Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

Form six gani Hiace anaita Hiance? Halafu wewe huu uandishi wako ushaharibiwa. Hakuna kitu umebaki nacho. Ndo maana mzee wako alitaka uende jeshini ukakaze misuli ya matako. Umeshalegea sana. Mwanaume hawezi omba saidiwa na mwanamke na hawezi lia eti anamwita mama yake. Wewe ni takataka. Ondoka hapa na uzi wako.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Habari!

Nilipomaliza form 6 zikatoka nafasi za kwenda jeshi wanaita "kwa mujibu" basi nikaangaza macho yangu kwenye orodha nikaona "Ephen - Rukwa"

Basi nikafurahi sana, furaha haikua kwasababu naenda jeshi hapana! Hata mpango nayo nilikua sina ila tu niliona ni bahati jina langu kua kwenye list sababu sio wote uchaguliwa.

Nikawasiliana na marafiki zangu kuna baadhi walichaguliwa pia lkn hakuna niliyechaguliwaa nae kambi moja, nikaanza kusikia story plus video za status, instagram watu wanaeka makuruta wanavyogaragara kwenye matope, mazoezi magumu hadi wanalia, nikapata uoga hapo ikawa mzozo nikasema mimi jeshi siendi kwanza kunyoa kipara hapana.

Mzee akaniambia lazima uende, huko Rukwa mkuu wa kambi ni rafiki yangu hivyo wewe mateso hutoyapata nikafikiria nikaona huyu mzee ananipiga fix ili nijae mimi jeshi siendi.

Ila nikawa nataka sitaki na kilichokua kinanitatiza kwenda ni yale mateso tu niliyokua naona kwenye video.

Kuna siku rafiki yangu akanipigia simu kunishawishi twende ila akaniambia "Ephen twende kambi ya mkoa X achana na Rukwa huko wana mazoezi makali sana" nikamwambia kama hivyo fresh acha nijiandae tutaenda next week sababu deadline ilikua bado. Rafiki yangu nampa jina Anna.

Anna ana kaka ake ni mjeda sasa akawa anatupa tips muhimu za kuzingatia mojawapo alisema tranka tutakalobeba tusijaze vitu vingi tuweke vitu vyepesi ikiwezekana vitu tukanunue kambini hukohuko.

Mimi niliona usumbufu yaani nitoke na tranka tupu vitu nikanunulie kambini? nikanunua vitu vyote nikajaza kwenye tranka. Kumbe yule mjeda alikua na maana yake Aisee bora ningemsikiliza.😂

SIKU YA SAFARI
Tukatoka zetu na Anna tukapanda gari tunaenda kambi ya mkoa X japokua tumepangiwa kambi tofauti kila mtu.

Tupo kwenye gari nina furaha naenda kupata experience mpya pia nilifurahi kwenda mkoa mwingine sababu nimezoea dar tu, safari ilichukua almost masaa 7 tukafika huo mkoa X mjini, gari ndo mwisho.

Sasa wote hatujui nini kinafata hapo Anna yeye tranka lake niseme lipo tupu kabeba vitu muhimu tu, mimi nimejaza hadi kubeba linanishinda.

Tukamfata konda kumuuliza, "Sisi tunaenda kambi X tunaomba utupe muongozo" akatuambia pandeni bajaji hadi kituo flani mkifika kuna hiance zinaenda huko jina la kambi ndo jina la kituo cha kushuka.

Tukafanya kama alivyotuambia, tumeingia kwenye hiance asilimia kubwa wana vipara hivyo nikajua wote tunaenda kambini.

Kule tuliposhuka na gari nilipapenda sana ni kuzuri panavutia hamna pilikapilika nyingi nakumbuka nilimpigia simu mama, akaniuliza umepaonaje nikamjibu kwa furaha ni pazuri nimepapenda akaniambia "ukifika kambini nijulishe lkn ukiona huko mateso yamezidi nipe taarifa nikufate urudi nyumbani"

Basi tulivyokua kwenye Hiance tunaenda huko wilaya yenye kambi mwanzoni nasmile na Anna wangu ghafla akili yangu ikavurugika tuliingia barabara ya vumbi sijawahi ona, gari zima hatuonani, kila mtu kwenye gari katapakaa vumbi hadi kope zote nyeupe ndani ya pua nywele vumbi hapo nikapata sign ninapoenda sio pazuri.

Safari ilichukua kama masaa 3 tukaambiwa wale wa kambini mmefika.

Katika maisha yangu bad moment niliyowahi kuexperience ni hii siku, Tumeshuka tu nikaona njia ya vumbi imekata kulia ni ndefu kama 2km nikasikia sauti "Hapohapo wote chuchumaa tranka kichwani ruka kichurachura uelekeo huu hapa kwenda kambini"
Kudadeq ndo nikajua kwanini niliambiwa niende na tranka tupu

Anna yeye chap kachuchumaa tranka kichwani, mimi machozi yashaanza kunitoka nikamwambia Anna mimi nimeghairi siendi narudi nyumbani, hata sijamaliza sentensi nishakula bao la mgongo kutoka kwa mjeda akaanza kufoka wewe bila shaka umetoka Dar naongea tii Amri kwanini umesimama ? Aya tranka kichwani kuruka uelekeo huu.

