Nimegomea pendekezo la tiba toka kwa daktari

Nimegomea pendekezo la tiba toka kwa daktari

Mbona it's not a big deal
Hicho kidonge angeweza kupewa mkeo akamwekea mtoto yeye mwenyewe
Kwa sisi tuliowahi kuuguza watoto mpaka unahisi nikiamka huyu simkuti hivyo vidonge ni kawaida sana
Unakuta mtoto anaumwa adi mshipa hauonekani kirahisi,dawa anatapika na homa iko juu,option hapo ni hiko kidonge tu
Sema ukiona una option ujue huyo mwanao hajafikia stage mbaya ila akifika nakwambia wala hiyo simu usingepiga wala kupigiwa wala usingetaka kujua wamemtibiaje bali ungetaka matokeo tu!
 
Dokta akamwambia "KWA JOTO HILO, ALIPASWA KUWEKEWA KIDONGE KATIKA NJIA YA HAJA KUBWA.

Yupo sahihi na hauna madhara, kweli inashusha homa haraka. Niliumia kwa wanangu waliokuwa wadogo miaka hiyo ilipobidi. Naongelea kwamba inatumika duniani.. mpende mwanao asiteseke na ugonjwa kushusha joto kwa haraka. Nchi zilizoendelea niliwaambia ni kawaida sana na haimdhuru mtoto.
 
Mkuu,

Ushawahi kukutana na wale Jehovah Witnesses ambao hawataki kuwekewa damu, hata wakiona wanakufa, wanaona ni bora wafe kuliko kuwekewa damu?

Basi na wabongo wengine nao wapo kama hao Jehovah Witnesses kwenye suala hili.

Ukiwaambia habari za puru ni kama unawapa dawa inayoingilia imani yao, kama kuna alternate bora wapewe hiyo tu kuepusha matatizo ya kimaadili ya matabibu kulazimisha dawa kinyume na matakwa ya kiimani ya wagonjwa.

Sasa siku wakiumwa bawasiri na kuambiwa wapake dawa kwenye puru au wabaki na bawasiri sijui itakuwa vipi hapo?
Mkuu hao sijawahi kutana nao kabisa ila nadhani hizi dini ni changamoto sana kupingana na science .

Niliwahi kukutana na muhindi mmoja yeye akasema anatumia Ayurveda tu , alikuwa na heart failure ila akagoma kutumia dawa za kawaida akasema tumtafutie ayurveda kama alternative.

Zilipatikana akaendelea na matibabu yake.
 
Ni mwanangu wa kiume, wa 3 kuzaliwa and he is 5 years now.

Kuepusha maneno mengi ni kwamba muda huu yuko hospitali, na mama yake na baada ya diagnosis ikaonekana ana mchafuko wa damu na homa iko juu ana joto flan .

Baada ya kupata majib maabara na kumuona dokta akauliza
"AMESHAPEWA DAWA?".

Wife akasema HAPANA, DAWA GANI?

Dokta akamwambia "KWA JOTO HILO, ALIPASWA KUWEKEWA KIDONGE KATIKA NJIA YA HAJA KUBWA.

Bas wakiwa kwenye mazumgumzo nikapiga simu (mimi ni type ile ya watu kero wasumbufu hasa napo hisi ishu ni kubwa na mimi ndio nilipaswa kuwepo sasa ndio hivyo tena sipo, sasa huwa napiga sana simu kutaka kujua everything going on)

Wife akapokea akanipa hayo maelezo na ndio alikua anaelekea kutimiza huo utaratibu.

Nikauliza "KUSHUSHA HOMA NDIO LAZIMA KIDONGE KIWEKWE huko?"

akasema "NDIO NIMEAMBIWA HIVYO".

Nikasema "MWAMBIE DOKTA MUMEO KAKATAA, KAMA HAKUNA NAMNA NYINGINE BASI WAMWACHE TU, HIYO HOMA MPATIE PARACETAMOL"

AKASEMA SAWA.

Bahati mbaya sana kila mshkaj wangu ambaye ni dokta nikimpigia hapatikani au hapokei simu.

Nilitaka japo nipate consent zao kitaalam nijue japo sidhan kama ningekubal..atleast nilitaka tu kusikia wanasemaje?

