Nimefikisha miezi miwili ya kufanya mazoezi bila kutumia vyuma vizito, nafanyia home tu

Kweli kuna kipindi nlikuwa nalalamika naanza na kuacha baada ya wiki kadhaa, ila kwa sasa nimepata ufumbuzi,, huu mwez wa pili sasa,, naendeleza mazoezi mkuu,,,
 
Hilo la vyuma hata mm nlipitia huko ila nkaona nnavoacha na mwili hupotea,, katika pitapita zangu nikakutana na jamaa angu mmoja mdau mkubwa wa zoez akanishauri niachane na vyuma,,,

Akasema ni bora push up na mazoez mengine ya kunyanyua uzito wako wa mwili kuliko wa vyuma,,,

Nikaanza ila baadae nikaacha baada ya yale maumivu ya mwanzo mwanzo,, hii ni miaka mitano nyuma ndo nlikuwa mtu wa kuacha mazoezi, ila huu mwaka nimeamua kutoka moyoni mazoezi yawe ndani ya ratiba yangu kila siku
 
Push up round 10@ reps20
Squat round 10@ reps 20
Squat left leg round 10@ reps20
Squat right leg round 10@ reps20
Trycep round 10@ reps20
Kukata tumbo 10@ reps20

= reps 1200

1 hour
Ebu tolea maelezo kama hautomaindi, hizi ndio zafanywajwe?
 
Inategemeana na aina ya mazoezi unayopendelea au malengo yako mkuu.
 
Ebu tolea maelezo kama hautomaindi, hizi ndio zafanywajwe?
Ipi mkuu, push up napiga round 10,, ktk kila round kule kubonyea chini juu chini juu naenda mara 20 ktk round 1, kwa hiyo naenda mara 200 Ndani ya round 10
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…