Nimeacha kuishabikia Arsenal

Nimeacha kuishabikia Arsenal


Duh mtoto mbaya huyu kapiga goli tatu peke yake,Mimi nilidhani waJapan hodari kipande hile ya sayansi na tekelinalokujia kumbe hata kandanda wamo.Kagawa amekuwa mchazaji wa kwanza toka bara la Asia kupiga hat trick EPL.


00_600x338_1683614a.jpg
 
Wakuu nimeamua kwa hiyari yangu na pasipo kulazimishwa na mtu yoyote kuitosa club ya Arsenal.Nina sababu nyingi za kuitosa The Gunners.

[1] Kukwepa magonjwa ya moyo.

[2] Imeshindwa kutwaa kikombe chochote kwa muda mrefu sana.

[3] Arsenal imekuwa gulio la kuuza wachezaji wake mahiri kwa Club nyingine

Baada ya kutafakari kwa kinaa na bila kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au kikundi chochote nimeamua kujiunga na Club ya Manchester United yenye kutumia uwanja Old Trafold.Zipo sababu kibao lakini nitazitaja chache.

[1] Manchester United inaongozwa na manager mwenye mafanikio makubwa kuliko makocha wote wa UK.

[2] Manchester United imechukua ubingwa wa ligi kuu ya UK mara 19,timu inayoikaribia ni Liverpool pekee yake imechukua ubingwa mar 18 tu.

[3] Manchester United inakaribia kuweka rekodi mpya kwa kuchukua ubingwa mara 20, mpaka leo hii inaongoza ligi kwa tofauti ya point 12.

[4] Ukiishabikia Mancheter United uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo na kisukari ni mdogo sana.Kila wakati una kuwa ni mtu wa kucheka na kufurahia maisha duniani.

[5] Mwaka 1999 iliweka historia kwa kuchukua vikombe vitatu.Ubingwa wa ulaya.ubingwa wa Uk na Kombe la ligi.

[6] Mashabiki wa Manchester United ni wakarimu, wapole na wenye kujua kuchambua soka. Sifa hizo zinanihakikishia kwamba nitapokelewa vizuri.

Wapenzi wa Arsenal mtanisamehe sana kuhama club ni jambo la kawaida kwa mashabiki kama ilivyo kawaida kwa wachezaji. Siwezi kuendelea kusononeka hapa duniania kisa kupenda Club mbovu.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Mphamvu Dark City gfsonwin The Boss BAK Rejao Viper mfarisayo MwafrikaHalisi Kibunango Maxence Melo EMT Balantanda Mwita Maranya

Hauna tofauti na wale wanawake wanao amua kuwa ma-blender kwa sababu wameumizwa na wanaume zao..
 
He he mbona unahamaki hivyo kijana we jana umeangalia mechi Man v/s Norwich,kama ungeliona hiyo machi hata wewe ungejiunga na mashetani wekundu.

Hauna tofauti na wale wanawake wanao amua kuwa ma-blender kwa sababu wameumizwa na wanaume zao..
 
He he mbona unahamaki hivyo kijana we jana umeangalia mechi Man v/s Norwich,kama ungeliona hiyo machi hata wewe ungejiunga na mashetani wekundu.

Wewe sio shabiki wa mpira wa miguu na inaonekana kwenye soka uliletwa na Morinyo. U are a disgrace to sporthood
 
Mke mwenyewe uliyemtolea mahari akikushinda unamwacha sembuse timu.


Wewe sio shabiki wa mpira wa miguu na inaonekana kwenye soka uliletwa na Morinyo. U are a disgrace to sporthood
 
J4 Man itacheza na Real Madrid katika Jiji la Manchester.Manchester United inategemea kuchezesha kikosi kifuatacho.

[1] David de Gea

[2] Rafael da Silva

[3] Patrice Evra

[4] Nemaja Vidic

[5] Rio Fernandes

[6] Michael Carrick

[7] Danny Welback

[8] Tom Cleverley

[9] RvP

[10] Rooney

[11] Shinji Kagawa.

Benchi litakuwa na wachezaji wafuatao.

[1]Anders Lindagaard

[2]Ryan Giggs

[3]Antonio Valencia

[4]Anderson

[6]Smalling

Kikosi hiki kinatarajiwa kupiga mabao matatu kwa uchache huku kikiruhusu bao tu na kusonga mbele katika mzunguko wa 8 bora.
 
Wewe ni shabiki siyo mpenzi, hata huko refarii-united utahama tu muda si mrefu..
Mwanaume unakiwa kuwa na msimamo duniani
 
Ngongo eeh! Kwanza mimi sishabikii Aseno, ila ni kitu gani walichokuwa nacho aseno kikakusababishia uwe mpenzi wa aseno? Au nini kilikufanya uwe shabiki wa arsenal? Mashabiki 95% wa aseno walianza kuipenda timu yao mwishoni mwa miaka ya 90. Baada ya Nwanko Kanu kuhamia pale akitokea Inter Milan. Kanu ambaye aliuteka ulimwengu wa soka kwenye olimpic ya 1996 pale marekani ni mmoja kati ya wachezaji walioipa shavu ligi ya uingereza barani Africa. Ilifika kipindi kuna tetesi za kanu kuhamia clab nyingine, baadhi ya washabiki wa aseno waliapa kutoishabikia tena aseno na kuhamia timu atakayohamia kanu kama ilivyokuwa kwa Agustine Lyatonga Mrema alivyokuwa akihama na wanachama toka ccm kwenda nccr na baadae tlp.
 
