Nimeachwa na mpenzi sababu anataka tuishi pasipo ndoa (sogea tuishi)

Nimeachwa na mpenzi sababu anataka tuishi pasipo ndoa (sogea tuishi)

Labda kweli ametafuta kisingizio cha kuniacha. Ila alikuwa anasisitiza sana niolewe kimyakimya ila hili halikuniingia akilini

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kwann asifate utaratibu mkafunga ndoa rasm! Mambo ya kimya kimya kwenye ishu ya msingi kama hyo inaleta ukakasi ana nia gani.
Pole ila life must go on na wala usihuzunike umshukuru Mungu kwa yote, mume wako atakuja wakati sahihi ukifika.
 
Mwanaume anayekupenda kweli hawezi kukwepa process wala kuogopa gharama, hapo jamaa yupo na ww ili siku ziende tu.
Alafu inaonekana wewe ndo unampenda zaidi, ukikubali huo ujinga kwanza atakudharau!!

NB: Ongea naye vizuri na uweke msimamo wako, mkishindwana njoo kwangu tuyajenge

Sent using Jamii Forums mobile app
Poa nitajitahidi kuongea nae

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kwann asifate utaratibu mkafunga ndoa rasm! Mambo ya kimya kimya kwenye ishu ya msingi kama hyo inaleta ukakasi ana nia gani.
Pole ila life must go on na wala usihuzunike umshukuru Mungu kwa yote, mume wako atakuja wakati sahihi ukifika.
Naamini hilo mkuu labda huyu alikuwa siyo mume wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo hakua anakupenda Wala, alikua anatafuta kisingizio Cha kukuacha tu ,alijua fika kwamba huwezi kukubaliana na Hilo jambo achana nae..hapo unaweza kukuta hata tayari kashavuta jiko lingine...shukuru umejua mapema.
Kwa sasa anasema hilo wazo la ndoa limeshamtoka hana tena mpango nalo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante mkuu mimi nimekuwa na huo msimamo sasa ameamua kuniacha kisa tu sijakubali kuolewa kimyakimya pasipo kuwapa taarifa nyumbani

Sent using Jamii Forums mobile app
Habari Kaka, mimi ni Binti wa miaka 28, sijaolewa ila nina mchumba wangu. Huyu Kaka nilikaa naye kwenye mahusiano kwa miaka mittano. Lakini alianza kubadilika ghafla mpaka akampa mwanamke mwingine ujauzito wakawa wanaishi naye. Alishanitambulisha mpaka kwao lakini baada ya kumpa huyo dada ujauzito aliniambia kuwa wazazi wake hawanitaki kwakua hawana uhakika kama nina kizazi au la hivyo wamemuambia kuwa amuoe huyo mwanamke mwingine.

Nilimuambia nimbebe mimba yake akagoma na kuniambia tuendelee kuwa marafiki tu lakini suala la ndoa haliwezekanai. Niliumia sana akawa anakuja kwangu ila anaishi kwa ule mwanamke mpaka alipojifungua. Baada ya kuanza kukusoma niliona kama ananipotezea muda hivyo niliamua kuchana naye. kuna Kaka alikua ananitongoza nikaamua kumkubalia na tukaanza mahusiano, huyo Kaka alikua siriasi kwani baada ya miezi minne tu alikuja kujitambulisha kwetu, akatoa mahari na mipango ya ndoa ilianza.

Baada ya kuona kuwa naolewa X wangu alinitafuta, aliomba tuonane na mimi kwakukua nilikua na mtu wangu basi nilikubali. Huko alianza kunielezea matatizo na mwanamke wake, aliniambia kwanza ni mchafu, mchotyo, hapendi ndugu zake na anafikiria kumuacha kwani Mama yake hamtaki tena anatamania angenioa mimi. Tuliongea mengi sana lakini sikumsikiliza, ila alianza kuomba msamaha, akawa anatuma mpaka na rafiki zake.

