Kuna mtoto wa rafiki yangu alipotea mara ya kwanza three days akaja okotwa porini na wachana mbao, alipoulizwa alikua wapi anasema hajui ila ameacha wenzake, last year alipotea one week alitafutwa mpaka wakakata tamaa kwamba atakua amekufa na kumbuka baada ya kupotea mara ya kwanza alipopatikana wakaanza kumfungia ndani hata shule wakamwachisha kwa muda, siku hyo walisahau kufunga mlango na watu wote wako kazini house girl yuko uani anafua dogo akachomoka akapotea, tulienda kwa fundi mmoja hv tukamwelezea akasema huyo mtoto bado yuko hai na anarudi, ndani ya dakika chache mke wa jamaa anapiga cm mtoto karudi ilikua saa mbili usiku anaulizwa ulikua wapi anasema alikua porini wanavuna karanga na amewaacha wenzake wanaendelea yy ameshamaliza, dogo alipelekwa kwa fundi akatengenezwa mpaka leo yuko vizur afungwi kamba hapotei na shuleni wana evening prepo anaenda na kurudi mwenyewe usiku, so uchawi upo nimeshuhudia kwa macho.