Nimeagiza mzigo wangu wa kwanza China kodi niliyokadiliwa na TRA ni kubwa mno je nawezaje kuomba kupunguziwa wakuu nishaurini nimechanganyikiwa

Siku hizi watu wanaweka adress za Rwanda mzigo unampita Bongo anauchukulia Rwanda...ila Sirikali yetu na sera zake ni kituko sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kodi haina bargains; kuna set up percentage ya import duty kutokana na bei ya kitu ulichonunua, ndio maana invoice inakuwa attached; sasa hapa wengi huwa wanacheza na invoice kuweka bei ndogo ili ulipe kidogo, lakini TRA wana mwongozo wao wa bei za vitu ambazo mara nyingi zinakuwa juu kidogo ila kama una documentation, invoice na receipts za malipo inaweza kusaidia, ila kama bei ni ndogo sana TAX officer atabisha na tatizo mzigo ukikaa sana unaweza kuanza kulipia storage, pia kumbuka kuna charges nyingine tofauti tofauti..

Ukiagiza mzigo wowote kama sio Door to Door (yaani mfano kina DHL, UPS, TNT ambao wanatoa pia service za clearing) yaani ukitumia air cargo au meli lazima utumie clearing and forward agent ambaye ndio anaruhusiwa kukutolea mzigo na charges zao huwa ni kama laki na zaidi kwa kila consignment, tatizo mara nyingine hawa wanakuwa waongo wanazidisha pesa ili wadanganye wale ganji na tax officers, ila kama ni wakweli watumie hao hao muongee na TAX officer vizuri ili aweze kufanya mabadiliko, kumbuka kama kwenye mtandao wao TRA wanajua bidhaa fulani nje huwa ni dollar kumi, hata kama ulinunua kwa dollar moja kwa ku-bargain hawatakubaliana kamwe na hio invoice watajua umedanganya
 
Maelezo yako sahihi kabisa ila hapo pa kusema Agent anaweza kutaka kula ganji na Tax officer kwenye kodi, nadhani sio sahihi kwa miaka hii labda zamani maana kuna mfumo wa makadilio ya kodi ambapo unalipa kwa control namba
Sent using Jamii Forums mobile app
 
makadirio unayopewa na agent yanakuwa fake yaani ile information sio ya kweli ili muongee aseme mcheze na invoice muweke info tofauti kwa gharama fulani kwa ujira fulani kwahio utakacholipia utaona kwamba ni kidogo kutokana na bargaining na msaada wa agent hence utatoa bakshishi
 
kama umefanya mzigo kuwa siri utapaje msaada
 
Sioni cha kuongezea hapa.

Kazi kwako mleta uzi....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu huyo agent wako ametumia HS CODE sahihi ?
 
Wapo humu akitaja tu sina ya mzigo na kodi aliyokadiriwa watampata kiurahisi sana!
Labda awe amepanga kudisclose I'd yake!
Ni kweli,angeweza kutaja kwa ujumla tu kama vitu vya electronics,plastic n.k wenye mizigo bandarini ni wengi
 
One third ni theluthi aka 1/3 na si robo tatu......1/3 pia ni 33.3%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…