Ukishaamini Mungu yupo, kimsingi unakosa sababu ya kukataa kuamini uwepo wa shetani na uchawi.nimekwambia naamini mungu yupo,,,ila shetani jini sijui uchawi hivyo vyote siamini hata dhambi siamini kama kuna dhambi
Usiye na akili ni wewe unayeamini UJINGA
Imani ya kichawi ni sababu kubwa iliyowarudisha nyuma watu weusi
Badala ya kuwekeza katika elimu na teknolojia wakawekeza katika Imani ya kishenzi kama unayoamini wewe Mshenzi
Mungu alietumba sisi binadamu naamin yupo,,ila izi mambo za uchawi mashetan majini malaika siamin kama vipoUkishaamini Mungu yupo, kimsingi unakosa sababu ya kukataa kuamini uwepo wa shetani na uchawi.
Unaamini Mungu gani?
mkuu niamini mm uchawi sijui majini shetani ni story tu,,, ngoja nikitulia ntakuletea kisa changu kwann nawaambia uchawi ni stori tuKama unaamini Mungu yupo, Shetani naye yupo, na ndiye huyu chanzo cha nguvu za giza
Asantehakuna uchawi hakuna mungu
Nipo tayari kutoa details zote hizi..nipe namba za huyo mchawi nimtumie WhatsAppHio challenge uli toa maelezo haya ?
*majina yako matatu
*majina ya baba yako na mama yako
*tarehe yako ya kuzaliwa
*picha yako
Weka haya maelezo au MPE haya maelezo mtu anayetaka kukuloga halafu uje utoe ushuhuda kama lakini utakua hai
Mimi nilikuwa sinaga Habari kabisa na uchawi, lakini yalivonikuta hadi mji wangu mwenyewe nikaukimbia.
Nawaza narudi vipi kwenye boma langu
acha kubisha usichokijua mkuu, huduma za ziada wanatoa sana madaktari hasa kwenye matatizo yanayoleta utata, kama una marafiki madaktari jaribu kuwaulizia utapata jawabu.Kuna explanations nyingi sana.
Nitaje mbili tu kwa sasa.
1. Wewe muongo, umetunga hadithi. Vinginevyo, thibitisha. Hii ilitakiwa kuwa habari kubwa sana, lakini hatukuisikia popote.
2. Hata kama wewe si muongo, hakuna kitu chochote ulichoelezea kinachothibitisha uchawi. Kumbuka, kuona kitu ambacho hukielewi kimetokeaje hakuthibitishi kitu hicho ni uchawi. Ukikimbukia jusai huu ni uchawi kwa sababu huelewi kitu tu, huo ni uvivu wa kufikiri.
Huyo daktari ni wakumfukuza kazi kabisaa...mnaopinga uwepo wa uchawi mnajifurahisha tu na wala hamna lolote, majuzi tu hapa wife alikua na ujauzito wakagombezana na jirani ajili ya watoto, kilichofuata siku za kuzaa zikapitiliza tukienda hospital akipimwa hamna tatizo, mwisho dokta akanishauri yawezekana kafungwa kichawi hivo akanielekeza nikanunue dawa fulani maduka ya asili, nikaileta akakorogewa akainywa baada ya kunywa hakuchukua muda akajifungua bt cha ajabu mtoto alitoka kazingirwa mfuko wa plastic hii ilozuiwa kutumika, kama hayajakukuta ya ulimwengu chunga sana ulimi kuongea usoyajua.
