Nimejaribu kuanzisha biashara mbalimbali lakini huwa hazidumu. Naombeni ushauri

Nimejaribu kuanzisha biashara mbalimbali lakini huwa hazidumu. Naombeni ushauri

Ukisoma masimulizi ya waliofanikiwa kwenye biashara mfano Elon Masks ama Macdonald's wanasema Kuna wakati hali ya biashara iliwaendea vibaya hadi wakatamani ku-quit biashara

Lakini pamoja na kuanguka mara kadhaa, lakini hatimaye alisimama Tena na kufanikiwa.

Endelea kujipa muda, utafanikiwa Siku Moja

Ukiona biashara hiyo ya Laundry (Ufuaji) hailipi kulingana na Msimu, jaribu kufanya biashara nyingine

Kila la heri Mkuu 🙏
Hawa nao sio wa kuwasikiliza sana 😆, walikuwa na foundation nzuri na connection. Bill Gate mama yake alikuwa anajuana na mwenyekiti wa IBM, na yeye mwenyewe Bill alikwara project ya watu japo ana uwezo mkubwa na maarifa makubwa.

Elon Musk nae baba yake alikuwa vizuri kifedha.

Dada yetu anatakiwa ashauriwe na asaidiwe kulingana na mazingira yetu na kwa mujibu wake ana changamoto
 
Habari Wana JamiiForums,

Nimekuja hapa nikiomba mawazo yenu, ushauri na msaada ikiwezekana. Katika maisha yangu nimejaribu sana kutafuta kazi sehemu mbali mbali bila mafanikio, na hata nikipata haidumu kabisa inatokea changamoto naikosa, nimekuwa mtu wa kutamani sana na Mimi niweze kuwa na sehemu moja ya kujipatia riziki lakini inashindikana, na sitaki kukata tamaa licha ya changamoto zote hizi.

Nimejaribu kuanzisha bihashara mbalimbali lakini huwa hazidumu, hata nilianzisha ya kufua na nilipostigi humu Kuna watu baadhi walijitokeza nikawafanyia kwa ufasaha lakini baadae ikatokea changamoto nikashindwa kuendelea. Nashindwa kuelewa ni kitu gani kinanizunguka kwenye maisha yangu na mtaji wangu, inafika kpindi nakosa hata pesa ya kula kwa siku lakini Muumba wetu anazidi kunipa nguvu ya kuendelea kusimama Tena na kupambana.

Na kipindi hiki cha mfungo kwangu kimekuwa ni kigumu sana kwa kukosa pesa ya kujikimu kwa kipindi kizima. Naombeni mnigaie ushauri nifanye nini niweze kusimama imara kwa uthabiti, mwenr kazi pia naomba anisaidie ili niweze kujikimu.

Naombeni mawazo yenu na ushauri wenu maana akili yangu imefikika mwisho kuwaza Mimi ndugu zangu. Nimechoka.
fanya biashara moja tu, mpaka uielewe changamoto zake zote na namna ya kukabolianza nazo. Ikianza kujiendeshaa yenyewe bila kuhitaji usimamizi wako ndiyo funguwa nyingine. Bila hivyo utahangaika sana.
 
Biashara uchawi ni location na bidhaa sahihi. Wakati mwingine unakuta unaenda anzisha biashara sehemu mbaya kwa kuhofia kodi kubwa eneo lenye mzunguko mzuri
Jamani wewe huko ulimwengu gani unayetaka location? Biashara ya sasaiv haitaji chumba cha kupanga, ni wewe tu na akili yako.
 
kuna mdada mmoja huku mtaani alianzisha biashara ya chakula alifanya biashara siku moja tu siku iliyofuata akafunga biashara sababu anasema biashara ngumu sasa anaendelea na biashara yake ya muda mrefu ya kuuza nyama (code)
Ipo siku atazeeka au maradhi kabla ya uzee.
 
Utapata msaada humuhumu jf usijali.kuna watu humu huna haja ya kuwajua .
Watakusaidia.
 
Hawa nao sio wa kuwasikiliza sana 😆, walikuwa na foundation nzuri na connection. Bill Gate mama yake alikuwa anajuana na mwenyekiti wa IBM, na yeye mwenyewe Bill alikwara project ya watu japo ana uwezo mkubwa na maarifa makubwa.

Elon Musk nae baba yake alikuwa vizuri kifedha.

Dada yetu anatakiwa ashauriwe na asaidiwe kulingana na mazingira yetu na kwa mujibu wake ana changamoto
Naungana na Wewe Mkuu, Kibongo Bongo mitaji yenyewe ya biashara ni changamoto. Japo pia tuna tatizo la kutofanya uchambuzi makini wa aina ya biashara za kufanya.

Kuna biashara nyingine, kama hauna taarifa za kutosha unaweza kujikuta unapoteza Mtaji wako
 
Back
Top Bottom