Nimechoka kuajiriwa sekta binafsi, vikampuni uchwara

Nimechoka kuajiriwa sekta binafsi, vikampuni uchwara

Jambo lolote ukitaka kupiga hatua lazima uwe na mipango ,Dar watu wanaishi kwasababu TU ya riziki ila si kwamba wanapakubali watu ni nyomii kwanini hayo mawazo yako usiyafanyie hapo hapo mkoani
Basi kama wanaishi kwa sababu ya riziki ni dhahiri kwamba riziki zipo na zinapatikana kwa haraka kulinganisha na mikoani.
 
Naombeni ushauri wadau waliofanikiwa baada ya kuwaza kama mimi. Mimi ni muajiliwa(kibarua) kampuni flani kwa sababu sina mkataba wowote sasa imefika muda kazi nimeifanya kwa muda mrefu sana nimechoka hivyo nataka nimwambie HR wa kampuni anipe barua yangu ya kuachishwa kazi ili niipeleke NSSF nikavute hicho kidogo kilichoko huko nikajiajiri Dar es Salaam.

N:B: Naishi mkoani, nimezaliwa mkoani, nimekulia mkoani lakinj ndoto zangu ni kuishi Dar na kuzeekea Dar.
 
Mwaka 2004 niliwahi kuwa na mawazo kama haya, nilipo chukua NSSF ilikwisha hata sikujua imeishaje.
Leo hii nimerudi, mwaka wa 20 kwenye ajira tuliokua tukiita (kazi za kijinga) na mafanikio nimeyaona aiseee
2004 ndo unaanza kazi duuh we ni mdogo wangu kabisa uwe unanisalimia mkuu
 
Jambo lolote ukitaka kupiga hatua lazima uwe na mipango ,Dar watu wanaishi kwasababu TU ya riziki ila si kwamba wanapakubali watu ni nyomii kwanini hayo mawazo yako usiyafanyie hapo hapo mkoani
Jamaa anapaswa aelewe licha ya dar kuwa na population kubwa ila maisha ni magumu mno! Ushindani wa kibiashara ni mkubwa mno kiasi kwamba hyo hela nsssf inaweza kuisha kabla hajasimama vizuri.
 
Naombeni ushauri wadau waliofanikiwa baada ya kuwaza kama mimi. Mimi ni muajiliwa(kibarua) kampuni flani kwa sababu sina mkataba wowote sasa imefika muda kazi nimeifanya kwa muda mrefu sana nimechoka hivyo nataka nimwambie HR wa kampuni anipe barua yangu ya kuachishwa kazi ili niipeleke NSSF nikavute hicho kidogo kilichoko huko nikajiajiri Dar es Salaam.

N:B: Naishi mkoani, nimezaliwa mkoani, nimekulia mkoani lakinj ndoto zangu ni kuishi Dar na kuzeekea Dar.
Fanya kitu roho inapenda ila ukweli nisiouficha ni kuwa Dar utaenda kupigika mpaka ukumbuke tukampuni uchwara
 
kampuni yenye uhai inatakiwa kila siku wafanyakazi waingie na kuwacha/wachishwa.

Serikali ndiyo mtu anaganda toka anamaliza shule mpaka anastaafu au anafia hapo hapo.

Ukiona mtu hawachiwi kuondoka na kampuni binafsi elewa kuwa huyo ni mali (asset) muhimu sana.

Mfanyakazi kwenye kampuni binafsi anapimwa kama mali (asset) yoyote ile, kuna "appreciation" na "depreciation". Mali (asset) ikifikia kuwa dhima (liability) haina sababu ya kubaki kwenye kampuni.
Huu ndio ukweli mchungu uliopo katika sekta binafsi. Watu hawaangalii utu au upendo, kinachojaliwa ni thamani gani unaongeza katika kampani

Haijalishi ulikuwa vizuri hadi kuiingizia pesa nyingi kampuni miaka mitano nyuma. Kama hauingizi tena faida au kuna mtu anafanya vyema kukuzidi ni lazma tu utaondoka
 
Hapana, ndoto zako tu.
kwahiyo kwako wewe mtu competent ni yule anaefikilia kuendelea kuajiliwa kuliko kujiairi akatanua ubongo wake kwa kuwaza nje ya box,hayo nayo ni mawazo ya kimasikini na woga wa maisha
 
kwahiyo kwako wewe mtu competent ni yule anaefikilia kuendelea kuajiliwa kuliko kujiairi akatanua ubongo wake kwa kuwaza nje ya box,hayo nayo ni mawazo ya kimasikini na woga wa maisha
= kuajiriwa.

Mimi hainihusu akijiajiri au akiajiriwa. Nakwenda na mada ilivyo, pitia tena maoni yangu juu huko.

Nisome kwa utulivu.
 
Back
Top Bottom