Nimeambiwa wanaoingia sekondari shule za serikali mtaala ni wa Kiswahili kwa masomo yote

Nimeambiwa wanaoingia sekondari shule za serikali mtaala ni wa Kiswahili kwa masomo yote

kwa-muda

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2018
Posts
2,097
Reaction score
5,348
Wana JF mimi si mwandishi mzuri kwa sababu niliishia na 5B, lakini ningependa tujadili suala fulani kuhusu elimu.

Toka serikali ijipange kwamba inabadilisha mtaala watoto primary watasoma kwa miaka sita, kuna mambo mengi ambayo bado hayajaeleweka. Hivyo nilielezwa na mwalimu jana haya yafuatayo:
Kwamba, wanafunzi ambao mwaka huu wako la tatu, hao ndiyo ambao wataishia la sita.

Hapa sasa nikawaza, kama kwenye shule za serikali kila mwaka madarasa na madawati hayatoshi, ina maana mwaka hao wanafunzi wa la 3 watakapokuwa wamehitimu la sita ili waendelee na sekondari, ndiyo huo huo mwaka ambao wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la nne mwaka huu watakapokuwa wanahitimu la saba ili nao waende sekondari. Ina maana kutakuwa na maelfu ya wanafunzi wanaoingia sekondari.

Sasa, sijui shule zetu zitaweza kuwapokea wote au maandalizi yatakuwa tayari au tutaanza kujiandaa baada ya kufika huo mwaka.

Nikaambiwa pia kuwa, mtaala umebadilika masomo ya sekondari yanafundishwa kwa kiswahili tena kuanzia wanaoingia sekondari mwaka kesho kwa shule za serikali. Hili sina hakika kama ni kweli, ila kama ni kweli je, tumejiandaa kwa vitabu.

Kama kuna jambo gumu ni kufundisha sayansi kwa kiingereza maana terms nyingi mwisho wa siku huwa tunarudia kuzitamka kwa kiingereza. Na kama vitabu tu vya kiingereza primary hivi vipya vina makosa mengi, itakuwaje pale vitabu vya chemistry, physics, biology vitakapotafsiriwa kwa kiswahili. Sijui serikali imejipanga vipi hapo.

Mtazamo wangu:
Najua watu watatoa mifano ya Ufaransa, China, Urusi na nchi kibao kuwa wanafundisha kwa lugha zao husia na wana maendeleo makubwa. Ila sidhani kama walifanya hivyo kwa kukurupuka. Nawaza kama hao watoto wakimaliza form 4, je, 5 na 6 nako wataenda kusoma kwa kiswahili?

Na kama lengo ni elimu iwe kwa kiswahili, mbona kwa sasa kuna shule nyingi za serikali zimejengwa ambazo zinafundisha kwa kutumia kiingereza? Mfano bunju nafahamu mbili baada ya moja kufungwa kwa sababu ilijengwa kwenye mkondo wa maji.

Vipi chuo? Wataenda kusoma kwa Kiswahili. Je, wataweza kucompete kwenye soko la ajira la kimataifa Isije kuwa wanaofanya na kuandaa haya, watoto wao wanasoma shule za mitaala ya Kiingereza tu mwanzo mwisho kwa sababu wanajua hii mitaala it won't work.

Sema, ifike wakati masuala ya elimu serikali iwe nayo serious. Hapa kuna uwezekano awamu nyingine akaja mwingine akabadilisha haya yote.
 
Kuhusu kuanza kwa mtaala wa Kiswahili sijui.
Kuanzishwa kwa utitiri wa state owned English Medium P/schools inaweza kuwa ndio maandalizi menyewe kwani watakaposwichi kwenda Kiswahili, wazazi wengi watapendelea watoto kusoma mtaala wa kimombo na hapa ndipo dili litakuwa limetiki kwa sirikali kupiga hela na ada itapanda halafu kule kwa waswahili itakuwa free education.
HAYO NI MAWAZO YANGU TU.

Kuhusu upungufu wa samani, hilo halitakuwepo kwa namna unavyofikiria kwani form one wa zama hizo watasoma masomo yao ya sekondari hapo hapo wanaposoma masomo ya shule ya msingi.
 
Nikaambiwa pia kuwa, mtaala umebadilika masomo ya sekondari yanafundishwa kwa kiswahili tena kuanzia wanaoingia sekondari mwaka kesho kwa shule za serikali. Hili sina hakika kama ni kweli,
Pata uhakika kwanza kabla ya kuleta jambo humu kujadiliwa.

Ila nakuhakikishia hakuna kitu kama hicho
 
Kosa letu la kwanza primary education kufundisha masomo yote kiswahili.
Kosa litakuzwa maradufu kufundisha masomo yote ya secondary education kwa kiswahili.
 
Hilo suala halipo kwa sasa, utaratibu wa lugha ya kufundishia kwa sekondari ni kiingereza isipokuwa somo la kiswahili na somo jipya la Historia ya Tanzania na maadili.

Kwa shule ya msingi hizi za swahili media somo la kiswahili litatumika kufundishia masomo yote isipokuwa somo la kiingereza pekee.
 
Kuhusu kuanza kwa mtaala wa Kiswahili sijui.
Kuanzishwa kwa utitiri wa state owned English Medium P/schools inaweza kuwa ndio maandalizi menyewe kwani watakaposwichi kwenda Kiswahili, wazazi wengi watapendelea watoto kusoma mtaala wa kimombo na hapa ndipo dili litakuwa limetiki kwa sirikali kupiga hela na ada itapanda halafu kule kwa waswahili itakuwa free education.
HAYO NI MAWAZO YANGU TU.

Kuhusu upungufu wa samani, hilo halitakuwepo kwa namna unavyofikiria kwani form one wa zama hizo watasoma masomo yao ya sekondari hapo hapo wanaposoma masomo ya shule ya msingi.
Mkuu ina maana hizo hizo shule za msingi zitaongezwa madarasa ziwe pia na sekondari? Vipi miundombinu ya majengo maana hili linakuwa tatizo kila mwaka madarasa na madawati? Nimesikia pia lazima kabla mtu hajamaliza form 4 apitie masomo ya ufundi kama veta. Najiuliza kama maabara tu zilikuwa kikwazo, hili litawezekana kweli au ndiyo mafunzo ya vitendo kusomwa kwa nadharia.
Hili la vocational training ni zuri, ila najiuliza kama litaweza kutekelezeka.
 
Mimi binafsi kugha ya kiswahili wala siifagiilii Bora tungekua tunaongea kingereza ndo dili sio kiswahili, hata kufundushia tuachane na kiswahili.
 
Mimi binafsi kugha ya kiswahili waka siifagiilii Bora tungekua tunaongea kingereza ndo dili sio kiswahili, hata kufundushia tuachane na kiswahili.
Mimi mwenyewe nina mawazo kama yako mkuu. Kwangu naona hili litaendelea kuwafanya vijana wetu wazidi kushindwa kushindana na vijana wengine katika soko la ajira.
 
Mm nilitegemea shule za selikali zianze kufundisha masomo yote kwa kingereza kuanzia darasa la 4,
Sekondari iwe kingereza mwendelezo sema kutakuwa na additional language subjects kama
Kifaransa
Kispain
Kireno
Kichina
Mwanafunzi lazima achague lugha walah moja kati ya izo aanze kujifunza
 
Unawaamini walimu wa shule za msingi. Kwanini usitafute taarifa wizara ya elimu? Walimu wa shule ya msingi sidhani kama watakua na taarifa nyeti kama hizo.
 
Back
Top Bottom