Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

🤣 🤣 kama sahizi tu sipindui meza, ukichota nyayo si itakua balaa.. nitarudi kwenye huu uzi kupinga yote.
Haha..!
Mwanangu bado hujakolea, nataka nikukoleze mpaka ukiskia jina langu popote unaamka..!
 
we ibilisi kuna siku nimelala kuamka asubuhi nywele zangu zimenyolewa pande mbili kulia na kushoto wakati kabla ya kulala nywele zangu zilikuwa vizuri tu . Kwa hiyo hapo natakiwa nitumie dawa ya akili sio?
Huo mtaa nilikuwa naambiwa kuna wachawi nikawa siamini. Hiyo siku ndo niliamini
Kumbe wachawi wanaenda majuzi eeh!! Me nilidhani kwa situation Kama hiyo akikukuta anakuua kabsa,Kama ndo hivyo back uchawi ni upuuzi
 
Kumpata huyo mtoto sio kigezo kwamba uchawi hauna nguvu,inawezekana huyo bibi hakuona sababu ya kukudhuru kwa sababu hauna kibaya ulichomfanyia alichukulia wewe ni rafiki wa mjukuu wake.
Na kingine pia confidence yako ilikusaidia kwa kuonesha kwamba wewe si mtu mbaya,ila ungekuwa unaenda kwa kuvizia hapo angekutilia mashaka.
"confidence yako ilikusaidia," really!? Huo uchawi wa kuzimwa kwa "confidence" wala hata siyo uchawi; itakuwa kitu kingine kabisa.
 
Kumpata huyo mtoto sio kigezo kwamba uchawi hauna nguvu,inawezekana huyo bibi hakuona sababu ya kukudhuru kwa sababu hauna kibaya ulichomfanyia alichukulia wewe ni rafiki wa mjukuu wake.
Na kingine pia confidence yako ilikusaidia kwa kuonesha kwamba wewe si mtu mbaya,ila ungekuwa unaenda kwa kuvizia hapo angekutilia mashaka.
Hapo kwenye kuona sababu ya kudhuru,kwann wactumie uchawi kumalizana na makundi ya kigaidi,etc
 
Hiyo huwa inatokea usiku wa manane unaisikia inafunguka na asubuh ukiamka unaikuta iko wazi.
Na kuna nyingine unasikia nyayo za mtu anatembea nje ya dirisha ukifungua pazia kuchungulia hakuna kitu hii nayo utasemaje?
Sasa ushasema mtu unasikia anatembea af unashangaa ukifungua dirisha humuoni,me nataka uniambie kwa mfano umekaa nje af unasikia hatua zinakufuata ila mtu mwenyewe humuon,
 
"confidence yako ilikusaidia," really!? Huo uchawi wa kuzimwa kwa "confidence" wala hata siyo uchawi; itakuwa kitu kingine kabisa.
hujaelewa,sijasema confidence ilizuia uchawi nilichosema kwamba huyo bibi aliamua kumpotezea kutokana na confidence yake kuonesha hana ubaya.
Kwani kuwa na urafiki na mtoto wa mchawi ni kosa?halafu ukizingatia wote ni watoto tu,akitaka kuthibitisha kama huyo bibi kweli ni mchawi au sio mchawi akishakuwa mkubwa aende kumdhulumu kiwanja au kitu chochote chenye thamani ndio ataona.
Uchawi huwa hautumiki kwa michezo ya kitoto
 
Sasa ushasema mtu unasikia anatembea af unashangaa ukifungua dirisha humuoni,me nataka uniambie kwa mfano umekaa nje af unasikia hatua zinakufuata ila mtu mwenyewe humuon,
nitatokaje nje wakati nahofia usalama wangu.
halafu nikidhurika utanisaidia nini zaidi ya ubishani wa kitoto tu hapa.
Hiyo labda uje kuifanya wewe ambaye huamini uwepo wa uchawi,uje ulale halafu tukisikia vishindo utoke nje ukawe mlinzi wetu
 
Mkuu nitaogopaje kitu ambacho hakina nguvu kama wewe uogope kwa sasa hivi karanga watu wakwambie karanga zinaua
Uchawi ni imani ambayo haiwezi kufanya kazi pasipo na ww kuikubali
Moja ya principle kubwa ya uchawi ni kukubali kuwa upo na una nguvu ya kufanya chochote juu yako ukikubali principle hii umekwisha
Sasa mm siwezi kuogopa kitu ambacho hakinan uwezo
Naona tunaelekea kuelewana sasa. Hoja kubwa hapa ni kwamba, Uchawi upo ama haupo??? Umesema wazi, "nitaogopaje" maana "haiwezi kufanya kazi pasipo na ww kuikubali;" ukiukubali "umekwisha." Kwa maelezo haya, hakuna mashaka tena kuwa unakubali na kuamini kuwa ushirikina siyo hadithi tu za kubuni -- upo na una madhara makubwa na unaua pia. Nimekuelewa sana!
 
