Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

SEHEMU YA 2
Ilipoishia..........
Sasa tulivyoloa vumbi hadi kope mtu ukimuangalia mwenzako unatamani kucheka ukisikilizia maumivu ya miguu unatamani kulia......

Endelea
Mpaka tumefanikiwa kulifikia geti kuna kuruta waliozimia njiani, wengine kilio kikubwa mimi mmojawapo Aisee wanajeshi waheshimiwe sio kwa mazoezi yale.

Getini tukaambiwa aya kila mtu alale chini mnaingia ndani kwa kubimbilika tranka liache hapohapo, Niliona Afadhali kubimbilika kuliko kuruka kichurachura fasta wazee tukaanza kuingia ndani kwa kubimbilika wengi hapa tuliumia sababu chini kuna vikokoto .

Tumeingia tumekuta kuruta wengi sana tukaungana nao hapo mimi wazo langu ni moja tu KURUDI NYUMBANI.

Tukaanza kupangwa unaitwa jina unaenda upande mwingine zoezi lilienda hadi saa 4 usiku.
Sasa mjeda mmoja akasema tumeita wote nyie majina yenu hayapo vipi? Tulikua wengi kiasi, mimi nilitoa sababu kua nimepangiwa Rukwa lkn kule baridi kali siwezi nina matatizo ya mbavu.
Walituelewa wote tukaruhusiwa.

Sasa majina yakaanzwa kuandikishwa, mimi narudi nyuma mjeda akaniona akanita alikua mmama.
Wewe vipi mbona unarudi nyuma? Nikaanza kulia! Kumbe ndo naharibu akashout "Maafande njooni muone kuruta analia" wote wakaja "Kuruta unalia?" Ebu chuchumaa nikachuchumaa fasta maswali yakaanza unaitwa nani nikataja jina umetokea wapi nikasema, unalia nini nikasema Nataka kurudi nyumbani.... Wewe nilikoma!!! Aya simama twende squat 100 nikaanza kupiga squat huku machozi kama yote basi wanacheka

Sikuzimaliza nikaambiwa ungana na wenzako hapa kuna kuingia hamna kutoka.

MAMBO RASMI
Tukakusanywa uwanja wa damu (uwanja wa damu - uwanja wa mazoezi, paredi) hapo kumbuka hatujapumzika tokea tumefika tukaanza kupewa risala huku tumesimama ole wako usinzie, tupo wengi na wajeda wengi pia ukigeuka huyu hapa

Tukafunguliwa stoo, ipo pembeni ya uwanja tunaingizwa kwa mafungu "ingia toka na godoro ole wako uchelewe kutoka"
Wanajeshi wakali kitu kidogo ushakula tusi tena la mzazi huna cha kumfanya na ole wako unune!
Mimi nilivyoingia chap nimetoka na godoro bahati nzuri yote ni mazuri yamejaa.

Mpaka tunaruhusiwa kwenda Angani (Angani - Hall la kulala) muda umeenda karibia alfajiri.
Nimeingia na marafiki zangu, hapo nimekutana na wale tuliosoma nao advance, sekondari tulikua kama 7 Anna akiwepo.
Tukashauriana tukaoge tulionyeshwa sehemu zote za muhimu mabomba, vyoo.
Sasa tunachota maji akaja mjeda anayejitolea akasema eee kuruta mnaenda kuoga sasa hivi? Sasa sisi tunabaki tunashangaa sababu tulikua kuruta wengi kumbuka hapo ni saa 9 alfajiri
"Bora mkalale dakika chache zilizobaki, muda si mrefu filimbi inalia"
Kudadeq " Anna mimi siwezi hapa kesho namwambia maza anifate" hapo nalia, wengi wanajuta kwenda jeshi muda huo.

Tukapiga moyo konde tukaenda kuoga, tunarudi lisaa hata haijafika tunasikia filimbi wajeda wakike kama wote wamekuja na virungu kutuamsha
Sasa hata hatujalala halafu tunaamshwa hii ni hatari.

Wengine waliolala bila kuoga wanaamka fasta wanachukua miswaki na ndoo eti wakaoge!
Wajeda walitembeza virunguu! "Mnaenda kuoga kwani hamjasikia filimbi, hapa hamna kupiga mswaki wote uwanja wa damu fastaa" kiaina nilishukuru Mungu nimeoga sababu sio kwa vumbi lile plus kugaragara chini.

Tukakusanyika uwanja wa damu saa 10 alfajiri, Kuna wale wanaojitolea wanoko sana! Tukapewa watusimamie uelekeo mchakamchaka basi tukawekwa ki kombania, Mimi nikafight nikawa kombania B pamoja na Anna.
Uelekeo ukaanza jogging tumekimbia huku tunaimba plus wajeda nyuma na gari, hilo gari kumbe ni kwaajili ya kubeba wale watakaozidiwa njiani au kuzimia.

Sasa tunakimbia nikicheki tunapita ile road tuliyokuja nayo jana kutoka mjini. Nikafikiria kwahiyo tunaenda hadi mjini au? Basi sina jinsi tulikimbia sana wengine wanazimia njiani wanapakiwa kwenye gari umbali ulikua kama kutoka Gongo la mboto hadi Airport kwa wanaojua hizo sehemu wataelewa.

Wakati tunarudi huku tunakimbia kushakucha ndo tunaonana vizuri, ilikua vichekesho tumeloa vumbi hadi kope ndani ya pua kote vumbi masikioni usipime ukimuangalia mwenzako unacheka huna mbavu.
Tumerudi kambini tunakutana na majembe, ndoo za michanga. Mimi nilijua tukirudi tunapumzika kumbe kazi inaendelea nilijihisi kukonda kwa siku moja.
Tukapangiwa kazi nikaangukia kwenda shamba, tena huko shamba ni kule tulipotoka kukimbia njia ile ya vumbi ya kutoka mjini katikati barabara pembeni kulia kushoto mashamba ya wajeda sina jinsi.

Tukapiga mguu huku nalia mbaya zaidi sikua na rafiki yangu niliyepangiwa nae kusema tungefarijiana, msidhani mimi mzembe wakuu hapana! Tuliolia tulikua wengi hadi wanaume, tena sikia hivihivi kwa ninavyohadithia kuliko ikutokee.

Njiani kuna mjeda akaniona ni wale wanaojitokea ni binti mzuri mweupe sijui alifata nini kule Wallah!
Akaniambia usilie utazoea mwaya, unaitwa nani nikamwambia Ephen, kumbe ni namesake wangu bhana akafurahi akaanza kunitambulisha kwa wale wajeda wengine huyu ni mdogo wangu. Kumbuka hawa wajeda tuliopewa twende nao shamba ni wale wanaojitolea sio waajiriwa.
Basi ikawa nafuu kwangu, "sasa huku tunaenda ni shamba kung'oa visiki, ningekujua mapema ningekupeleka kule shamba la kuvuna machungwa kule bata, ila usijali kesho utaenda huko" akaniambia

Tulifika shamba kama saa 2 hivi kazi ikaanza kung'oa visiki hawajali mwanaume wala mwanamke wote kazi kazi!
Kisiki kimoja watu watatu tena vile visiki vinene, nilipiga panga na jembe hadi marengerenge yananitoka nayaona
Nilisikitika sana nikajuta kwenda jeshi, nikakumbuka nyumbani nilijihisi nipo dunia ya peke yangu watu wote wameniacha.

Itaendelea...

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Emb acha kunikumbusha mateso ya jeshi🤣🤣🤣 ina episode ngapi? Duuh kumbe na wewe uliitwa kuruta?
 
SEHEMU YA 7
Nashangaa muda unaenda mbona haturuhusiwi kwenda kulala?
Yule bakabaka akastopisha kwata akasema hivi sasa ni saa 2 usiku muda bado kabisaa!
Kuruta tunaulizana muda bado kivipi akati tumetumia muda mwingi kombania.
kuruta wakisinzia wanapewa kazi ya kushindana kukimbia
Mimi sikua nasinzia nilikua najipa moyo muda simrefu tunaenda kulala ila wapiiiii.... kila muda bakabaka anasema ndo kwanza saa 2 kamili usiku.

Tunaimba chenja, mazoezi ya viungo kwenye mazoezi nilikua napenda viroba (squats) hata 100 nashuka tu nasihisi kuchoka. then bakabaka anasema hapohapo ulipo jilaze ulale! Basi watu fasta tunajilaza kwenye vumbi
Dakika 5 nyingi anasema inuka rukaruka kichura
Kuruta tulipata hasira hadi wengine wakaanza kusonya.

Hapa nilishangaa kitu! Kuruta anamsonya bakabaka halafu hafanywi kitu zaidi tu anasmile halafu anasema "kuruta fungua moyo huo"
Ila walikua wanaudhi fikiria mtu anakuambia lala ghafla ruka kichura anarudia mara nyingi zile hasira plus usingizi watoto wengine hawana adabu wanamsonya na yeye anablush tu.

Hamuwezi amini alfajiri ilifika tukishuhudia kwa macho! Sasa tunaulizana "mbona leo hatujaenda kulala?" Tutafanya nini ndo ishapita hiyoo

Tukapanga foleni mabio yakaanza, kama nilivyosema muda wa mabio niliupenda sana zile chenja ndo ugonjwa wangu nikawa nakimbia bila kutegea nafurahia kukimbia.

Tumerudi jogging uelekeo shambani, tukitoka shambani chai kuipata hadi ukimbie 2km, tukitoka chai uelekeo kwata
Sikupenda kwata nilikua nanga nimekula mabao mengi tu mpaka bakabaka akanichoka! Akaniambia labda utaweza vitu vingine kama ngoma coy, karate au kazi mchanganyiko.

Ratiba iliendelea mpaka wiki ikakata hatukurudi angani hatukulala wiki nzima!

Baada ya wiki sasa bila kulala! vituko vilianza mtu anachuma machungwa huku kafumba macho anaota kabisa
Mimi ile mabio nikawa nakimbia huku nasinzia, chenja naitikia miguu inaenda mbele lakini nimelala ila naota nakimbia.
Unaweza usiamini lakini hali ndio hiyo.

Bakabaka wakawa wanasema hawa itabidi leo wakalale wasije kutufia bure hapa!
Kitengo cha kuvuna machungwa tulikua tunapiga story sana na bakabaka.
Wiki ilipita bila kuoga.


Usiku ukafika mimi najua kabisa leo tunaenda kulala, nikawa na furaha , sasa muda unaenda ila haturuhusiwi, njaa ikawa inaniuma nikasema subiri nitoroke niende kunywa chai jikoni halafu nirudi fasta kombania nilihisi tulidanganywa leo tena tunakesha.

Lahaula nilijuta kwanini nilitoroka........

Itaendelea.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Mbona waliwapa vitengo mapema hivyo? Me nakumbuka kwata ilikua after a month or so... kama sio 6 weeks! Me sikupenda viroba hata kidogo ila kambi yenu waliwakomesha ila labda wakawa sawa maana mm nilienda second batch nikakuta wameshapiga hilo doso la ufunguzi
 
SEHEMU YA 8
Nikafanikiwa kutoroka hadi jikoni, kule maeneo mengi giza ndo maana sikubambwa
Nikanunua maandazi nikanywa na chai haraka, sasa nikawa naona kuruta wanakimbia wameruhusiwa kwenda kulala
Sasa nikawa nasuuza kikombe fasta na mimi nikalale

Kwa mbali namuona bakabaka anakuja na service man ( wanaojitolea) wetu
Basi service man akasema "Ephen mwenyewe yule pale" moyo ulishtuka ukaenda kasi sana

Nilipokea mvua ya matusi kutoka kwa yule bakabaka halafu mwanamke "Wenzako wapo kombania wewe huku unafanya nini? Nikaongezewa bao la mgongo
"Kuruta naongea unanitizama badala ya kupunguza urefu?'
"Punguza urefu haraka!"
Basi nikachuchumaa ndo kupunguza urefu.

Pembeni kulikua na bomba la maji nikapelekwa pale yakafunguliwa nikaloa chapachapa
"Aya roll uelekeo kombania"
Ilikua ngumu kwangu njia ya kuroll ina kokoto, mimi nina kidonda kibichi gotini kinaniuma na nimefungwa bandage.

"Afande naomba unibadilishie adhabu nina kidonda kibichi"
kuruta unanidindia?
Nikaona huyu anataka kukuza mambo! Nikaanza kuroll goti maumivu kama yote damu zikaanza kutoka na afande hanionei huruma

Kulikua na umbali hadi kombania ila nikafika!
Wenzangu walivyoniona wakaanza kunisonya wanalalamika.
Kombania zipo A hadi D kama sijakosea, A, C na D wakaruhusiwa kwenda kulala muda mrefu tu.
Na kombania B wanaume waliruhusiwa pia kasoro wasichana ndo hawakuruhusiwa sababu hawakutimia
Nani hakutimia ni mimi hapa.

Jeshini ikitokea kuruta ametoroka kwenye kombania hamuendi kulala hadi apatikane.
Muda huo saa 7 usiku damu zinatoka gotini maumivu hadi nalia.

"Sasa sikieni! Leo mnakesha na mimi hapa! mpaka asubuhi!
Nyie si hamjaiva, mlimtuma mwenzenu akanywe chai muda wa kombania haya wote kichurachura mnaenda na kurudi hadi kukuche, Wazii kuruta?