Kwakua ni mtu ambaye nilikua nampenda nilijikuta kuwa narudi wkake, nikajikuta sina hamu tena na mchumba wangu na mwisho nikaamua kumuambia mchumba wangu mpya kuwa tuliharakisha lakini mimi simpendi hivyo nataka tuachane. Alilia sana akaumia kw2ani alidai nimemuaibisha kwao kwakua kila kitu kilishaandaliwa ila sikua na namna, niliona hakuna haja ya kuingia kwenye ndoa na mwanaume ambaye simpendi wakati mtu ninayempenda amerudi.

Ndugu zangu walinisihi sana nisimuache lakini nilishafanya maamuzi. Sababu ya kuja kwako Kaka ni hivi, baada ya kuchana na mchumba wangu huyu mwanaume alinishawishi kubeba mimba yake ili iwe rtahisi yeye kunitambulisha kwa wazazi wake kwani hawawezi kunikubali kama hawajui kuwa nazaa. Nilibeba mimba yake kweli na sasa hivi nina ujauzito wa miezi nane ila kuna mambo yamebadilika Kaka naomba unisaidie kwani nimechanganyikiwa.

Kwanza bado anaishi na X wake, mwanzo aliniambia kuwa wanaishi pamoja kwasababu ya mtoto ila yeye hana mapenzi naye kwani hata tendo la ndoa hawafanyi. Lakini Kaka mimi mimba yangu ina miezi nane nimechunguza nimegundua kuwa kumbe hata huyo mwanamke naye ana mimba ya mtoto wa pili. Kumbuka aliniambia wanalea tu mtoto, sasa Kaka namuuliza kwanini amempa ujauzito ananiambia ilikua ni bahati mbaya.

Anadai kuna siku alirudi nyumbani kalewa ndiyo mwanamke akammbaka na kumlazimisha kufanya naye mapenzi lakini yeye hamtaki. Tuligombana sana nikamuambia kuwa amuache huyo mwanamke, basi siku iliyofuata alichukua vitu vyake kwa huyo mwanamke na kuhamia kwangu. Aliniambia kuwa kaamua kumuacha mwanamke wake, lakini Kaka sio hivyo nimechunguza nimegundua kuwa kule kwa yule mwanamke kamuaga kuwa anasafiri kikazi na wala hajamuambia kuhusu mimi.

Nimemuambia si nina mimba basi anipeleke kwao kunitambulisha ananizungusha ananiambia kuwa Mama yake sasa hivi ana presha kwahiyo tutamchanganya tusubiri mpaka apone ndiyo anipeleke. Kaka naomba nisaidie, mwanuame kaja anaishi kwangu, ana kazi nzuri lakini hatoi chochote, kila kitu nahudumia mimi, yaani hata umeme ukikatika hawezi kununua. Kifurushi cha Azam kikiisha basi kama kuna mpira atanunua cha wiki nisiponunua ila ndiyo basi, naomba nisaidie kuna mapenzi kweli hapa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama mwanaume hawezi kuoa basi hawezi kulea mtoto, narudia kama mwanaume hawezi kuoa, hawezi kuhudumia mke, hana uwezo au hata ujasiri wa kufanya maamuzi kuwa sasa naoa basi jua huyo mwanaume hawezi kulea mtoto. Hii Makala ni kama narudia lakini kwakua ukiingia kwenye inbox yangu nina meseji karibu elfu moja na kila unapofungua meseji kumi tatu zinakuambia mwanaume amenitelekeza basi naomba niirudie hata kama nakuchosha.

Kuna wanaume wanadhani ni rahisi kulea mtoto, ni kweli ni rahisi kama huyo mtoto hatataka kula,. Kama hataumwa, kama hatavaa na kama hatataka kwenda shule. Ukipata mtoto wa namna hiyo aisee ni rahisi na hakuna mwanaume anashindwa kulea. Lakini kama ni hawa watoto ambao wanakula, wanakunywa, wanaumwa nakuambia ndugu yangu kama mwanaume hajawa na ujasiri wa kukuoa, akakuambia nizalie tu nitalea basi jua kuwa siku akianza kuumwa anakukimbia.

