Nimefuatilia Soka Tanzania tangu 1980s sijaona kama Chama

Vyamavingi

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
5,818
Reaction score
5,555
Siku hizi sio mpenzi sana wa soka Tanzania. Niliwafahamu kwa kusikiliza RTD, kusoma magazeti ya Uhuru/Mzalendo, na Mfanyakazi la mwandishi James Nhende aliyepigwa na Zamoyoni Mogella kwa madai ya kumuandika vibaya.

Walikuwepo viungo wa maana kama Charles Boniface Mkwasa (Master), Nico Njohole (Mapafu ya Mbwa), Hussein Ngulungu, Said Mwamba (Kizota), Ramadhan Lenny, Athumani China, nk.

Kutoka enzi za hao niliowataja hapa, sijawahi kuona kiungo mwenye akili kama Clatous Chota Chama (Mwamba wa Lusaka). Goli alilofunga leo dhidi ya Vipers, ni yeye pekee katika Tanzania anayeweza kufunga katika mazingira ya namna ile, wengine wangekuwa na papara ya kupiga ama cross au shuti kali kipa apambane nalo, lkn Chama akatulia na kumgeuza beki wa Vipers na kisha kumuangalia kipa na kumfunga kirahisi.

Chama ana akili sana ya mpira, tatizo lake [weakness] ni kutokuwa na haraka, yawezekana pia hawezi kucheza kwa haraka na makocha wengine hawawezi kuvumilia hilo, lakini hiyo kwa kuwa matokeo yake ni chanya inabidi tu makocha hata wasiopenda kasi yake wamkubali tu hivyohivyo. Kwa upande wangutangu nianze kufuatilia soka letu, sijaona kama Chama.

Vv
 
Chama anawafaa Simba, kwenye timu za ushindani hawezi hata kupata nafasi ya kuvaa jezi kukaa benchi
 
Huenda ulikuwa ulikuwa unafuatilia kitu usichokielewa. Akina Nonda wamecheza hapo Yanga mpaka club bingwa Ulaya wanafananishwa na reject ya Berkene. Kiuhalisia Chama hafiki nusu ya akina Said Mwamba au Dua Said.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 

Uyo chama anawafaa simba na sio timu nyingine yoyote yenye kucheza mpira wa kasi na nguvu anapoteana mapema sana
 
Reject ya Berkene ni mfalme wa Simba. Mmecheza na timu ambayo ndani ya game 7 hawajaweza kufunga goli lolote. Timu pale hakuna.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Walikuwa wanaomba mpira uishe licha ya kukutana na timu yenye safu butu ya ushambuliaji, wameshikilia bomba kwa maombi ya kila namna, lakini sio kila mechi watakutana na vipers na hapo ndipo pumba na mchele zitapojitenga
 
Dua Said na Said Sued Scad ni wachezaji wa matukio hawakuwa na maajabu. Chama ni mchezaji wa kawaida sana hauwezi kumfananisha na wanaume mfano Dani Muhoja ama Michael Paul Mkopo ama Nylon. Huyu Chama zama za akina Method Mogela angekuwa anabeba jezi tu. Utamfananisha na OCD huyu
 
Nafikiri waliokuwa wanamfananisha Chama na Aziz Ki wamejibiwa kwa vitendo na Chama mwenyewe.
 
Walikuwa wanaomba mpira uishe licha ya kukutana na timu yenye safu butu ya ushambuliaji, wameshikilia bomba kwa maombi ya kila namna, lakini sio kila mechi watakutana na vipers na hapo ndipo pumba na mchele zitapojitenga
Timu reject zipo shirikisho , timu iliyopo champions lazima uiheshimu. Je vipers ni vibonde pia kwenu?
 
Hao kina Said Mwamba na Dua Said wamewahi kufanya nini cha ajabu kwenye mashindano nje ya Tanzania?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…