Nimekukosea sana baba yangu, naomba Msamaha

Nimekukosea sana baba yangu, naomba Msamaha

Usitafute excuse

Umaskini ni uzembe.
Umaskini NI Laana
Umaskini ni uvivu
Umaskini ni ûjinga
Umaskini ni DHULMA

Mungu hajawahi kumpangia Mtu umaskini. Huyo hatakuwa Mungu Bali ni kibwengo.

Binafsi Naamini MTU kuwa Maskini íwe NI Baba, Mama au Mimi mwenyewe Mungu hahusiki.
Na kama anahusika Basi huyo hastahili kuitwa MUNGU.

Baba au Mimi ninastahili kulaumiwa Ikiwa nitasababisha Umaskini.

Hapo anachofanya ni kumtetea Baba yako tuu ili kutafuta kichaka cha kujificha na kisingizio cha wewe nawe kuwa Maskini ili usilaumiwe na Watoto wako.

Umaskini pia unatokana na mfumo wa dhulma àmbao upo kwèñye jamii.

Kama Baba au kama kijana kitendo cha kukubaliana kuishi kwèñye mfumo unaomkandamiza ili awe Maskini ni Sababu tosha inayomfanya astahili lawama kwa kizazi chake.

Mungu Hana Muda wa kumpangia Mtu Mvivu, Mjinga, mzembe, na anayekubali kuonewa na kudhulumiwa.

Baba anastahili Lawama kama vile àmbavyo angepatia angestahili Pongezi.
Lol
 
Sio kwamba enzi hzo wao kidogo kulikuwa na unafuu sio kama sasa
Hakuna unafuu wowote hata saiv kuna vijana wenzio wanapesa kibao zakuchezea ambazo wew huna jifunze kuheshim hustle zamazaz wako usipende kumwona et alikua fala mbona akina mwinjaku wanajenga kirahis tu nasie tumefulia unazan watoto wetu watatuelewa kirahis
 
Na ukilijua hili mapema, mtoto utaishi kwa amani saana. Ukipewa 50 ya shule hewala, ukikosa sawa, ukipewa 200 sherehe, siku ukipewa 30 burudani pia.
Nakumbuka bimkubwa mara nyingi asubuhi alikuwa akipenda tuongozane, tukifika kigamboni pale kabla ya kuoanda pantoni ananinulia biscuit flani hivi zilikuwa zinaitwa mabrooq kama sikosei, akinipa na shilingi 100 yangu au 200 ya noti aah, enzi hizo nauli ni 20 ama 30 kwa mwanafunzi kama sikosei.napanda mabasi mawili kwenda shule na mawili kurudi, so nikija nae mpaka feri maana yake daladala la kwanza anakuwa kanilipia, hapo Naenda shule naamani kabisa.
Mapumziko nikijibless mihogo na ka SUNVITA kangu, siku hiyo ni muruwa kabisa.

Siku 1😂 nipo feri, tayari gari la kwanza nishalipiwa, kaninunulia biscuit na kanipa 200 yangu, nakutana na watoto wamenitolea buku, wananiomba chenji nikawajibu sina, nina 200 tu, wakaniuliza unaenda shule na 200, nikajibu ndio, aah, walicheka saana, moyoni nikajisemea hawa maKUMER nini, sasa kinachowachekesha nini, wakati mie mwenyewe hapa naenjoy.. Nikipewa buku si ninaweza gongwa na gari kwa kuwehuka. 😂🤣
buku kwa miaka hiyo mimi nikipewa nabebewa hadi begi tena wanafanya hadi kugawana madaftari, sambusa, bagia tsh 10 miaka hiyo 😂
 
Najaribu kubeba mawazo yako kuyacovert kwenye maisha yangu naona hayakubali kabisa

Haimaanishi Mimi namaisha mazuri ila ikitokea Mpaka dakika ya mwisho nimeshindwa ninastahili kubeba lawama Kwa sababu Maisha ni yàngu.
Watoto nitakaowazaa ni wàngu.
Mungu ni wàngu.

Watoto na kizazi changu kitakuwa na Haki ya kunipongeza Ikiwa nitafanikiwa na hapohapo kitakuwa na Haki kunilaumu na kunikejeli Ikiwa sitafanikiwa.

Ukiwa na mawazo kuwa Mungu anakupangia kushindwa Jua unakosea pakubwa Sana.

