Deejay nasmile
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 5,794
- 5,352
- Thread starter
-
- #21
Huna adabu kijana...Ni mchawi alikuwa anakuotesha hiyo ndoto ili apate pa kuanzia kukupakua humo humo ndotoni usingestuka mdoto ilikuwa hivi.Yule mchawi angekuotea na hela zake angekuambia ukitaka akuachie zile hela akupakue kwanza najua ungekubali tu mbele ya milioni tisa? Hivyo angekupakua kwa hiari yako mwenyewe na ungechukua hizo milioni tisa,ukiamka ahsubuhi unagundua ni ndoto tu ila kwenye ulimwengu wa kiroho mchawi anakuwa amakukamua kiukweliukweli.Kijana siku nyingine humo ndotoni usipende kuokotaokota kitu
Isingekuwa ndoto ingekuwa ni gahawaYaan hapa nimechanganyikiwa hatari
Nilikuwa natoka natoka hapa mitaa ya mabibo hostel naelekea riverside.mbele kidogo nikaona kifungashio cheusi kando kidogo ya barabara kinaonesha kama kina kitu ndani.watu wanakipita tu, sasa sijui hawakukiona au ndo ubize tu wa mjini.
basi nilipokikaribia bila aibu nikaokota na kuendelea na safari mdogo nikitafuta sehem niangalie kuna nn...basi nikaingia kiduka flan kinauza uza vinywaji kuna ile miavuli ya jua nje..nikakaa nikachungulia ndani nikaona bahasha ya kaki ina nembo ya nmb na kadi ya bank (atm card).
Nikiwa na presha na hofu tele nikaichana ile bahasha ikiwa mule mule ndani ya kifungashio. Daaah!! Nakuta noti kibaoo za elfu 10 ..nikafunga fasta na kuinuka kuelekea upande wa pili kuna baa moja hivi..
nikaingia na kupitiliza moja kwa moja chooni nikajifungia huko na kuanza kuhesabu....ni pesa taslimi milion 9 zilikuwa mule..yaani nilipata kiwewe hatari kilichochanganyika na furaha na sala kama zote yaani.
Ghafla kuna mtu akagonga mlango ule wa chooni..kwa mshituko nikazifunga tena fresh na kutoka nje..ili niangalie utaratibu wa kurudi gheto nikaanze kupanga bajeti sasa.
Ghafla nikashtuka toka usingizini.kumbe nilikuwa nao ta tu ndugu zangu..sasa sijui hii ndoto ina maana gani wakuu...watalaam wa ndoto naombeni mnitafsirie ndoto hii!!
We itakuwa sio mzoefu wa kushika pesa ndefu....wale teller wa benk wanahesabu hizo dk 2 tuIsingekuwa ndoto ingekuwa ni gahawa
Kwanza pesa zina harufu ungejua kuwa ni pesa before hujafungua
Lakini kuhesabu milion9 taslimu choo cha baa ni kipengele ukiwa na wenge la hiyo hela huwezi hesabu ukamaliza
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Teller wa bank sasa ndiyo nani ni weweWe itakuwa sio mzoefu wa kushika pesa ndefu....wale teller wa benk wanahesabu hizo dk 2 tu
sawa bosiTeller wa bank sasa ndiyo nani ni wewe
Unajua wenge la kuokota hela tena kipande kama hicho hii ilikuwa ni chai tu huna namna ya kutuelewesha wenye akili lakin
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app