Nimekubali Mpira wa leo ni PESA

Nimekubali Mpira wa leo ni PESA

Bwana fuso. Umeongea point kuntu sana na mimi kama mfanyabiashara nimekubali mawazo yako mazuri.

ila akili mgando za upande wa 2 wanakubeza kwa kuleta ualisia wa kijinga katika biashara. Ndio maana wana tembeza mabakuli na kujipachika majina ya mabingwa wa kihistoria mara timu ya wananchi, ili kutafuta huruma za kusaidiwa.

ila wangejua mpira ni pesa wangemtumia bwana manji angeibadilisha yanga kwa haraka sana.
 
Yaani kichekesho kikubwa mno. Sidhani ata huko Ulaya kama kuna timu inauza hizo jezi
Mtoa mada hakujua alichopost... maana alisema 50,000 kila mkoa hapo ndipo watu wanapokataa yaani mauzo ya jezi 1,500,000 kwa SIMBA PEKEE na wale YANGA nao wakiuza zao ziwe jumla 3M ya jezi...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Matunda yote haya yote ni kutokana na uwekezaji mdogo wa Simba msimu uliopita, leo tunaona watani wetu nao wakifaidi matunda.

Sasa leo ntapiga hesabu ndogo tu kukuhakikishia kwamba mpira wa leo ni PESA yaani unaweka PESA unapata PESA.

Tuseme tuna mikoa 20 Tanzania nzima, kila mkoa upangiwe jezi 50,000 tu. Kila jezi ya Simba ni 30,000,
i
Twende kazi:-

20 x 50,000x 30,000 = Billion 30. Hii ni kwa JEZI tu.

Kweli, Weka PESA upate PESA, huna PESA kaa pembeni au tembeza BAKURI.
Profit =TR - TC
Faida = M
auzo - gha
rama za uzalishaji,,

Hiyi 30 Bil inabidi tutoe na gharama za kutengeneza jezi + usafilishaji+ kodi + n.k

Ila faida itakuwepo tu kubwa
 
Watanzania hamjielewi kaeni hivyo hivvyo, kuwa na timu yenye washabiki na wanachama approx 100,000 Tanzania ni mtaji mkubwa sana. Capital huwa si hela tu bali hata Brand ni capital.
Kudhihirisha kwamba hamjui kitu ni mtu eti anabisha kwamba huwezi kuuza jezi 50,000 katika Taifa lenye watu zaidi ya Mil 50.

Kinachohitajika ni marketing strategies,,,kwisha habari.
Kwani kasema 50,000 nchi nzima? Si kasema kila mkoa?
 
Tatizo USIMAMIZI.
mm Mimi ni shabiki wa Simba.ila kuna watu hapa mtaani kwetu ni wapenzi wa simba kabisaa.wanaipenda balaa.
Watu kama hawa ukiwaletea jezi original lazma wanunue.
Na ukitaka uwachanganye zaidi.
Haji manara ndo awe anawauzia.
 
Pia mwambie hata hao waliovaa jezi sio jezi zote ni original.... Kuna copy kibao! Kuna mtu kadunduliza ktk kibubu mwezi mzima ili apate kiingilio cha SIMBA DAY...
Tatizo lako mkuu una generalize, sio wote unawaona hapo wamejaza uwanja ndo mashabiki wa simba kisa ni simba day. NO. Ingekuwa ni rahisi hivyo unavyowaza basi leo ambayo ndo kama sherehe ya simba ungeona uzi mwekundu tupu nadhani
 
wewe unayejua elimu ya biashara endelea kubisha kwamba huwezi kuuza jezi 50,000 kwenye Taifa lenye watu milion 60. Biashara ya vitabuni inawatesa watanzania sana na wewe ni mfano tosha.
kwa hiyo zile bilioni tano akizokopesha Mo zitazalisha bilioni 30 kwa mwaka kwenye jezi tu? Acha masihara!
 
Mie namuunga mkono mtoa post.
Lazima uanze na mahesabu kabla ya kuanza business.
tatizo washabiki wa simba furaha zimewazidi mpaka sasa uwezo wa kufikiri umewapungua wanaona kila kitu kinawezekana, ndio maana manara aliropoka hata akija barca taifa anakufa, na washabiki wakaunga mkono juhudi za manara. Tulieni mwaka huu muone.
 
We huna ujualo ww umesema kila mkoa jezi 50,000 so ukizidisha na 30 unapata jezi 1,500,000... hapo ukizidisha na TZS 30,000 unapata pesa kubwa mno. WAHINDI WANGEDEAL NA HII ISHU.

Mtoa mada hakujua alichopost... maana alisema 50,000 kila mkoa hapo ndipo watu wanapokataa yaani mauzo ya jezi 1,500,000 kwa SIMBA PEKEE na wale YANGA nao wakiuza zao ziwe jumla 3M ya jezi...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Labda kama mtoa mada ame edit post yake, lakini macho yangu yanasoma ameandika 5,000 kila mkoa
 
Yanga wamepanga kuuza jezi laki moja msimu huu..kama Yanga watu wa maisha ya Kati wako kwa mamilioni..hawashindwi watu laki moja kununua jezi....
 
Ameedit aliandika 50,000 kila mkoa afu akazidisha only mikoa 20. Akapata 30B
 
Matunda yote haya yote ni kutokana na uwekezaji mdogo wa Simba msimu uliopita, leo tunaona watani wetu nao wakifaidi matunda.

Sasa leo ntapiga hesabu ndogo tu kukuhakikishia kwamba mpira wa leo ni PESA yaani unaweka PESA unapata PESA.

Tuseme tuna mikoa 20 Tanzania nzima, kila mkoa upangiwe jezi 5000 tu. Kila jezi ya Simba ni 30,000,
i
Twende kazi:-

20 x 5000x 30,000 = Billion 3. Hii ni kwa JEZI tu.

Kweli, Weka PESA upate PESA, huna PESA kaa pembeni au tembeza BAKURI.
Mauzo ya jerseys yanaingiza pesa kuliko gates collection
 
Back
Top Bottom