Umaskini haupangwi na Mungu ndîo maana kûna Ardhi, Watu, mimea, maziwa, madini, Wanyama.
NI wewe Akili yako ijue namna ya kuyatumia. Na kukabiliana na washindani wenzako(binadamu).


Kaini anamuonea wivu nduguye Habili Kwa kufanikiwa, Mungu namuambia Fanya kama yeye(Kaini)

Hiyo ndîo Kanuni. Ukiona Mtu kafanikiwa Fanya kama yeye.
Kama anauza Madawa ya kulevya na wéwe Uza.
Kama ni mshenzi nawe kuwa Mshenzi. Kama lengo Lako ni kuwa na Maisha ya Aina Fulani.

Unàtaka utajiri alafu unamwomba Mungu unaumwa wewe.
Mungu anatoa Ñguvu za kuwa tajiri ila hatoi utajiri. Kwa sababu utajiri upogo tuu.

Narudia kama lengo Lako ni kuwa tajiri Fanya kama wanavyofanya matajiri Wengine. Simple
 
Acha kulia lia kijana.

This world is not for the weak.

You either go hard, go home or you die.
 
Nimefanya makosa makubwa na nimekukosea pakubwa imetosha sasa na nimeamua kukuomba msamaha popote pale ulipo,.

Baba nimekua mjeuri kwako kwa kuzani kuna mahitaji ulipaswa kuyatimiza kwangu na umeshindwa kizembe,

Nilikuwa nawaza kuwa:-
1) kusomesha mtoto kwenye shule za gharama ni kitu rahisi,
2) kujenga mjini ni kitu rahisi na ulijisahau kwa hanasa za mjini,
3) kumiliki mashamba na viwanja ulizembea na kuendekeza starehe,
4) pia nilikuwa najua ni uzembe wako ndio maana hauna mali kama wazee wenzako, ni uzembe wako ukashindwa kumiliki gari, pikipiki, hata baiskeli!.

Baba haukupaswa kulaumiwa kumbe.

Sasa na mimi mwanao naanza kuzeeka na hakuna nilichounda katika dunia,. Nilichogundua ni kuwa Maisha ni ghali sana na hakuna mtu anayependa kufedheheka, ni Mungu tu mwenye umchagua nani asimame wapi na wapi.
Sio kwa uzembe wako wala sio kwa ujanja wao.

Wala sio makosa ya baba wa mababa zako ma babu wa mababu zako ni Mungu tu mwenyewe.,

Pia nimegundua kuwa hata kuihifadhi PESA yenyewe ni jambo kubwa sana katika dunia ya leo,

Unapata pesa kidogo mara mtoto anaumwa mke anaumwa mara madeni mara makesi mara PESA hakuna mara uzee nao HUO.

Baba haukupaswa kulaumiwa maisha ni MAGUMU mno.
🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Una uhakika babako yupo humu jukwaani na anajua ID yako mkuu?
 
Wenzako walivyokuwa wanashushwa na magari ya njano ulikuwa unawaonea gere eeh, ushakuwa umeyaona sasa.

Mfano mdogo, Wengine toka udogoni tulitambua hali ya kweti, sikuwahi kumuona mama yangu kanifanyia dogo, mie vitu vingi saana nilikuwa naona ananifanyia kwa kujiumiza,
Nilikataa kununuliwa nguo za sikukuu nikiwa darasa la 4, nyumbani kuna watoto kibao, mara sijui wa mjomba, mara wa mama mkubwa, mara sijui wa nani, na wote anawajali kama wanae, hakuwa na ubaguzi, sikukuu moja nikamsikia anaongea na mama wa jirani sikukuu inakuja na hajui pakushika, jioni yale nikamwambia kuanzia leo, kuanzia sikukuu hii sitaki kabisa nguo za sikukuu, nikaulizwa kwaninj.

1. Sikukuu nguo zinauzwa kwa bei juu sana tofauti na uhalisia, hiyo pesa ikitumika siku za kawaida huwa napata nguo 3 mpaka 5 za kawaida na ni nzuri tu.
2. Siinjoi, kuvaa miguo ile na kuzurura kwangu ni kero, napenda kwemda beach niogelee tu.

Nikamshawishi akanielewa, kumbe lengo langu ni kumpunguzia gharama, ni bora nikose mimi lakini watoto wa ndugu zake wapate, mie mzaliwa siwezi kuwa na kinyongo.

