Nimefiwa na Mama Mzazi

Pole sana mkuu, mungu akupe uvumilivu na ustahimilivu
 
Duh! Hii nilikuwa sijaiona...........Pole sana mkuu, Mwenye Enzi Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mama yako mzazi........
Tupo Pamoja Mkuu.
 
X-PASTER
pole sana mkuu..hiyo ni safari ya kila nafsi.RIP mama
 
Pole sana mkuu X-Paster, nakuombea wewe na familia yako faraja wakati huu wa msiba mzito wa familia. Mungu mwenyewe awasimamie na kuwainua.
 
Yakhe hii habari nzito kwelikweli!
Pole sana mkuu! Kazi ya Mungu haina makosa.
Hakika kwake tulitoka na kwake siku moja tutarejea.
Bwana Alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Poleni sana.
 
Innalillah wainna ilayhi raajiun.
 
Pole sana x-paster mungu akupe moyo wenye uvumilivu kwa kipindi hiki kigumu yote mapenzi ya mungu apumzike kwa aman.
 
"Sisi ni wa Allaah nasi Kwake tutarejea, Ee Allaah Utulipe wafiwa kwa msiba huu na utupe badili yake bora kuliko huo na utukutanishe tena peponi Insha'Allah"
"Inna lillahi wa inna ilayhi raaji'un"
Pole sana Mkuu. Mwenyezi Mungu awape subira kwa msiba huu na amjaalie mzazi wetu na wote waliotutangulia malzi mema peponi - Amin!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…