Nimeanza kutumia PEP saa ya 38 tangu kujichoma sindano ya mtu aliyeathirika na VVU

Baada ya kumaliza utapima tena, halafu utapima tena (watakuelekeza muda wa kupima mara ya tatu)...
Kwaiyo Mara zote izo kusubuiria unakua haushiriki tendo au nihuu mwezi mmoja tu baada ya hapo ukipima ukiwa negative unaendelea kufanya tendo la ndoa
 
Mkuu saiv Wala hazina maudhi yoyote ni Kama za kawaida izo ndoto na kuona maluweluwe ni zamani sio kwa sasa,
 
Mzee komaa sana... Malza dozi...

We nae ni mtaalamu wa afya,,, au ndio ulileta demu getto mkachomana na lancet moja wote wawili????

Tumia dozi na next time kuwa makini,,, hio dawa huwa ina matokeo chanya kwa walio wengi so usiwe na shaka
 
Mkuu saiv Wala hazina maudhi yoyote ni Kama za kawaida izo ndoto na kuona maluweluwe ni zamani sio kwa sasa,
Naam Mkuu wangu, Mapokezi ya hizo dawa toka kwa MTU mmoja hadi mwingine ni tofauti kabisa.



Zamani wakati IPO Efavirenz kwenye regimen ya TLE ,changamoto izo zilikua nyingi, kuja kwa Dolutegravir , kwa wengine kumewaondolewa hayo maudhi, wengine bado wanayapata hasa hasa mwezi wa kwanza wa Utumiaji.


TLD ni more advanced...kwa mtumiaji mzuri kabisa na zikamkubali ,,,, Aaahhh ngoma inogile.
 
Kwaiyo Mara zote izo kusubuiria unakua haushiriki tendo au nihuu mwezi mmoja tu baada ya hapo ukipima ukiwa negative unaendelea kufanya tendo la ndoa

Hadi utapoambiwa sasa ni salama...hapa kati watakushauri utumie condom...
 
[emoji38][emoji38][emoji38]nimecheka hapo kuota unapaa, mara unaitwa duh mbona balaa sasa
 
Mkuu saiv Wala hazina maudhi yoyote ni Kama za kawaida izo ndoto na kuona maluweluwe ni zamani sio kwa sasa,
Mbona minaota ndoto za ajabu ajabu Kama Jana usiku nimemeza nkaenda lala usiku nastuka naskia barid la hatar
 
Yaani ukachukua sindano uliyotumia kumchoma mteja mwathirika alafu ukaitumia kujichoma wewe.Wenzetu mkitumia sindano mnatunza hakuna kutupa?
 
Yaani ukachukua sindano uliyotumia kumchoma mteja mwathirika alafu ukaitumia kujichoma wewe.Wenzetu mkitumia sindano mnatunza hakuna kutupa?
Itakua katika process za kumchoma nae akajichoma kwa bahati mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…