Kodi haina bargains; kuna set up percentage ya import duty kutokana na bei ya kitu ulichonunua, ndio maana invoice inakuwa attached; sasa hapa wengi huwa wanacheza na invoice kuweka bei ndogo ili ulipe kidogo, lakini TRA wana mwongozo wao wa bei za vitu ambazo mara nyingi zinakuwa juu kidogo ila kama una documentation, invoice na receipts za malipo inaweza kusaidia, ila kama bei ni ndogo sana TAX officer atabisha na tatizo mzigo ukikaa sana unaweza kuanza kulipia storage, pia kumbuka kuna charges nyingine tofauti tofauti..
Ukiagiza mzigo wowote kama sio Door to Door (yaani mfano kina DHL, UPS, TNT ambao wanatoa pia service za clearing) yaani ukitumia air cargo au meli lazima utumie clearing and forward agent ambaye ndio anaruhusiwa kukutolea mzigo na charges zao huwa ni kama laki na zaidi kwa kila consignment, tatizo mara nyingine hawa wanakuwa waongo wanazidisha pesa ili wadanganye wale ganji na tax officers, ila kama ni wakweli watumie hao hao muongee na TAX officer vizuri ili aweze kufanya mabadiliko, kumbuka kama kwenye mtandao wao TRA wanajua bidhaa fulani nje huwa ni dollar kumi, hata kama ulinunua kwa dollar moja kwa ku-bargain hawatakubaliana kamwe na hio invoice watajua umedanganya