hujanielewa vizuri nafikir.
Hakushindwa kukuroga kama angehitaji ila confidence ilikusaidia uonekane hauna lengo baya nao.
Ni sawa sawa unspotembelea kwenye nyumba inayofuga mbwa mkali ukiingia getini yule mbwa huwa hakurupuki kumng'ata mtu from nowhere bali huwa anaisoma saikolojia yako ukienda kwa kujiamini anakuacha anajua wewe ni mgeni salama ila ukienda kwa kubabaika huku unatetemeka atakuona wewe ni mhalifu na kukudhuru.
Ndio sawa sawa na huyo bibi mchawi saikolojia aliyoitumia ila hao wenzako wa mtaani walikuwa wanashindwa kwenda na kukosa confidence kwa sababu tayari wanajulikana ni wahuni sio watu wazuri.
Mbona unashupalia vitu ambavyo guns uhakika navyo yan ngozi bwana!! Sasa hapo wewe una uhakika gan Kama kweli hiyo bibi ni mchawi,na nyie ndo mabingwa wa kuchukua story za vijiweni af unapeleka pale utasema wewe ndo mhusika,
 
ukitaka kujua uchawi upo au haupo nenda vijijini kama usukumani halafu uwaambie wazee kwamba hakuna kitu kinaitwa uchawi na kama kipo kitu kinaitwa uchawi wakuoneshe
Kwann ukiongelea uchawi back lazima uhusuanishe na maeneo ya kijijini kuliko mjini,kushadadia uchawi unapatikana zaidi kijijini inaonesha wazi kuwa uchawi ni udumavu wa akili kwan dunia inatambua washamba,wasioelimika,wakings,vilaza etc wengi wanapatikana zaidi maeneo ya vijijin
 
Kwann ukiongelea uchawi back lazima uhusuanishe na maeneo ya kijijini kuliko mjini,kushadadia uchawi unapatikana zaidi kijijini inaonesha wazi kuwa uchawi ni udumavu wa akili kwan dunia inatambua washamba,wasioelimika,wakings,vilaza etc wengi wanapatikana zaidi maeneo ya vijijin
No uchawi unafanyika sana kwa sababu ya usiri uliopo kule kijijini.
Mjini kutokana na population ya watu waliopo limawanyima uhuru wachawi kuishi mahali hapo kwa kuona aibu kuwa mambo yao mengi yatastukiwa.
 
nitatokaje nje wakati nahofia usalama wangu.
halafu nikidhurika utanisaidia nini zaidi ya ubishani wa kitoto tu hapa.
Hiyo labda uje kuifanya wewe ambaye huamini uwepo wa uchawi,uje ulale halafu tukisikia vishindo utoke nje ukawe mlinzi wetu
Me nlipokuwa nilikuwa natoka saa name za ucku naenda kuisoma darasa zima unanikuta peke yangu,ukiuliza waskaji watakwambia wanaogopa huo uduwanzi
 
mbona wabunge na mawaziri ni matajiri na wanapishana kwenda kwa waganga kuroga hapo utasemaje?
Mosi, sina ushahidi wowote shakinifu na tajisimu (tangible & physical) kwamba viongozi "wanapishana kwenda kwa waganga kuroga"!? Lakini, swali la msingi pengine linahusu sababu ya wao kuwa matajiri ilhali wameenda kwa waganga? Ambacho tunapaswa kujua ni kwamba nguvu ya ushirikina na uchawi inaweza kukupatia vitu karibu vyote unavyoweza kutamani hapa duniani -- mali, elimu, utajiri na mapochopocho na mambo mengine mengi tu. Kila mtu anapewa kwa kadiri ya utashi na tamaa na vipaji na uwezo wake na uwezekano (potential) wa jinsi anavyoweza kuwa baadaye na kutumiwa kifanisi kwa maslahi ya "bosi" wake. Ndiyo maana utakuta kwenye ujinga na ushirikina, matokeo ndiyo hayo -- kunapatikana ujinga na ushirikina; penye mwamko wa elimu na ustaarabu na utajiri -- ushirikina unakupatia vitu hivyo na zaidi. In short, kiwango chako cha uelewa ndicho kitaamua unapewa kiasi & kiwango gani cha "hazina ya kuzimu." Anakupatia uwezo na ushawishi mkubwa ili ukasaidie vizuri kuwaghilimu wengi na kuujenga ufalme wake wa giza.
 
