Nimegundua udhaifu mkubwa sana wa Serikali ya Tanzania katika kukabili suala la COVID-19

Nimegundua udhaifu mkubwa sana wa Serikali ya Tanzania katika kukabili suala la COVID-19

Kwa kujibu wa taarifa kwenye hiyo link, Kenya wanapewa alternative, (hadi hostel za chuo zinatumika). Na hata hiyo hotel aghali iliyotajwa rate yake ni US$ 60 ambayo ni chini ya laki mbili inayotozwa hapa kwetu.
Hapa kweti kuna hotel ya US$50 kulingana na clip ya yule mama aliyekuwa analalamika.
 
Vita ya corona Tz
Hivi Tanzania wakiweka karantii ya kutoka kama hizo nchi nyingine si watu wengi watakufa kwa kukosa chakula kuliko hata vifo vya corona yenyewe? Tusijifananishe na nchi hizo. Maisha ya Bongo asilimia kubwa fedha ya kula kesho inatafutwa leo na wakati mwingine ya kula leo inatafutwa leo leo. Utamwambia mtu asiyejua anakula nini kujifungia ndani?
 
Sasa kipi kifanyike au tukae lockdown mwez1 tupime upepo.

Viongozi wetu wote bila kujali ni serikali au upinzani mko wapi? Viongozi wa dini mko wapi?

Kwa nini tusiiombe serikali sote kwa umoja wetu kuitaka ichukue hatua kama mataifa mengine?

Sudan, ivory coast, Senegal ni baadhi ya mataifa ya karibu kabisa kwenda total lockdown.

Kwa nini sisi hatuchukui hatua?
 
Hivi Tanzania wakiweka karantii ya kutoka kama hizo nchi nyingine si watu wengi watakufa kwa kukosa chakula kuliko hata vifo vya corona yenyewe? Tusijifananishe na nchi hizo. Maisha ya Bongo asilimia kubwa fedha ya kula kesho inatafutwa leo na wakati mwingine ya kula leo inatafutwa leo leo. Utamwambia mtu asiyejua anakula nini kujifungia ndani?

Nchi masikini kama Rwanda ilivyofanya lockdown so far umeshasikia wananchi wake wangapi wamekufa kwa kukosa chakula?

Au huko hua wanafanya kazi gani za kuwafanya wawe na saving ya wiki 2?
 
Hivi Tanzania wakiweka karantii ya kutoka kama hizo nchi nyingine si watu wengi watakufa kwa kukosa chakula kuliko hata vifo vya corona yenyewe? Tusijifananishe na nchi hizo. Maisha ya Bongo asilimia kubwa fedha ya kula kesho inatafutwa leo na wakati mwingine ya kula leo inatafutwa leo leo. Utamwambia mtu asiyejua anakula nini kujifungia ndani?

Sasa ndio tukiri kuwa nchi yetu ni ya watu maskini wa kutupwa. Kujifaragua kote kwa ccm hii kunamalizwa na corona.
 
Mbaya mwamba alipoingia hela ya majanga hakuna.. Zaman chakula cha akiba kilikuwa kinanunuliwa cha kutosha,ila mwamba alisema hatoi chakula wakati wa majanga...

Ivyo Corona ikishika hatam, watu watakufa na Corona na njaa pia..

Tuombe Mungu ipite pembeni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli serikali ya Tanzania imelichukilia janga la COVID-19 kama jambo la mzaha kupita kiasi, hali hii imewafanya baadhi ya wananchi kubweteka kupita kiasi kutokana na janga hili.

Kwa haya niliyoshuhudia, nachelea kusema kuwa ikitokea COVID-19 ikaiathiri Tanzania kwa kiwango kikubwa basi mataifa mengine yataandika nne na kutucheka kwa kejeli. Haya yanasababishwa kwa kiwango chote na viongozi wetu wa serikali tuliowapa mamlaka ya kutuongoza. Nitaainisha uzembe huu uliopindukia katika maeneo machache.

1. Ni jambo la aibu sana baadhi ya raia wa Tanzania kuvuka mpaka wa Tanzania na Uganda na kisha kukamatwa ndani ya Uganda wakati kila nchi inalichukulia jambo hili kwa uzito wa aina yake labda isipokuwa Tanzania. Ni jambo la aibu kwa sisi kutumia uzembe wetu na kutokujua mambo kupeleka mzigo kwa wenzetu, kwa hili najisikia aibu sana kama Mtanzania.

