Nimefanya Maamuzi Sahihi na Makini Niliyoahidi Takribani Saa 72 zilizopita, Naelekea ....

Nimefanya Maamuzi Sahihi na Makini Niliyoahidi Takribani Saa 72 zilizopita, Naelekea ....

oooh nataka kuwatumikia....wananchi wameniomba....oooh mie mzalendo...bra...bra kibao...
fuateni taratibu za chama...subiri kiwapitishe kwanza...ikumbukwe kuna UKAWA pia.
We unadhani Lipumba au Mbowe akisema kaamua nae kugombea urais itakuwaje...epukeni kutengeneza makundi.
 
Naona ukisikia tu jina la zitto unachanganyikiwa tulia siasa siyo ugomvi, umemtuhumu kuwa msaliti kwa maneno ya mtaani lakini anaendelea na harakati zake tena kwa spidi kali. Kwa taarifa yako hoja yangu kubwa haikuwa zitto ila lugha za kejeli toka kwa wanachadema zisizokuwa na vyanzo vya uhakika, watu hawatafuti ukweli ila wanafuata upepo na uzi niliokuwa nauzungumzia ni huu Tetesi: Ben Saanane kuhamia ACT - Wazalendo siku ya Ijumaa . Fanya ulinganishi wa michango ya wadau kwenye huo uzi na huu unaoendelea. Kama Ben alikosea 2012 akasamehewa je hizi lugha kumwita tena msaliti 2015 zinatoka wapi?

Picha mnayotoa ni kwamba kuna uchafu mwingi ndani ya chadema ila hausemwi hadi mtu atangaze kuhama.

Rudia kusoma comment yangu, utagundua kuwa yote unayoyasema kwenye comment yako hii nimeyajibu. Aidha ukinifatilia kwenye ule uzi sijacomment maana siyo yeye aliyeanzisha ule uzi, wakati huohuo alikuwa hewani hakujibu ule uzi akisoma.
Ni hulka ya binadamu kukiweka zaidi kichwani kitu ulichokifanya mlipoonana mara ya kwanza, though sio wote maana sio lazima. CHADEMA haimuogopi zitto ndio maana yeye alienda mahakamani kupinga kumjadili. Yeye ndie anaogopa.
You just wait, time will tell
 
Rudia kusoma comment yangu, utagundua kuwa yote unayoyasema kwenye comment yako hii nimeyajibu. Aidha ukinifatilia kwenye ule uzi sijacomment maana siyo yeye aliyeanzisha ule uzi, wakati huohuo alikuwa hewani hakujibu ule uzi akisoma.
Ni hulka ya binadamu kukiweka zaidi kichwani kitu ulichokifanya mlipoonana mara ya kwanza, though sio wote maana sio lazima. CHADEMA haimuogopi zitto ndio maana yeye alienda mahakamani kupinga kumjadili. Yeye ndie anaogopa.
You just wait, time will tell

Sijasema wewe ila michango ya makamanda wenzako ilijaa lugha za kejeli, uropokaji na mengineyo pasipo kutafuta ukweli. Bahati mbaya hii tabia haijaanza kwa ben tu ila hata kwenye uzi wa shibuda, mdee na wengineo. Ndio maana nasema kuna harufu ya uchafu mwingi ndani ya chadema ila hausemwi hadi mtu ahamie chama kingine

Lingine ni kwamba huwezi kuchukua dolla kwa kutukana au kukejeli wapinzani wako kwa sababu hujui nani atakayekufaa na wakati gani. Bahati mbaya hizi lugha zenu hata viongozi wanaitumia. Mlisema CUF ni CCM B sijui waaaliti na mengineyo. Mfano Wakati waziri kivuli wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi wenye akisoma bajeti yake ya 2013/14 bungeni alitamka kuwa CU..F ni liberals so kwa ideology hiyo wanaruhusu ndoa za jinsia moja ushoga na usagaji (nenda youtube utaiona) lakini leo mmeungana. je mmeungana kwa kufuta kauli yenu au vinginevyo? ???.

ipo siku chadema itakaa meza moja an act siyo miujiza ni siasa tu.
 
Sijasema wewe ila michango ya makamanda wenzako ilijaa lugha za kejeli, uropokaji na mengineyo pasipo kutafuta ukweli. Bahati mbaya hii tabia haijaanza kwa ben tu ila hata kwenye uzi wa shibuda, mdee na wengineo. Ndio maana nasema kuna harufu ya uchafu mwingi ndani ya chadema ila hausemwi hadi mtu ahamie chama kingine

Lingine ni kwamba huwezi kuchukua dolla kwa kutukana au kukejeli wapinzani wako kwa sababu hujui nani atakayekufaa na wakati gani. Bahati mbaya hizi lugha zenu hata viongozi wanaitumia. Mlisema CUF ni CCM B sijui waaaliti na mengineyo. Mfano Wakati waziri kivuli wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi wenye akisoma bajeti yake ya 2013/14 bungeni alitamka kuwa CU..F ni liberals so kwa ideology hiyo wanaruhusu ndoa za jinsia moja ushoga na usagaji (nenda youtube utaiona) lakini leo mmeungana. je mmeungana kwa kufuta kauli yenu au vinginevyo? ???.

ipo siku chadema itakaa meza moja an act siyo miujiza ni siasa tu.

Ukiiisoma MOU ya UKAWA utagundua kuwa malengo ya umoja huu ni tofauti na unavyodhani na kuandika hapa.
Ukitaka kujua UKAWA ipo kwa misingi na makubaliano yapi ni vema ukaisoma ili uelewe. Sitashangaa kuona hayo unayosema maana mazungumzo yakifikia mnaweka mwafaka na makubaliano.

Vilevile hata CCM inaweza kaa meza moja na UKAWA yakifika maji ya shingo. Zotto alipogeresha kutaka kumuondoa PM, hata wabunge wa CCM walisaini.
 
Ukiiisoma MOU ya UKAWA utagundua kuwa malengo ya umoja huu ni tofauti na unavyodhani na kuandika hapa.
Ukitaka kujua UKAWA ipo kwa misingi na makubaliano yapi ni vema ukaisoma ili uelewe. Sitashangaa kuona hayo unayosema maana mazungumzo yakifikia mnaweka mwafaka na makubaliano.

Vilevile hata CCM inaweza kaa meza moja na UKAWA yakifika maji ya shingo. Zotto alipogeresha kutaka kumuondoa PM, hata wabunge wa CCM walisaini.

Vipi kuhusu lugha? Naomba hiyo MOU kama siyo top secret
 
Vipi kuhusu lugha? Naomba hiyo MOU kama siyo top secret

Kuhusu lugha we jiongeze mwenyewe maana lugha za Kibajaji i.e Lusinde unazijua.
MOU fuata taratibu zilizopo katita ofisi za vyama wana um9ja wa UKAWA utapata.
 
Naunga mkono vijana wote wanaotaka kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika Taifa letu, lakini sasa acheni nyimbo za kupigana vita Vijana wenyewe kwa wenyewe hili ni jambo la aibu. ni matumaini yetu kwamba kutoka kwako na Yeriko Nyerere hatutasikia tena mkiwapiga vita vijana wenzenu popote walipo, katika siasa popote duniani kutofautiana mawazo hakumfanyi mtu kua -------. Tumeona vijana wengi DEO, BULAYA na wengineo wakienda kinyume na Chama chao lakini hatujasikia kwamba ni --------. Vyama vyenu viige hili kama CCM inavyo chota SERA za vyama vya upinzani katika utekelezaji. Ongezeni mwendo lakini bila kupiga vita Vijana wenzenu...

“Naelekea Bungeni”

Ndugu marafiki zangu wa karibu na wa mbali, Baada ya kupitia taarifa ya kamati za kiutafiti iliyokamilisha kazi yake jana kutoka jimboni mniwie radhi kwa kukawia dakika kadhaa kuitimiza ahadi hii niliyoidokeza takribani saa 72 zilizopita kutokana na dharura iliyojitokeza ya kiutendaji katika majukumu yangu ndani ya chama ngazi ya taifa,majukumu yaliyokua na maslahi mapana zaidi kwa chama chetu na taifa kwa ujumla.

Naam, naelekea bungeni. Nimeamua kwa uhakika kabisa kujitosa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu 2015 kupitia chama changu – Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Tangazo langu hili limezingatia mambo yafuatayo;

Kwanza, nimesukumwa na maono, uwezo na umahiri wa kiuongozi, pamoja na dhamira ya dhati ya kuwa kiongozi wa watu, niliye tayari kutumia kila fursa, mikakati na mbinu zote za kiuongozi kuboresha maendeleo ya wananchi. Nawiwa kuwa mwakilishi tofauti wa wananchi, nitakaye tengeneza tofauti yenye tija kwenye maisha yao, nikitumia weledi na karama zangu za kiuongozi kama ifuatavyo;

Malezi yangu kisiasa ndani ya CHADEMA ndiyo yaliyochochea kiu na dhamira yangu ya muda mrefu katika kuwatumikia wananchi wenzangu bila kutetereka, nikiakisi misingi ya kifalsafa,kiitikadi na kisera ya chama chetu. Ni katika malezi hayo hadi sasa chama chama chetu kimeniamini kuwa ninatosha na kunikabidhi majukumu mbalimbali likiwemo jukumu jipya la kuongoza Idara ya Sera na Utafiti chini ya Kurugenzi husika katikaMakao Makuu ya Chama.Nimeutumikia wadhifa huu na ninaendelea kuutumikia kwa uaminifu mkubwa na kwa dhamira na moyo wa kizalendo kwa chama chetu na taifa kwa ujumla.

Mathalan, kwa kipindi kifupi sana tumeweza kuzindua sera tano mpya za chama ambazo ni Sera ya Elimu(ambayo zaidi ya 75% serikali ya CCM imeinakili na kuifanya sera yake ya elimu),Sera ya Maendeleo ya Vijana,Sera ya Afya,Sera ya Uchumi na Sera ya Nishati na Madini. Sera hizi mpya zimetoa mwelekeo bora kabisa wa serikali ijayo ya itakayoundwa na chama chetu kama sehemu ya Serikali ya Umoja wa UKAWA, serikali inayosubiri kuapishwa miezi saba ijayo.

Naamini, ninao uzoefu wa kutosha kitaaluma na kiutendaji pamoja na ukomavu unaostahili kisiasa katika kubeba wajibu huu wa kuwatumikia wananchi jimboni na pia kubeba ajenda za kitaifa na kutekeleza wajibu wa ziada mbali na wajibu wa mbunge kama ilivyo kikatiba.

Nimekulia na kusoma katika mazingira ya kawaida kabisa ya vijijini ambako wanaishi zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania. Nimesoma Shule ya Msingi Hiti iliyopo Kijiji cha Mrere Wilayani Rombo na kujiunga na Shule ya Sekondari Lyamungo kabla ya kujiunga na masomo ya juu ya Sekondari katika Shule ya Sekondari Galanos Mkoani Tanga. Mwaka 2005 kwa udhamini wa Serikali ya Tanzania nilijiunga na Chuo Kikuu cha Allahabad nchini India na kusomea Shahada ya Biashara nikibobea katika masuala ya fedha. Mwaka 2008 nilijiunga na Shahada ya Uzamili katika Masuala ya Uchumi(M.A Economics).

Kutokana na mapenzi yangu katika fani ya Diplomasia na siasa za kimataifa nilijiunga na Chuo kikuu cha Annamalai na kuhitimu Shahada ya Uzamili katika Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa. Kwa sasa ni Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Sera na Uongozi (Ph.D in Governance and Policy Analysis) kwenye Chuo cha Maastricht nchini Uholanzi.

Ninaelewa adha wanayopata watoto kutoka familia za masikini,kwa kuwa nimesoma na kukulia katika mazingira hayo. Na nina uhakika kuwa adha na dhiki zote zinazowasibu Watanzania wenzangu hazitokani na mapenzi ya Mungu, nuksi wala kurogana, bali zinatokana na udhaifu wa kisera na kiuwajibikaji katika mfumo wa utawala wa nchi yetu; mfumo uliolea mataifa mawili ndani ya nchi moja katika sekta ya Elimu,Afya,Ajira na nyinginezo – taifa la mafukara na taifa lenye nacho; taifa la wale wanaoweza kusomesha watoto wao kwenye shule bora hasa English Mediums na kutibiwa kwenye hospitali za ughaibuni, na taifa la akina siye tunaosomesha kwenye shule za kata na kutibiwa kwenye zahanati chache zilizo mbali na zisizo na dawa.

Nitaongeza idadi ya wabunge makini bungeni katika kuvunja matabaka haya mawilina kubakisha taifa moja lenye kusimamia fursa na mgawanyo wa rasilimali kwa usawa katika kuwawezesha wananchi kujiendeleza!
Katika kupanga na kutekeleza Mikakati na vipaumbele vyangu kwa jimbo nitazingatia zaidi maoni na matakwa ya wananchi na ushauri wa kitaalamu.

Ninaamini ninao uwezo wa kubuni,kupanga,kuchanganua,kusimamia na kuandika Ripoti za Miradi ya Maendeleo kutokana na uzoefu wangu wa kiutendaji katika taasisi za Fedha, Asasi za Kiraia na Sekta binafsi. Mathalan, hadi sasa nimeshavuka hatua ya awali ya kushirikiana na taasisi ya ‘’Yunus Social Business-Global Initiatives(YSB)’’ yenye makao yake nchini Frankfurt,Ujerumani iliyoanzishwa na Profesa Muhammad Yunus na kubadili hali ya uchumi na maisha ya mamilioni ya watu nchini Bangladesh kwa kutoa mikopo ya ujasirimali kwa wanawake na vijana katika sekta mbalimbali.

Nitashirikiana na asasi kama hizi za ndani na nje ya nchi yetu katika kuhakikisha mikakati nitakayoipanga kwa ajili ya wananchi inatekelezeka huku tukiendelea kuibana Halmashauri katika matumizisahihi ya fedha za umma.

Nitajenga hoja na kuaibnisha mikakati kukishawishi chama changu kwanini tunaweza kufanya vizuri zaidi.Tutawashawishi wananchi kwanini tunaweza kufanya vyema zaidi kuliko miaka mingine yote iliyopita katika uwakilishi wa nafasi ya ubunge

Nikipewa ridhaa na chama changu,sitapeleka bungeni ajenda ya kuongezewa posho kwa kisingizio chochote kile, bali nitaainisha vipaumbele, nitashauri na hata kuishinikiza serikali kwa hatua za kibunge na kiharakati nje ya bunge kuhakikisha wananchi nitakaowawakilisha wanapata haki wanayostahili.

Sitajisikia fahari kuhudhuria misiba mingi ya wananchi,bali nitajivunia rekodi ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana na kuokoa vifo visivyo vya lazima.Hiki ndicho nitakachojivunia baada ya miaka mitano

Ninasikitika sana kuona kwamba nchi maskini kama Tanzania inachezea fedha za umma kwa kutoa Fedha majimboni ukaguzi na udhibiti mzuri wa fedha hizo, zinazotolewa kwa jina zuri la Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo(CDF) ambao unakua chini ya Mbunge na DED

Je,Wabunge watakapotumia fedha hizo kwa manufaa yao na hasa kipindi hiki cha uchaguzi ambacho wabunge wengi wanazitumia fedha za umma majimboni kuwaghilibu wananchi kwa misaada ya mifuko ya bati na Saruji na kuwahadaa kuwa zimetoka mifukoni mwao sio ufisadi? Ni lazima tupiganie misingi ya uwajibikaji kuanzia ngazi za chini ili pia tuweze kujenga hoja za kuiwajibisha serikali katika masuala ya maadili hasa dhidi ya tatizo sugu la ufisadi, uzembe na kuacha tabia ya kulindana.

Sheria kandamizi zisizokua za haki na zilizopitwa na wakati zitakua adui yangu mkubwa ndani ya chombo hicho kutunga sheria nchini.Ni lazima nihakikishe kwa nafasi yangu Bunge letu linasimama na kutetea haki ya watanzania na kurejesha heshima ya kibunge na kitaifa miongoni mwa mabunge mengine duniani.Sitatetea sheria hata kama ina maslahi binafsi kwangu.

Kwa mfano sheria na kanuni zinazoruhusu wabunge kulipwa mafao yao baada tu ya kumaliza muda wao wa kibunge ni sheria chochezi kiatika ufisadi na rushwa kwenye uchaguzi.Ni kwanini wabunge wasilipwe baada ya uchaguzi ili kuhakikisha kuwa hakuna mianya ya rushwa katika chaguzi zetu?Watumishi wa umma hasa walimu na madaktari wanalipwa mafao yao miezi sita baada ya kustaafu na wanavumilia,je kwanini wabunge wasivumilie?

Katika bunge linalomaliza muda wake,miongoni mwa wabunge waliotekeleza kwa weledi wajibu wao wa kibunge ni wabunge vijana. Ninapotangaza uamuzi wangu huu,ninasimama juu ya mabega ya baadhi ya kaka na dada zangu waliotuwakilisha vyema ndani ya bunge la 10 linaloelekea ukingoni.

Wengi wao nimefanya nao kazi kwa karibu katika utekelezaji wa majukumu yao kibunge kulingana na nafasi yangu.Ni muda wangu sasa kuomba ridhaa ya chama changu ili niweze kupata ridhaa ya wananchi katika safari hii mpya tunayoianza,safari ya utumishi wa kweli kwa wananchi wa jimbo langu na Watanzania kwa ujumla.

Pili, ninazo sifa za jumla na vigezo vyote vilivyotajwa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 67(1).

Tatu, tangazo langu hili la “Naelekea Bungeni” linazingatia ukweli kuwa mpaka sasa nimeshafanya kazi kubwa iliyozaa matunda ya kuimarika kwa mtandao wa chama changu katika jimbo ninalokusudia kugombea na kuchangia kwa kiasi kikubwa chama changu kufanya vizuri kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita kama kilivyofanya vizuri pia maeneo mengi nchini. Naomba tuendelee kuidumisha nguvu hii kubwa ya uungwaji mkono kuelekea kura za maoni na hatimaye nitaunda timu ya kampeni kabambe kuelekea Bungeni Oktoba 2015.

Ninapotangaza uamuzi wangu huu,ninasimama juu ya mabega ya baadhi ya kaka na dada zangu waliotuwakilisha vyema ndani ya bunge la 10 linaloelekea ukingoni.Wengi wao nimefanya nao kazi kwa karibu katika utekelezaji wa majukumu yao kibunge kulingana na nafasi yangu.Ni muda wangu sasa kuomba ridhaa ya chama changu ili niweze kupata
 
Ben tunawahitaji viongozi wanaojua ABC za maisha yetu, ambao watawania nafasi za uongozi, si kwa kuwa wanataka maisha mema kwa familia na ndugu zao tu bali kutumia fursa na nafasi walizopata kusaidia wengine kujikwamua kimaisha....

Heko Ben... umefanya vyema kutangaza nia, binafsi nataka upate nafasi kisha uwakilishe wananchi kwenye chombo kikuu cha maamuzi na sisi tukiwa nyuma yako kukukumbusha pale tutakapoona umesahau jambo ili kwa pamoja tufikie malengo...
 
Kuhusu lugha we jiongeze mwenyewe maana lugha za Kibajaji i.e Lusinde unazijua.
MOU fuata taratibu zilizopo katita ofisi za vyama wana um9ja wa UKAWA utapata.

Kama Una justify huo upuuzi (hizo lugha chafu) kwa sababu ya kibajaji???? After all anachofanya kibajaji ni kuwaonesha kuwa kila mtu anaweza kutukana nothing else. ..........

Na kama MOU ni siri ngoja ngoja nijiandae for Manchester derby
 
Tunahitaji wengi wenye nia na maono kama hayo, ili Watanzania wapate walau nafuu kwa mzigo waliobebeshwa!

NENDA KIJANA.
 
Zito alipoonesha nia ya kugombea nafasi ya mwenyekiti ndani ya chama, aliitwa ------- na baadae kuundiwa zengwe na kufukuzwa. Lakini Ben kutangaza nia ya kugombea jimbo ambalo bado lina uwakilishi na hatujasikia kama mhusika kutangaza kutogombea tena, hakuna kauli za usaliti wala mikakati ya kufukuzwa Chama, hii ni sawa?? je kanuni za demokrasia zimetumika sawa kwa hawa watu wawili. Kama bado huyu nae hajafikia huko alipopelekwa mwenzake, inamaana na yeye atafukuzwa uanachama. Kwahiyo tunaweza kusubiri chama kipya cha Ben kama akishindwa kupata nafasi ya kugombea ubunge. ama ni kweli atahama ili atimize ndoto yake.
 
Kama Una justify huo upuuzi (hizo lugha chafu) kwa sababu ya kibajaji???? After all anachofanya kibajaji ni kuwaonesha kuwa kila mtu anaweza kutukana nothing else. ..........

Na kama MOU ni siri ngoja ngoja nijiandae for Manchester derby

Umeambiwa "jiongeze" this doesn't make a sentence justified. Hiyo inamaanisha "think" or use your capabilites. MOU inatolewa kwa application rasmi yenye constructive reasons for need of it.
 
Umeambiwa "jiongeze" this doesn't make sentence jusfied. Hiyo inamaanisha "think" or use your capabilites. MOU inatolewa kwa application rasmi yenye constructive reasons for need of it.

Okay nitajiongeza lakini waambie hao wenzako siyo fresh.
Hahaaa MOU ni siri???? sasa kwanini mnapiga kelele bungeni kwamba mikataba iwekwe wazi kama hata ile wanayoingia viongozi wenu ni siri kwa wanachama???
 
Okay nitajiongeza lakini waambie hao wenzako siyo fresh.
Hahaaa MOU ni siri???? sasa kwanini mnapiga kelele bungeni kwamba mikataba iwekwe wazi kama hata ile wanayoingia viongozi wenu ni siri kwa wanachama???

Unataka iwekwe wazi ili chama chako kipate gear? Hilo sahau.
Kamwambie Katibu mkuu kiongozi awapewanahabari nakala ya hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
 
Okay nitajiongeza lakini waambie hao wenzako siyo fresh.
Hahaaa MOU ni siri???? sasa kwanini mnapiga kelele bungeni kwamba mikataba iwekwe wazi kama hata ile wanayoingia viongozi wenu ni siri kwa wanachama???

Bomoa upinzani kazi mnayo.
 
kaka umefanya uamuzi sahihi wakati muafaka...mungu aendelee kuwa na wewe. wana mrere tunakuahidi kila aina ya ushirikiano....keep going kamanda...nitupie namba yako pls.
 
Maelezo mengi lakini hakuna la maana hata moja hapo. Imekushinda BAVICHA, jimbo utaliwezea wapi wewe?

Hamy dada ulichokitegemea sicho, ulitegemea huyu kamanda atangaze kuwa kahamia Against Chadema Tanzania basi hapo roho yako ingekuwa kwatu! Hata angeandika page tatu.
 
Nawatakia kila la kheri makamanda wangu na mimi nipo kwenye safari moja na nyie ijapokuwa mimi nitachelewa kufika huko labda mungu akisaidia 2025 Kamanda Ben utaniachia jimbo kwa sasa ngoja nielekeze nguvu zangu council ili nijenge chama, niwe karibu na wananchi na kuongeza uzoefu.

safari yenu ni safari yetu sote. kila la kheri kwenye safari yetu ya mafanikio

Safari yako ni safari yangu, Safari yangu ni safari yako, Safari yetu ni safari ya Watanzania.

Twende Bungeni na Ben Saanane!
 
Back
Top Bottom