Miezi kadhaa nyuma niliomba ushari kuhusu ujenzi. Leo narudi tena kwenu. Wazoefu na wajuzi mnisaidie.
Nitatumia tofali za kuchoma na ntajengea tope mpaka lenta ambapo ntamalizia kwa cement (ushauri wa fundi ni kwamba wakati wa upauaji tope halitahimili gonga gonga)
Nimeanza na msingi na kesho nategemea utakamilika ntaleta mrejesho hapa na gharama zake siku zijazo.
Ushauri wenu nauhitaji hapa.
Ukweli ni kwamba sitakua na uwezo wa kujenga hadi kupaua kwa mara moja nilipenda niende kwa steps.
Je, nitunze pesa mpaka zitakapo timia mpaka upauaji?? Au nijenge tu then stage ya upauaji isubiri kwa miezi mnne mpaka mitano?
Ramani niliyopewa ina roof plan ambayo sijaipenda sana je mafundi wa upauaji wanaweza kuja roof plan nzuri baada ya ujenzi kukamilika?
( Uzi huu utakua endelevu nataka uwe motivation kwa vijana wenzangu)
Gharama za MSINGI.
Wakati nanunua kiwanja kulikua na msingi mfupi wa ramani ya vumba viwili so ilinibidi nibomoe
So...
Mawe gari mbili @70,000 = 140000 hapa endapo usingekuepo mzingi ingenilazimu kununua trip 5
Mchanga gari mbili @60,000 = 120000 (huu utatumika mpaka lenta)
Maji (vinatumika visima) kusomba day 8000*3 =24000
Cement 6
20000 = 120000 zimetumika kucover nje na juu ya mawe msingi nimeyumia tope)
Fundi = 250000 (hapa fundi alitoa punguzo kutoka 350000) ametaget ujenzi wa boma apewe kazi (kulinda ofisi)/
Kamba na mambo = 15000 ( hapa fundi aliomba tu na nkampa kutoka na punguzo lake mana hua wanavyo hivi)
Usafi visiki na kubomoa msingi =20000
Kifusi = 50000 ( kipo kwa jirani yangu so nimetumia mahusiano tu) hapa kupunguza gharama ntaanza na shimo (chamber) udongo utatumika kama kifusi pia.
JUMLA 739,000 (KAMA NIKIWEKA NA GHARAMA NDOGO KAMA MAFUTA NK NI 750,000/-
Awamu ya kwanza imeishia hapa tutaendelea awamu yapi
UPDATES:
Baada ya kujenga msingi likaja swala la kujaza kifusi ambapo nilifikiria sana kuja ingehitaji gari 5 mpaka 6 kwa kila gari TSH 65,000/=
So ikanilazimu kuchumba shimo (chamber ya chooo) udongo utakaotolewa utumike kama kifusi.
Gharama ni kama ifuatavyo.
Kuchimba shimo Ft 14 (5*5) =195,000
Tofali 200 =210,000
Cement 4 =80,000
Fundi = 100,000
Wiremesh 1 + nondo mm12(1) +nondo mm 10 (5) + misumari ½ + mabanzi (7) + mbao 14 (za kukodi) + binding wire +maji + nk
GHARAMA ZA SHIMO MPAKA KUFUNIKA 736,000/=
KIFUSI KILIJAZA NA IKABAKI SEHEMU NDOGO SANAAA
NOTE.
KAZI YA KUJAZA KIFUSI NILIIFANYA MWENYEWE .
.............
MAPAKA SASA nimekwama kwenye msingi baada ya kugundua
1.mawe mengi yamesimamishwa badala ya kulazwa
2. Kina kifupi cha msingi japo ardhi ni ngumu ila kinanipa.mashaka.
Baadhi ya mafundi wanashauri niweke bim katika msingi, wengine wanasema hautaleta shida niendelee tu, mmoja alinambia atalaza nondo sehem zenye nyufa hata ndogoo tu itazuia, mwingine akasema nitafute angles muhimu niweke nguzo zitakazo kuja kuungana na bim ya msingi. mpaka sasa nimekwama cha kufanya
Ushauri wenu ni muhimu.... je nianze ujenzi au niimairishe msingi na nitumie mbinu gani kuuimarisha?
Salaaam.
Subscribe tujenge wote.