Nimejaa hofu kwa nilichokishuhudia kwa mpenzi wangu

Nimejaa hofu kwa nilichokishuhudia kwa mpenzi wangu

Wana jukwaa naomba nisipoteze muda niende moja kwa moja kwenye mada.

Nimepitia misuko suko mingi sana katika mahusiano,ilifika mahali nikaomba wadau mnishauri kwa baadhi ya mambo yaliyonikumba,nawashukuru wengi mlinishauri na maisha yakaendelea.

Nilipata binti,mpole na mtaratibu sana,nimekuwa naye katika vipindi vigumu na hakuwahi kuonyesha hali yoyote yenye mashaka.

Nimeshitushwa sana leo baada ya kuona vitu vya ajabu kwenye mkoba wake,(ambao sikuwahi kuuona tangu nimefahamiana naye,).

Naviweka hapa,wataalamu wa lugha ya kiarabu naomba mnisaidie kutafsiri maana ya maneno haya,nimekuta karatasi ikiwa na picha yangu,imeandikwa kwa maandishi mekundu kwa lugha ya kiarabu,halafu imefungwa na karatasi nyeusi!!!

View attachment 532069View attachment 532071View attachment 532072
It was supposed to be something called KOMBE but huyo mganga aliyeandika kamuongopea.. In short demu wako alitaka kukuchanganya kimapenz kwa kutumia njia za kishirikina so huyo demu amekuletea what was meant to be the LIMBWATA but hamna kitu kitu hapo..!
Mbane atakwambia kila kitu!
 
Leo unatakiwa usimamie kucha mkuu! Hakikisha hatumwi mtoto dukani leo...
 
Naamini humu kuna watu wa imani tofauti tofauti,na wenye kujua lugha mbali mbali,nisaidieni tafsiri kwanza,kabla ya maoni binafsi mengine,nina wakati mgumu kweli,sio kwa sababu naogopa kufa kama baadhi ya watu wanavyonitisha hapa,(kila mmoja atakufa tu,kama sio leo,kesho)isipo kuwa wakati mgumu ni kwanini anifanyie hili,(kama ni kwa ubaya)
 
Duh JF kumbe kuna wachawi. Kwa nini mshana jr na wenzako hamjitokezi kumsaidia huyu bandugu, au mnaogopa mtayaumbua majini yenu?
 
It was supposed to be something called KOMBE but huyo mganga aliyeandika kamuongopea.. In short demu wako alitaka kukuchanganya kimapenz kwa kutumia njia za kishirikina so huyo demu amekuletea what was meant to be the LIMBWATA but hamna kitu kitu hapo..!
Mbane atakwambia kila kitu!
Nimefungua hicho kifungashio,nimekuta kuna baadhi ya vitu nisivyovijua,vina rangi nyeusi na vinatoa harufu ambayo nashindwa kuielezea but kama nyama ilivunda hivi,what is iiiit!!???
 
Ndio maana mm sipendi kukagua pochi ya mwanamke...mzee umekuta mpk pu.mbu ya paka iliyokaushwa....subiri mshana aje kwny fani yake
Sijawahi kuikagua,lakini amesafiri na akanambia nitafute ufunguo kwenye pochi,katika harakati za kutafuta funguo ndo nimekutana na hii kitu!!!
 
Back
Top Bottom