Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

Kwani nilazima kukaa kambini Ndugu Mwandishi!?? Mbona wengi tuko nao huku Buhongwa na Draft pamoja na Shimhaa tunapimiana
Sio lazima mkuu
Ila mimi kua mwanajeshi siwezi yale mazoezi kwangu hapana!
 
Unafikiri ulifundishwa uzalendo jeshini, kuijali nchi yako?

Kwanini hawana sera za kufundisha kilimo cha kisasa, umwagiliaji, kutumia trekta, mbolea, mbegu bora au wanavyo?

Inatakiwa kijana akitoka pale awe mzalendo, mchapakazi, anaweza kujitegemea na kuwa na ujuzi.
Binafsi sijui ila naona JKT hasa hawa Mujibu naona ni upotevu tu wa muda kwa kupima Faida zaidi naona hakuna cha maana ni kupoteza pesa kwa kuwahudumia!!!


May be wale wa kujitolea naona at least!!
 
Binafsi sijui ila naona JKT hasa hawa Mujibu naona ni upotevu tu wa muda kwa kupima Faida zaidi naona hakuna cha maana ni kupoteza pesa kwa kuwahudumia!!!


May be wale wa kujitolea naona at least!!
Mkuu fikiria vizuri kama ulichosema ni sahihi.
 
SEHEMU YA 8
Nikafanikiwa kutoroka hadi jikoni, kule maeneo mengi giza ndo maana sikubambwa
Nikanunua maandazi nikanywa na chai haraka, sasa nikawa naona kuruta wanakimbia wameruhusiwa kwenda kulala
Sasa nikawa nasuuza kikombe fasta na mimi nikalale

Kwa mbali namuona bakabaka anakuja na service man ( wanaojitolea) wetu
Basi service man akasema "Ephen mwenyewe yule pale" moyo ulishtuka ukaenda kasi sana

Nilipokea mvua ya matusi kutoka kwa yule bakabaka halafu mwanamke "Wenzako wapo kombania wewe huku unafanya nini? Nikaongezewa bao la mgongo
"Kuruta naongea unanitizama badala ya kupunguza urefu?'
"Punguza urefu haraka!"
Basi nikachuchumaa ndo kupunguza urefu.

Pembeni kulikua na bomba la maji nikapelekwa pale yakafunguliwa nikaloa chapachapa
"Aya roll uelekeo kombania"
Ilikua ngumu kwangu njia ya kuroll ina kokoto, mimi nina kidonda kibichi gotini kinaniuma na nimefungwa bandage.

"Afande naomba unibadilishie adhabu nina kidonda kibichi"
kuruta unanidindia?
Nikaona huyu anataka kukuza mambo! Nikaanza kuroll goti maumivu kama yote damu zikaanza kutoka na afande hanionei huruma

Kulikua na umbali hadi kombania ila nikafika!
Wenzangu walivyoniona wakaanza kunisonya wanalalamika.
Kombania zipo A hadi D kama sijakosea, A, C na D wakaruhusiwa kwenda kulala muda mrefu tu.
Na kombania B wanaume waliruhusiwa pia kasoro wasichana ndo hawakuruhusiwa sababu hawakutimia
Nani hakutimia ni mimi hapa.

Jeshini ikitokea kuruta ametoroka kwenye kombania hamuendi kulala hadi apatikane.
Muda huo saa 7 usiku damu zinatoka gotini maumivu hadi nalia.

"Sasa sikieni! Leo mnakesha na mimi hapa! mpaka asubuhi!
Nyie si hamjaiva, mlimtuma mwenzenu akanywe chai muda wa kombania haya wote kichurachura mnaenda na kurudi hadi kukuche, Wazii kuruta?