Majukumu ya mtoto ni makubwa kuliko ya mke, mtu unaweza kuoa ukamuambia mke wako leo tupige deshi hakuna chakula mkavumilia, akaumwa ukamtafutia mitishamba mambo yakaenda. Lakini mtoto akija, akiumwa kwanzai hakuna cha mitishamba lakini chakula sio kwamba tu atataka lakini pia atachagua na chakula, kama maziwa atataka yale ya elfu 18, haya ya lita elfu mbili hataki na wala hajali chochote.

Hii ndiyo maana wanaume wakiona tu nugumu kidogo hukimbia, tena wengina hata mtoto hajazaliwa, ile tu mwanamke kila siku kuumwa, hospitali mimba inasumbua, sijui bedrest na mavitamin na mambo hayo anakimbia kwani anapakukimbilia. Lakini dada yangu mimba umebeba wewe, tena jamaa mjanja kabisa anasubiri mpaka mimba ikifikisha meizi sita anajua hapa hawezi kutoa akitoa anakufa ndiyo anakimbia hapokei tena simu zako.

Yaani mara nyingi wakinipigia simu nawauliza lini kaanza kukimbia, wengi kama si miezi sita ni saba na wachache miezi minne, ni ngumu kuona mwanaume anatakaa mimba ya wiki mbilili kwani hapo anajua kuwa unaweza kuitoa dakika mbili tu. Ukiona anaikataa ya wiki mbili jua hata mtoto alikua hataki, wewe mwenyewe umejibebesha umehsindwa kuhesbau tarehe basi, lakini kwa wale wanaokuambia nataka mtoto dada yangu wewe beba tu.

Ile mikiki mikiki ya miezi sita ikianza hutamuona, yaani atatafuta sababu ya kugombana na wewe mpaka basi. Nakuamb9ia hivi ujue kuwa kama hawezi kukuhudumia kama mke basi hawezi kukuhudumia kama Mama wa watoto wake. Tena hapa mnielewe, unajua sisemi labda mwanaume ana hela u la, mwanaume kuhudumia mke haina uhusiano na hela, hapana bali ni ule utayari wa kubeba majukumu.

Kwamba usijipe moyo kuwa yeye ana hela basi atahudumia, hapana huhitaji kuwa bilionea kuhudumia mtoto. Kinachoshidna wengi ni zile kero za mtoto hivyo wengi wanakua hawako tayari na kukimbia. Hembu jiulize tofauti ya kuoa na kuzalisha mwanamke. Kuoa inamaana anakuchukua wewe mtu mmoja, mnaishi naye tena mtu mzima anakuhudumia wewe na kama ni kero basi ni zako mwenyewe.

Lakini sasa kuhudumia mtoto nialzima uhudumie watu wawili, kwamba ili mtoto ashibe ni alzima mama ashibe, ili mtoto awe na furaha ni lazima mama awe na furaha hivyo ni sawa na kuoa mara mbili. Sasa kama hawezi kuoa hiyo mara moja hiyo ya pili ataiweza wapi? Nimalize kwa kusema na kurudia tena nyie ambao mnaniuliza hili swali kila siku kuwa kaniambia tuzae kwanza? Jibu ni moja zaa kama unataka kuwa single mother ila kama ni kuolewa dada yangu hapana!

Si semi wote hawaoi hapana wapo wengi tu wanaoa lakini wakati anakuambia kuwa umzalie kwanza unatakiwa kujua kuwa hajapanga kukuoa, atapanga huko baadaye, anakuambia umzalie kwakua anjua unaweza kulea basi. Naomba leo nimalizane na hii mada, sikukatazi kubeba mimba ila beba ukijua kuwa huyo unayembebea hatataka umsumbue huko mbeleni, siku akichoka kulea na kuondoka basi uwe tayari kulea pake yako na si kusumbua watu wa ustawi wa jamii!

Iddi Makengo facebook

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom