Nimehitimu chuo mwaka huu; mtaji wa Tsh. 500,000 naweza kufanya biashara gani?

Nimehitimu chuo mwaka huu; mtaji wa Tsh. 500,000 naweza kufanya biashara gani?

Wang chung

Member
Joined
Oct 26, 2024
Posts
26
Reaction score
36
Mimi baada ya kumaliza chuo mwezi wa saba nimejaribu kuomba kazi maeneo mengi ila nimekosa kisa Sina uzoefu wa kazi.

Nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu WanajamiiForums mnisaidie.

Je, ni biashara gani nzuri ambayo naweza kufanya nikiwa na mtaji wa laki tano?
 
Karibu kitaa kijana! Kuna watu watakuambia Katoe zaka kanisani! Wengine nenda ukabeti! Wengine anzisha biashara ya kuuza supu na mishikaki na chipsi sehemu yenye msongamano lakini pasiwe pa kulipa kodi ya pango! Mwingine anzisha kijiwe cha tuisheni darasa la saba mpaka kidato cha sita! Mwingine anzisha ki_grocery uza sungura na vilevi wanavyovipenda walala hoi na weka TV kuangalia mechi kwa malipo japo hapa changamoto ni frame na ulinzi! Mwingine tafuta wataalam wa IT uanze kujifunza "code" mdogo mdogo isipokuwa changamoto uwe na laptop inayorun "iOS" kama "mac book aka apple"! Wengine watakuita uje pm! akili kichwani!
 
Kijana anauliza jambo la msingi wewe unaleta mizaha ya kipuuzi, haifai!
Sio mzaha mkuu, humu ndani ushauri ni mwingi sana, kila mtu atampatia ushauri kulingana na kile ambacho kimemjia kichwani kwake bila ya kujua kuwa biashara mdomoni ni nyepesi kuliko biashara yenyewe (matendo)

Nimempa huo ushauri nikiamini kuwa yeye ni mhitimu wa chuo kikuu, hivyo atumie elimu yake kung'amua biashara itakayomfaa pasi na kisikiliza porojo za watu wengine

Aanzie kwenye mtaa aliopo, aangalie biashara zipi zinakwenda kea kasi na je wafanyabiashara wa biashara husika wanastatus zipi kwenye familia zao, je wanaweza kumudu mahitaji ya familia?

Lakini habari za kusikiliza Anonymous Participants wa humu ndani kwa lengo la manufaa ya biashara ni uongo mkuu
 
Unataka umpigie Dogo wa watu tukio. Acha hizo bwana! 🤣
Maisha ni kusaidizana mkuu🤣 Si unajua tena pesa ni zetu sote kwa kuwa tu watoto wa baba mmoja, watoto wa Hayati🤣

Haya maisha hayana formula, kikubwa matumbo yetu yaneemeke, hayo mambo ya biashara si muhimu sana kwa kuwa Mola yu pamoja nasi. Wangapi wanaishi kwa mtaji wa buku kwa siku? (Wazee wa mikeka)
 
Karibu kitaa kijana! Kuna watu watakuambia Katoe zaka kanisani! Wengine nenda ukabeti! Wengine anzisha biashara ya kuuza supu na mishikaki na chipsi sehemu yenye msongamano lakini pasiwe pa kulipa kodi ya pango! Mwingine anzisha kijiwe cha tuisheni darasa la saba mpaka kidato cha sita! Mwingine anzisha ki_grocery uza sungura na vilevi wanavyovipenda walala hoi na weka TV kuangalia mechi kwa malipo japo hapa changamoto ni frame na ulinzi! Mwingine tafuta wataalam wa IT uanze kujifunza "code" mdogo mdogo isipokuwa changamoto uwe na laptop inayorun "iOS" kama "mac book aka apple"! Wengine watakuita uje pm! akili kichwani!
Ila we jamaa 😁😁😁.
 