Ndio hivyo wakuu NIMEGOMA.Mwanangu mwenyewe wa kiume ndio huyo huyo, wemgime wote watatu ni wakike, sasa waanze tena kumuweka vidongo njia ya hajakubwa viyeyukie humo halaf nini kitafuata.HAPANA KWAKWEL.

IMAWEZEKANA NIMEKOSEA ILA NDIO HIVYO, NIMEGOMA.
Mjinga kweli wewe. Kama joto liko juu sana mbona ndio njia rahc zaid ya kushusha joto.
 
Diclofenac tangu lini ikachomwa kwenye mshipa jamani, kama vitu hamvijui/hamuelewa ni vyema kukaa kimya au ungeishia kusema kuchoma diclofenac tu
Zipo Diclofenac IV mkuu, na nikushauri kitu katika mijadala ambayo usikurupuke kubisha ni hii inayohusu afya, watu wanafanya tafiti kila leo na mambo yanabadilika kwa kasi sana, so Jitahid kujiupdate na kusoma soma sana. Khan app na Medscape wawe rafiki yako sana.
 
Ni mwanangu wa kiume, wa 3 kuzaliwa and he is 5 years now.

Kuepusha maneno mengi ni kwamba muda huu yuko hospitali, na mama yake na baada ya diagnosis ikaonekana ana mchafuko wa damu na homa iko juu ana joto flan .

Baada ya kupata majib maabara na kumuona dokta akauliza
"AMESHAPEWA DAWA?".

Wife akasema HAPANA, DAWA GANI?

Dokta akamwambia "KWA JOTO HILO, ALIPASWA KUWEKEWA KIDONGE KATIKA NJIA YA HAJA KUBWA.

Bas wakiwa kwenye mazumgumzo nikapiga simu (mimi ni type ile ya watu kero wasumbufu hasa napo hisi ishu ni kubwa na mimi ndio nilipaswa kuwepo sasa ndio hivyo tena sipo, sasa huwa napiga sana simu kutaka kujua everything going on)

Wife akapokea akanipa hayo maelezo na ndio alikua anaelekea kutimiza huo utaratibu.

Nikauliza "KUSHUSHA HOMA NDIO LAZIMA KIDONGE KIWEKWE huko?"

akasema "NDIO NIMEAMBIWA HIVYO".

Nikasema "MWAMBIE DOKTA MUMEO KAKATAA, KAMA HAKUNA NAMNA NYINGINE BASI WAMWACHE TU, HIYO HOMA MPATIE PARACETAMOL"

AKASEMA SAWA.

Bahati mbaya sana kila mshkaj wangu ambaye ni dokta nikimpigia hapatikani au hapokei simu.

Nilitaka japo nipate consent zao kitaalam nijue japo sidhan kama ningekubal..atleast nilitaka tu kusikia wanasemaje?

Ndio hivyo wakuu NIMEGOMA.Mwanangu mwenyewe wa kiume ndio huyo huyo, wemgime wote watatu ni wakike, sasa waanze tena kumuweka vidongo njia ya hajakubwa viyeyukie humo halaf nini kitafuata.HAPANA KWAKWEL.

IMAWEZEKANA NIMEKOSEA ILA NDIO HIVYO, NIMEGOMA.

Habari!

1: Suala la kutokubaliana na matibabu au njia ya utoaji matibabu ni HAKI ya msingi kwa mgonjwa.

Daktari na mgonjwa hutakiwa kuelimishana juu ya kwa nini huyu anashauri hili na huyu hajakubaliana. Mwafaka hufikiwa na matibabu kutolewa kulingana na UHITAJI. Mbadala huweza kutumika kama upo kutatua kinachokwamisha.

2: Pale ambapo kuna UHITAJI WA HARAKA na hakuna kukubaliana, daktari anatakiwa kuhusisha uongozi wa hospitali/kituo cha afya (ETHICAL COMMITTEE) ili kupata ufumbuzi. Kama mambo yatakuwa bado na utata wa utoaji huduma, basi Hospitali na mgonjwa/ndugu wa mgonjwa huweza kuangalia mwafaka.

A: Weka mazingiza husika kwa kuhusisha wanasheria pia.

B: Kumpa mgonjwa rufaa ili akapate huduma mbadala kama inapatikana mwingine na ni salama kuhamishwa.

3: Watoa husima ya afya wanafanamu na wanatakiwa kutoa husuma kwa kizingatia MILA, DESTURI UTAMADUNI NA IMANI ya mteja kwa kuzingatia namba 1 na 2 hapo juu.

4: Kwa dawa kutolewa kupitia nhia ya haja kubwa. Dawa zipo na zimekuwa zikitolewa bila shida yoyote mfano: dawa ya kuzuia degedege, dawa ya kutibu bawasili, dawa ya kupunguza homa na uongezaji wa maji/drip kwa wale waliofanya kazi zamani. Msingi wa kutumia njia hii ni UHARAKA wa kufyonzwa dawa kupitia njia husika na kupunguza madhara. Pia kutobu tatizo husika kama liko swhemu husika.

Binafsi, huwa sipendelei kwa watoto zaidi ya miaka 3 (mitatu) kupewa dawa hizi kwa njia husika (Paracetamol vs Diclofenac) kutokana na kuanza kuwa na ufahamu wao. Bali pale ambapo ni hitaji muhimu kwelikweli au hatari mnele kulingana na aina ua mgonjwa.

5: Kwa kesi husika, hatuwezi kuizungumzia sana. Baba katimiza wajibu wake. Daktari pia alitakiwa kutimiza wajibu wake. Tatozo hatina maelezo ya upande wa pili. Hivyo, tuombe na kushukuru tu kwamba mtoto awe amepata huduma hitajika na kurejea kwenye afya yake.

Wito ni kuendela kuzingatia kupeana haki, nafasi na heshima kati yetu wote. Pia kuzingatia mahitaji ya kila mmoja yaliyopo kimaadili.
 
Nlidhani nilishayaona yote,what's the point to put medicine in the ass wakati Kuna a ton ambazo ni za kunywa?Walianza na kupima tezi dume Kwa kidole na nakumbuka hadi Mzee wa msoga alitumika,wazungu najua wanataka ushoga usambae Kwa Kasi ila hizi njia zao wanazotumia ni zakipuuzi sijawahi ona,nimewadharau kuanzia Leo.
 
Mjinga kweli wewe. Kama joto liko juu sana mbona ndio njia rahc zaid ya kushusha joto.
Ujinga ni suala mtambuka. Aliye mjinga haina maana hajui, noo..ila anajua kwa level yake na kwa mipaka aliojiwekea mwisho wa kujua
 
Siku mwanao akija kupata convulsion daktari akitaka kumuwekea diazepam per rectal uje ugome tena sawa?
Mkuu tatizo mnashindwa kunielewa..nilichokataa ni suala la homa (kitu ambacho mimi naona ni jambo la kawaida tuuuu) ukatumie njia ngumu hiyo (tena kwangu ni mara ya kwanza kuijua). Lingekua tatizo kubwa na la hatar nisingepinga.

NB.
unatumia 4figure table ku solve 25x4???
 
Ikiwa hauna utaalamu na maswala ya Afya usipende kufanya mabishano kuhusu Afya ya MTO to wako .


Kuhusu MTU kuwa shoga hakutokani na kuwekea kidonge nyuma

Kuwa MTU Wa kufikiri Kwa kina
 
Mbona it's not a big deal
Hicho kidonge angeweza kupewa mkeo akamwekea mtoto yeye mwenyewe
Kwa sisi tuliowahi kuuguza watoto mpaka unahisi nikiamka huyu simkuti hivyo vidonge ni kawaida sana
Unakuta mtoto anaumwa adi mshipa hauonekani kirahisi,dawa anatapika na homa iko juu,option hapo ni hiko kidonge tu
Sema ukiona una option ujue huyo mwanao hajafikia stage mbaya ila akifika nakwambia wala hiyo simu usingepiga wala kupigiwa wala usingetaka kujua wamemtibiaje bali ungetaka matokeo tu!
THERE YOU ARE chief.. hiki umeongea ndio na mimi kilinifanya nifike hapa.

Mtoto si kwamba alikua kwenye severe situation namna ambayo ingeshindikana kumpatikia alternative.. Dawa anakunywa bila shida..Vipimo vya damu walimchukua mkononi bila tabu ya mishipa kutoonekana.. then why Anal?????

NB.
Sijisifii shida ila nishauguzaga huyu dogo kuna time mpaka alifikia hii stage ya kukosa mishipa. wakapendekeza ATAFUTWE MISHIPA KICHWANI.. aisee licha ya kuumwa serious NILIGOMA KATA KATA.

Hospital hiz za kibongo hapana..Wachome mtoto kichwan watu wenyewe ma nurse tu vidada na vishkaji tuu ..NIKASEMA NOOOOO KICHWANI SINDANO.

KWAKIFUPI MIMI NINA MIPAKA YANGI KWENYE KILA JAMBO. Na hii binafsi imenifanyabkuwa mtu wa kutafutavsana njia mbadala always na nimekua nikifanikiwa ALWAYS
 
Ikiwa hauna utaalamu na maswala ya Afya usipende kufanya mabishano kuhusu Afya ya MTO to wako .


Kuhusu MTU kuwa shoga hakutokani na kuwekea kidonge nyuma

Kuwa MTU Wa kufikiri Kwa kina
Sijaongelea habar za ushoga..nimeonngelea kuto ridhishwa kwangu na njia hiyo so wanipe nyingine maanq sikuona kama ni lazima kwa halinya mtoto ilivyokua
 
Daah watoto mabadiliko ya mwili na meno kukua yanawafanya wapate Joto kali na wengine kupata home kali nayo kwa Wazazi wenye watoto wengi huwa wanajua hii miguu akianza tu anampa Paracetamol ili kupunguza joto na kurudi kwenye hali yake ya kawaida...
 
Ni mwanangu wa kiume, wa 3 kuzaliwa and he is 5 years now.

Kuepusha maneno mengi ni kwamba muda huu yuko hospitali, na mama yake na baada ya diagnosis ikaonekana ana mchafuko wa damu na homa iko juu ana joto flan .

Baada ya kupata majib maabara na kumuona dokta akauliza
"AMESHAPEWA DAWA?".

Wife akasema HAPANA, DAWA GANI?

Dokta akamwambia "KWA JOTO HILO, ALIPASWA KUWEKEWA KIDONGE KATIKA NJIA YA HAJA KUBWA.

Bas wakiwa kwenye mazumgumzo nikapiga simu (mimi ni type ile ya watu kero wasumbufu hasa napo hisi ishu ni kubwa na mimi ndio nilipaswa kuwepo sasa ndio hivyo tena sipo, sasa huwa napiga sana simu kutaka kujua everything going on)

Wife akapokea akanipa hayo maelezo na ndio alikua anaelekea kutimiza huo utaratibu.

Nikauliza "KUSHUSHA HOMA NDIO LAZIMA KIDONGE KIWEKWE huko?"

akasema "NDIO NIMEAMBIWA HIVYO".

Nikasema "MWAMBIE DOKTA MUMEO KAKATAA, KAMA HAKUNA NAMNA NYINGINE BASI WAMWACHE TU, HIYO HOMA MPATIE PARACETAMOL"

AKASEMA SAWA.

Bahati mbaya sana kila mshkaj wangu ambaye ni dokta nikimpigia hapatikani au hapokei simu.

Nilitaka japo nipate consent zao kitaalam nijue japo sidhan kama ningekubal..atleast nilitaka tu kusikia wanasemaje?

Ndio hivyo wakuu NIMEGOMA.Mwanangu mwenyewe wa kiume ndio huyo huyo, wemgime wote watatu ni wakike, sasa waanze tena kumuweka vidongo njia ya hajakubwa viyeyukie humo halaf nini kitafuata.HAPANA KWAKWEL.

IMAWEZEKANA NIMEKOSEA ILA NDIO HIVYO, NIMEGOMA.
Naona iyo Dawa inakuwa Recommended sana kwa watoto siku hizi
 
Ujinga ni suala mtambuka. Aliye mjinga haina maana hajui, noo..ila anajua kwa level yake na kwa mipaka aliojiwekea mwisho wa kujua
Sasa ungemtibu wewe. Huwez kumgomea Dr bila kuja na sababu. Unakataa tu bila sababu then umempeleka mwenyewe hospital. Hujui joto likivuka 42 mtoto anaweza kupata degedege na kukakamaa kunakosababisha kilema cha maisha. Usifanye tena huu ujinga next time. Hujui kitu uliza acha ushamba wa kujifanya unaleta ubabe kwenye kila kitu.
 
Back
Top Bottom