Walinirudisha nyuma sana, kila ninachofanya hakiendi biashara zote zikafa na mwisho wakaamua waninyoe nywele, wakanyoa mara ya kwanza ikabidi niende saluni kuzikata zote maana hazikufaa Tena kuwa hivyo, zilivyoota mara ya pili wakaninyoa tena. Nikaona bora niondoke kwanza nikae mbali na hapo.Usiende unless ushajipigilia FIREWALLS za kutosha
Unaamini Mungu yupo lkn shetani na uchawi haupo wewe unachekesha.nimekwambia naamini mungu yupo,,,ila shetani jini sijui uchawi hivyo vyote siamini hata dhambi siamini kama kuna dhambi
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Walinirudisha nyuma sana, kila ninachofanya hakiendi biashara zote zikafa na mwisho wakaamua waninyoe nywele, wakanyoa mara ya kwanza ikabidi niende saluni kuzikata zote maana hazikufaa Tena kuwa hivyo, zilivyoota mara ya pili wakaninyoa tena. Nikaona bora niondoke kwanza nikae mbali na hapo.
Naona walifanya hapo kwangu ndio Center ya kukutana[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Hatari sana hao wachawi wanadharau.
Nguvu za giza ziko kila mahali, aisee! Acha kumtukana huyo jamaa, aisee
Nakubaliana na wewe kabisa.Muwe mnasikai tu fulani karogwa, anasumbuliwa na wachawi usiku, n.k haya mambo yakiwakuta.
Nguvu za giza haziwezi kuonekana kwa macho yetu ya kawaida wala kupimwa na vifaa vya kisayansi, Ni sawa na kurekodi ndoto ya mtu uione kwenye video, haiwezekani, hata mtu akirogwa bado ipo gizani ndio mana hata ukienda hospitalini utaambiwa mashine haziwezi kugundua chanzo cha ugonjwa wako
Binafsi nilikaa nyumba moja, ikifika saa saba kuna vishindo mithiri ya mtu anakwangua ukuta kwa nondo, na hii ilikuwa kwa wapangaji wote ila ukitoka nje kucheku huko nyuma hakuna kitu.
Ni mpaka siku moja mida hio saa saba kikalia kishindo kikubwa sana paaaa! juu ya bati kila mpangaji alitoka nje ila hakukuonekana kitu, baada ya kufatilia kumbe kuna mlangaji moja alikuwa anateswa na hawa watu usiku, babu yake alikuja siku hio hapo na kuweka mtego wake.
Tukio lengine kuna mtoto moja alikuwa na miaka mitano alikuwa mzima wa afya, ghafla akawa kipofu, kiziwi na hata kushindwa kuongea, Wazazi wake wakagundua hii hali si kawaida, walimpeleka hospitali nyingi muhimbili, kcmc, n.k ilibidi apelekwe kijijini kwa mzee wake, siku hio hio walirudi na mtoto akawa hali ya kawaida kabisa
Hapo zamani sijui kama sikuhizi bado vipo, Mashuleni ya porini huko boarding visa vya wanafunzi kukutana na vibwengo ilikuwa ni kawaida sana
Mwengine nakumbuka alivimba sana miguu, walimsihi sana waende kwao kuchekiwa ila alikua haamini hvi vitu, hata miezi miwili haikufika tukamzika.
Haha.
Nasubiri uje nikuchote nyayo.!!
Mkuu hujatulia tuu nasubir story yakomkuu niamini mm uchawi sijui majini shetani ni story tu,,, ngoja nikitulia ntakuletea kisa changu kwann nawaambia uchawi ni stori tu
Uchawi siyo just supernatural power & knowledge of exceptional mysteries, pia lengo lake ni ultimate control of humanity, degradation na destruction. Hata mtu anaeenda kwa waganga kutafuta njia mkato ya utajiri, kwa nguvu za giza anaweza kupata lakini hatimaye lengo kuu ni kumwangamiza yeye na kuwaangamiza wengine kupitia kwake. Kwa hiyo, utajiri unakuwa kama chambo tu cha kunasia.Unajuaje huu ni uchawi na hiki ni kitu ambacho sijakijua tu?
Mababu zetu walioishi miaka 140 iliyopita wangeoneshwa TV na internet leo, wangesema uchawi.
Lakini si uchawi, ni sayansi tu ambayo hawakupata kuijua.
Unahakikishaje hicho unachosema ni uchawi si kitu tofauti tu ambacho hukijui?