Tafuta Machinjio ya MBUZI, fanya yafuatayo :-
1. Nunua vichwa vya mbuzi kwa 2500 - 3000/- kila kichwa
2. Andaa sehemu ya kupikia, ( Karibu na grocery/bar au sehemu yenye mkusanyiko)

3. Andaa Vifaa kama vile, sufuria kubwa, jiko, visu, bakuli, sahani.

4. Mahitaji, unga, chumvi, pili pili, nyanya, vitunguu, kiberiti, mkaa,

Maandalizi
Chukua kichwa cha mbuzi, kiandae ukiwa bado upo nyumbani ( koka moto wa kuni, choma vichwa hakikisha manyoya yote yanaungua, baada ya hapo tafuta sufuria kubwa vichemshe mpaka vinaiva kisawa sawa, ( kazi hii ifanyike asubuhi ikifika mchana kila kitu kiwe tayari,)

. Mida ya saa nane andaa sufuria ndogo ndogo kwa ajili ya ku roast vichwa vya mbuzi, ( nyanya, kitunguu, chumvi, pilipili ni mhimu, ) ( usiuze kichwa kama kilivyo unakiponda ponda kama ulojo fulani vile, Wataalam wa haya mambo waananielewa ninacho maanisha)

. Kichwa kimoja fanya elfu 6000 - 7000/- nusu kichwa fanya elfu 3000 - 4000/- plus ugali 4000 - 8000/-,

. Vichwa 5 × 2500 = 11500/-( gulioni)
. Baada ya kuuza 6000 × 5 = 30000/-
. Ugali 1000 matonge 10 =?

. NB: kwenye kila mteja atakaye kuja kuorder iwe nusu au Kichwa kizima hakikisha unapunguza nyama 2 au 3, mpaka unapata kichwa kingine cha ziada, ( hii utalipia nauli, kuni, chumvi na kitunguu), but Tamaa ni mbaya, ukigundulika wataje watahama wote.

. Mwisho Acha ubishoo na kupenda uliko zaliwa/toka..

Jumla ni laki 3, alafu unabakiwa na salio la laki 2 mfukoni
 
Mimi baada ya kumaliza chuo mwezi wa saba nimejaribu kuomba kazi maeneo mengi ila nimekosa kisa Sina uzoefu wa kazi.

Nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu WanajamiiForums mnisaidie.

Je, ni biashara gani nzuri ambayo naweza kufanya nikiwa na mtaji wa laki tano?
Kabla ya kupata ushauri....

Uko wapi, na una interest na mambo gani, uanzie huko kupata ideas.
 
Sio mzaha mkuu, humu ndani ushauri ni mwingi sana, kila mtu atampatia ushauri kulingana na kile ambacho kimemjia kichwani kwake bila ya kujua kuwa biashara mdomoni ni nyepesi kuliko biashara yenyewe (matendo)

Nimempa huo ushauri nikiamini kuwa yeye ni mhitimu wa chuo kikuu, hivyo atumie elimu yake kung'amua biashara itakayomfaa pasi na kisikiliza porojo za watu wengine

Aanzie kwenye mtaa aliopo, aangalie biashara zipi zinakwenda kea kasi na je wafanyabiashara wa biashara husika wanastatus zipi kwenye familia zao, je wanaweza kumudu mahitaji ya familia?

Lakini habari za kusikiliza Anonymous Participants wa humu ndani kwa lengo la manufaa ya biashara ni uongo mkuu
Hayo uliyomshauri hapo ulipaswa uyaseme huko juu kuliko kumsihi aje baani.

Jamiiforums imesaidia wengi kutokana na michango chanya ya wanajamiiforums.

Tuheshimu shida za watu, tuwasaidie inapobidi ndiyo maana ya kuwamo humu jukwaani.
 
Mimi baada ya kumaliza chuo mwezi wa saba nimejaribu kuomba kazi maeneo mengi ila nimekosa kisa Sina uzoefu wa kazi.

Nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu WanajamiiForums mnisaidie.

Je, ni biashara gani nzuri ambayo naweza kufanya nikiwa na mtaji wa laki tano?
Mungu akupe hitaji la moyo juice ya "miwa chief" kazi kwako kuuliza bei ya Ile machine hapo utafte eneo la watu weng kama ni daslam "Usione aibu" maana maisha ni yako hakuna mtu atakaekuuliza umekula au haujala
 
Back
Top Bottom