Nimejaa hofu kwa nilichokishuhudia kwa mpenzi wangu

Nimejaa hofu kwa nilichokishuhudia kwa mpenzi wangu

Nenda kwenye ule uzi wao wa uchawi uulize huenda wakakupa jibu
 
Naamini hakuna atakayeleta tafsiri ya kweli kabisa hata kama kilichoandikwa hapo ni fekero,.wengi wataishia kusema hamna kitu, katapeliwa n.k...
 
Inaonekana binti alikwenda kwa fundi labda kukutengeneza ila amekutana na findi tapeli kwa sie tunaejua lugha hii hapo hakuna neno la maana linaloweza kusomeka kwa ufupi naweza kusema fundi kajua huyo binti hajui hyo lugha so ndo maana kaamua kumdanganya

Hapo kaandika herufi tu za kiarabu ni sawa na wewe uandike z,x,c,v,t,y,w,a yaan ilimradi tu umuhadae mtu ila niamini mimi kuwa hakuna maana yeyote hapo na wala hakuna neno lolote la maana lililoandikwa hapo.

Hapa huwa ndo naamini maneno ya dada faiza foxy kuwa "wajinga ndo waliwao" hapo mwanamke wako kadanganywa

NOTE.
Huyo binti anaonekana ni mshirikina leo kapata fundi tapeli kesho aweza pata mkweli na akakutengeneza vizuri tu so kuwa makini sana.
Muombe Mola hakuna linalomshinda sisi waislam tunafundishwa kuwa uchawi upo ila usiuamini sana maana hutomuamini mola.
Muamini mola hakuna linalomshinda na tunafundishwa katika uislam kukaa mbali na shirki (ushirikina) na watu wake.
kakutana na fundi wa kidigital mtoto wa Muji wakala mpunga.Yawezekana hata kumla wamemla .Usicheze na Jeshi la shetani
 
Naamini hakuna atakayeleta tafsiri ya kweli kabisa hata kama kilichoandikwa hapo ni fekero,.wengi wataishia kusema hamna kitu, katapeliwa n.k...
wewe tupe tafsiri sahihi mkuu,hata kwa macho ya nyama kiarabu hakiandikwi hivo.
 
Mkuu kwanza Pole sana. Ila Ukweli hayo maandishi yana Maana kubwa sana katika Lugha ya Majini na Uganga. Hata kama Mtu anajua kiaruabu kama hana Jini au Uganga hawezi kuelewa maana na ndiyo maana siyo Kila anayejua Kiarabu ni Mganga au anaweza ita Jini.

Ila kama akajitokeza Mganga humu ndani ataelewa hiyo Lugha na Maana yake. Japo tunaambiwa tusiamini Uchawi ila Uchawi wa Mapenzi upo asikudanganye Mtu. Ishara ya Kukuta Picha yako na Hicho Kinyama kilichoko kwenye huo Mfuko mara Nyingi wanatumia nyama ya Bundi ili uwe zezeta na kumsikiliza yeye tu.

Kwanza Mshukuru Mungu Kukufunulia hilo. Kama ni Mcha Mungu Omba sana na Kama huyo ni Mke wako Mbane atakwambia ukweli.

Mimi Nayafahamu haya na siku zote hayo Mambo yakigeuka Mwanamke ndiyo ambaye hukimbia Nyumba kwa kukiuka Masharti.

Hiyo ni Lugha ya Kiganga na Huwezi itafsiri kwa kuwa Unajua Kiarabu.

Pole
 
Wana jukwaa naomba nisipoteze muda niende moja kwa moja kwenye mada.

Nimepitia misuko suko mingi sana katika mahusiano,ilifika mahali nikaomba wadau mnishauri kwa baadhi ya mambo yaliyonikumba,nawashukuru wengi mlinishauri na maisha yakaendelea.

Nilipata binti,mpole na mtaratibu sana,nimekuwa naye katika vipindi vigumu na hakuwahi kuonyesha hali yoyote yenye mashaka.

Nimeshitushwa sana leo baada ya kuona vitu vya ajabu kwenye mkoba wake,(ambao sikuwahi kuuona tangu nimefahamiana naye,).

Naviweka hapa,wataalamu wa lugha ya kiarabu naomba mnisaidie kutafsiri maana ya maneno haya,nimekuta karatasi ikiwa na picha yangu,imeandikwa kwa maandishi mekundu kwa lugha ya kiarabu,halafu imefungwa na karatasi nyeusi!!!

View attachment 532069View attachment 532071View attachment 532072

Labda alitaka kukuloga lakini icho sio kiarab.
 
Naamini hakuna atakayeleta tafsiri ya kweli kabisa hata kama kilichoandikwa hapo ni fekero,.wengi wataishia kusema hamna kitu, katapeliwa n.k...
Mkuu hakuna tafsiri yoyote hapo kwa kuwa hakuna maneno ya maana yaliyoandikwa hapo

Hivi unaweza kutafsiri neno hili xsjtky???
Kwa hakika huwezi.
Basi kama huwezi tafsiri neno hapo juu ndo vile vile huwezi tafsiri hayo maneno ya mshirikina tapeli kwenye hiyo karatasi.
 
wewe tupe tafsiri sahihi mkuu,hata kwa macho ya nyama kiarabu hakiandikwi hivo.
Ningekuwa nakijua na kama kilichoandikwa ni kiarab bas nongetoa...hata kama ni mapalanganyata au herufi/ namba ningetafsiri kama ilivyo...
Naamin umeelewa nlichomaanisha...
 
Alisema. Kuanzia Leo utoe ubahili umpe chochote atakacho. Umpende yeye pekee na ukichepuka ka dudu kako kalegee kama mlenda .fungua waleti toa ubahili.
 
Duh.. mlikutana nae wapi huyo mwanamke kwenye mitandao nini???? Hatari sana ingawa siaminigi hayo mambo kama yana nguvu kweli.... Imani tuuuuuu ukiweka hofu ndio itakusumbua sanaaaaaaa
 
Lugha ya Kichawwi siyo Lugha sawa na Kibinandamu.. Ndiyo Mana unakuta Mtu wako Uchi Mahospitalini lakini hakuna anayejua kama kuna watu waliopo Uchi mahopitalini wanatembea mpaka uwe na macho ambayo yapo kati Dunia yao. Hakuna Lugha ya Kiganga ambayo inaweza tafsiriwa na kila Mtu kama ingekuwa hivyo basi wote wangekuwa ni waganga.
 
Nina imani aliwahi kukuuliza jina la mama yako na ukamtajia, manuizi hayo ni hatari but utashinda. Fanya maamzi magumu hizo ni dawa za mapenzi.
 
Mkuu msaada wangu hapo ni kujikausha.. Then unakurupuka kama umepanda mashetani vile..! Unasema sema maneno ya ajabu ajabu yasioeleweka.. Then unamgeukia huyo demu! Unampiga mikwara ya kutisha ukijifanya mashetani yako yamestukia uchawi wake..! Then shetani anasema atoe vitu vyote kwenye mkoba..![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Akitoa na madude yake unamkazia kuwa leo umemsamehe ila akirudia tena kutaka kumchezea kiti ATAKIONA CHA MTEMA KUNI!
Nakwambia harudii tena huyo!
 
Ningekuwa nakijua na kama kilichoandikwa ni kiarab bas nongetoa...hata kama ni mapalanganyata au herufi/ namba ningetafsiri kama ilivyo...
Naamin umeelewa nlichomaanisha...
hicho kiarabu alichoandika hata mie Mgalatia naandika
 
Back
Top Bottom