Nimekutana na gari la matangazo ya mnada nimeogopa mikopo toka taasisi za fedha

Nimekutana na gari la matangazo ya mnada nimeogopa mikopo toka taasisi za fedha

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Leo asubuhi nikiwa nazurura zurura mtaani kama kawaida yangu.

Nimekutana na gari la matangazo ya mnada wa hadhara likitangaza uwepo wa mnada kwa mali za watu walioshindwa kufanya marejesho ya fedha walizochukua toka taasisi za kifedha kama mikopo.

Mali zinazouzwa ni majumba na magari.

Jambo hili liliniweka kwenye tafakuri ya kina kuhusiana na nini hasa kimewakuta wahanga wa huu mnada.

1. Je, ni riba kubwa??

2. Kutokuwa na mipango ya kueleweka?

3. Matumizi mabaya ya fedha (kutumia fedha nje ya malengo).

4. Kuharibika kwa biashara kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wa mkopaji.

5. Hali ya uchumi.??

Nikikumbuka hilo gari la mnada, nimeziogopa taasisi za kifedha.

Tusaidiane namna ya kukwepa aibu kama hizi kama mtu akichukua mkopo pale itapobidi.
 
Halafu unakuta kila siku wanapiga mnada mali tofauti tofauti lazima usinyae hlf hela zao huwa kama na mashetani fulani kila jambo ulilopanga linakuwa linakwama hela hufanyii chochote

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Wanaofanikiwa kulipa madeni ni wachache Sana sijui tatizo nini.
 
Sio kila anaeshindwa kulipa mkopo bank ana Hali ngumu wengine ndio biashara zao hizo.


Nasema hivi " Hizo ndio biashara za watu wengine" mjini hapa.
Fafanua kwa faida ya wengi mkuu sijakuelewa kabisa.

Kukopa kunakuwaje biashara??
 
Hii biashara niliiskia juu juu tu....ebu dadavua kidogo mkuu
Sometimes wakopaji wanafanya michongo na watu wa tathmini.

Labda nyumba ya 30M yeye anakukadiria ina thamani ya 60M. Hivyo ukikopa hiyo 60M lengo linakuwa siyo kurejesha bali ndio imetoka hiyo, wao watauza hiyo nyumba.

Na kuna watu kila wakijaribu kuuza nyumba zao wanakwama, wanaamua kuzichukulia mikopo
 
Sometimes wakopaji wanafanya michongo na watu tathmini.

Labda nyumba ya 30M yeye anakukadiria ina thamani ya 60M. Hivyo ukikopa hiyo 60M lengo linakuwa siyo kurejesha bali ndio imetoka hiyo, wao watauza hiyo nyumba.

Na kuna watu kila wakijaribu kuuza nyumba zao wanakwama, wanaamua kuzichukulia mikopo
Kwahiyo hapo benki inakuwa imeuziwa nyumba kwa mlango wa nyuma.
 
Leo asubuhi nikiwa nazurura zurura mtaani kama kawaida yangu.

Nimekutana na gari la matangazo ya mnada wa hadhara likitangaza uwepo wa mnada kwa mali za watu walioshindwa kufanya marejesho ya fedha walizochukua toka taasisi za kifedha kama mikopo.

Mali zinazouzwa ni majumba na magari.

Jambo hili liliniweka kwenye tafakuri ya kina kuhusiana na nini hasa kimewakuta wahanga wa huu mnada.

1. Je, ni riba kubwa??

2. Kutokuwa na mipango ya kueleweka?

3. Matumizi mabaya ya fedha (kutumia fedha nje ya malengo).

4. Kuharibika kwa biashara kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wa mkopaji.

5. Hali ya uchumi.??

Nikikumbuka hilo gari la mnada, nimeziogopa taasisi za kifedha.

Tusaidiane namna ya kukwepa aibu kama hizi kama mtu akichukua mkopo pale itapobidi.
Usiwaamini sana maana sometime ni mbinu za kuuza bidhaa wakisingizia ni za walioshindwa kulipa mikopo yao
 
Sometimes wakopaji wanafanya michongo na watu tathmini.

Labda nyumba ya 30M yeye anakukadiria ina thamani ya 60M. Hivyo ukikopa hiyo 60M lengo linakuwa siyo kurejesha bali ndio imetoka hiyo, wao watauza hiyo nyumba.

Na kuna watu kila wakijaribu kuuza nyumba zao wanakwama, wanaamua kuzichukulia mikopo
Tunatoa Siri tunaharibu biashara za watu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hapo sasa nimekuelewa mkuu, vipi na wale wanaohangaika mahakamani kuzuia nyumba zao zisiuzwe??
Mkuu kwenye msafara wa mamba na kenge wanakuwepo.


Hivyo wengine Nia inakuwa kukopa ili walipe inatokea wanakwama.


Wengine tangu mwanzo wanakuwa wameamua wakope Ila wasilipe.

So wanaoenda kuzuia ni hao ambao haikuwa Nia nyumba iuzwe
 
Leo asubuhi nikiwa nazurura zurura mtaani kama kawaida yangu.

Nimekutana na gari la matangazo ya mnada wa hadhara likitangaza uwepo wa mnada kwa mali za watu walioshindwa kufanya marejesho ya fedha walizochukua toka taasisi za kifedha kama mikopo.

Mali zinazouzwa ni majumba na magari.

Jambo hili liliniweka kwenye tafakuri ya kina kuhusiana na nini hasa kimewakuta wahanga wa huu mnada.

1. Je, ni riba kubwa??

2. Kutokuwa na mipango ya kueleweka?

3. Matumizi mabaya ya fedha (kutumia fedha nje ya malengo).

4. Kuharibika kwa biashara kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wa mkopaji.

5. Hali ya uchumi.??

Nikikumbuka hilo gari la mnada, nimeziogopa taasisi za kifedha.

Tusaidiane namna ya kukwepa aibu kama hizi kama mtu akichukua mkopo pale itapobidi.
Mkuu hakuna aibu hapo,Kama una aseti yako unauza hupati bei nzuri unaenda unakopa kisha unawaachia benki wahnagaike nayo.Mfano tu.Kuuziwa kitu kwa mnada ni sehemu ya changamoto za maisha na biashara
 
Back
Top Bottom