Nimekubali kurudisha muamala wa mpesa kiasi cha shillingi 1.4M uliotumwa kwenye namba yangu kimakosa

Nimekubali kurudisha muamala wa mpesa kiasi cha shillingi 1.4M uliotumwa kwenye namba yangu kimakosa

Ishawahi kunitokea, nilitumiwa laki 8 na nusu namba siijui na wala sina makubaliano na mtu kunitumia iyo hela. Nikajua kuna mtu kakosea namba mpaka kufika asubuhi kimya, kwa sababu njia ya kuelekea kazini napitia ofisi za voda nikaingia ofisini kwao nikawaambia nimepokea hela ambayo sijui inatoka kwa nani. Wakafanya mambo yao mhamala ukarudishwa, mchana wake napigiwa simu sikuweza kupokea kwa muda huo ilivyokata nikamwambia alienipigia atume text. Ndio jamaa aliekosea mhamala akatuma text kushukuru
 
Na kwanini mkaamua kuwasumbua huduma kwa wateja ilihali angeweza tu kujirudishia muamala mwenyewee??
 
Habari wana jamvi

Jana jioni mida ya saa 12 katika mtaa mmoja ninaoishi nilikuwa nimekaa na washikaji zangu tukibishana kuhusu kanuni za mpira baada ya bodi ya ligi kuahirisha mechi ya watani wa jadi simba na yanga

Simu yangu mfukoni ika,vibrate kuashiria kwamba kuna sms imeingia, sikuifungua haraka kutokana na mabishano kuhusu kanuni kunoga, nilitulia kama dakika tatu hivi ndio nikaifungua, nikakuta sms ni ya mpesa ikionyesha nimepokea kiasi cha shilingi million moja na laki nne kutoka kwenye namba ambayo sikuifahamu, nikarudisha simu mfukoni nikaendelea na mabishano na washikaji zangu

Baada ya dakika kama tano hivi nikapigiwa simu kucheki ni namba ngeni ambayo sikuifahamu, nikapokea baada ya salam akajitambulisha kuwa yeye anaitwa Saidi Ramadhan (Hili sio jina lake halisi) akaniambia kuwa amekosea kutuma pesa hivyo anaomba nimrudishie pesa yake kwani alikuwa anatuma ada kwa binti yake chuoni.

Binafsi nilikiri kupokea kiasi hicho cha pesa na mimi sikuona shida yoyote nikamwambia awasiliane na mtoa huduma wa mtandao husuka (huduma kwa wateja) amwambie arudishe muamala huo tukawa tumekubaliana hivyo akakata simu, baada ya kama dakika kumi muamala ukawa umerudi.

Leo asubuhi mda wa saa mbili nikapokea tena muamala wa mpesa kiasi cha shilingi laki mbili kutoka kwa namba ile ile iliyonitumia pesa jana, nikapiga simu kwenye hiyo namba baada ya salam jamaa akaniambia kuwa hiyo pesa laki mbili amenitumia kama shukurani kukubali kurudisha pesa, pia akaniomba tuonane ili tufahamiane nikamwambia hapana maana sioni umuhumu wa kufanya hivyo, hata hivyo haitawezekana maana tupo mbali yeye yupo Dar mimi mkoani.
Mtu akikosea muanala hurudishi wanakushauri umwambie aende kwenye menu aurudishe mwenyewe. Wewe la kufanya hutoi huo muamala unamwacha yeye aurudishe mwenyewe.
Mitandao ya simu inashauri jambo hili kwa sababu ya utapeli unaoendelea wa watu kupokea sms fake wakakuta wanatuma pesa yao wenyewe wakidhani wanarudisha miamala.
Nikupongeze pia maana uaminifu ni bidhaa ya bei rahisi lakini adimu sana.
 
Back
Top Bottom