Bimkubwa katulia kisteringi saaana, ukizingatia dingi alikata moto mapema.
Alikuwa na ajira yake ambayo kama si kuwa ndugu wengi huenda tungeinjoi kiadi kikubwa maisha, ila familia ilikuwa kubwa na katulea kwa upendo kiasi familia ikiwa kubwa watoto wa nyumba ile tunafurahi zaidi, ilikuwa ukija kwetu usiku jungu la wali linalopikwa hapo unaweza kusema kuna shughuli ndogo, nyumba yetu watu wachaache kabisa unakuta 15, nyumba ya vyumba vi4 lakini inafika pointi kuna watu wanalala sebuleni.

Mama yangu ni mtu special kuliko maelezo, ♥️♥️♥️
Kwa sasa utakuwa mbali. Katika ukoo wetu ni marufuku mtoto kurithi. Kwamantiki hiyo kila mtu hutafuta vyake. Babu alinieleza kuwa hakurithi, baba pia hakurithi na mimi sikurithi. Hata kijana wangu wa kwanza alipokuwa chuo nilimuuliza ni kiasi gani nimpe kila mwezi, akasema nimepata mkopo na kama hautatosha nitakueleza. Namshukuru mungu hakutaka hata senti moja. Alipomaliza akaanzisha kampuni ambapo sasa ana pesa kunizidi.

Mchawi wetu waafrika ni mentality ya URITHI au urisi kwa kichagga. Urisi ni kushirikiana umasikini (share poverty)
 
🥹🥹🥹

🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌🤐🤐🙄🙄
 
Kwa sasa utakuwa mbali. Katika ukoo wetu ni marufuku mtoto kurithi. Kwamantiki hiyo kila mtu hutafuta vyake. Babu alinieleza kuwa hakurithi, baba pia hakurithi na mimi sikurithi. Hata kijana wangu wa kwanza alipokuwa chuo nilimuuliza ni kiasi gani nimpe kila mwezi, akasema nimepata mkopo na kama hautatosha nitakueleza. Namshukuru mungu hakutaka hata senti moja. Alipomaliza akaanzisha kampuni ambapo sasa ana pesa kunizidi.

Mchawi wetu waafrika ni mentality ya URITHI au urisi kwa kichagga. Urisi ni kushirikiana umasikini (share poverty)
Life la kawaida tu mkuu, namshukuru mungu.
 
Shuleni kuna bimkubwa alikuwa anauza kibakuli cha viazi vimechemshwa kakatia hoho humo humo kwa sh 15, wali maharage ilikuwa sijui ni 30 vile, yaani unakula unasaza
Maisha yamebadilika sana kwasasa, nadhani miaka hiyo tulifurahia maisha ya shule kuzidi watoto wa sasa.
 
Usitafute excuse

Umaskini ni uzembe.
Umaskini NI Laana
Umaskini ni uvivu
Umaskini ni ûjinga
Umaskini ni DHULMA

Mungu hajawahi kumpangia Mtu umaskini. Huyo hatakuwa Mungu Bali ni kibwengo.

Binafsi Naamini MTU kuwa Maskini íwe NI Baba, Mama au Mimi mwenyewe Mungu hahusiki.
Na kama anahusika Basi huyo hastahili kuitwa MUNGU.

Baba au Mimi ninastahili kulaumiwa Ikiwa nitasababisha Umaskini.

Hapo anachofanya ni kumtetea Baba yako tuu ili kutafuta kichaka cha kujificha na kisingizio cha wewe nawe kuwa Maskini ili usilaumiwe na Watoto wako.

Umaskini pia unatokana na mfumo wa dhulma àmbao upo kwèñye jamii.

Kama Baba au kama kijana kitendo cha kukubaliana kuishi kwèñye mfumo unaomkandamiza ili awe Maskini ni Sababu tosha inayomfanya astahili lawama kwa kizazi chake.

Mungu Hana Muda wa kumpangia Mtu Mvivu, Mjinga, mzembe, na anayekubali kuonewa na kudhulumiwa.

Baba anastahili Lawama kama vile àmbavyo angepatia angestahili Pongezi.
Waefeso 6:5
"Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;"

Mkuu unaposema Mungu unamaanisha huyu anayetambua uwepo wa watumwa na kuamrisha watumwa wawatii mabwana zao kama vile ni kumtii kristo?
 
Back
Top Bottom