Nimeamini, kila zama ina kitabu chake. Leo Polepole ni Musiba 'aliyechangamka'. Siasa si mchezo!

Nimeamini, kila zama ina kitabu chake. Leo Polepole ni Musiba 'aliyechangamka'. Siasa si mchezo!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Alipata kusema Rais Mstaafu wa Tanzania wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kuwa 'kila zama ina kitabu chake'. Nami sasa nimeamini baada ya 'kuweka' tafsiri yangu binafsi kwenye msemo huo uliojaa hekima na busara kubwa. Binafsi nimetafsiri kuwa 'kila awamu ina wake wa 'kutrend''. Yaani, kila awamu ya urais wa nchi hii yupo kiongozi wa kiserikali au kichama au mwananchi wa kawaida tu anayesikika na kusomeka sana.

Nitatoa mifano minne. Ulipoanza uongozi wa Hayati Magufuli, alikuwepo Dada Mange Kimambi. Alisikika na kusomeka sana akiukosoa utawala wa Hayati Magufuli-tena kwa maneno makali makali. Alikuwepo pia mwanamtandao aitwaye Kigogo2014. Hawa waliikosoa Serikali ya hayati Magufuli na kujiweka kama wenye kujua 'siri' mbalimbali za viongozi na uongozi kwa ujumla wake. Wakapita na sasa wamepoa.

Katika wakati huohuo, alijitokeza Cyprian Musiba. Huyu alijipambanua kama mwanaharakati huru. Lakini, kimsingi, alikuwa mwanaharakati mtetezi wa kufa na kupona wa uongozi wa Hayati Magufuli. Yeye alitumia maneno makali, vitisho na kashfa kwa wale alioamini kuwa walikuwa wakimpinga Hayati Magufuli. Akasikika na kusomeka sana kupitia runinga, mitandao ya kijamii na magazeti. Akapita na kupoa.

Sasa, mara tu baada ya kuanza kwa uongozi wa Rais na Mama yetu Samia Suluhu Hassan, amejitokeza Humphrey Polepole. Yeye hakosoi wala hatetei moja kwa moja uongozi uliopo madarakani. Kuona kukosoa au kuunga kwake mkono ni hadi msikiaji au msomaji atafakari kwa kina. Wapo wanaomuona kuwa ni mkosoaji wa serikali hii. Wapo wanamuona kuwa ni muungaji mkono wa serikali hii.

Polepole-akitokea kuwa mjasiriamali na mwanaharakati, Mjumbe wa Tume ya Katiba, Kiongozi wa serikali (Mkuu wa Wilaya) na chama (Katibu Mwenezi wa CCM) na sasa ni Mbunge wa kuteuliwa na Rais. Polepole amejibanza kwenye kutoa 'darasa' na elimu ya uongozi. Huchombeza pia kwa kukemea matendo na maneno ya viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao. Ndiyo hapo anapoonekana kuwa mkosoaji.

Polepole sasa ni Musiba mpya-lakini yeye amechangamka kwa kuficha lengo lake la moja kwa moja la maneno na matendo yake. Polepole ni kitabu cha zama hii. Ni anaye-trend kuliko wengine. Hawa wote-Kimambi, Kigogo2014, Musiba na Polepole hutumiwa na nani na maslahi gani? Tuendelee kufanya tafakuri za kisiasa.
 
Hakuna anaemtumia Polepole zaidi ya Polepole mwenyewe na tumbo lake. Polepole anamithilika na hawara alieahidiwa ndoa halafu dakika ya mwisho akatoswa na kuolewa mtu mwingine. Mwanamke akiachwa solemba baada ya kuwa aliahidiwa ndoa na huku alikuwa akipewa kila matunzo huanza kebehi za kila aina. Utasikia mwanaume mwenyewe hajiwezi kitandani, ana ukimwi n.k. Lakini kila wasaa atakaopata atampigia bwana kujiliza na kuomba kurudiwa.
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Polepole sasa, amekuwa kama Sungura wa sizitaki mbichi hizi. Leo hii Polepole akipewa wadhifa wa maana darasa litaisha, kukosoa kutaisha na atakuwa muimba mapambio mzuri sana. Adui wa Polepole ni tumbo lake mwenyewe.
 
