Nimeambiwa wanaoingia sekondari shule za serikali mtaala ni wa Kiswahili kwa masomo yote

Nimeambiwa wanaoingia sekondari shule za serikali mtaala ni wa Kiswahili kwa masomo yote

Mambo ya kipumbavu kabisa kuwahi kutokea unawaigaje wajapan,wachina na mataifa mengine yaliyoendelea kutumia lugha zao kufundishia na huu ukapuku wetu si ndio tunazidi kuzama gizani, kiswahili kinakupeleka wapi
 
Mm nilitegemea shule za selikali zianze kufundisha masomo yote kwa kingereza kuanzia darasa la 4,
Sekondari iwe kingereza mwendelezo sema kutakuwa na additional language subjects kama
Kifaransa
Kispain
Kireno
Kichina
Mwanafunzi lazima achague lugha walah moja kati ya izo aanze kujifunza
Walimu sasa wa hizo lugha nyinginezo kuacha kiingereza ndiyo hakuna kwa idadi kubwa.

Serikali ianzishe course ya ualimu yenye lugha nyingine kama kispain, kiItaly, kichina, kifaransa n.k ili sasa Walimu hao wakafundishe sekondari kuanzia kidato cha kwanza, na waweke ULAZIMA kwa mwanafunzi kuchukua somo mojawapo atakalofanyia NECTA ya form 4.

Na ili wanafunzi wawe siriazi na hizo lugha, warudishe PENALTI ya lazima endapo atafeli kama ilivyokua awali kwa Mathematics.
 
Luggage ndio nini, wachina bila kujua kiingereza wala wasingefika hapo walipo, tuulize sisi tunaofanya nao biashara, na mchina kama hajui kiingereza aajiriki na wana kiingereza safi sio hicho chenu cha prof.Ndalichako.
Uwenakiasi basi katika kuwelezea hao wachina wanoongea kiingereza safi maana sio wewe peke yako unayefanya kazi na wachina hapa Tanzania.
 
Hakika ni kurudi nyuma.
Kwa mantiki hii kwa upande wa ajira za kuajiriwa tunakuwa tunalenga soko la ndani tu ambalo nalo litabase kwenye ajira za Serikali kwa kiasi kikubwa.

Wakenya na Wanyarwanda wataendelea kutake over.
Na wanaopanga hiyo mipango watoto wao hawasomi hizo shule.
 
Kung'ang'ania Kiswahili Kwa nchi masikini kama Tanzania ilihali haina technolojia wala viwanda kiasi cha watu kusimama na miguu yao ni UPUMBAVU NA KUENDELEA KUFANYA WATU MASIKINI.

Soko la ajira la ndani ni kichefuchefu, vijana wanamaliza shule hawana ajira na hatuwezi kuwaaccomodate kwenye soko la ndani, kijana inabiti avuke mipaka akajitafutie - huko aendako lugha ni kiingereza - NI KUUANA NJAA TU.
Soko la ndani la ajira Kwa kiasi kikubwa ni sekta binafsi ambako mahitaji ni lugha ya kiingereza, tena inawekwa kabisa kama moja ya kigezo cha kupata kazi na interview inakuwa ni kiiingereza kabisa.

Kiingereza kwasasa hakiepukiki, tumeshachelewa kukikwepa, tuweje nguvu na juhudi watu wetu waongee kiingereza waweze kupata fursa nyingi.

China kwasasa watu wanajifunza kiingereza Kwa nguvu ili waweze kuwasiliana na dunia nyingine, maana Kwasasa watu wao wanatoka sana nje ya mipaka yao.
Kingine wachina wananguvu ya kiuchumi hivyo watu wao na makampuni yao oversees wanakuwa na wakarimani kurahisisha kazi zao.
Mchina anatoa sana scholarship watu kwenda China kusoma na moja ya sharti ni kujifunza kuchina, tafsiri watu wengi watakuwa wanajua kuchina na kuwasiliana nao wanapokuwa oversee.
Mchina kupitia ushawishi wake wa kisiasa na kiuchumi, amelazimisha na kuinfluence watu kuongea kichina.
 
Wana JF mimi si mwandishi mzuri kwa sababu niliishia na 5B, lakini ningependa tujadili suala fulani kuhusu elimu.

Toka serikali ijipange kwamba inabadilisha mtaala watoto primary watasoma kwa miaka sita, kuna mambo mengi ambayo bado hayajaeleweka. Hivyo nilielezwa na mwalimu jana haya yafuatayo:
Kwamba, wanafunzi ambao mwaka huu wako la tatu, hao ndiyo ambao wataishia la sita.

Hapa sasa nikawaza, kama kwenye shule za serikali kila mwaka madarasa na madawati hayatoshi, ina maana mwaka hao wanafunzi wa la 3 watakapokuwa wamehitimu la sita ili waendelee na sekondari, ndiyo huo huo mwaka ambao wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la nne mwaka huu watakapokuwa wanahitimu la saba ili nao waende sekondari. Ina maana kutakuwa na maelfu ya wanafunzi wanaoingia sekondari.

Sasa, sijui shule zetu zitaweza kuwapokea wote au maandalizi yatakuwa tayari au tutaanza kujiandaa baada ya kufika huo mwaka.

Nikaambiwa pia kuwa, mtaala umebadilika masomo ya sekondari yanafundishwa kwa kiswahili tena kuanzia wanaoingia sekondari mwaka kesho kwa shule za serikali. Hili sina hakika kama ni kweli, ila kama ni kweli je, tumejiandaa kwa vitabu.

Kama kuna jambo gumu ni kufundisha sayansi kwa kiingereza maana terms nyingi mwisho wa siku huwa tunarudia kuzitamka kwa kiingereza. Na kama vitabu tu vya kiingereza primary hivi vipya vina makosa mengi, itakuwaje pale vitabu vya chemistry, physics, biology vitakapotafsiriwa kwa kiswahili. Sijui serikali imejipanga vipi hapo.

Mtazamo wangu:
Najua watu watatoa mifano ya Ufaransa, China, Urusi na nchi kibao kuwa wanafundisha kwa lugha zao husia na wana maendeleo makubwa. Ila sidhani kama walifanya hivyo kwa kukurupuka. Nawaza kama hao watoto wakimaliza form 4, je, 5 na 6 nako wataenda kusoma kwa kiswahili?

Na kama lengo ni elimu iwe kwa kiswahili, mbona kwa sasa kuna shule nyingi za serikali zimejengwa ambazo zinafundisha kwa kutumia kiingereza? Mfano bunju nafahamu mbili baada ya moja kufungwa kwa sababu ilijengwa kwenye mkondo wa maji.

Vipi chuo? Wataenda kusoma kwa Kiswahili. Je, wataweza kucompete kwenye soko la ajira la kimataifa Isije kuwa wanaofanya na kuandaa haya, watoto wao wanasoma shule za mitaala ya Kiingereza tu mwanzo mwisho kwa sababu wanajua hii mitaala it won't work.

Sema, ifike wakati masuala ya elimu serikali iwe nayo serious. Hapa kuna uwezekano awamu nyingine akaja mwingine akabadilisha haya yote.
Mtaala ulioboreshwa kwa kidato cha kwanza utaanza kutekelezwa mwakani, yaani 2025. Vitabu vya kiada vya kidato cha kwanza vipo tayari, na madarasa mengine maandalizi yanaendelea.

Mitaala iliyoboreshwa inapatikana kwenye website ya TET hapa TAASISI YA ELIMU TANZANIA (TET)
 
Back
Top Bottom