Kwa jambo kama hili Uganda watatuona sisi kama watu wa mzaha sana kiasi kwamba mzaha wetu tunaupeleka hadi kwenye nchi za wenzetu ambazo kwa namna ya kipekee wamelichukulia jambo hili kwa umuhimu na ukubwa wa kiwango chake. Kwanini mamlaka za Tanzania mipakani hazikuwazuia watu hawa hadi wakavuka mpaka kati ya Uganda na Tanzania? Hawakuona umuhimu wa kuwaheshimu wenzetu walioamua kufunga mipaka yao ili kuikabili Corona kwa vitendo?

2. Hoteli zetu kutoza kiwango cha chini cha Tshs laki 2 kwa watakaojiweka karantini kwa siku moja pekee. Hili ni jambo la aibu sana kwetu kama nchi. Kwa wenzetu jambo hili limeihusisha jamii yote huku Rais wa nchi akiwa kamanda mkuu wa kikosi pambanaji. Hapa kwetu hakuna control yoyote juu ya jambo hili iliyoandaliwa hadi pale walipogutuka baada ya watu kulalamika.

Hili ni jambo la aibu na fedheha kubwa. Nimejiuliza, hata kwa hili hawakujiandaa? Yani mtu mwenye matatizo ambapo imembidi kuwekwa ama kujiweka pale ili kuwanusuru wengine anaenda kutozwa hela ya malazi ya anasa? What a shame! Mbaya zaidi kamanda mkuu yupo Dodoma anapiga picha akiwa amelala juu ya jiwe! Huu ni mzaha na kuwachukulia watu wako "Too low"

3. Utolewaji wa taarifa za mara kwa mara na kuwekeza nguvu kwenye vituo vya kupimia ugonjwa huu pamoja na kuwekeza nguvu kwenye kudhibiti usambaaji. Ni aibu kubwa kuwa Rais kasema kuwa anapeleka fedha za Mwenge kwenye kupambana na ugonjwa huu ila hakuna lolote kuhusu kupambana huko. Vituo vya usafiri wa umma, mahospitali mengi hakuna viosha mikono, hakuna kupulizia dawa.

Yani tupo kila mtu na lake. Mbaya zaidi hakuna taarifa za mara kwa mara kutoka kwa wahusika wa kutoa taarifa. Yani kwa kifupi ni kama serikali imelala kupita kiasi! Ni aibu eti sampuli zote ndani ya nchi zinapelekwa kituo kimoja pekee cha kupimia. Hatuoni kuwa tutakuwa tunachelewesha kuwabaini waathirika kwa haraka? Hatuoni madhara haya ya ucheleweshaji mpaka sasa?

4. Swala la mkuu wa mkoa wa Dar kutoka asubuhi asubuhi na kupeleka ujumbe kwa watu kuwa kuna mtoto wa Mbowe anaugua Corona. Ukiusoma uso wa Paul Makonda ni kama amepata "relief" fulani kwa mtoto wa Mbowe kuumwa ugonjwa tena kwake furaha zaidi ni Corona. Hakuna kiongozi hata mmoja aliyekosoa ujinga huu! Tunaanzaje kuwaamini kuwa mpo serious? Alichofanya Paul Makonda ni utoto mtupu na kwa alichofanya hakutakiwa kuendelea kuwa kiongozi. Lakini kwakuwa tayari kuna udhaifu, basi limeonekana ni jambo la kawaida kabisa kwa viongozi wa kitaifa wenye dhamana.

5. Hakuna uhamasishaji kwa watu wenye uwezo kujitoa ili jamii nzima iwe salama. Hili kimsingi linatakiwa kufanywa na serikali. Lakini kwakuwa hakuna kujali basi na wao wameamua kujikalia kimya tuu ili mradi liende huko litakakotua.

Mwisho naomba nieleze masikitiko yangu kuwa kwa hili jambo basi ni hatuna serikali makini. Pia ni heri watu wakajichukulia tahadhari wenyewe na pengine wanayoambiwa na serikali ya Tanzania basi wachanganye na zao! Hakuna uaminifu kwa kiwango kikubwa mno kutoka serikalini kuhusu janga hili la COVID-19.
Lawama kwa serikali…lawama kwa serikali…lawama kwa serikali!
Ni wajibu wa kila mtz kujikinga na ugonjwa huu na magonjwa mengine! Kama unasubiri serikali ije ikukinge baada ya kutoa taarifa juu ya uwepo wa ugonjwa huu nchini basi utasubiri sana! Kwa maoni yangu serikali inafanya kinachotakiwa. Imetoa elimu, imefunga shule na vyuo na kuzuia mikusanyiko! haya yanapaswa yapige kengere kwenye masikio ya kila mtz maana siyo mambo ya kawaida kutokea! Unapoona mpaka serikali imechukua hatua hizo ujue imechukulia covd-19 kwa uzito unaostahili!
Na tz kihihivi tutavuka salama na mataifa mengine yatashangaa, Mungu yupo!
 
