Nimejifunza pakubwa kuhusu elimu ya fedha baada ya jamaa yangu kuchukua mkopo wa Milioni 10 kazini kwake ili anunue gari

Nimejifunza pakubwa kuhusu elimu ya fedha baada ya jamaa yangu kuchukua mkopo wa Milioni 10 kazini kwake ili anunue gari

inasikitisha sana asilimia kubwa ya watumishi hawana elimu na uelewa wa fedha kinachotuponza watanzania wengi tunaishi kwenye macho ya watu zaidi kuliko uhalisia wetu..... tunateswa sana na maisha ya wengine hatuishi kufanya makosa yale yale tunayoona wenzetu wamekosea
 
Watu wengi wanajidanganya eti huwezi kuendelea bila kukopa. Kimsingi unakopa ili uzalishe uweze kulipa riba na wewe kubaki na faida.

So kabla ya kukopa piga hesabu. Riba ni shs ngapi kwa mwezi? Je utapata faida ya kiasi gani kwa mwezi? Je faida ni kubwa kuliko riba?

Kama faida ni kubwa kuliko riba unaweza kukopa.

Sasa tatizo la watu wengi wanakopa wanaenda kutumia mikopo kwenye vitu visivyo zalisha kama kununua gari au kujenga nyumba.
Yaani mtu ajenge nyumba halafu useme ametumia mkopo kwenye vitu visivyo na faida?

Anyway siwezi kukulaumu sana maana inawezekana unaishi maeneo ya ndanindani huko ambako thamani ya nyumba haionekani ila kwa mtu aliyepo kwenye miji iliyochangamka hawezi kutamka hii kauli nyumba eti ni matumizi mabaya ya mkopo.

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Watumishi msiogope kukopa. Kopa Kwa malengo mazuri yenye faida hata Kwa baadae( uwekezaji), Usikope mkopo wa Muda mrefu ishia miaka mi tatu. Usikope Kwa riba kubwa.
Maisha ya ajira ni mafupi Sana.
 
Wengi wa staffs wenzangu waliochukua mikopo kwa mambo mbalimbali, hakuna walilofanikisha, tuko nao level moja, ila wao stress ya mikopo inawatesa.

Kuna Theory inasema hiviii: "99% ya employees huwa wana idea ya ujasiriamali pindi wanapoajuriwa, na wengi huingia kwenye ujasiriamali. Lakini ni 1% tu ndiyo hufanikiwa kujikwamua kiuchumi".
 
Maisha ya sasa usipokuwa na financial literacy (elimu ya pesa) unaweza kujikuta umeingia kwenye utumwa wa matumizi makubwa, ambayo baadaye yanakupeleka kwenye uraibu wa mikopo usioisha.

Mambo haya huwa yanawakumba sana watumishi wa serikali, hasa walimu. Watumishi wa sasa wengi wanatamani kuishi maisha ya ndoto zao, kama kumiliki nyumba nzuri, kuwa na magari, kuwa na miradi ya kuongeza kipato kama mashamba na fremu za biashara.

Kutokana na kuwa na mishahara ya wastani huku wengi wao wakiwa na extended family, hushindwa kujizuia na msukumo wao wa ndani wa kutaka kulazimisha mambo bila kujali wataathirika vipi.

Mfano, kuna jamaa yangu mmoja ambaye ni mtumishi wa serikali (mwalimu) alitaka kununua Toyota IST kwa bei ya Shilingi milioni 14. Alikuwa na Shilingi milioni 6 na alihitaji kukopa benki kiasi cha Shilingi milioni 10 ili aweze kukamilisha manunuzi yake.

Kwa sasa, karibu kila benki inatoza riba ya asilimia 16. Jamaa alishawishiwa achague muda mrefu wa malipo ili alipe kidogo kidogo, akaingia mkenge.

Kitu ambacho hakujua ni hiki: (72 ÷ riba), yaani (72 ÷ 16) = 4.5. Mkopo wowote kwa riba hiyo ukifika miaka 4.5 na kuendelea, utalipa mara mbili ya kiasi ulichokopa. Hivyo, kama alichukua milioni 10, atalipa milioni 20.

Sasa mwenzangu alichukua mkopo wa miaka 6 ili awe analipa Shilingi 300,000 kila mwezi. Aliposanuliwa kwamba atalipa mara mbili ya alichokopa, alichoka sana maana ilikuwa too late.

Hivi ninavyoandika haya, hana hamu ya kuendesha gari hilo, kwani anategemea mshahara pekee na gari halimuingizii pesa, bali linahitaji gharama za mafuta na matengenezo mbalimbali.

Watumishi mkumbuke kuwa serikali imewaajiri wenyewe, haijaajiri matumizi yenu.

Kwa haraka, pato lako kwa siku ni Shilingi 20,000. Hivyo, chunga matumizi yako, usijitumbukize kwenye mzigo wa madeni bila mpango.
Ila Kuna muda walimu tunazingua,

Kuna mjinga mwingine tulikuwa naye school moja, ameajiriwa baada ya kupata baria ya uthibitisho tu kakopa kachukua RAUM

Wakati huo amenumua gari anakaa kwenye nyumba za walimu hapo hapo shuleni, maana shule ni ya boarding

Ameendesha gari mwaka tu akapata ajali (alikuwa amelewa)

Pesa ya matengenezo hana, akaamua kuiuza
 
Waalimu huwa wanafundishwa kozi ya ujinga kwa siri wakiwa vyuoni? Hakuna mtu makini atachukua mkopo bila kupiga vizuri hesabu za riba. Na inajulikana ukilipa mapema ndo riba inakuwa ndogo. 10m kuilipa kwa 6yrs ni umaskini uliokithiri.
Ujinga huo afundishe nani?

Shida kubwa walimu wengi wametoka mazingira ya kimaskini ( automatically umaskini upo ndani ya comfort zone na kutoka humo ni shida nyingine)

Kesi hizo zipo sana kwa watumishi wengi ila walimu ni representative tu kwa kuwa wapo wengi
 
Watumishi wengi wamekuwa masikini sababu ya mabenk.
Bank si msaada ni mfumo wa kifreemason wa kuchukua pesa bila jasho toka kwa watu masikini.
 
Bora angebeti,mabenk yapo kwa ajili ya kuwafilisi watumishi.
Nmb na crdb bila watumishi wa serikali zingeshajifia.

watumishi wao wana hasara gani. kwani wao wanfanya biashara gani hadi useme wanafilisiwa.

kuna mwl flani ana likizo ya ugonjwa mwaka wa tatu sasa Yuko nyumbani mwisho wa mwezi anakwenda kuzikinga kunako ATM Machine
 
Maisha ya sasa usipokuwa na financial literacy (elimu ya pesa) unaweza kujikuta umeingia kwenye utumwa wa matumizi makubwa, ambayo baadaye yanakupeleka kwenye uraibu wa mikopo usioisha.

Mambo haya huwa yanawakumba sana watumishi wa serikali, hasa walimu. Watumishi wa sasa wengi wanatamani kuishi maisha ya ndoto zao, kama kumiliki nyumba nzuri, kuwa na magari, kuwa na miradi ya kuongeza kipato kama mashamba na fremu za biashara.

Kutokana na kuwa na mishahara ya wastani huku wengi wao wakiwa na extended family, hushindwa kujizuia na msukumo wao wa ndani wa kutaka kulazimisha mambo bila kujali wataathirika vipi.

Mfano, kuna jamaa yangu mmoja ambaye ni mtumishi wa serikali (mwalimu) alitaka kununua Toyota IST kwa bei ya Shilingi milioni 14. Alikuwa na Shilingi milioni 6 na alihitaji kukopa benki kiasi cha Shilingi milioni 10 ili aweze kukamilisha manunuzi yake.

Kwa sasa, karibu kila benki inatoza riba ya asilimia 16. Jamaa alishawishiwa achague muda mrefu wa malipo ili alipe kidogo kidogo, akaingia mkenge.

Kitu ambacho hakujua ni hiki: (72 ÷ riba), yaani (72 ÷ 16) = 4.5. Mkopo wowote kwa riba hiyo ukifika miaka 4.5 na kuendelea, utalipa mara mbili ya kiasi ulichokopa. Hivyo, kama alichukua milioni 10, atalipa milioni 20.

Sasa mwenzangu alichukua mkopo wa miaka 6 ili awe analipa Shilingi 300,000 kila mwezi. Aliposanuliwa kwamba atalipa mara mbili ya alichokopa, alichoka sana maana ilikuwa too late.

Hivi ninavyoandika haya, hana hamu ya kuendesha gari hilo, kwani anategemea mshahara pekee na gari halimuingizii pesa, bali linahitaji gharama za mafuta na matengenezo mbalimbali.

Watumishi mkumbuke kuwa serikali imewaajiri wenyewe, haijaajiri matumizi yenu.

Kwa haraka, pato lako kwa siku ni Shilingi 20,000. Hivyo, chunga matumizi yako, usijitumbukize kwenye mzigo wa madeni bila mpango.
Hii chai kama chai nyingine 😂😂
Ukikopa 10M kwa miaka 5 unalipa roughly 15M sio hio 20M yako
 
Back
Top Bottom