Leo asubuhi nimekutana na kitu cha ajabu. Mpaka sasa mwili unasisimka!Tofauti na binadamu wa kawaida yeye macho yake yako kifuani na siyo mawili bali manne!Ukweli miguu sikuiona ila kichwa kilikuwepo na hata mikono!Kadri nilivyozidi kumsogelea nilikuwa nikipigwa na upepo mithili ya beach.
Ilifika hatua uzalendo ukanishinda na kutimua mbio mpaka nilipofika barabara kuu ambapo nashukuru magari yalikuwa yakipita.Ajabu alikuwa kavaa nguo ambayo hadi sasa nimeshindwa kujua ni rangi gani maana ilikuwa ikibadilika.Macho niliweza kuyaona kwasababu mboni zilikuwa za kijani kali.
Pole kwa mkasa huo,hayo ndiyo yanaitwa mashetani,mapepo, majini nk. Lengo lake kubwa ni kukutisha na kukutumia salamu za jinsi ulivyo ukuu wao.
Na kwa kawaida hayamtokei mtu bila sababu, ipo sababu kwanini ulione wewe. Kama vile kumuona Malaika wa Mungu kuna sababu hata hilo jamaa kuonekana kwako kuna sababu pia, hivyo usidhani ni illusion tu ipo sababu kwanini wewe. Sababu sio rahisi kuzijua lakini mara nyingi zina kuwa za kupunguza hatima ya maisha ya mtu kiufanisi kwa kukuingizia uoga na hofu. Ukifanya juhudi ya kutafuta unaweza kujua baada ya muda
Pia ni kukutumia salam kuwa tupo, hasa kama uliwahikutaka kurithiswa mambo ya giza ukakataaa, au lifanya bifu na mtu mwenye nguvu hizo, au unafanya kitu kizuri wengine hawapendi, au unaakili sana na nyota kali watu wanaitaka. Mambo hayo yanaatract ujio wao. Hata kama ni mtumishi wa Mungu au muumini mzuri wa kristo yanaweza kukujia kutoa salam kuwa pia nasi tupo kama njia ya kukuchallenge
Hapa sikutishi na kusaidia, maranyingi waliowahi kuonana na haya madude kuna jambo lilipungua kwenye maisha yao. Either ufanisi ulipungua,magonjwa yaliongia, mikosi, nk. Sababu kubwa ni kuwa hujui kwanini alikuja kukuvisiti na alitaka nn kwako.kwa sababu ni jambo la rohoni na wewe uko mwilini usifikiri mliishia tu kuonana, mision accomplished.
Kumbuka malaika wanapokuja kwa mtu toka kwa Mungu wanakuja na ujumbe na wanauaccomplish, hivyo kama ni taarifa utapata,kama ni baraka utapewa, kama ni maonyo yatakuja nk. Hata mashetani wanakuja hivyohivyo na kutimiza haja zao.
Ushauri.
Nenda kwa watumishi wa Mungu waliojazwa nguvu za Mungu waambie umeona jambo hilo utapewa huduma.
Ukiweza tupe feedback iliwengine wajifunze. Dunia hakuna jambo la bahati mbaya yote yamepangwa either na Mungu au na shetani kufuatana na Nguvu yako mwanadamu.