Nape Nnauye njoo usome hapa.
Screenshot_20211216-084130_Lite.jpg
 
Hakuna anaemtumia Polepole zaidi ya Polepole mwenyewe na tumbo lake. Polepole anamithilika na hawara alieahidiwa ndoa halafu dakika ya mwisho akatoswa na kuolewa mtu mwingine. Mwanamke akiachwa solemba baada ya kuwa aliahidiwa ndoa na huku alikuwa akipewa kila matunzo huanza kebehi za kila aina. Utasikia mwanaume mwenyewe hajiwezi kitandani, ana ukimwi n.k. Lakini kila wasaa atakaopata atampigia bwana kujiliza.
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Polepole sasa, amekuwa kama Sungura wa sizitaki mbichi hizi. Leo hii Polepole akipewa wadhifa wa maana darasa litaisha, kukosoa kutaisha na atakuwa muimba mapambio mzuri sana. Adui wa Polepole ni tumbo lake mwenyewe.
It makes sense Mkuu
 
Alipata kusema Rais Mstaafu wa Tanzania wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kuwa 'kila zama ina kitabu chake'. Nami sasa nimeamini baada ya 'kuweka' tafsiri yangu binafsi kwenye msemo huo uliojaa hekima na busara kubwa. Binafsi nimetafsiri kuwa 'kila awamu ina wake wa 'kutrend''. Yaani, kila awamu ya urais wa nchi hii yupo kiongozi wa kiserikali au kichama au mwananchi wa kawaida tu anayesikika na kusomeka sana.

Nitatoa mifano minne. Ulipoanza uongozi wa Hayati Magufuli, alikuwepo Dada Mange Kimambi. Alisikika na kusomeka sana akiukosoa utawala wa Hayati Magufuli-tena kwa maneno makali makali. Alikuwepo pia mwanamtandao aitwaye Kigogo2014. Hawa waliikosoa Serikali ya hayati Magufuli na kujiweka kama wenye kujua 'siri' mbalimbali za viongozi na uongozi kwa ujumla wake. Wakapita na sasa wamepoa.

Katika wakati huohuo, alijitokeza Cyprian Musiba. Huyu alijipambanua kama mwanaharakati huru. Lakini, kimsingi, alikuwa mwanaharakati mtetezi wa kufa na kupona wa uongozi wa Hayati Magufuli. Yeye alitumia maneno makali, vitisho na kashfa kwa wale alioamini kuwa walikuwa wakimpinga Hayati Magufuli. Akasikika na kusomeka sana kupitia runinga, mitandao ya kijamii na magazeti. Akapita na kupoa.

Sasa, mara tu baada ya kuanza kwa uongozi wa Rais na Mama yetu Samia Suluhu Hassan, amejitokeza Humphrey Polepole. Yeye hakosoi wala hatetei moja kwa moja uongozi uliopo madarakani. Kuona kukosoa au kuunga kwake mkono ni hadi msikiaji au msomaji atafakari kwa kina. Wapo wanaomuona kuwa ni mkosoaji wa serikali hii. Wapo wanamuona kuwa ni muungaji mkono wa serikali hii.

Polepole-akitokea kuwa mjasiriamali na mwanaharakati, Mjumbe wa Tume ya Katiba, Kiongozi wa serikali (Mkuu wa Wilaya) na chama (Katibu Mwenezi wa CCM) na sasa ni Mbunge wa kuteuliwa na Rais. Polepole amejibanza kwenye kutoa 'darasa' na elimu ya uongozi. Huchombeza pia kwa kukemea matendo na maneno ya viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao. Ndiyo hapo anapoonekana kuwa mkosoaji.

