Nimeamini Tanzania tuna vichambuzi uchwara vya michezo

Au waende wakaajiliwe kwenye magazeti, radio na tv za timu husika. Mfano, Mimi nikisoma gazeti la Uhuru sishangai kuona CCM imesifiwa sana, lakini nikisoma gazeti la Mwananchi na kuona CCM inasifiwa kupita kiasi nitajiuliza maswali mengi, what happened.
 
Kiemba na Ally Mayai tu ndio wachambuzi bongo .

waliobaki ni takataka tu mpira uchambue ukiwa uliucheza kwa kiwango Cha juu.
Uko sahihi mkuu, hata walio na elimu ya ukocha pia wakina Dominick salamba na George ambangile
 
Job wa wasafi nilimsikia anatoa mbofu Kuhusu Zahera na Cédric kurudi Yanga. Ambangile nae aliwapa Simba ushindi. Stupid kabisa hawa wachambuzi njaa.
 
Waandishi Wa Habari Fulani Wako Kwenye Hizi Platform za Radio kutoa Machungu Yao Dhidi Ya Viongozi Wa Team Fulani.

Jemadari Kwa SSa Ana Hasira Na Yanga Kisa Yule Goli Kipa Wake Alitemwa ndio Maana anatema Sana Nyongo
Anatumia mike kuleta mtafaruku kati ya mchezaji na mchezaji, mchezaji na mwalimu, mwalimu na uongozi, uongozi na mdhamini na kiongozi na TFF. Wanamsema mchezaji hadi kumkatisha Tamaa utadhani ni mtoto wao. Kama unataka kumshauri mchezaji, kocha, kocha au kiongozi kwanini usimuite au kumpigia simu badala ya kutumia mike kumzungumzia maisha binafsi ya mchezaji.
 
Yule ni kilaza sana.
 
George JOB hataki kuisifia Yanga kisa ataonekana anamsifia mdogo ake DCKSON JOB
Hizi zama huwa zinabadilika na wanashindwa kujua kwamba ile simba ilikuwa imetengenezwa nyuma ya clatous chota chama na mafanikio ndo yalianzia hapo
 
George JOB hataki kuisifia Yanga kisa ataonekana anamsifia mdogo ake DCKSON JOB
Anatakiwa kusema kilichoko sio kusifia au kulaumu. Kuhoji kwanini Cedric amerudi tena yanga si amuukize Cedric badala ya kumponda kwenye redio? Mbona akina Morihno, Zidane, nk wanaondoka na kurudi kwenye timu zao. Kurudi kama kocha msaidizi au Mkurugenzi Kuna shida gani? Unafahamu wamekubaliana nini?
 
Ushindi unakufanya usahau tulipotoka au unamapenzi tu na hao makocha. Zahera kipindi anafundisha Yanga Fc hatukuwa tunacheza vizuri ni bahati ilikuwa inatubeba, mechi nyingi ilikuwa tunategemea ajibu apige pass au cross moja nzuri kwa Makambo afunge shughuli iishe zaidi ilikuwa hakuna cha maana tunacheza mechi nzima. Kaze nae alifeli tofauti na tulivyoaminishwa kwamba anafundisha mpira wa kuvutia na ana uwezo wa kunyanyua uwezo wa wachezaji.
Binafsi pia sijafurahia kurudi kwa hao watu wawili. Mifano uliyotoa kuhusu makocha wa ulaya kurudi kwenye timu za awali walizofundisha ni kwamba hao walishaleta mafanikio kipindi wanafundisha hizo timu kitu ambacho hawa makocha tuliowarudisha hawana.
 
Mtoa mada hujalazimishwa kuwasikiliza,kama wanakukera hamisha stesheni.

Hata wewe unaweza kuwa mchambuzi ukitaka.
 
Sikuungi mkono, Zahera pamoja na kukuta timu yenye wachezaji waliovunjika moyo kwa ukata lakini alishikwa nafasi ya pili kwenye ligi. Wachezaji muhimu walikuwa na migomo ya wazi na migomo baridi. Hata Barcelona ilikuwa inamtegemea Messi, Real Madrid Ronaldo, PSG Naymar kupata ushindi, Simba Chama na Miquissone. Kuna shida gani Zahera kuwategemea Ajib na Makambo kupata magoli?

Kaze kakuta wachezaji wameletwa hapo na watu wasiojulikana, alikuwa anahaika kupata kikosi chake Cha ushindi kutoka kwa wachezaji ambao aliwakuta. Hawa walikuwa ni wachezaji walikuwa hawapati matokeo pia kwa makocha 3 waliomtangulia Cedric.

Unasema uongo kuhusu Zahera na Cedric, mazingira Yao yalikuwa sio wezeshi.
 
Well said.
 
Chama na Miquissone wanategemewa lakini timu inacheza vizuri kitu ambacho hakikuwepo Yanga Fc. Kipindi cha Zahera kulikuwa hakuna system of play muda mwingi tulikuwa nyuma tu tunategema counter hii kwangu naona haikuwa sawa sababu wachezaji tuliokuwa nao walikuwa bora kuliko timu nyingi za ligi kuu wakati ule. Timu inaweza kucheza vizuri na isipate matokeo kutokana na ubora wa wachezaji fulani mf.( Timo Werner na ukosaji wa nafasi za wazi) lakini hiyo haiondoi umuhimu wa kucheza vizuri kwa sababu ni rahisi kufanya marekebisho.

Kuhusu Kaze hakukuwa hata na dalili ya improvement kwahiyo nae ni wa kawaida aliefanyiwa promo kubwa. Kipindi cha Luc Eymael kidogo Yanga ilianza kuonesha mwanga kabla kufukuzwa kwa ubaguzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…