Kuruta wenzangu wakaanza kulia "Afande sisi hatujamtuma! Tunaomba tukalale"

Nauliza tena "Wazii kuruta?"
Tukaitikia waziii Afande!
Huku wenzangu wananitukana nimewaponza hawaendi kula utawala (kula utawala- kupumzika)

Bakabaka sasa "Kila mtu akachukue ndoo ya maji mje kumwaga hapa na poda ya kutosha mje mumpake usoni" (Poda-Vumbi)
Nililia sana basi wakaenda kuchukua poda wakanipaka, maji yakamwagwa kwenye vumbi kukawa na tope nikaambiwa,
"Wewe siumekuja hapa kula! Aya twende kama kambare"
Nikaanza kuroll kwenye tope.

Yule afande alikua na roho ngumu sanaaa
"Aya kuruta simama hapo uanze kupiga makofi wao wanafatisha"

Nikaanza nikipiga kofi wanasimama nikipiga wanalala chini! Ngoma ilienda hadi afande akasema nasimama pale nyie endeleeni!

Kumbe aliondoka sisi tukaendelea tukidhani anatuangalia, tumeshtuliwa na filimbi ya alfajiri

Tulikesha tena na wenzangu!!
Walinichukia! siku hio nikawa na kazi ya kuwaomba msamaha. Niliwafanya wasilale tena kwa usiku mwingine ukijumlisha na siku 7 za mwanzo.

Itaendelea.......

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Duuh uliyatimba, unadoji mda wa roll-call? Doji vyote ila sio hio. Kama ni kweli basi ulionja utamu wa jeshi😅 ulikuwa wa demo....
 
SEHEMU YA 13
MAOKOTO

mwanzoni kuruta wote tulipewa kopo la uani na sanitizer sisi tukajua ni upendo tunapendwa sanaaa na bakabaka.
Mwisho wa mwezi ukafika kuruta njoeni kuna maokoto yenu jeshi tunawapa iwasogeze siku.

Tumekaa kombania bakabaka kashika burungutu mimi jina langu ni herufi ya mwanzo kwahiyo hela nilikua napewa wa kwanza

Nikaitwa jina nikaenda nikapewa hela halafu nisign, nikapiga jicho kwenye amount iliyoandikwa ni tofauti na niliyopewa, nikimaanisha nimepewa nusu ya hela.

Wote tukapewa tukaanza kuulizana vipi mbona tumepewa hela nusu?
Bakabaka akatuambia "Mlivyokuja mlichukua makopo yetu na sanitizer mlidhani tumewapa bure?"

Ikawa kila mwezi tunapewa maokoto nusu kisingizio ety tulivyokuja walitupa makopo na sanitizer zao!

NADHARIA YA WANAJESHI KUTEMBEA NA KURUTI

NIilivyotoka nyumbani usia ulikua kua makini huko wajeda sio watu wazuri!
Nikiri kwa nilichokiona WANAJESHI MNAWASINGIZIA!

Labda kama hiyo tabia ipo kambi zingine lakini kambi niliyokuepo mimi wanajeshi walikua wanajiheshimu sana.

Hawakua hata hivyo kusema wanatusumbua kuruta hapana.
Ila wanaoharibu sifa ni wale service man, wale ni vichomi kazi nyingi tunakua nao hivyo wanachukua nafasi hiyo kupenyeza nia yao ovu.

Ole wako service man umkatae utapata adhabu kama zote.
Mzazi usiogope mtoto kwenda kwa mujibu, faida ni nyingi kuliko hasara

"If it's bitter at the start, then it's sweeter in the end"
It was good ila umesimulia kwa ufupi na nime enjoy kukumbuka madoso na vitimbi vya jeshi
 
Yaani Service galz ndo walikuwa wanaongoza kwa kuumwa??
Nilikua sijakuelewa!
Kuruta wanaoumwa walikua wanaenda zahanati saa 11 alfajiri, saa 1 kila mtu anaenda kwenye kazi yake hamna kudoji
 
Mbona waliwapa vitengo mapema hivyo? Me nakumbuka kwata ilikua after a month or so... kama sio 6 weeks! Me sikupenda viroba hata kidogo ila kambi yenu waliwakomesha ila labda wakawa sawa maana mm nilienda second batch nikakuta wameshapiga hilo doso la ufunguzi
Course inakuaga 3months, ila mwaka wetu waliweka miezi miwili sababu kulikua na ishu ya kitaifa
 
Back
Top Bottom