Akaja mjeda mwingine akanitwika tranka kichwani hapo nishachuchumaa sikuweza kuimili kuruka na tranka.

Anna akaniambia lete nikusaidie chukua langu, yule mjeda aliona tu hata akinipiga ule mzigo siuwezi na Anna pia hauwezi akamwita mjeda anayejitolea chukua hili tranka wasaidie, basi nikapona hivyo.

Kimbembe kikawa hiyo kichurachura nikiangalia mbele sioni geti, ni mbali almost 2km ndo niruke kichurachura? Hapo machozi yananitoka nalia nkamwambia Anna "mimi namwambia mama anifate siwezi hizi mambo" Anna nae analia Ephen usiondoke ukaniacha mwenyewe bora hivi tupo wote Afadhali.

Nilihisi miguu inawaka moto inataka kupasuka, msafara tupo wengi hadi wanaume wanalia, sasa tulivyoloa vumbi hadi kope mtu ukimuangalia mwenzako unatamani kucheka ukisikilizia maumivu ya miguu unatamani kulia.

Itaendelea......
Katika kazi ambazo zilishanishinda na sizitaki ni kazi zote Zenye nature ya Ulinzi.

Siko interested hata kidogo,zaidi ya kufundishwa matumizi ya silaha ila masuala mengine yote naweza pata mtaani.
 
Kweli kabisa. Wanazani utaanza mazoezi magumu bila kuandaa mwili.
Jeshi kwa hapo nawapa hongera ni kama wana mtaala kabisa na wanajua kabisa lazma mtu wakuandae kabla ya kukupa vitu vizito.

Ningetoka home na wakanianzishia six weeks moja kwa moja, lazma ningezima 😁😁

Ila phase ya uraia tu inakusaidia kuuweka mwili tayari kwa vitu vinavyokuja
 
Hata mimi sikuwa interested kabisaaa ila nilivyoingia kwenye lile geti nikafungua moyo

Sikuwahi kudoji na hata baada ya muda zilipopatikana chance za kutoka, niliwahi toka one time tu. Nilisubiri hadi siku ifike niondoke

Na wajeda baadhi walikuwa wananiheshimu kwa sababu nilikuwa naenda na mfumo na nilikuwa sio lopolopo. Kuna baadhi walinambia kama naweza jifikiria kuingia ila nilijua haiwezekani..

japo nakumbuka ile siku narudi home baba alishtuka na ndugu yangu mmoja alinisahau kabisaa, sikuwahi pata extra care kama ile siku 😁😁😁
Ukifungua moyo unatoboa sasa wewe jifanye umemkumbuka mama, wewe wakishua utajua hujui..
RSM wanaa sijapa kuona..
 
Ukifungua moyo unatoboa sasa wewe jifanye umemkumbuka mama, wewe wakishua utajua hujui..
RSM wanaa sijapa kuona..

mtoa mada ni wa kike ndio maana walimdekeza na kumpoza. Ingekuwa wa kiume unadhani kuna mtu anajali

Kwanza ukilia wanafurahia ili wakukolezee doso. Japo kuna wajeda wapo peace tu ingawa wengi ndo matatizo maana kuna huyo bakabaka toka niingie ile kambi, nilimuona katabasamu mara moja tu na ukikutana nae, unaona sura ya kukutamani kukuhenyesha tu😁😁😁
 
Kwa jinsi nilivyosoma uzi wake mpaka hapa unacomment huyu sio mwanaume ni mwanamke! Soma vizuri mkuu, hadi anasema Kuna mwanajeshi wa kike aliyemuonea huruma wanafanana majina.
JKT na JWTZ nk hawaangalii wanampokea kuwa Mwanamke au mwanaume mziki uko pale pale kupokelewa ni syllabus ya mafunzo ya Jeshi hupokelewi kienyeji uwe mwanajeshi wa kike au kiume wanazingatia syllabus sio matakwa ya mpokeaji au jinsia

Jeshi Wana syllabus kama ya primary au secondary au chuo kikuu kama zilikiukwa huyo aliyedharau hiyo syllabus aweza chukuliwa hatua za kisheria za kijeshii na Mahakama ya kijeshi yaani Court Martial ambayo Ina majaji mawakili waliosajiliwa mahakama ya kiraia na chama chama Cha mawakili Tanzania


ikiwemo kufukuzwa kazi akikukutwa na hatia ya kutozingatia military legal procedures za kuajiri
 
Umenikumbusha mbali bro..
Kukwepa ndege ni hatari, waweza haribu kiuno hivi hivi
Kuna boya mmoja alinipiga nua nika crawl kwenye matope akanipaka majivu mwili mzima alaf akanipigisha hilo tifu la kukwepa ndege akanizungusha kombania nzima masaa mawili

Jamaa alikua anatafuta kujengea jina kupitia mimi maana aliamua tu kunipiga tifu bila sababu
 
Back
Top Bottom