mawazo yenye tija zaidi ya Kupiga dili.
Kila idara ni hovyo Kwa sababu ya mifumo ya kuweka Welfare nzuri Kwa watumishi.
Enzi za mkoloni na mwanzoni mwa miaka ya 62 kabla ya kuja Chama Cha majambazi watumishi wengi walikua ni Darasa la Saba lakini walikua na uwezo mkubwa sana na walifanya kazi Kwa juhudi na ubunifu kuliko wasomi wa Leo waliotelekezwa na serikali ili kila mmoja ale Kwa urefu wa kamba yake akajenge anakojua Kwa pesa atakazojua Mwenyewe pa kuzipata kulingana na kamba yake.

Tusiwalaumu Walimu ,urefu wa kamba yao ni Kukopa ili nao wajenge mana hata kiinwa mgongo nacho serikali imekichukua Kwa Siri.
 
Hii post imehitimisha kila kitu.
Kuanzia sasa hata nikimwona mtumishi wa umma anaishi stand sitamdharau.
Hii serikali ya Tanzania ilishakufa. Haiwezekani umwajiri mtumishi hujui anaishi wapi halafu unampa majukumu ukimtaka awahi kazini.
Mtu akibahatika kuiba atajenga vikindu, Chanika, Kibada au Goba mwisho halafu kazini mbalimbali kinoma.
Hapo atakuwa anapiga timing aibe mzigo mwingine anunue usafiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…