Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna uzi kwa kijeshi kwa vijana walio pita jeshini ,kwa miaka ya 1970s-1990s ni wa moto sana ,utafute hutajuta simulizi zilizomoSAMAHANI WADAU MBONA NAONA KAMA WENGI HUMU NI KAMA MMEZALIWA KUANZIA 1993???
SISI TULIOZALIWA 1970,S TUNA STORY ZETU TOFAUTI KABISA KUHUSU JESHI
Wow nimetamani kujua vingi about you but najiskitia itakuwa too hard kufanikisha ilo.Najishughulisha na siasa
😂😂 ujue mtoto anaedeka huwaga hana plan B, hana uvumilivu, hawezi fanya kitu peke yake bila usaidizi.Uonevu mkuu 😚
HII imenikumbusha siku niliyoripoti JKT mimi nilinyoa kipara Sasa wakati nafika kwenye gari la kuelekea kambini nilikutana na wadada wawili wao walikuwa hawajanyoa, Ile tunafika nikaulizwa Hawa unawafahamu nikajibu ndiyo, wakaniambia kwahiyo wewe umewadanganya wasinyoe alafu ukanyoa peke yako, aisee palepale getini nilianza kuroll na kurukishwa vichura, nikamwagiwa maji, Kisha nikaambiwa niwapake poda usoni yaani vumbi, alafu niwanyoe yaani palepale hamu yote ya JESHI iliisha
Mambo kama haya matam sana mkuuSEHEMU YA 3
Watu tunang'oa visiki huku tunasinzia, yule mjeda namesake akanifata "njoo huku" nikaenda sasa kuna vichaka vingi akanipeleka kichaka flani hivi majani yamekaa kimduara katikati uwazi upepo unapita. Akaniambia "lala hapo muda wa kuondoka ukifika nitakufata" nikapiga zangu mbonji.
Nakuja kushtuliwa na mateke, nimekurupuka namuona bakabaka ananitizama tena ana nyota mbili (bakabaka - mwanajeshi aliyeajiriwa) "toka huko chuchumaa hapa haraka" nikatii amri mzee.
Umefikaje huku? Swali nimepigwa...
Nikafikiria nikaona siwezi kumchoma mjeda namesake ni vyema nipambane na hali yangu.
Nikaanza kujitetea pale, "Mimi naumwa vidonda vya tumbo nimezidiwa nikaona nipumzike hapa" akamwita mjeda hana cheo akamwambia naomba umshughulikie huyu.
Yule mjeda akaniambia "adhabu yako utabeba kisiki kikubwa peke yako kupeleka kambini". Nikaona nishaanza kupata msala mapema muhimu nikurudi nyumbani.
Nimekaa kihuzuni mjeda namesake akaja "nimekutafuta kule sijakuona" nikamwambia nilifumwa nikampa mkasa wote akaniambia nisijali atanisaidia. Kweli saa 4 ikafika filimbi ikalia kisiki kimoja mnabeba watu wawili kwenda kambini. Yule bakabaka akasema yule mwenye adhabu yangu yuko wapi? Nikaenda akanipa kisiki kikubwa machozi yakaanza kunilenga.
Akaniambia unatoka mkoa gani nikamwambia Dar! Akacheka sana "mbona watu wa dar wajanja? Wewe kitu kidogo unalia ebu acha usen....."
Nikapewa kisiki kikubwa peke yangu yeye akaondoka, namesake akawapasia kile kisiki kuruta wengine, akawaita wakaka wawili akawaambia kisiki chao wanipe mimi changu wabebe. Hawakupinga fasta wakabeba.
Kama kawaida uelekeo kambini, umbali kutoka pale shamba hadi huko ni kama 2km, kutembea ni mchakamchaka.
Tumefika tukaenda dining, tukakuta bakabaka kama wote
"Aya kila mtu ana kikombe chake! chukua ndoo nenda kituoni kajaze mchanga ulete hapa ndo uchukue chai"
Kituoni ni kule siku ya kwanza tuliposhuka na gari
Njaa inauma, muda huo nikawa sisikii tena kulia ila hasira kama zote nikajuta kwenda jeshi.
Kufika huko kituoni michanga yenyewe ina maji, nikatiliwa mchanga nikamuomba yule mjeda aniwekee ndoo nusu sababu kipara plus ndoo ya mchanga nzito, akaniwekea.
Niliporudi jikoni kumbe bakabaka wanakagua kama ndoo imejaa au ipo nusu........
Tupo kwenye foleni ya kukaguliwa machozi yananilenga najua kabisa narudishwa nikajaze ndoo, akaja mjeda namesake akaniuliza "ndoo yako imejaa? Nikamwambia hapana
Basi kuna kuruta alikua anapita amerudishwa akajaze ndoo mjeda namesake akamwambia chukua mchanga wako muongezee huyu wewe ukajaze tena!
Yule akupinga akanijaziwa ndoo nikakaguliwa imejaa nikachukua chai na mkate.
Uzuri chai imekolea sukari na mkate mzuri mkubwa nikala nikashiba ila majonzi yakawa palepale ninayo moyoni.
Yaani siwezi kupewa msosi mpaka jasho linitoke?
Nikipata upenyo lazima nimpigie mama aje kunifata.
Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Sio maramba tanga kweli manake na penyew hilo vumbi 😂Non of the above
ShukranUsiku wa kuamkia sherehe ulikua mzuri, nilipata kombati na buti kama nilivyotamani
Siku ya sherehe niliperform vizuri karate
Nilifurahi nimemaliza course, kesho nikapanda kwenye gari kurudi home hapo nikapata hisia a huzuni nikahisi kumiss jeshi kabla hata ya kufika nyumbani.
Nilivyoshuka ubungo sista angu alikuja kunipokea, naongea nae kwenye simu kumuelekeza nilipo aje kunifata
Nikashangaa mtu amefika nilipo halafu ananipita, nikamuita "dada" alivyogeuka akaanza kucheka "Aisee ndo umekua hivyo! Unajua sikukujua kabisa umebadilika"
Nilivyotoka jeshi nilikua mweusi sana
Mama alifurahi kuniona
Mwanzoni walikua wananishangaa jinsi nilivyochangamka nimekua mchapakazi.
Wadogo wa kupiga nao story kama
ulivyouliza sikua nao, mimi kwetu ndo lastborn.
Naam.Karibu! I hope nimekujibu maswali yako yote
Mmh.wengine bado wana moyo wa kiraia aseeBONUS
Mwanzoni wiki 6 mjeda namesake alinifata kuniaga, kwa kumwangalia hakua sawa kama amelia muda mrefu.
"Mimi naondoka kwaheri"
Sababu gani nikamuuliza
"Kuna nafasi za kwenda course ya kuajiriwa migration zilitoka, nikapata nafasi, lakini nimepimwa nina mimba hivyo safari yangu imeishia hapa"
NIlimuonea huruma katika kumchimba ndo nikagundua
Alipata mimba ya yule bakabaka yeye akawa anaficha, nafasi zilivyotoka jina lake lipo ilibidi amwambie mchumba ake.
Bakabaka akamwambia unaitoa ili upate nafasi ya kwenda mafunzoni au unabaki nayo?
Yeye akachagua kubaki nayo akose jeshi!
Alikua ameshajitolea zaidi ya miaka miwili.
Nilimuonea huruma, nilimuona ana moyo mzuri sana! Mwingine angeitoa ili akamilishe ndoto yake ya kua mwanajeshi.
Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Sio kwamnkonga ni komkongaKwamsisi,kwamkonga.....
Kwanini maana ya raia,wewe ni raia wa nchi gani? Nani sio raia?Transformation maisha ya uraiani kwenda yasiyo ya kiraia.
Ndio maana unapiga kwanza kipara kutoa uraia.
Exactly mtoto wa kota Ana advantage kubwa hao watu amekaaa nao Kwa muda mrefuNgoma coy aka nengu nengu,wanakuwaga walaini sana watoto wa michezo coy.
Kuna jamaa angu alikimbilia nengu nengu baada ya mziki wa kombania kuwa mgumu.
Jeshini kitengo mura,ukiwa na kitengo shuruba zinakuwa chache,kama ukipata nafasi ya kujichanganya kwenye kitengo nenda,iwe ujenzi ,iwe ngoma,iwe mpira au sanaa yoyote
Kukaa bila kitengo ina maana utakuwa kombania mda wote,na kombania haipumziki ,kila kazi zinatazama kombania,kwa hiyo ukiwa kombania kila kazi utafanya,iwe kubeba magogo,kupasua kuni,kubeba tofari,kung'oa visiki,kulima ,kuvuna nk.
Na vibangala vya watu wetu vinakuga na usimamizi sana ,unakuta maafande wapo zaidi ya mmoja mana mnakuwa kuruta wengi hivyo usimamizi unakuwa sio wa mtu mmoja,hali kwenye vitengo usimamizi unakuwa wa viongozi wa kawaida au hakuna kabisa ni kujisimamie wenyewe tu,
Watoto wa kota huwa wanaenda jeshini wana abc za kutosha ,hiyo husaidia kukabiliana na upepo wa kule.
Jeshini ubishi hakuna ,kila kitu ndio afandee hata kama kinakukera moyoni, utafanyaje ,ndo mana unaambiwa fungua moyo
Kumaliza ukuruta ni kazi ngumu sana ,hadi ndege wa angani wakipita wana wahurumia .
Utapauka,utakonda,ngozi itabadilika,wana kutoa umaarufu,hata kwenu ni mambo fresh lakini utakuwa sare tu na mtoto wa mkulima[emoji1][emoji1][emoji1]YAANI NDO MAANA HALISI YA KUKUTOA URAIA NA KUWA ASKARI.
IO ndo kifupi chake....Mp ni watu wengine wanahusika na nidhamu na pia kuna usalama wa taifa wanakuwepo... Wao hawawajibiki kwa kamanda kikosi
Kambini kwetu walikuwepo watatu nadhani..
Mps vichwa vibovu vile😅👐na kofia zao nyekundu...
Mzeee wangu Moja siku nilikuwa na piga nae story anasema siku hizi ma brigedia wamekuwa wengi sana njia ya mwenge una weza pishana na gari Tano au Saba zote za ma brigedia .....anasema Enzi zao wako kazini wapya , jamaaa amekaaa kazini miaka 2 ajawahi kuonana na brigedia siku amekuja Kumuona alipagawa jinsi kachafuka vyeo Kwa wenge,alipiga saluti mikono yote miwiliKuna uzi kwa kijeshi kwa vijana walio pita jeshini ,kwa miaka ya 1970s-1990s ni wa moto sana ,utafute hutajuta simulizi zilizomo