Mashabiki wa The Gunners sasa mtakubaliana na Ngongo alifanya uamuzi wa maana kulikimbia chama la Wenger kila siku kichapo hakuna siku ya kufurahi.
 
Ngongo umeona mba
li tima ya watoto uwongo mtupu kila msimu kikombe tutapata msimu ujao Wenger toka 1996 mpaka leo 5 trophies nenda kapumzike au njoo Liver ujatupa kikombe tunakufukuza
 
Haya mkuu uliyehamia Man Utd, umekosea ..huo haukuwa wakati sahihi..sasa umeona walichofanywa na Real Madrid?
 
Heshima sana wapenzi wa ligi kuu ya UK.

Jana majira ya saa 4 usiku Manchester United waliitandika bila huruma Aston Villa bao 3 bila majibu.Mabao yote ya Man Utd
yalifungwa kipindi cha kwanza na mshambuliaji mahiri mtakatifu RvP.Kila goli lilikuwa na sababu zake hapa nahainisha kwa kifupi sana.

Goli la kwanza lilikuwa kwaajili ya kuchukua ubingwa mara 20.

Goli la pili lilikuwa goli bora la msimu mzima (Goli la mwaka).

Goli la tatu kuhakikisha RvP anakuwa mfungaji bora wa msimu huu.

Wale waliodhani Ngongo alikurupuka kukimbia chama la Wenger sasa wanatahayari na kujutia uamuzi wa kuendelea kushabikia timu inayopigania nafasi ya nne.

Karibuni Man Utd tufurahie makombe na mpira mzuri,karibuni Man Utd tufurahie mabao ya RvP.

Machester United Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.Raha dunia.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Dark City EMT Balantanda Maxence Melo mfarisayo Kibunango Mphamvu gfsonwin MwafikaHalisi Mwita Maranya BelindaJacob Peasant Godlisten Masawe ACCOUNT FULL BAK Nzi Pianist.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ngongo hukuwa na mapenzi ya kweli kwa Arsenal. Wewe ni wale washabiki wanaopenda timu ambazo zinakuwa mabingwa tu, timu ikianza kusuasua unasepa haraka sana. Kila la heri na MANU ila msimu ujao ukiona wanasuasua sitashangaa ukitutaarifu kwamba umeamua kuhamia MANC lol!!! Hongera kwa ubingwa

Good day 🙂
 
man u iko juu. naskitika tu kwamba hii mechi niliikosa live
 
Heshima sana wapenzi wa ligi kuu ya UK.

Jana majira ya saa 4 usiku Manchester United waliitandika bila huruma Aston Villa bao 3 bila majibu.Mabao yote ya Man Utd
yalifungwa kipindi cha kwanza na mshambuliaji mahiri mtakatifu RvP.Kila goli lilikuwa na sababu zake hapa nahainisha kwa kifupi sana.

Goli la kwanza lilikuwa kwaajili ya kuchukua ubingwa mara 20.

Goli la pili lilikuwa goli bora la msimu mzima (Goli la mwaka).

Goli la tatu kuhakikisha RvP anakuwa mfungaji bora wa msimu huu.

Wale waliodhani Ngongo alikurupuka kukimbia chama la Wenger sasa wanatahayari na kujutia uamuzi wa kuendelea kushabikia timu inayopigania nafasi ya nne.

Karibuni Man Utd tufurahie makombe na mpira mzuri,karibuni Man Utd tufurahie mabao ya RvP.

Machester United Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.Raha dunia.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Dark City EMT Balantanda Maxence Melo mfarisayo Kibunango Mphamvu gfsonwin MwafikaHalisi Mwita Maranya @BelindaJacob Peasant Godlisten Masawe ACCOUNT FULL BAK Nzi Pianist.
Haukuwa na mapenzi yoyote kwa Arsenal.....Na hauna mapenzi yoyote kwa Man Utd...........Nina uhakika Utd wakiteleza utahamia Spurs.....Kama sio City au Chelsea.....Na mwisho utajikuta umerudi Arsenal.....

GLORY HUNTER.................
 
Balantanda wacha fujo aisee tumeshachukua ndoo tunajiandaa tena msimu ujao tuchukue tena.Ebu niambie umejiandaa kutoa pongezi Emirate Jumapili ?.

Haukuwa na mapenzi yoyote kwa Arsenal.....Na hauna mapenzi yoyote kwa Man Utd...........Nina uhakika Utd wakiteleza utahamia Spurs.....Kama sio City au Chelsea.....Na mwisho utajikuta umerudi Arsenal.....

GLORY HUNTER.................
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ngongo hukuwa na mapenzi ya kweli kwa Arsenal. Wewe ni wale washabiki wanaopenda timu ambazo zinakuwa mabingwa tu, timu ikianza kusuasua unasepa haraka sana. Kila la heri na MANU ila msimu ujao ukiona wanasuasua sitashangaa ukitutaarifu kwamba umeamua kuhamia MANC lol!!! Hongera kwa ubingwa

Good day 🙂
teh teh tehhhhh, hata mimi nahamia airtel, lol!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom