Pole mkuu ,mi pia ni muhanga wa uraibu wa kamari...nlianza kwa kutest tu nione experience ya wachezaji betting ikoje ..kama ilivyoada mwanzo kabisa nilibeti timu moja nikashinda..nikaona mchezo si ndio huu...ebanaa kilichotokea baadae ni vipigo...ikitokea nimemla kanji nasema hii faida ngoja ni re invest tena huenda nitapata zaidi nirudishe pesa zangu nilizoliwa ila daaaa vipigo vinaendela...mbaya zaidi nikasema ngoja niangalie upepo wa virtual games kama instant virtual, virtual football leagues, roulette, spin wheel,black jack,Crypto crash games,baccarat, poker n.k nimefanikiwa kujua hizi games na strategies kibao za kuzicheza ila nimeona ni upumbavu mchezo wa kamari hasa huu wa online kwani the house always wins kama alivyowahi kunambia
KeyserSoze ,mwanzo sikumuelewa nini anamaanisha nikasema ngoja niendelee kuexplore this industry dah ni mwendo wa hasara tu....
Side effects nilizokwisha kuzipata ni kama depression, stress,anxiety, kujitenga na jamii , naweza kucheza kamari siku nzima na usiku pia sipati usingizi nakesha na simu kucheza kamari, kupatwa na uvivu wa kufanya kazi, hata imani yangu ktk dini imeshuka, nimekuwa mtu wa kutegemea lucky, sometimes unapoloose sana inakuvurugia moods kiasi hata hamu ya tendo la ndoa na mke wangu nakuwa silipati nawaza tu jinsi gani naweza kuirudisha pesa yangu.Pesa imekuwa haikai mkononi mwangu tofauti na kipindi sijaujua huu mchezo. Kifupi betting is a recipe for poverty.
Pia betting inaweza kukusababishia matatizo ya kiafya kama kupata shinikizo la damu.The way pressure inavyojaa mwilini pindi unapobeti na kusubiria matokeo. Inaweza kukupelekea hata ukazimia. Ni mchezo hatari kiafya unapoloose sana hata hamu ya kula chakula inapotea.
Kiufupi nakiri kuwa mraibu wa kamari ila kuanzia sasa hivi nakula yamini kuuacha huu mchezo forever.Pia namuomba Mungu aniongoze nisiweze kurejea kwenye huu ushetani.
Online casinos ndio zimenimaliza pesa aisee...yaani kama roulette unaback options zote kasoro labda namba mbili tu ukitegemea kuwa una zaidi ya 95% ya kushinda kuzingatia hii kitu wanayoitangaza kuwa wanatumia RNG (Random number generator) ila kiuhalisia hizi games zinakuwa rigged...utashangaa kila muda namba zinazojirudia ni zile ambazo hujaziwekea. Kitu ambacho kiuhalisia katika roulette hakipo hivyo. Hakuna strategy system inayoweza kuzishinda hizi betting companies.. Si martingale,fibbonacci n.k hakuna kila system utakayoitumia jua mbeleni unakwensa kulia.Hizi games wameziwekea Artificial intelligence technology ili kusoma pattern ya strategy unayoitumia so unaposhinda sana tu hii system inaanza kugeuka na kukumalizia bankroll.
Mwisho nawaasa wengine waachane na huuchezo hakuna utajiri katika kamari unless una unlimited funds na hata hao mabilionea bado wanaliwa sana na haya makampuni ya kinyonyaji.
Chris wood vp ndugu umefanikiwa kuacha au umerejea tena.?