Amicus Curiae
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 5,351
- 7,639
- Thread starter
- #121
Nimesema ninachokiamini mkuu.Kumtetea ndo ujinga unapoanzia, Uyo anabandulia kwingi kwingi ndo maana hana msimamo juu yako.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimesema ninachokiamini mkuu.Kumtetea ndo ujinga unapoanzia, Uyo anabandulia kwingi kwingi ndo maana hana msimamo juu yako.
Lakini sasa hivi si tupo mkuu? Lazima tuishi sasa sio baadaye.Miaka 300. ijayo wote hatutakuwepo duniani ,! Pain najua unayo ishi mwamba achana na hizo habari ,,
###TUTASAHAULIKA#####
Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Gari mkuu, tena la juu.Nimeona umeandika kwamba "nikasimama kwanza ili nisisabishe ajari", kwahiyo mkuu una gari au una honda au una baiskel,, au ulimanisha ajari ya kugongwa?
Wakili wa KujitegemeaUnafanya kazi gani?
Ukiionesha kumtaka saana basi ndio anakuwa na advantage juu Yako.Please elaborate...
Sawa mkuu.mpe muda
Atarudi, kaa tu hivyo utashangaa anarudi mwenyewe. Wanawake wa hivyo wanajulikana, wanayumbishwa sana ila huyu atarudi tu.Achana na utamu, alikuwa ni mwanamke aliyekidhi vigezo vyangu vyote mkuu.
Samalekooo ✋!Auntie....🤗🤗🤗
Hoja yangu usibebe mizigo usiyoiweza bure wakati hata ukifa watu wataendelea na mishe zaoLakini sasa hivi si tupo mkuu? Lazima tuishi sasa sio baadaye.
W.salamu za wewe aunt..Samalekooo ✋!
Mkuu, nakushukuru sana kwa busara hizi.Na pia nadhani ulijitoa sana kwake kwa kila kitu. Going forward be careful unapodeal na mwanadamu; na angalau uwe tayari kwa lo lote maana mwanadamu anaweza kubadilika wakati wo wote.
Lakini pia kama malengo yako yalikuwa safi kwa huyu binti (if your intentions were pure) basi ondoka na dhamira safi huku ukijua kuwa hukumpotezea muda wake...and the Universe will reward you handsomely. Mwache aende na mtakie mema ila usije ukashangaa huko mbele ya safari kama atataka kurudi tena.
Kwa sasa hakuna njia ya mkato. Kuumia ni lazima utaumia lakini utavuka. Kwa kadri muda unavyokwenda maumivu nayo polepole yatapungua; na nati hizo zinazokaza kwenye moyo zitaanza kuachia na furaha yako itarudi.
Sasa umekua!
Asante sana mkuu. Nakushukuru mno. Sasa naamini kwamba watu wema bado mpo JF, wengine wanaishia kunifanyia mizaha tu humu.Bora Huyo alokwambia live unajua na kushika 50 zako .. kuna miamba inaacha kimya kimya no calls no sms no o anything mwisho wa siku ujiongeze mwenyewe tu kuwa nishaachwa. !
Mapenzi ni Hekaheka mkuu Mungu akuponye majeraha yako haraka!
Angekuwa hajasema tungekuwa hapa kwenye huu uwanja...?Mbona bado ajasema...!!!🤓🤓🤓😂😂
Inauma sana.
Pole sana,tunda limeponyoka kimasihara🤩🤩🤩Maisha ni lazima yaendelee.
Nakiri kwamba nilikuwa malaya sana zamani lakini nikaamua kubadilika baada ya kugundua kwamba mahusiano mengi kwa wakati mmoja yanapoteza muda, rasilimali fedha, yanadhoofisha mwili, akili n.k.
Nimekuwa kwenye mahusiano serious kwa takribani mwaka na nusu na Mwl mmoja wa Shule ya msingi. Mpole, msikivu, mcha Mungu, mnyenyekevu, sio mbinafsi, mshauri mzuri na zaidi ya yote amekuwa mfano bora wa mama wa familia. Nikaamua kumpenda kwa dhati. Nikawaambia hadi ma-x wangu. Nikawa najiachia nae, nikamtambulisha kwa baadhi ya wana.
Nikakaa kitako na Baba nipeleke barua ya posa, binti akaridhia. Barua ikaandikwa, mwanangu mmoja ambaye ameshaoa akakubali kuwa mshenga. Barua ilikuwa ipelekwe tangu j5 ya wiki iliyopita ila nikapata dharura tukaahirisha. Ilikuwa baada ya kupeleka posa ndio nikamtambulishe home.
J'mosi ya juzi akaanza kubadilika kuanzia kwenye mawasiliano na kila kitu. Jana nampigia simu aniambie barua tupeleke lini, akashtuka kama hajui kinachoendelea! Akajibu nisubiri kwanza, mara anaomba tupeane muda kuna mambo ajiridhishe!
Nikajiongeza, nikamwambia muda siwezi kumpa kwasababu tulishalizungumza hili. Aseme tu kama anadhani hatuwezi kuwa pamoja tena nitamuelewa. Akasisitiza nimpe muda! Nikamjaribu kwa kumwambia tuachane ili tusipotezeane muda (kumbuka hapa nilikuwa namjaribu); ili nione anawaza nini.
Lahaulaa, akasema 'SAWA'. Nikaishiwa nguvu. Nilikuwa barabarani nikasimama kwanza kwasababu nilipatwa na wenge nikahisi naweza kusababisha ajali.
Ina maana ile kupenana muda ilikuwa ni gia tu, alishaamua tuachane. Sikumtafuta tena tangu jana na yeye kakaa kimya mpaka muda huu!
Huyu ni msichana aliyeniaminisha kwamba hawezi kuniacha. Kwamba hata nikijaribu kumuacha atafanya jambo baya (ni kama alikuwa anatishia kujiua).
LAWAMA ZANGU ZOTE NAZIELEKEZA KWA RAFIKI YAKE MWENYE JINA LINALOANZA NA HERUFI 'J', ANAYEISHI MKOA UNAOANZA NA HERUFI 'M'. Mpenzi wangu alikuwa anamsikiliza sana, na mara nyingi wamekuwa wakiniongelea, nina kila sababu ya kuamini kwamba ushauri wake umechangia kumfanya mwanamke wangu afikie uamuzi huu. Huyu dada yeye kaolewa, leo kaamua kumfanyia figisu rafiki yake! We dada wewee....
Biblia imesema tushukuru kwa kila jambo. Pengine kuna jambo Mungu ameniepusha nalo. Naumia ila najikaza.
Sawa mkuu. Nimekuelewa sana.Kama ana hizo Sifa unazotaka hebu mpe muda kidogo, hujui kafikwa na lipi, usiseme Neno la mwisho!!