Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

Nakumbuka nilienda kambi ya Kanembwa Kigoma kulikuwa na afande wanamwita " Cyborg" yule mwamba alikuwa hacheki alooh na anaogopeka balaa.

Mazoezi ya kule acha tuu kuna afande alikuwa anaitwa John Magesa na mwingine Dakanyama walifanya maisha yetu ya jeshi yawe magukumu.

Nilipata rafiki basi kwenye mchakamchaka alikuwa anapenda sana kuniimba " Sio lako Trudie la mchina hilooooo, umechoma sindano la mchina hilooooo, umepaka mafuta la mchina hiloooo" Nimekumbuka mbali sana
 
Kwahiyo tunda ephen_ ilikulazimu umpe tunda service man ili kukwepa adhabu? Na hiki ndiyo kinatisha wazazi na wale wote ambao hatujaenda jeshini. Kuna tabia mbaya.

Katika simulizi yako yote hujaeleza faida yoyote ya maana uliyoipata huko jeshini kwa maana ya ujuzi ama maarifa.

Kweli mtu unaenda kupakaa matope, kukesha ukiimba na kichimbq visiki ktk karne hii? So what?

Nilitegemea mnafundiahwa namna ya kubadilisha mbegu za mimea ziwe ziendane na mabadiliko ya tabia nchi. Mngefindishwa namna bora ya kufuga, kulima na ubunifu wa kutengeneza silaha za kisasa.

Kuoga tope? Kukesha? Halafu mnaishia kugawa tunda kwa service man!!!!?? Aghhhj!! No! No!
Mimi nadhani jeshini philosophy muhimu ni kuufanya mwili uondokane na uvivu! Kiasili mwili ni mvivu kufanya kazi na hapo ndo wengi wanafeli. Kwa mfano! Ili ufaulu mitihani ya darasani lazima usome! Ukitaka kusoma mwili hautaki unakuletea usingizi! Ili ufaulu inakutaka uamke asubuhi saa 11 kufanya maandalizi, n.k. kwahiyo nadharia ya kuushughulisha mwili jeshini ni muhimu! Mambo ya maharifa na technolojia utakuta darasani/shuleni
 
kabla ya kuingia kambini nilifuatilia vitu vingi kuhusu maisha ndani ya kambi jeshini, hvyo nilifungua moyo kabla hata ya kugusa lango la kambi ,nilifurahia kila kitu jeshini isipokiwa kitu kimoja tu mkianza rasmi zile wiki 6 mwendo wa kuruti huwa unabadilika mnatembe kwa mwendo wa (kunyanyukua) kuinua goti usawa wa kidevu huku ukiimba UP, UP, UP, UP. yaani hiko kitu ndo kilikuwa mateso makuu kwangu
 
KUNA COMMENTS ZINALALAMIKA HAWAJAONA UMUHIMU WA JESHI KATIKA STORY NI KAMA VILE MTOTO ANAPOTEZA MUDA...
Sikuainisha umuhimu nilijua wote kwa kusoma story A to Z mngeona umuhimu watoto tunaoupata kule.

FAIDA WATOTO WANAZOZIPATA KULE
1. Ukakamavu na utimamu wa akili na mwili; Nyakati ngumu kule zinaimarisha akili zetu uwezo wa kufikiria mambo kwa upana. Mazoezi kama viroba, mabio inaupa mwili utimamu.

2.Kuongeza nidhamu na utii; Kwa wazazi waliopokea watoto baada ya kutoka jeshi watakua shahidi wa hili, tukirudi tunakua wasikivu zaidi ya mwanza kabla ya kwenda jeshi.

3. Kujifunza kazi za mikono/kazi za nyumbani
Mfano mzuri mimi, nina uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja bila kuhisi kuchoka. Experience hii nilianza kuipata jkt mtu unapewa uwanja ufagie ukubwa kama nusu ya kiwanja cha mpira.

4. Ukitoka jeshi unakua na uwezo wa kuishi na watu wenye tabia tofautitofauti.

5. Inaongeza uzalendo na uelewa mpana kwa nchi yetu.


6. Inakuza vipaja na mafunzo mapya kwenye sanaa.
Mfano, Anna anapenda kuimba kipaji chake kilizidi kukuzwa, kuna walimu wa mziki kule ngoma coy.
Mimi nilipata mafunzo mapya ya karate kitu ambacho sikua nacho kabla ya kwenda jeshi.

7. Inaongeza ujuzi wa kujilinda dhidi ya adui na uwezo wa kulenga shabaha.
Kupitia mafunzo ya silaha kule range.
Asilimia kubwa ya waliotoka jeshi wapeni silaha muone kama hawajawafyatua.

8. Inatoa mafunzo ya kilimo
Kwenye mashamba/ bustani zao zinazopatikana kambini.
Mfano mimi nyumbani nina bustani yangu ya matembele, nimepanda na mahindi.

9.Inampa mtoto uwezo wa kujitegemea.
 
BONUS
Mwanzoni wiki 6 mjeda namesake alinifata kuniaga, kwa kumwangalia hakua sawa kama amelia muda mrefu.

"Mimi naondoka kwaheri"
Sababu gani nikamuuliza
"Kuna nafasi za kwenda course ya kuajiriwa migration zilitoka, nikapata nafasi, lakini nimepimwa nina mimba hivyo safari yangu imeishia hapa"

NIlimuonea huruma katika kumchimba ndo nikagundua
Alipata mimba ya yule bakabaka yeye akawa anaficha, nafasi zilivyotoka jina lake lipo ilibidi amwambie mchumba ake.

Bakabaka akamwambia unaitoa ili upate nafasi ya kwenda mafunzoni au unabaki nayo?
Yeye akachagua kubaki nayo akose jeshi!
Alikua ameshajitolea zaidi ya miaka miwili.

Nilimuonea huruma, nilimuona ana moyo mzuri sana! Mwingine angeitoa ili akamilishe ndoto yake ya kua mwanajeshi.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini

Aisee mi ningeitoa mapema sana uwiii
 
Nishajiapiza, nikipata mtoto wa kike mzurii yani ule uzuri wa kila mtu lazma ageuze shingo halafu akawa laini na moyo wa ustahimilivu hana.
Jeshi hatoenda labda waje wamchukue wakiwa na mitutu mizito

Kwanini mkuu
Mdogo wetu wa mwisho ni pisi kali rangi ya mtume akienda huko nna wasiwasi wajinga wasije muharibu uwiii[emoji2304]
 
@
SEHEMU YA 2
Ilipoishia..........
Sasa tulivyoloa vumbi hadi kope mtu ukimuangalia mwenzako unatamani kucheka ukisikilizia maumivu ya miguu unatamani kulia......

Endelea
Mpaka tumefanikiwa kulifikia geti kuna kuruta waliozimia njiani, wengine kilio kikubwa mimi mmojawapo Aisee wanajeshi waheshimiwe sio kwa mazoezi yale.

Getini tukaambiwa aya kila mtu alale chini mnaingia ndani kwa kubimbilika tranka liache hapohapo, Niliona Afadhali kubimbilika kuliko kuruka kichurachura fasta wazee tukaanza kuingia ndani kwa kubimbilika wengi hapa tuliumia sababu chini kuna vikokoto .

Tumeingia tumekuta kuruta wengi sana tukaungana nao hapo mimi wazo langu ni moja tu KURUDI NYUMBANI.

Tukaanza kupangwa unaitwa jina unaenda upande mwingine zoezi lilienda hadi saa 4 usiku.
Sasa mjeda mmoja akasema tumeita wote nyie majina yenu hayapo vipi? Tulikua wengi kiasi, mimi nilitoa sababu kua nimepangiwa Rukwa lkn kule baridi kali siwezi nina matatizo ya mbavu.
Walituelewa wote tukaruhusiwa.

Sasa majina yakaanzwa kuandikishwa, mimi narudi nyuma mjeda akaniona akanita alikua mmama.
Wewe vipi mbona unarudi nyuma? Nikaanza kulia! Kumbe ndo naharibu akashout "Maafande njooni muone kuruta analia" wote wakaja "Kuruta unalia?" Ebu chuchumaa nikachuchumaa fasta maswali yakaanza unaitwa nani nikataja jina umetokea wapi nikasema, unalia nini nikasema Nataka kurudi nyumbani.... Wewe nilikoma!!! Aya simama twende squat 100 nikaanza kupiga squat huku machozi kama yote basi wanacheka

Sikuzimaliza nikaambiwa ungana na wenzako hapa kuna kuingia hamna kutoka.

MAMBO RASMI
Tukakusanywa uwanja wa damu (uwanja wa damu - uwanja wa mazoezi, paredi) hapo kumbuka hatujapumzika tokea tumefika tukaanza kupewa risala huku tumesimama ole wako usinzie, tupo wengi na wajeda wengi pia ukigeuka huyu hapa

Tukafunguliwa stoo, ipo pembeni ya uwanja tunaingizwa kwa mafungu "ingia toka na godoro ole wako uchelewe kutoka"
Wanajeshi wakali kitu kidogo ushakula tusi tena la mzazi huna cha kumfanya na ole wako unune😂
Mimi nilivyoingia chap nimetoka na godoro bahati nzuri yote ni mazuri yamejaa.

Mpaka tunaruhusiwa kwenda Angani (Angani - Hall la kulala) muda umeenda karibia alfajiri.
Nimeingia na marafiki zangu, hapo nimekutana na wale tuliosoma nao advance, sekondari tulikua kama 7 Anna akiwepo.
Tukashauriana tukaoge tulionyeshwa sehemu zote za muhimu mabomba, vyoo.
Sasa tunachota maji akaja mjeda anayejitolea akasema eee kuruta mnaenda kuoga sasa hivi? Sasa sisi tunabaki tunashangaa sababu tulikua kuruta wengi kumbuka hapo ni saa 9 alfajiri
"Bora mkalale dakika chache zilizobaki, muda si mrefu filimbi inalia"
Kudadeq " Anna mimi siwezi hapa kesho namwambia maza anifate" hapo nalia, wengi wanajuta kwenda jeshi muda huo.

Tukapiga moyo konde tukaenda kuoga, tunarudi lisaa hata haijafika tunasikia filimbi wajeda wakike kama wote wamekuja na virungu kutuamsha
Sasa hata hatujalala halafu tunaamshwa hii ni hatari.

Wengine waliolala bila kuoga wanaamka fasta wanachukua miswaki na ndoo eti wakaoge! 😂
Wajeda walitembeza virunguu! "Mnaenda kuoga kwani hamjasikia filimbi, hapa hamna kupiga mswaki wote uwanja wa damu fastaa" kiaina nilishukuru Mungu nimeoga sababu sio kwa vumbi lile plus kugaragara chini.

Tukakusanyika uwanja wa damu saa 10 alfajiri, Kuna wale wanaojitolea wanoko sana! Tukapewa watusimamie uelekeo mchakamchaka basi tukawekwa ki kombania, Mimi nikafight nikawa kombania B pamoja na Anna.
Uelekeo ukaanza jogging tumekimbia huku tunaimba plus wajeda nyuma na gari, hilo gari kumbe ni kwaajili ya kubeba wale watakaozidiwa njiani au kuzimia.

Sasa tunakimbia nikicheki tunapita ile road tuliyokuja nayo jana kutoka mjini. Nikafikiria kwahiyo tunaenda hadi mjini au? Basi sina jinsi tulikimbia sana wengine wanazimia njiani wanapakiwa kwenye gari umbali ulikua kama kutoka Gongo la mboto hadi Airport kwa wanaojua hizo sehemu wataelewa.

Wakati tunarudi huku tunakimbia kushakucha ndo tunaonana vizuri😄ilikua vichekesho tumeloa vumbi hadi kope ndani ya pua kote vumbi masikioni usipime ukimuangalia mwenzako unacheka huna mbavu.
Tumerudi kambini tunakutana na majembe, ndoo za michanga. Mimi nilijua tukirudi tunapumzika kumbe kazi inaendelea nilijihisi kukonda kwa siku moja.
Tukapangiwa kazi nikaangukia kwenda shamba, tena huko shamba ni kule tulipotoka kukimbia njia ile ya vumbi ya kutoka mjini katikati barabara pembeni kulia kushoto mashamba ya wajeda sina jinsi.

Tukapiga mguu huku nalia mbaya zaidi sikua na rafiki yangu niliyepangiwa nae kusema tungefarijiana, msidhani mimi mzembe wakuu hapana! Tuliolia tulikua wengi hadi wanaume, tena sikia hivihivi kwa ninavyohadithia kuliko ikutokee.

Njiani kuna mjeda akaniona ni wale wanaojitokea ni binti mzuri mweupe sijui alifata nini kule Wallah!
Akaniambia usilie utazoea mwaya, unaitwa nani nikamwambia Ephen, kumbe ni namesake wangu bhana akafurahi akaanza kunitambulisha kwa wale wajeda wengine huyu ni mdogo wangu. Kumbuka hawa wajeda tuliopewa twende nao shamba ni wale wanaojitolea sio waajiriwa.
Basi ikawa nafuu kwangu, "sasa huku tunaenda ni shamba kung'oa visiki, ningekujua mapema ningekupeleka kule shamba la kuvuna machungwa kule bata, ila usijali kesho utaenda huko" akaniambia

Tulifika shamba kama saa 2 hivi kazi ikaanza kung'oa visiki hawajali mwanaume wala mwanamke wote kazi kazi!
Kisiki kimoja watu watatu tena vile visiki vinene, nilipiga panga na jembe hadi marengerenge yananitoka nayaona
Nilisikitika sana nikajuta kwenda jeshi, nikakumbuka nyumbani nilijihisi nipo dunia ya peke yangu watu wote wameniacha.

Itaendelea...

Muemdelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Nakubusu
 
Kwanini mkuu
Mdogo wetu wa mwisho ni pisi kali rangi ya mtume akienda huko nna wasiwasi wajinga wasije muharibu uwiii[emoji2304]
Kama ni mpambanaji haina shida na wala usiogope sana kwa sababu mahusiano ni sehemu ya maisha ila tu yasifanyike kama namna ya kutaka favour. Kwa hiyo kuna watoto wa kike wenye mentality ya kuutumia mwili kuepuka shurba, hiyo ndio maana yangu

Hata hivyo, jeshini warembo ni wengi tu kama uraiani na wanakaza fresh tu. So, usiogope 😁🙏🏽
 
Kama ni mpambanaji haina shida na wala usiogope sana kwa sababu mahusiano ni sehemu ya maisha ila tu yasifanyike kama namna ya kutaka favour. Kwa hiyo kuna watoto wa kike wenye mentality ya kuutumia mwili kuepuka shurba, hiyo ndio maana yangu

Hata hivyo, jeshini warembo ni wengi tu kama uraiani na wanakaza fresh tu. So, usiogope 😁🙏🏽
Umesema ukweli mtupu!!
 
Back
Top Bottom