Nimekuja kugundua kwamba vita dhidi ya Uganda ilitengenezwa na Israel ili kumuondoa adui yao Idd Amin

Nimekuja kugundua kwamba vita dhidi ya Uganda ilitengenezwa na Israel ili kumuondoa adui yao Idd Amin

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
images (17).jpeg

1 + 1 = 2, watanzania wengi tume focuss kwenye 2 kwamba Idd Amin alivamia Kagera na ndio chanzo, tunasahau kwamba Kuna 1 + 1 zilizosababisha ikawa hio 2 na hata ukienda Wikipedia nao hawajui chanzo kamili cha 1+1 kilichoanzisha vita ila ni wazi kabisa mtu aliefaidika kwa kupinduliwa Idd Amin alikuwa ni Israel,

Idd Amin alikuwa anaichukia sana na kufanya vitendo vya kuwashambulia indirectly na alifikia nia ya kuwashambulia directly, hii ulikuwa ni mwiba kwa Israel na wakamuona ni tatizo la kulitatua haraka kabla halijakuwa kubwa.

Mwaka 1976 Idd Amin aliwapa hifadhi magaidi pale uwanja wa ndege wa Entebbe, Magaidi waliteka abiria wa Israel na maombi yao yalikuwa ni Israel waachie huru wafungwa wa Palestine wenye kesi za ugaidi, Israel hawakukubabali haya maombi wakaenda kuuvamia huo uwanja bila ushirikiano wa Uganda, waliweza kuokoa abiria wa Israel japo kulikuwa na vifo vichache kwa makomandoo kama Kaka yake Benjamin Netanyahu, Operation haikuwa ya kitoto Ile, jeshi la Uganda ilibidi lianze kuwashambulia Israel lakini walitulizwa na vifaru vilivyotua na jeshi la Israel. Idd Amin alikuwa na hasira sana na Israel, hapa Israel walishaona wazi kabisa huyu mtu ni hatari Kwa usalama wa raia wa Israel na inabidi ashughulikiwe.

images (18).jpeg
Kwenye mahojiano yaliyowahi kufanyika, Idd Amin aliapa kuja kuivamia Israel, kiuhalisia Uganda wangejaribu hivi wangepigwa kama ngoma lakini kwa muda huo Israel tayari walikuwa wana matatizo yao mengi hasa ya kigaid ndani ya nchi, waliona hili tatizo la Idd Amin watafute mbinu lishughulikiwe na majirani zake.



Vita ya Uganda na Tanzania ni ngumu sana kuujua ukweli wake lakini uki connect dots unaona Kuna uwezekano mkubwa Israel ndie alikuwa nyuma ya pazia kutamani Idd Amin atolewe madarani Kwa namna yoyote, Kuondoka Kwa Idd Amin ilikuwa Ahueni kwao
 
Ila kama ni kweli imekaa kimkakati fulani. Ile movie na history imewekwa chumvi chumvi hiv kuihusu.
Ila pia nae huenda kweli alikuwa na shida kwanza kwa jinsi alivyoichukua nchi kwa kupindua serikali.
 
Kwahiyo MOSSAD walitaka kumtoa Iddi Amin kwasababu alikuwa tishio kwao?
Mkuu, kua tishio sio lazima uwe tishio kijeshi au kiuchumi. Bob Marley aliuawa coz alikua tishio kwa maudhui ya nyimbo zake, so hata Idd amini alikua anaeneza chuki dhidi ya Israel verbally.
 
Chanzo ni hiki

Kagera
Kagera
Kagera

Hata wahaya wenyewe hua wanajichukulia km waganda

Nakuja..
 
Sawa mtoa hoja ila maelezo yako tuyaweke Sawa kidogo, special force ya Israel hawakwenda entebe na tanks!, details za operation ile na walioshiriki sio siri tena RPG's na jeeps zilizokuwa mounted na 100mm ,grunets, machine gun's.
 
Sawa mtoa hoja ila maelezo yako tuyaweke Sawa kidogo, special force ya Israel hawakwenda entebe na tanks!, details za operation ile na walioshiriki sio siri tena RPG's na jeeps zilizokuwa mounted na 100mm ,grunets, machine gun's.
Mkuu Kuna documentary niliicheki kulikiwa na vifaru vilishuahwa pale Entebbe
 
Israel ingetaka kumuua au kumuondoa Iddi Amin ingeweza bila kutumia vita kutuingiza gharama. Labda tuunganishe dots kwamba sisi tulikuwa wajamaa na wakati huo angalau uchumi wetu ulikuwa unakujakuja tukiwa na viwanda kiasi. Haikupendeza nchi ya kijamaa kustawi wakati mabepari wanataka nchi zinazowafuata kama Kenya ndio ziwe mfano wa kuigwa.

Kwa hiyo agenda zikawa mbili. Moja kumuondoa Amin ambaye hakupendwa na Israel, pili kuiingiza hasara Tanzania ili hatimaye ifanye mageuzi na kuwa ya kibepari, hii agenda labda ilikuwa ya US au mwingine. Yote hayo yalifanikiwa.

The same way muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulivyowapendeza mabepari ili kuondoa influence ya China na USSR kwa Zanzibar ambayo ilikuwa imeanza. Tutazame historia ya watu kama Babu pale visiwani na misimamo yao
 
Israel ingetaka kumuua au kumuondoa Iddi Amin ingeweza bila kutumia vita kutuingiza gharama. Labda tuunganishe dots kwamba sisi tulikuwa wajamaa na wakati huo angalau uchumi wetu ulikuwa unakujakuja tukiwa na viwanda kiasi. Haikupendeza nchi ya kijamaa kustawi wakati mabepari wanataka nchi zinazowafuata kama Kenya ndio ziwe mfano wa kuigwa.

Kwa hiyo agenda zikawa mbili. Moja kumuondoa Amin ambaye hakupendwa na Israel, pili kuiingiza hasara Tanzania ili hatimaye ifanye mageuzi na kuwa ya kibepari, hii agenda labda ilikuwa ya US au mwingine. Yote hayo yalifanikiwa.

The same way muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulivyowapendeza mabepari ili kuondoa influence ya China na USSR kwa Zanzibar ambayo ilikuwa imeanza. Tutazame historia ya watu kama Babu pale visiwani na misimamo yao

Hata huu upumbavu tu wa mtoto wa museven unaweza kuleta vita lakini mtakuja na dhana za ajabu ajabu tu kuonyesha kwa sisi waafrika hakuna kitu chochote tunaweza kufanaya..... yaani kiwe kibaya au kizuri ni lazima wazungu wametupikia
 
Du; Amin kaanza chokochoko kwa Tanzania siku nyingi sana; kaingia tu madarakani akaanza uchokozi kwa Tanzania, Nyerere alimvumilia sana muhuni yule; finali katoa hotuba ya kunyang'anya mkoa mzima wa Kagera then atapiga hadi Dar; kwamba hapa Israeli wanahusika? Nadhani hajui vizuri historia ya Idd Amino Dada
 
✍️Uganda ni mwanachama WA jumuiya ya nchi za kiislam (OIC).
✍️TICHA aliitambua Biafra.
✍️Muungano WA Tanganyika na znz.
Unganisha hizo dondoo Kwa makini,, utapata jibu
FB_IMG_1654103401853.jpg
 
Back
Top Bottom