Kuna kitu unachanganya kidogo.
Kila kitu kina madhumuni yake na dhumuni la wachawi sio kuleta maendeleo ya nchi.
Kanuni na lengo za wachawi ni kumkomoa ndugu,jirani asifanikiwe kimaisha na kuwachezea usiku basi hiyo ndio furaha yao.
Mchawi wala hawazi kama wewe kujenga nyumba kubwa au kununua gari yeye hana muda huo.
Sasa kutowaloga chadema haiwezi kuwa justification kwamba uchawi haupo,au kukosa maendeleo kwa nchi sio sababu kwamba uchawi haupo.
Na ukizingatia uchawi ni kitu cha siri sasa utaenda kuwaita wapi hao wachawi wakakurogee wakina mbowe
Kama hivyo vitu havipo basi ujue uchawi hauna nguvu
Uchawi ni imani kama vitu vingine kijana acha kuogopa lakn siwezi kukulazimisha kukubali endelea kuugopa uchawi mm nadunda duniani lkn kuhusu uchawi siwezi kurogwa wala kufa kwa uchawi kwangu mm hiko kitu hakitotokea never
Ila kwako kinaweza kukutokea ila sio lazima ukubali navyosema
 
Naona tunaelekea kuelewana sasa. Hoja kubwa hapa ni kwamba, Uchawi upo ama haupo??? Umesema wazi, "nitaogopaje" maana "haiwezi kufanya kazi pasipo na ww kuikubali;" ukiukubali "umekwisha." Kwa maelezo haya, hakuna mashaka tena kuwa unakubali na kuamini kuwa ushirikina siyo hadithi tu za kubuni -- upo na una madhara makubwa na unaua pia. Nimekuelewa sana!
Hata mm nimekubali kwa unayosema wala sipingi kwangu mm uchawi hauna nguvu wala hauniwezi kwa lolote siwezi kurogwa mpk nife kwa uchawi hiko kitu hakuna kwangu
Ila kwako uchawi upo tena una nguvu na tena una nguvu na unaweza kukuroga ww na ukafa mara moja
 
Ndio maana nikakuambia uchawi lazima uukubali kwanza kuwa upo na una nguvu ndio utafanya kazi huko usukumani wengi wanaabudu ushirikina that's why uchawi upo na ndio maana wachawi wengi maskini kwakuwa uchawi hauna nguvu kama una nguvu wafanye uchawi waweze kujikwamua na umasikini
Pili kuwepo uchawi haimanishi kuwa una nguvu kushinda vitu vyote duniani kila kitu kina mipaka yake
Kama kweli uchawi upo na una nguvu kwanini serikali isingetumia njia rahisi kuwatumia huo uchawi wapinzani wote wafe waende huko kijijini kukusanya wachawi na wawatumie kuwaua wapinzani
Na hivyo hivyo wapinzani waende huko kijijini kutafuta uchawi na kuwatumia viongozi wote wa CCM wafe
Badala yake hayo yote yanashindikana why unadhani jibu uchawi hauna nguvu
Unaweza usikubali kwamba uchawi upo, lakini ukarogwa na ukafa mazima. Usicheze, aisee! Mshukuru sana Mungu. Pili, wapo wachawi maskini, wapo wachawi matajiri. Hakuna nyanja ya maisha hapa duniani ambapo Iblisi hajafanikiwa kupenyeza usibifu na uchafuzi wake wa kishetani. Magonjwa, ajali na matatizo mengi, yeye ndiye chanzo na mshika-usukani. Tatu, ukishaingia kwenye uwanja wa mashetani, uamuzi wa mwenendo wa maisha yako unakuwa umesalimishwa kwa Shetani mwenyewe. Anachotaka uwe ama ufanye ndivyo utakavyofanya maadamu bado ungali kwenye anga za giza. Anaweza akakutumia kwenye utajiri au katika umaskini au kwenye elimu na mafanikio na umaarufu wako. Anachohitaji yeye lengo lake litimie la kujikusanyia watu wengi kadiri iwezekanavyo katika ufalme wake. Mwisho, kwa nini serikali za dunia zisitumie uchawi kuwaroga wapinzani wao??? Kumbuka hili si jambo geni, mambo kama haya yanatokea duniani. Na visa vipo, vingi tu. Lakini pia, uamuzi wa mwisho wa hatma ya uhai wa mwanadamu yeyote haujawekwa kwa mwanadamu mwingine, bali upo kwa Mungu! Mtu fulani akifanyiwa mauaji, hata kama siyo kwa namna ya kawaida au kifo cha asili, basi lazima Mungu anakuwa ameridhia uhai wake ufikie ukomo -- ingawa mwuaji wake anabaki kuwa mwalifu na mkosaji.
 
Back
Top Bottom