Lawama kwa serikali…lawama kwa serikali…lawama kwa serikali!
Ni wajibu wa kila mtz kujikinga na ugonjwa huu na magonjwa mengine! Kama unasubiri serikali ije ikukinge baada ya kutoa taarifa juu ya uwepo wa ugonjwa huu nchini basi utasubiri sana! Kwa maoni yangu serikali inafanya kinachotakiwa. Imetoa elimu, imefunga shule na vyuo na kuzuia mikusanyiko! haya yanapaswa yapige kengere kwenye masikio ya kila mtz maana siyo mambo ya kawaida kutokea! Unapoona mpaka serikali imechukua hatua hizo ujue imechukulia covd-19 kwa uzito unaostahili!
Na tz kihihivi tutavuka salama na mataifa mengine yatashangaa, Mungu yupo!

Unaongea pumba...Serikali ndo tumeipa dhamana ya kutuongoza na kusimamia rasilimali zetu so inawajibu mkubwa katika hili hivyo ni lazima kulaumiwa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Rwanda ni nchi yenye population ndogo sana / Hiko kama watu awazidi 10 Million.... Usijaribu sumu kwa kuionja.

Wako zaidi ya Mil 12.

Vipi khs South Africa wao wana population kiasi gani maana nao wameweka hio lockdown.
 
Mi nawaza tu,ule alioufanya Makonda pale ubungo si mkusanyiko?Hivi tuko serious kweli au?Kuna jambo gani la maana ameenda kulifanya pale?shame

Watu na wenyewe ni Wajinga mitako mikubwa wanaenda kumsikiza ili iweje ??


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Lengo la hii mada ni hapo namba 4 tu
Huyu jamaa ana ujumbe wa maana ila jinsi ya kuutoa ndipo kachemsha. Ukiwa ni mtu wa mrengo fulani na unajulikana, ni vyema kuhakikisha huongelei cheap politics kam kupiga picha juu ya jiwe. Bashite kutamka kuwa fulani ana.... mihemko inapozidi hata umahiri wa uandishi unakuwa shakani. Ni maoni yangu tu
 
namba hazidanganyi! Africa is resistant to Corona virus ikiaminiwa kama si joto kubwa basi ni Melanin, waafrika wangapi wamekufa kwa Corona? wengi kati ya waafrica waliokufa kwa Corona walikuwa na magonjwa mengine makubwa na weak immune system Corona imewapiga teke tu, hatupaswi kupanic kama wazungu huu ugonjwa ni hatari sana na unatupata na tunausambaza ila si wa kusimamisha maisha yetu, yule mgonjwa wa kwanza bongo hakuambukiza mtu yoyote katika wote aliokutana nao tofauti na uzunguni huyu angeua mji mzima hivyo lockdown si lazima cha msingi ni kuwa na bajeti na timu maalum kuhakikisha inasimamia karantini kwa kila anaeingia bongo! wasio na uwezo wa hotel nashauri walipiwe na fedha ya umma because this is a public health problem si individual case na the fact is si kila msafiri anaeshuka bongo ana mawe sababu almost 90+ percent ya watu wako kwenye informal based economy! mtu anaetoka nje kabla hajapanda ndege anaweka bajeti ni ukweli kwa asie muajiriwa bajeti ya hotel ya wiki mbili za karantini hawezi kuwa nayo kwa hela za mawazo!! i speak from personal experience!

Corona virus is an invisible enemy who hits you severely but you cannot revenge or fight back!The global wealth that was created from sell of weapons, loan interests and low prices of goods from poor countries is going to be spent the same way it was created! nani kaelewa?

Ukifikiri sana utaona labda Corona ni adhabu toka juu sasa tujiulize wenzetu wa west walichomkosea muumba! je ni watu weupe kuwakandamiza kuwaibia na kuwabagua kuwanyanyasa na kuwadharau watu weusi ? je ni high interest loans to poor countries au kutupa low prices? au ni slave trade and colonialism? au ni kutuingilia mambo yetu? au ni ushoga, au ni kutengeneza silaha na kutuuzia watu weusi tuuane? au ni vita yao dhidi ya magaidi na uislam?

mi nawaza Corona si binadamu tu wanaisambaza hata wanyama wa nyumbani pets, upepo, birds, ambulances, majengo ya hospital , aircrafts na nguo za wahudumu wa afya wa Corona!!!sababu kuna wagonjwa wapya wa Corona walikaa zao home bila kuwa na contact na waathirika wala majengo yenye corona!!
 
Mi nawaza tu,ule alioufanya Makonda pale ubungo si mkusanyiko?Hivi tuko serious kweli au?Kuna jambo gani la maana ameenda kulifanya pale?shame
Taf.Tuwekeeni hiyo clip nasi tumshangae.
 
Back
Top Bottom