Kuruta wenzangu wakaanza kulia "Afande sisi hatujamtuma! Tunaomba tukalale"

Nauliza tena "Wazii kuruta?"
Tukaitikia waziii Afande!
Huku wenzangu wananitukana nimewaponza hawaendi kula utawala (kula utawala- kupumzika)

Bakabaka sasa "Kila mtu akachukue ndoo ya maji mje kumwaga hapa na poda ya kutosha mje mumpake usoni" 😄 (Poda-Vumbi)
Nililia sana basi wakaenda kuchukua poda wakanipaka, maji yakamwagwa kwenye vumbi kukawa na tope nikaambiwa,
"Wewe siumekuja hapa kula! Aya twende kama kambare"
Nikaanza kuroll kwenye tope.

Yule afande alikua na roho ngumu sanaaa
"Aya kuruta simama hapo uanze kupiga makofi wao wanafatisha"

Nikaanza nikipiga kofi wanasimama nikipiga wanalala chini! Ngoma ilienda hadi afande akasema nasimama pale nyie endeleeni!

Kumbe aliondoka sisi tukaendelea tukidhani anatuangalia, tumeshtuliwa na filimbi ya alfajiri

Tulikesha tena na wenzangu!!
Walinichukia! siku hio nikawa na kazi ya kuwaomba msamaha. Niliwafanya wasilale tena kwa usiku mwingine ukijumlisha na siku 7 za mwanzo.

Itaendelea.......

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Daaa Poleee sanaa kwa siku hii ambayo pia uliwaponza wenzako ephen
 
Mkuu fikiria vizuri kama ulichosema ni sahihi.
Najitahidi mkuu ila nashindwa kuoanisha kabisa hizo faida!!

Uzalendo kama Faida na lengo namba moja Graduates wengi ndio majizi haswaa huku kazini!! Viongozi wetu wengi ambao wao walikaa JKT mwaka mmoja hawa ndio kabisa kila siku tunasikiliza report zao kwa CAG!!

Yaan ukiangalia Inputs ni kubwa ila Outputs ndogo

May be jaribu basi kunishawishi nikuamiamini jaribu mkuu!!
 
Najitahidi mkuu ila nashindwa kuoanisha kabisa hizo faida!!

Uzalendo kama Faida na lengo namba moja Graduates wengi ndio majizi haswaa huku kazini!! Viongozi wetu wengi ambao wao walikaa JKT mwaka mmoja hawa ndio kabisa kila siku tunasikiliza report zao kwa CAG!!

Yaan ukiangalia Inputs ni kubwa ila Outputs ndogo

May be jaribu basi kunishawishi nikuamiamini jaribu mkuu!!
Ufisadi ni utamaduni
Wazalendo wapo, ila wengine wanaanza kazi wakiwa wazalendo ila mwisho wa siku wanasema wenzangu wanaiba mimi nasubiri nini?
Faida zipo nyingi soma post namba 815

Una hoja usikilizwe!
 
Mkuu fikiria vizuri kama ulichosema ni sahihi.
Hajaelewa. Nadhan jkt ni kitu ambacho hatujakitumia ipasavyo, nataman nchi nzima wangehusika kwenda jkt, jkt inazalisha, watz sote tungehusika kuzalisha, nashangaa sana vijana kukaa mtaani vijiweni kuna vijana wana vipaji wamekaa navy, kumbuka usemi punda haendi bila bakora, ndio maana hamkuwapenda waliokuwa wanajitolea, kwa sabab wangesaidia sana nchi hii kwenda mbele.


Vijana eti wanajiajiri kwenye bodaboda, nitamshukuru rais ambaye atapata upeo wa kuwapeleka vijana jkt wakazalishe badala ya kuwafanya kuwa bodaboda, huu usafiri (boda boda)unatakiwa uangaliwe upya ufutwe uwekwe mfumo mzur wa bodaboda, kwanza nadhan zipande bei, boda ikiuzwa 10 min hutaona vijana wakiingia huko. Pili wawe na lesseni na ilatikane kwa gharama kubwa, pkli wawe closely observed.

Kundi kubwa lenders jeshini wakazalishe
 
Back
Top Bottom