KERO Nimeibiwa kamera Tabata, sikupata msaada stahiki Kituo cha Polisi Stakishari. Mwizi anajulikana maeneo yale, amefanya tukio jingine na bado anapeta tu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Yaani kesi ya kibaka unampelekea jambazi unategemea nini?

Ila kiukweli haya mambo ya polisi tuendelee kuyasikia tu usiombe siku uwe na shida na kutaka msaada kutoka kwao ndio utawajua vizuri hawa wapumbavu
 
Ndio maana nawachukia wezi.. Mwizi anapokuibia anakuletea matatizo tu.. Hata ukienda polisi nao badala ya kufanya kazi yao ndio wanaona ATM imejileta.. Huku kwetu tunawabanika tu ili wengine wajifunze .
 
Babu uswahilini unaweza pita nyumbani kwa mtu hata sio mwenu na usiulizwe kitu.
 
NIkushauri jambo zuri.

Kesho ni jumaa mubarak, nitaenda kuswalisha katika msikitini Fulani, je upo tayari kumdhuru mwizi wako kwa kumtupia jini baya la maangamizi ya maradhi, kama upo tayari niambie nisome dua kesho masjid. 😃😃😃
 
Au aende Nachingwea kule kuna fundi mmoja, wamama wa mjini Daslamu na Unguja wanamtumia sana kupora waume za watu. Fundi mwenyewe ni wale waganga ambao wanaua kabisa yani jina lako likipelekwa kwake leo basi kesho unazikwa.
Hahaa mkuu noma sana . Huyu Babu hataki uite albadili wanaita kumshtakia Mungu
 
Mkuu kama ni serious funguka kuna watu walitupiga matukio ya hatari
 
Ndugu wa mwizi watalipa kivipi na kwa njia gani?
 
Au aende Nachingwea kule kuna fundi mmoja, wamama wa mjini Daslamu na Unguja wanamtumia sana kupora waume za watu. Fundi mwenyewe ni wale waganga ambao wanaua kabisa yani jina lako likipelekwa kwake leo basi kesho unazikwa.
😀😀😀😀😀😀Yaani jina likipelekwa tu watu kesho wanafunga Maturubai na kula wali maharage bure
 
Rahisi huyu kumdaka, awe na Rb yake tu mfukoni amsake kwenye mabaa ya Tabata na huko Kinyerezi..
 
Ungewaambia tu Polisi kuna mtu wa CHADEMA anapanga maandamano, tayari angekuwa amekamatwa ndio baada ya hapo ueleze kesi yako ya msingi.
 
Pole sana mimi 2017 walichukua 7m zangu walikua ni polisi ....nlienda kwa rco ambae sasa ni rpc manyara.walirudisha 8m kwa kuniomba sana ...tuliozaliwa mjini tunadeal na majizi kimenomeno tu
 
Hawa wapuuzi wanakera...Kama una uwezo mloge awe mwehu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…