Polepole sasa ni Musiba mpya-lakini yeye amechangamka kwa kuficha lengo lake la moja kwa moja la maneno na matendo yake. Polepole ni kitabu cha zama hii. Ni anaye-trend kuliko wengine. Hawa wote-Kimambi, Kigogo2014, Musiba na Polepole hutumiwa na nani na maslahi gani? Tuendelee kufanya tafakuri za kisiasa.
Nakutafuta sana wakili
Alipata kusema Rais Mstaafu wa Tanzania wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kuwa 'kila zama ina kitabu chake'. Nami sasa nimeamini baada ya 'kuweka' tafsiri yangu binafsi kwenye msemo huo uliojaa hekima na busara kubwa. Binafsi nimetafsiri kuwa 'kila awamu ina wake wa 'kutrend''. Yaani, kila awamu ya urais wa nchi hii yupo kiongozi wa kiserikali au kichama au mwananchi wa kawaida tu anayesikika na kusomeka sana.

Nitatoa mifano minne. Ulipoanza uongozi wa Hayati Magufuli, alikuwepo Dada Mange Kimambi. Alisikika na kusomeka sana akiukosoa utawala wa Hayati Magufuli-tena kwa maneno makali makali. Alikuwepo pia mwanamtandao aitwaye Kigogo2014. Hawa waliikosoa Serikali ya hayati Magufuli na kujiweka kama wenye kujua 'siri' mbalimbali za viongozi na uongozi kwa ujumla wake. Wakapita na sasa wamepoa.

Katika wakati huohuo, alijitokeza Cyprian Musiba. Huyu alijipambanua kama mwanaharakati huru. Lakini, kimsingi, alikuwa mwanaharakati mtetezi wa kufa na kupona wa uongozi wa Hayati Magufuli. Yeye alitumia maneno makali, vitisho na kashfa kwa wale alioamini kuwa walikuwa wakimpinga Hayati Magufuli. Akasikika na kusomeka sana kupitia runinga, mitandao ya kijamii na magazeti. Akapita na kupoa.

Sasa, mara tu baada ya kuanza kwa uongozi wa Rais na Mama yetu Samia Suluhu Hassan, amejitokeza Humphrey Polepole. Yeye hakosoi wala hatetei moja kwa moja uongozi uliopo madarakani. Kuona kukosoa au kuunga kwake mkono ni hadi msikiaji au msomaji atafakari kwa kina. Wapo wanaomuona kuwa ni mkosoaji wa serikali hii. Wapo wanamuona kuwa ni muungaji mkono wa serikali hii.

Polepole-akitokea kuwa mjasiriamali na mwanaharakati, Mjumbe wa Tume ya Katiba, Kiongozi wa serikali (Mkuu wa Wilaya) na chama (Katibu Mwenezi wa CCM) na sasa ni Mbunge wa kuteuliwa na Rais. Polepole amejibanza kwenye kutoa 'darasa' na elimu ya uongozi. Huchombeza pia kwa kukemea matendo na maneno ya viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao. Ndiyo hapo anapoonekana kuwa mkosoaji.

Polepole sasa ni Musiba mpya-lakini yeye amechangamka kwa kuficha lengo lake la moja kwa moja la maneno na matendo yake. Polepole ni kitabu cha zama hii. Ni anaye-trend kuliko wengine. Hawa wote-Kimambi, Kigogo2014, Musiba na Polepole hutumiwa na nani na maslahi gani? Tuendelee kufanya tafakuri za kisiasa.
Nakutafuta sana wakili
 
..Samia wakati Magufuli yuko hai alikuwa ktk genge linalodai miradi zinajengwa kwa kutumia fedha za ndani.

..Samia baada ya Magufuli kufa kabadili kauli anadai miradi yote imekuwa ikijengwa kwa mikopo.
 
Pole pole ametoka katika genge la matapeli waliokuwa wanapiga pesa za wazungu wakijifanya Wana NGO, kaibia sana wazungu
 
Back
Top Bottom